Ndiyo nikiwa mbali natafakari sana kuhusu eneo nililopo la LUNDU,nafikiria sana kuhusu kijiji changu.Nakumbuka mengi niliyofanya,burudani,utulivu,upendo na amani,porojo na kila kitu ilimradi siku zisonge mbele kwa furaha,kijijini hakuna msongamano,hakuna vurugu kama mijini yaani raha tupu.
Nikiwa mbali natafakari sana kuhusu kijiji hicho namna ninavyokipenda,nalitzama jua la mawio na machweo katika ziwa murua la Nyasa,ziwa lenye dhoruba kali kuliko yote ulimwenguni lakini likitulia utapenda ndio maana rafiki yangu Mark Wood wa Uingereza,hachoki kuja NYASA,hachoki kwasababu anapenda mandhari yake safiiiii.
Maji salama yasiyo na chumvi kama hilo bahari lenu la hindi,ufukwe haunuki kama huo wa kwenu wa hindi achilia mbali kuwa mchafu ovyo kabisa sijui wamekufa kibudu.
Karibuni sana Nyasa msiogope wageni tunawakaribisha dira yetu ni upendo na amani.
Karibuuuuuu
August 20, 2007
Nikiwa mbali...
Madhumuni
utulivu
Fomu za Big Brother ilikuwa moto?
Heee! inaweza kuwa ngeni hata kwangu lakini ndio ukweli kwamba uchukuaji wa fomu za kushiriki katika shindano la Big Brother Afrika ilikuwa moto mkali sana,
Hebu tafakari Salama Jabir(EATV),Tayana(Clouds FM)Witness(Wakilisha) na wengine,ama ilikuwa bonge la ushindani.Lakini mwishowe kijana Richard akaibuka kinara,kwanini?Najiuliza sana hapo, imekuwa dada zangu hao kutoswa?kulikoni hawa waendashaji?Duuu! kwa maana hiyo wanahitaji mtu asiyefahamina au siyo,
Jamani hebu fananisha ujulikanaji wa akina dada hao na huyu mchizi wangu Rich we acha tu yaani maajabu.
Lakini naamini kwamba kijana atafanya zaidi ya mwenzetu 'Mwisho Mwampamba' mwenye bonge la jina la kitanzania!upo hapo...hebu soma jina la mwakilishi huyo wa 2003.
OOh bahati mbaya mwaka huu sijawa mtazamaji kama shindano la kwanza hii ni kutokana na kupoteza kitu fulani katika shindano la mwaka huu,yaani kwa mtaalamu wa vitu aliyeona lililopita 2003 kwa hili ataona kama mdoli tu na ndivyo nilionavyo,maana wamepelekwa wazee watupu tazama umri wao....
aaaah ni porojo tu burudani
Ingia katika tovuti yao ya www.mnetafrica.com
Hebu tafakari Salama Jabir(EATV),Tayana(Clouds FM)Witness(Wakilisha) na wengine,ama ilikuwa bonge la ushindani.Lakini mwishowe kijana Richard akaibuka kinara,kwanini?Najiuliza sana hapo, imekuwa dada zangu hao kutoswa?kulikoni hawa waendashaji?Duuu! kwa maana hiyo wanahitaji mtu asiyefahamina au siyo,
Jamani hebu fananisha ujulikanaji wa akina dada hao na huyu mchizi wangu Rich we acha tu yaani maajabu.
Lakini naamini kwamba kijana atafanya zaidi ya mwenzetu 'Mwisho Mwampamba' mwenye bonge la jina la kitanzania!upo hapo...hebu soma jina la mwakilishi huyo wa 2003.
OOh bahati mbaya mwaka huu sijawa mtazamaji kama shindano la kwanza hii ni kutokana na kupoteza kitu fulani katika shindano la mwaka huu,yaani kwa mtaalamu wa vitu aliyeona lililopita 2003 kwa hili ataona kama mdoli tu na ndivyo nilionavyo,maana wamepelekwa wazee watupu tazama umri wao....
aaaah ni porojo tu burudani
Ingia katika tovuti yao ya www.mnetafrica.com
Madhumuni
burudani
August 19, 2007
Utumwani tena!!!
Mateso ya moyo katika mtumizi ya lugha za kikoloni.Kila siku kuna wasomi wasiojua kitu na ambao vichwa vyao vimejaa nukuuu za kikoloni.
Hakuna jambo lisilofanywa kwa nukuu za kikoloni,mfano unaweza kumkuta mtu akizungumza lugha ya kiswahili huku akichapia maneno mengi tu ya lugha ya kigeni hususani ya kijivuni(kiingereza) maarufu kama 'code mixing','code switching','code alteration' n.k wengi wawasomi wetu wamefilisika kichwani mwao hawana tena uzito unao stahili.Mfano unaweza kuwa na cheti za Uzamili lakini matokeo yake au usomi wako hauwezi kukufanya uwe na maarifa kadhaa hivyo kujikuta ukibabaika sababu ya lugha ya kikoloni huku jambo hilo unalijua vyema.
Wanafunzi wa elimu ya juu wengi wanatumia kitu kinachoitwa "copy and Paste" yaani si hao tu kuna idadi kubwa sana ya vijana tunaotumia silaha hiyo matokeo yake kila mtu anapigana namna ya kufaulu darasani,huko sekondari ndio kabisaaaaa ndipo mauaji haya yanapoanzia.
Kwanini tusitumie lugha yetu yenye kukupa hamu ya kuizungumza?inakupa uwezo wakunyumbulisha,kupambanua na kuelewa zaidi mambo...
Je kwanini tusitumie lugha hiyo(kiswahili) katika vyuo vyetu sasa,hakuna lugha iliyokamilika hapa ulimwenguni.Kiingereza kina maneno mengi ya kuazima toka kifaransa,kilatini,kireno,kiswahili(tazama neno;'safari')utakubali.
Njoo tuungane,kiswahili kina maneno ya kutosha kinachoogopwa eti gharama kubwa; ni ujinga...au nini maudhi ******
Hakuna jambo lisilofanywa kwa nukuu za kikoloni,mfano unaweza kumkuta mtu akizungumza lugha ya kiswahili huku akichapia maneno mengi tu ya lugha ya kigeni hususani ya kijivuni(kiingereza) maarufu kama 'code mixing','code switching','code alteration' n.k wengi wawasomi wetu wamefilisika kichwani mwao hawana tena uzito unao stahili.Mfano unaweza kuwa na cheti za Uzamili lakini matokeo yake au usomi wako hauwezi kukufanya uwe na maarifa kadhaa hivyo kujikuta ukibabaika sababu ya lugha ya kikoloni huku jambo hilo unalijua vyema.
Wanafunzi wa elimu ya juu wengi wanatumia kitu kinachoitwa "copy and Paste" yaani si hao tu kuna idadi kubwa sana ya vijana tunaotumia silaha hiyo matokeo yake kila mtu anapigana namna ya kufaulu darasani,huko sekondari ndio kabisaaaaa ndipo mauaji haya yanapoanzia.
Kwanini tusitumie lugha yetu yenye kukupa hamu ya kuizungumza?inakupa uwezo wakunyumbulisha,kupambanua na kuelewa zaidi mambo...
Je kwanini tusitumie lugha hiyo(kiswahili) katika vyuo vyetu sasa,hakuna lugha iliyokamilika hapa ulimwenguni.Kiingereza kina maneno mengi ya kuazima toka kifaransa,kilatini,kireno,kiswahili(tazama neno;'safari')utakubali.
Njoo tuungane,kiswahili kina maneno ya kutosha kinachoogopwa eti gharama kubwa; ni ujinga...au nini maudhi ******
Madhumuni
habari
BUNGE; Somo la uraia limepotea..
MOYO KABLA YA SILAHA......
Hakuna asiyefahamu kwamba hivi sasa habari za mbunge Zitto Kabwe zinarindima kila kona ya nchi kwani kusimamishwa ubunge imekuwa kama wanachochea nguvu ya raia kukubali kwamba bunge letu limepoteza somo mahiri la uarai.
Hivi tatizo ni lipi hasa hadi tunaogopa kuwa na tume hiyo aliyopendekeza?
kwani kujua ukweli uko wapi kwa porojo za siku hiyo zinaweza kumaliza nguvu za chama tawala? kushushwa hadhi maana yake nini?kwani ukishushwa hadhi unaweza kufa?
Haya mwingine alishatanguliza adhabu kabla hata Big bunge hajatoa uamuzi,bila shaka alipangwa huyo,wazee wetu hawatujali tena ni wakati wa mapinduzi sasa,ewe kijana simama usiogope,umasikini wako si tija bali nguvu zako na hekima zako zikuondoe katika utumwa,pesa si kila kitu bali moyo wa huruma kwakizazi kinachokuja.
Tuache ushabiki kwa suala hili;kwanini mkataba usainiwe wakati Rais alishasema kwamba hakuna kufanyika hilo hadi mikataba mingine ipitiwe upya?Nini maana ya kwenda kusainiwa London? Haijalishi kwamba ilikuwa hotelini au wapi ilahoja kwanini ilifanyika huko?.
Toa maoni..uspitwe
uhuru daima
Hakuna asiyefahamu kwamba hivi sasa habari za mbunge Zitto Kabwe zinarindima kila kona ya nchi kwani kusimamishwa ubunge imekuwa kama wanachochea nguvu ya raia kukubali kwamba bunge letu limepoteza somo mahiri la uarai.
Hivi tatizo ni lipi hasa hadi tunaogopa kuwa na tume hiyo aliyopendekeza?
kwani kujua ukweli uko wapi kwa porojo za siku hiyo zinaweza kumaliza nguvu za chama tawala? kushushwa hadhi maana yake nini?kwani ukishushwa hadhi unaweza kufa?
Haya mwingine alishatanguliza adhabu kabla hata Big bunge hajatoa uamuzi,bila shaka alipangwa huyo,wazee wetu hawatujali tena ni wakati wa mapinduzi sasa,ewe kijana simama usiogope,umasikini wako si tija bali nguvu zako na hekima zako zikuondoe katika utumwa,pesa si kila kitu bali moyo wa huruma kwakizazi kinachokuja.
Tuache ushabiki kwa suala hili;kwanini mkataba usainiwe wakati Rais alishasema kwamba hakuna kufanyika hilo hadi mikataba mingine ipitiwe upya?Nini maana ya kwenda kusainiwa London? Haijalishi kwamba ilikuwa hotelini au wapi ilahoja kwanini ilifanyika huko?.
Toa maoni..uspitwe
uhuru daima
Madhumuni
siasa.
August 18, 2007
ETHANOL ni jibu?
Ili kuondokana na Utegemezi wa mafuta,inaonekana kwamba hili lijamaa 'ethanol' ni njia sahihi ya kupata nishati mbadala.
Lakini nishati hii inapingwa na magwiji kama Rais Hugo Chavez,Fidel Castro kwa madai kwamba itasababisha njaa duniani.
Ikumbukwe 'ethanol' ni nishati kwa kutumia mimea hasa mahindi na miwa n.k.Magwiji hao wanapingana na Rais joji kichaka wa marekani kwamba inaweza kusababisha madhara ulimwenguni hasa kutokana na kwamba bei ya chakula itapanda na watu masikini watakosa chakula.
Brazil ndiko hasa 'ethanol'ilikogunduliwa na huku kichaka akitangaza kuwa ni bora zaidi ili kuonmdokana na gharama za nishati ya mafuta.
Je kama Tanzania tuna ardhi ya kulima chakula tunazidi kuomba,tutaweza wakati huo?
Lakini nishati hii inapingwa na magwiji kama Rais Hugo Chavez,Fidel Castro kwa madai kwamba itasababisha njaa duniani.
Ikumbukwe 'ethanol' ni nishati kwa kutumia mimea hasa mahindi na miwa n.k.Magwiji hao wanapingana na Rais joji kichaka wa marekani kwamba inaweza kusababisha madhara ulimwenguni hasa kutokana na kwamba bei ya chakula itapanda na watu masikini watakosa chakula.
Brazil ndiko hasa 'ethanol'ilikogunduliwa na huku kichaka akitangaza kuwa ni bora zaidi ili kuonmdokana na gharama za nishati ya mafuta.
Je kama Tanzania tuna ardhi ya kulima chakula tunazidi kuomba,tutaweza wakati huo?
Madhumuni
siasa.
Lundu & karibuni Nyasa: Si Vita,ni kujiweka sawa tu
johari ya matumaini
nimeirudisha hii nikikumbuka nilipoanza kublogu, daaa imenikumbusha mbali sana nakesha nasoma mistari ya NDESANJO kila jumapili. Leo nimeisoma tena si unajua kuhifadhi ukipendacho
Madhumuni
amani na upendo,
kumbukumbu,
urafiki
Nikiwa Mbeya;kidato cha sita 2005
Madhumuni
utulivu
Ni wakati wa kujiliwaza; kwetu Nyasa
August 17, 2007
HUYU HAPA..
Kwa wapenzi wa filamu lazima wamtambue huyu kijana wa kitanzania ambaye anafanya vitu vyake huko majuu..
Nani huyo?
Ingia hapa...<strong>www.kibirafims.com au www.tzuk.net
Nani huyo?
Ingia hapa...<strong>www.kibirafims.com au www.tzuk.net
Unatafuta kazi....ingia hapa
Kwa wale wanaosaka kazi huko majuu(ughaibuni) na wenye usongo wa kubomoa tamaduni zao kwa masuala mbalimbali,wanaweza kujipatia kazi safi na salama zaidi kama unapenda kazi hizo.
Usipitwe hebu jaribu kuingia katika mitandao ili utimize ndoto zako za kwenda majuu
Ingia hapa haraka......www.myprimejob.com
kuna nafasi nyingi za kazi.
Usipitwe hebu jaribu kuingia katika mitandao ili utimize ndoto zako za kwenda majuu
Ingia hapa haraka......www.myprimejob.com
kuna nafasi nyingi za kazi.
Unayajua maneno haya..
Inawezakana kwamba katika lugha yetu maridadi ikawa inachezewa na watu wasioelewa umuhimu wake.Wengi wanadhani kuongea lugha za Wakoloni ni njia salama zaidi ili kujiunga katikadunia tambarare hii..
Hebu tutazame maneno haya....
KISAGALIMA(vi-)=Ni jembe lililochakaa,kiselemo.
KIPWEPWE=Ugonjwa wa ngozi wenye kutoa madoa mekundu.
KIPETE=Kibahasha
MZAFAFA=Mwendo wa maringo.
NSONO-Tendo la kukoroma.
MNUMAMNUMA=Mtu apendaye sana kutafuta mambo ya uramali,mtukutu,apendaye kuulizia mambo ya uchawi,mshirikina.
MLEO (mi-)=Mwendo wa kupepesuka.
MGALABA(mi-)=Mshindani.
Hebu tutazame maneno haya....
KISAGALIMA(vi-)=Ni jembe lililochakaa,kiselemo.
KIPWEPWE=Ugonjwa wa ngozi wenye kutoa madoa mekundu.
KIPETE=Kibahasha
MZAFAFA=Mwendo wa maringo.
NSONO-Tendo la kukoroma.
MNUMAMNUMA=Mtu apendaye sana kutafuta mambo ya uramali,mtukutu,apendaye kuulizia mambo ya uchawi,mshirikina.
MLEO (mi-)=Mwendo wa kupepesuka.
MGALABA(mi-)=Mshindani.
August 16, 2007
Blogu ni nini?
Nimeona ni vyema nikaweka hapa maana ya Blogu ili kuwezesha wengine wajifunze kama mimi nilivyojifunza.
Haya twende sambamba ili tusamabze maarifa kwa wengine.............
"BLOGU" ni neno la lugha ya kikoloni(kiingereza) limetokana na neno "Weblog".
"BLOGU" ni teknolojia mpya inayowezesha mtu yoyote,kikundi chochote au shirika lolote kuwa na ukurasa wake katika mtandao.
Hii ni kama shajara "notibuku" ya mtandaoni kazi yake ni sawa na ya vyombo vya habari mfano Magazeti,Redio,Runinga n.k.Aidha Blogu haihitaji kuwa na gharama zozote maana huduma hii ni bure.Bali kinachohitajika ni muda wako tu kuanzisha Blogu yako tena inakufanya utumie dakika 5 tu ili kukamilisha ndoto zako za kuwa na safu yako.
Hii inakuwezesha kuwa na safu yako mwenyewe kama vile ilivyo kwa wanasafu wa magazetini.Pia inahitaji wewe kuwa na hamu ya mabadiliko ya habari duniani,ambayo huenda mbio mithili ya upepo mkali lakini huu si upepo wa kupita bali ni upepo endelevu........maana hii nimeazima na imetolewa na kufundishwa mara kwa mara na......"Ndesanjo Macha" ;muone katika.."www.jikomboe.com'
Namna ya kuanzisha BLOGU yako.
Ingia hapa; HYPERLINK "http// mwongozo.wordpress.com,http//mwongozo.wordpress.com.
Blogu za kitanzania;ingia hapa; http//tinyurl.com/rwyow
Haya twende sambamba ili tusamabze maarifa kwa wengine.............
"BLOGU" ni neno la lugha ya kikoloni(kiingereza) limetokana na neno "Weblog".
"BLOGU" ni teknolojia mpya inayowezesha mtu yoyote,kikundi chochote au shirika lolote kuwa na ukurasa wake katika mtandao.
Hii ni kama shajara "notibuku" ya mtandaoni kazi yake ni sawa na ya vyombo vya habari mfano Magazeti,Redio,Runinga n.k.Aidha Blogu haihitaji kuwa na gharama zozote maana huduma hii ni bure.Bali kinachohitajika ni muda wako tu kuanzisha Blogu yako tena inakufanya utumie dakika 5 tu ili kukamilisha ndoto zako za kuwa na safu yako.
Hii inakuwezesha kuwa na safu yako mwenyewe kama vile ilivyo kwa wanasafu wa magazetini.Pia inahitaji wewe kuwa na hamu ya mabadiliko ya habari duniani,ambayo huenda mbio mithili ya upepo mkali lakini huu si upepo wa kupita bali ni upepo endelevu........maana hii nimeazima na imetolewa na kufundishwa mara kwa mara na......"Ndesanjo Macha" ;muone katika.."www.jikomboe.com'
Namna ya kuanzisha BLOGU yako.
Ingia hapa; HYPERLINK "http// mwongozo.wordpress.com,http//mwongozo.wordpress.com.
Blogu za kitanzania;ingia hapa; http//tinyurl.com/rwyow
August 15, 2007
Lundu & karibuni Nyasa
Ni wakati ninaowaza ni sehemu gani nitaipenda kama ninavyoipenda nyasa.Wapi nitapapenda zaidi ya kijiji changu cha lundu?
yote heri bali ni kwa wakaazi wenye kupenda utulivu si fujo za mijini ambako hatautamaduni hakuna,watu wanishi kama mbayuwayu,wanatenda maovu kama hawana miongozo ya kanuni za maisha yao.
KARIBUNI SANA LUNDU KARIBUNI SANA NYASA
yote heri bali ni kwa wakaazi wenye kupenda utulivu si fujo za mijini ambako hatautamaduni hakuna,watu wanishi kama mbayuwayu,wanatenda maovu kama hawana miongozo ya kanuni za maisha yao.
KARIBUNI SANA LUNDU KARIBUNI SANA NYASA
Picha zipo.......!
Naam wasomaji kwanza niwatake radhi kwamba sijawea picha yoyote,lakini hii haimaanishi kwamba sipendi bali najaribu kuwasiliana na wataalamu ili waweze kufanya hilo na siku chache zijazo naweza kuweka picha maporojo mengine kibao si mnajua kwamba mwanzo mgumu?
kila heri fikra za maisha yenye maarifa zaidi lakini tukumbuke kwamba kila jambo lina wakati wake na nafasi yake tutunze nuda,tuutumie vyema ni wakati maarifa mapya
kila heri fikra za maisha yenye maarifa zaidi lakini tukumbuke kwamba kila jambo lina wakati wake na nafasi yake tutunze nuda,tuutumie vyema ni wakati maarifa mapya
Tumepigwa na butwaa!!!!!!!!!!!!????????????
Mbona kimya wana kwetu kulikoni nchi yetu imebong'a hivi
yaani kila mtu ipo siku atakuwa dobi kwa waishiwa wa kubwata na mabata huko mpwapwa
unaguna?
kazi kwenu wana nchi ya kujidai wa amani na utulivu mtaliwa kweupeeeeeee
hoja ya msingi imekuwa ya kupakana matope si kuhoji uhalisia wa mambo?
yaani kila mtu ipo siku atakuwa dobi kwa waishiwa wa kubwata na mabata huko mpwapwa
unaguna?
kazi kwenu wana nchi ya kujidai wa amani na utulivu mtaliwa kweupeeeeeee
hoja ya msingi imekuwa ya kupakana matope si kuhoji uhalisia wa mambo?
Tumepigwa na butwaa!!!!!!!!!!!!????????????
Eeee! unashangaa nini tena jamani hawa ndio wabunge wetu tunaojidai kwamba tumewachagua kwa wingi wa kura.Naapa kwamba mmeliwa mwaka huu mchana kweupeeeeeeeeeeee,si mmeona jinsi huko Dom kijana alivyokatwa ngebe kama mtuhumiwa....maajabu ya wanakwetu hawa hata ndugu zangu kule nyasa hawawezi kukubali hata kidogo...wallahi....
Ni bunge letu nimempeleka mwakilishi wa sauti za wanaotaabika kwamba hana ushahidi waklti hoja yenyewe ni ndogo tu kwamba tuchunguze.....
Mpaka januari 2008 ...mwanangu yaani hakuna cha masurufu wala marupurupu yote kayamwaga..duuu...
halafu wajinga fulani wanadai kuwa mwanasiasa mpaka uwe na hela ...haki ya mwenyezi hivi wameliwa mpaka nguo wanazo vaa.
Ndio huko dom kumetokea kusimamishwa kwa kijana anayedaiwa kuwa machachari toka chama cha watu wanaodai kwamba wanawakilisha maendeleo ya wanaohuzunika leo na kesho
usipitwe toa maoni yako ndugu......
uhuru daima....
Ni bunge letu nimempeleka mwakilishi wa sauti za wanaotaabika kwamba hana ushahidi waklti hoja yenyewe ni ndogo tu kwamba tuchunguze.....
Mpaka januari 2008 ...mwanangu yaani hakuna cha masurufu wala marupurupu yote kayamwaga..duuu...
halafu wajinga fulani wanadai kuwa mwanasiasa mpaka uwe na hela ...haki ya mwenyezi hivi wameliwa mpaka nguo wanazo vaa.
Ndio huko dom kumetokea kusimamishwa kwa kijana anayedaiwa kuwa machachari toka chama cha watu wanaodai kwamba wanawakilisha maendeleo ya wanaohuzunika leo na kesho
usipitwe toa maoni yako ndugu......
uhuru daima....
Ni siku nyingi sana bado nawaza namna ambavyo umekuwa ukisumbua akili yangu.Lakini kwa hakika nimejitahidi kutafakari mambo mengi katika mustakabali wa maisha yangu tokana na njia yako uliyopita,hata hivyo jibu ni kwamba sina wakati wa kupoteza katika maisha na mtazamo wangu ulivyo sas na mtazamo mpya ninaoujenga ni hatari kughilibiwa!ipo kazi ndugu zanguni maisha haya jamani......
Msomaji unaweza kudhani ni lawana haba lakini ni nyingi kuliko jinsi ambavyo msichana huyu alivyofanya.Pia siwezi kulaumu lolote kuhusu maamuzi yake na mwenendo wake wa maisha,lakini anapaswa kutazama upya,kwani siafiki mtazamo huo ndio maana tunahitilafiana.
Msichana huyu aitwaye YASINTA ni msichana ambaye tulikua pamoja toka sekondari mkoani kwangu Ruvuma,nilijikuta nikiamini kwamba ukiwa na msichana ni bonge la ujiko kumbe ulikuwa ujuha tu.Wacha niseme msomaji wangu ni mbaya sana ukawa na mtu ambaye unampenda halafu ukaachwa njiani kwa sabau tu kuna tofauti za mtazamo ambazo haziwezi kufanana hivyo mnakubalina kidogo na mnatofautiana sana,hivi unatarajia nini?
Basi ikawa kama ni ujiko ambao hata hivyo ulinisaidia kwa kipindi kifupi tu,kwani wakati huo 1999-2000 hadi nilipo maliza kidato cha nne 2001 nilikuwa tayari nimejikwaa kidogo lakini niliamini ipo siku yanaweza kujirudia masuala yale,ambayo nilidhani ni mema.Kwa kawaida vijana wengi hupenda sana ujiko hasa tukiwa mashuleni ambako tunajumuiya za wanafunzi wa aina mbalimbali hivyo kila mmoja anajitahidi kuonyesha umahiri wake wa masuala kadhaa.
Kwangu kuwa na msichana mwanzo lilikuwa jambo gumu sana lakini kwa huyu ilitokea kwa nia ya ujiko hapo shule,hata hivyo bado najiuliza mbona nina maumivu mimi kuliko yeye alivyofanya?Kifupi ni kwamba imefikia wakati binadamu kutazama upya mitazamo yetu juu ya masuala haya ya mapenzi,tunahutaji kuweka kanuni imara ili ukichanganua mlinganyo wa maisha yako ubaini kwamba kama ulikosea kanuni basi lazima majibu yatakugomea tu.
Sasa wakati narejea rejea kisa hiki ambacho kwa kweli kinanichanganya sana kukitatua kwasababu nhusika sinaye karibu,huwa nachanganya sana hoja zangu hilo mnisamehe sana.
Ni hivi msichana huyu tulijumuika pamoja enzi hizo tukiwa shule LUNDO SEKONDARI(kwa waliofika Mbamba Bay au Liuli wanaifahamu).Nilikuwa kama nimeona dunia yote yangu nikajiona bonge la mjanja huku nikiwa na ka umaarufu fulani kwanza nilikuwa mchezaji wa "volleyball" mkali na ambaye alifundisha wengi pale shule,usishangae ujiko huo.
Msichana huyu basi akawa hanijui wala kuniaona najichanganya na watu wengi isipo kuwa rafiki yangu mkubwa wakati huo Simon Haule na niliokuwa na urafiki wa maarifa sana kama Michael Mkate na Libaga Mapunda(wanisamehe kwa kuwataja) au nikiwa pale bweni nakula muda mzuri wa kusoma vitabu kama "kikosi cha kisasi" n.k.Huyu rafiki yagu wa kwanza alikuwa mtu wa "vidosho" sana hivyo hatukuweza kulingana katika falsafa na itikadi lakini wawili wa mwisho hapo juu nilikuwa nao bega kwa bega katika kusaka maarifa kwa njia za kikoloni.
Basi kijana nikawa na matokeo mema darasani na hapo ndipo huyu ninayemwandika leo akajitokeza kwangu kwa kudadisi hivi mimi ni nani na natokea wapi.Wengi walijua kijana nimetokea pale Mbinga mjini kumbe wapi kijana pale nilikuwa nakula muda mzuri wa mapumziko ya baada ya shule kufungwa.Naam... tukazoeana kidogo kama ujuavyo akinadada kwa mikogo,wala kijana sikuwa na mchecheto kwani nilikuwa najiamini utadhani Hitler(usiogope) yaani nilijiona gangwe kama Okonkwo,nilikuwa na kasumba za kutojiunga na makundi yasiyo na jipya wala mtazamo wowote wa maisha,nilijiona natafuta maarifa kwa nguvu za kibitozi tui lakini sikua na hata kauchembe ka huo unini.....
Ilikuwa kama mzaha tu kwa msichana kama huyu ambaye alichukuliwa na wanafunzi kuwa wa hadhi ya juu si uanajua tena vijana wa shule.Ikawa mchana ,ikawa siku basi maua tukayapanda wenyewe.Tukaendelea hivyo hadi pale kisanga ambacho amekuwahi kuniuliza kwanini nilifanya vile.Kisanga hicho kilitokea nikiwa katika kambi ya UMISETA yaani duu!haya ikawaje?kisanga kikaishia hapo(sitakisema) naona haya. Ni hivi nilishangaa mtoto kawa kama kavurugwa akili na jambo fulani ila roho ikawa inampwita aanzeje maana baada ya kambi hiyo kumalizika na wachezaji kuruhusiwa kurejea mashuleni kwetu ikawa kama kawaida kufika Mbinga toka Songea kijana nikaona ngoja nionane kwanza na washikadau wangu ili nikija likizo wajue kijana alikwisha kuwapatia jambo langu muhimu la likizo hiyo.
Lakini huko shule binti akawa anasubiri kijana nije,lakini si kama mwanzo bali ni kama kuunganisha UJAMAA na UNYANG'AU(ubepari),ilikuwaje? Niligundua siku moja hivi maana si unajua kwamba ukisoama vitabu vyenye akili unapata mwanya wa kuchanganua mambo? Nilipobaini jambo sikuhoji nilinyamaza tu huku kijana wangu wa kazi(rafiki)Godfrey Christopher akinipa habari nzima basi nikasema mimi ni ngangari nitalimaliza kijeuri!lakini wapi,.ikawa kama nachelewa tu kwani alitakiwa kunieleza kitambo lakini aliposuasua nami nikala jiwe tu kusubiri nini kitajiri ili kuokoa muda.
Lakini kumbuka kwamba yalioyojiri wakati ule tayari nilishatemwa kikosini na nilijaribu kujirejesha katika kiwango changu ikashindikana,tukabaki kupiga stori za hapa na pale na WATU wasijue kama hakuna tena ujiko kama wa kale,tukabaki kuwa marafiki kama ilivyoada kwa binadamu sote ni ndugu.ikawa mchana ,ikawa usiku mambo hayakubadilika nikakukabli matokeo kwa kauli kwamba ipo siku tutaonana na tutajiuliza sababu pia kwamba mimi ni mtu sahihi kwake kuliko wengi wanaomtazama kama chui mwenye uchu wa kula nyama.
2006 hiyo kijana nipo jiji la matapeli DAR naona na binti lakini hii ni baada ya kutoonana kule Mbeya na nyumbani mkoani hapa Ruvuma hususani kijiweni kwangu Mbinga mjini ambapo yeye ni makani yake tofauti na mimi toto la kinyasa la kuvua samaki wa kitoweo;tunajaribu kusahihisha kwanini sisi tulifarakana hatua ile?(kutemana)lakini jibu likawa nani alianza?tuhuma kibao mara kijana anayeandika hapa alikuwa ana kimada kwa siri.Jibu la mwisho kijana anayeandika hapa akasema msichana ndiye aliyeanza na hoja hii ikakubalika,tatizo ni kwamba tulidhani ni wakati wa kufanya kweli sasa kwasababu tumekuwa angalau umri wa kati kama 10+10+3= sijui nini huko! kwamba muda wa kuwa pamoja kwa umakini.eeeeeeeeeeeeeeehhhh wapi bwana yaani ni balaa tupu,nashusha aya.......
Siku moja nikapokea sauti ya kutisha toka katika simu kisha ujumbe wa simu ukaingia baada ya mazungumzo na kijana aliyenihoji kuwa mimi ni nani.Duu nikajua kwamba nimeingia anga mbaya kwa kuruhusu mtu aliyeimwaga enzi hizo eti sasa nione chungu kapata kivuno...........,.,,,.Nikaambiwa kwamba huyu ndio "waubani" wake hivyo nisitume ujumbe wala kubipu si mnajua za kibongo kwa kubipu.Lakini hii ilikuja baada ya kutoonana kwa miaka 3 kwani hata huo 2006 ulikuwa wa 4 nikaona iwe vyema ninyamaze....AAh hapana niandika ujumbe, kwani nilishabaini kuwa aliyelonga kwenye simu si kidume kweli ila nimefukuzwa kwa njia kupitia kidume mwenzangu tu kwa hofu kuwa mimi ni msema kweli kwa kumfanyia marekebisho kwani alikuwa na mwendo mgumu usiohatarisha,haya yote yanatokea baada ya hitilafu kubwa kati yetu lakini si hitilafu ya kuhatarisha bali ni itikadi za maisha kila mmoja anajiona yuko sawa zaidi ya mwingine,mitazamo iko kinyume nyume.
Nikaona mambo yanakwenada upogo sasa,nikatulia nikajihoji kwanini,nikasalimu amri nikaseama yote heri lakini nikachia ujumbe kama huu utambae kichwani mwake ..........."Praise of the Folly,shall forza companie".....daa sentensi kali sana hii na naipendamno na kuiamini na ikiwa andhani ni utoto mwanangu ameumia sana.Maana walijisifia kwamba wanapendana mno kumbe ni kiini macho...mara leo namba ninayopigiwa....mpigaji haongei...mara...niwekewe sauti ya zima moto mara..... lakini sijibu kitu.....yaani ni "dirty off you shoulder" ....ukurasa mwingine .....,,.,,..,,n.k
Hivi kwanini YASINTA umefanya hivyo?kwanini unachukulia maisha kama mbio za vijiti? maana mbio hizo ukichoka bora kujitoa kuliko kujifanya kinara huku uhai unatoweka.
bado kauli niliyoambiwa mwaka 2000 naikumbuka kwamba...."mwongoze mwanamke mkiwa barabarani.." yaani sikuelewa ila siku hizi nimebaini kumbe ni kujifanya unampenda sana msichana basi umkumbatie hadharani yaani popote...sijui kupigana mibusu......na nini...sijui barabarni...n.k .. hadharani nayo ni njema au vipi maana kijana sijui kitu waungwana,yaani siyajui hayo toto lililozoea kuvua samaki na kuogelea na watalii waliokuja ziwa nyasa enzi za mapadre wa kizungu(wa kikoloni) we aah acha tu.
Nilishasema kwamba ndugu yangu mimi ni mtu sahihi,lakini kazi bure wanapenda kuvinjari na maisha ya kwenye runinga za kimagharibi..lakini kijana sijui hayo si kwa ujinga bali msimamo,hoja n.k. Huyu binti ananifanya niwaze wasichana wote kama ni majeruhi wa maisha yaani hawana kile wanachoamini katika mahaba yao(samahani najua si wote).Yaani angejua sasa ninavyo watazama wasichana kwa jicho la pembeni nikiamini kuwa siku yoyote yatatokea kama ya WTC huko marekani,yaani nakimbia kama mbio za akina mzee Bayi.
Yaani naogopa kuelekeza mawazo haya na mtazamo wangu juu ya masuala haya tena basi bali ni kujibisha katika shughuli zangu ikiwemo kuandika porojo zangu katika anuani hii,bora kuliko kumtaka mtu ambaye haoni umuhimu wa kutakiwa na asiyemtaka.Hivi kwanini alifanya hivyo au wasichana wanapenda sana kubembelezwa? aaaaahhh hapa najua si hivyo ila nauliza tu.wala sijui kubembeleza ndio nini jamani...
Basi ndio hivyo nimeamua kuwa na maarifa mapya,mtazamo mpya,fikra mpya,mapinduzi mpya, sitaki kupoteza muda wa kuinua maisha yangu kama alivyotuasa 2PAC.Wasomaji niacheni nizungumze kama mwndawazimu maana huyu dada hajui kama mimi nilikuwa namhitaji sana na nadhani ipo siku atatambua kwamba aliyekuwa akimhitaji ni mimi,potelea mbali sasa nimefunga masikio nasaka fikra mpya kutoka sayari mpya na siyo dunia tena labda wasizaliwe na mwanzo wa HAWA na ADAMU.aaaaaaaaaaaaaaaaaaahhhhhhh...acheni nicheke...ooooooiiiiiih
Si mkwara bali akiona hapa aone kama sitanii kitu nimekuwa mwanaharakati wa mapinduzi ya kweli hakuna muda wa kuzubaa tena.
Pole kwa kunifuatlia sana lakini huyu binti naamini ninaweza kuonana naye muda wowote ila tatizo ni mitazano tu,yupo anajidai anakamua kitabu cha sheria za shahada huko.......na naamini kwamba ananiheshimu kama ninavyomheshimu kama wanadamu wengine.
kila la heri kwa maisha yake hayo....lakini kwanini alifanya hivyo?alidanganya kwamba aliyeongea nami katika simu ni waubani wake wakati naitambua sauti ile,hata hivyo mtu aliye karibu yake anashindwa kuniambia ukwEli kwa kuwa anajua sina muda wa kuujua UKWELI HUO TENA kwani nimeshaujua na sihitajiki kuujua zaidi bali.......
KWAHERI.......
Msomaji unaweza kudhani ni lawana haba lakini ni nyingi kuliko jinsi ambavyo msichana huyu alivyofanya.Pia siwezi kulaumu lolote kuhusu maamuzi yake na mwenendo wake wa maisha,lakini anapaswa kutazama upya,kwani siafiki mtazamo huo ndio maana tunahitilafiana.
Msichana huyu aitwaye YASINTA ni msichana ambaye tulikua pamoja toka sekondari mkoani kwangu Ruvuma,nilijikuta nikiamini kwamba ukiwa na msichana ni bonge la ujiko kumbe ulikuwa ujuha tu.Wacha niseme msomaji wangu ni mbaya sana ukawa na mtu ambaye unampenda halafu ukaachwa njiani kwa sabau tu kuna tofauti za mtazamo ambazo haziwezi kufanana hivyo mnakubalina kidogo na mnatofautiana sana,hivi unatarajia nini?
Basi ikawa kama ni ujiko ambao hata hivyo ulinisaidia kwa kipindi kifupi tu,kwani wakati huo 1999-2000 hadi nilipo maliza kidato cha nne 2001 nilikuwa tayari nimejikwaa kidogo lakini niliamini ipo siku yanaweza kujirudia masuala yale,ambayo nilidhani ni mema.Kwa kawaida vijana wengi hupenda sana ujiko hasa tukiwa mashuleni ambako tunajumuiya za wanafunzi wa aina mbalimbali hivyo kila mmoja anajitahidi kuonyesha umahiri wake wa masuala kadhaa.
Kwangu kuwa na msichana mwanzo lilikuwa jambo gumu sana lakini kwa huyu ilitokea kwa nia ya ujiko hapo shule,hata hivyo bado najiuliza mbona nina maumivu mimi kuliko yeye alivyofanya?Kifupi ni kwamba imefikia wakati binadamu kutazama upya mitazamo yetu juu ya masuala haya ya mapenzi,tunahutaji kuweka kanuni imara ili ukichanganua mlinganyo wa maisha yako ubaini kwamba kama ulikosea kanuni basi lazima majibu yatakugomea tu.
Sasa wakati narejea rejea kisa hiki ambacho kwa kweli kinanichanganya sana kukitatua kwasababu nhusika sinaye karibu,huwa nachanganya sana hoja zangu hilo mnisamehe sana.
Ni hivi msichana huyu tulijumuika pamoja enzi hizo tukiwa shule LUNDO SEKONDARI(kwa waliofika Mbamba Bay au Liuli wanaifahamu).Nilikuwa kama nimeona dunia yote yangu nikajiona bonge la mjanja huku nikiwa na ka umaarufu fulani kwanza nilikuwa mchezaji wa "volleyball" mkali na ambaye alifundisha wengi pale shule,usishangae ujiko huo.
Msichana huyu basi akawa hanijui wala kuniaona najichanganya na watu wengi isipo kuwa rafiki yangu mkubwa wakati huo Simon Haule na niliokuwa na urafiki wa maarifa sana kama Michael Mkate na Libaga Mapunda(wanisamehe kwa kuwataja) au nikiwa pale bweni nakula muda mzuri wa kusoma vitabu kama "kikosi cha kisasi" n.k.Huyu rafiki yagu wa kwanza alikuwa mtu wa "vidosho" sana hivyo hatukuweza kulingana katika falsafa na itikadi lakini wawili wa mwisho hapo juu nilikuwa nao bega kwa bega katika kusaka maarifa kwa njia za kikoloni.
Basi kijana nikawa na matokeo mema darasani na hapo ndipo huyu ninayemwandika leo akajitokeza kwangu kwa kudadisi hivi mimi ni nani na natokea wapi.Wengi walijua kijana nimetokea pale Mbinga mjini kumbe wapi kijana pale nilikuwa nakula muda mzuri wa mapumziko ya baada ya shule kufungwa.Naam... tukazoeana kidogo kama ujuavyo akinadada kwa mikogo,wala kijana sikuwa na mchecheto kwani nilikuwa najiamini utadhani Hitler(usiogope) yaani nilijiona gangwe kama Okonkwo,nilikuwa na kasumba za kutojiunga na makundi yasiyo na jipya wala mtazamo wowote wa maisha,nilijiona natafuta maarifa kwa nguvu za kibitozi tui lakini sikua na hata kauchembe ka huo unini.....
Ilikuwa kama mzaha tu kwa msichana kama huyu ambaye alichukuliwa na wanafunzi kuwa wa hadhi ya juu si uanajua tena vijana wa shule.Ikawa mchana ,ikawa siku basi maua tukayapanda wenyewe.Tukaendelea hivyo hadi pale kisanga ambacho amekuwahi kuniuliza kwanini nilifanya vile.Kisanga hicho kilitokea nikiwa katika kambi ya UMISETA yaani duu!haya ikawaje?kisanga kikaishia hapo(sitakisema) naona haya. Ni hivi nilishangaa mtoto kawa kama kavurugwa akili na jambo fulani ila roho ikawa inampwita aanzeje maana baada ya kambi hiyo kumalizika na wachezaji kuruhusiwa kurejea mashuleni kwetu ikawa kama kawaida kufika Mbinga toka Songea kijana nikaona ngoja nionane kwanza na washikadau wangu ili nikija likizo wajue kijana alikwisha kuwapatia jambo langu muhimu la likizo hiyo.
Lakini huko shule binti akawa anasubiri kijana nije,lakini si kama mwanzo bali ni kama kuunganisha UJAMAA na UNYANG'AU(ubepari),ilikuwaje? Niligundua siku moja hivi maana si unajua kwamba ukisoama vitabu vyenye akili unapata mwanya wa kuchanganua mambo? Nilipobaini jambo sikuhoji nilinyamaza tu huku kijana wangu wa kazi(rafiki)Godfrey Christopher akinipa habari nzima basi nikasema mimi ni ngangari nitalimaliza kijeuri!lakini wapi,.ikawa kama nachelewa tu kwani alitakiwa kunieleza kitambo lakini aliposuasua nami nikala jiwe tu kusubiri nini kitajiri ili kuokoa muda.
Lakini kumbuka kwamba yalioyojiri wakati ule tayari nilishatemwa kikosini na nilijaribu kujirejesha katika kiwango changu ikashindikana,tukabaki kupiga stori za hapa na pale na WATU wasijue kama hakuna tena ujiko kama wa kale,tukabaki kuwa marafiki kama ilivyoada kwa binadamu sote ni ndugu.ikawa mchana ,ikawa usiku mambo hayakubadilika nikakukabli matokeo kwa kauli kwamba ipo siku tutaonana na tutajiuliza sababu pia kwamba mimi ni mtu sahihi kwake kuliko wengi wanaomtazama kama chui mwenye uchu wa kula nyama.
2006 hiyo kijana nipo jiji la matapeli DAR naona na binti lakini hii ni baada ya kutoonana kule Mbeya na nyumbani mkoani hapa Ruvuma hususani kijiweni kwangu Mbinga mjini ambapo yeye ni makani yake tofauti na mimi toto la kinyasa la kuvua samaki wa kitoweo;tunajaribu kusahihisha kwanini sisi tulifarakana hatua ile?(kutemana)lakini jibu likawa nani alianza?tuhuma kibao mara kijana anayeandika hapa alikuwa ana kimada kwa siri.Jibu la mwisho kijana anayeandika hapa akasema msichana ndiye aliyeanza na hoja hii ikakubalika,tatizo ni kwamba tulidhani ni wakati wa kufanya kweli sasa kwasababu tumekuwa angalau umri wa kati kama 10+10+3= sijui nini huko! kwamba muda wa kuwa pamoja kwa umakini.eeeeeeeeeeeeeeehhhh wapi bwana yaani ni balaa tupu,nashusha aya.......
Siku moja nikapokea sauti ya kutisha toka katika simu kisha ujumbe wa simu ukaingia baada ya mazungumzo na kijana aliyenihoji kuwa mimi ni nani.Duu nikajua kwamba nimeingia anga mbaya kwa kuruhusu mtu aliyeimwaga enzi hizo eti sasa nione chungu kapata kivuno...........,.,,,.Nikaambiwa kwamba huyu ndio "waubani" wake hivyo nisitume ujumbe wala kubipu si mnajua za kibongo kwa kubipu.Lakini hii ilikuja baada ya kutoonana kwa miaka 3 kwani hata huo 2006 ulikuwa wa 4 nikaona iwe vyema ninyamaze....AAh hapana niandika ujumbe, kwani nilishabaini kuwa aliyelonga kwenye simu si kidume kweli ila nimefukuzwa kwa njia kupitia kidume mwenzangu tu kwa hofu kuwa mimi ni msema kweli kwa kumfanyia marekebisho kwani alikuwa na mwendo mgumu usiohatarisha,haya yote yanatokea baada ya hitilafu kubwa kati yetu lakini si hitilafu ya kuhatarisha bali ni itikadi za maisha kila mmoja anajiona yuko sawa zaidi ya mwingine,mitazamo iko kinyume nyume.
Nikaona mambo yanakwenada upogo sasa,nikatulia nikajihoji kwanini,nikasalimu amri nikaseama yote heri lakini nikachia ujumbe kama huu utambae kichwani mwake ..........."Praise of the Folly,shall forza companie".....daa sentensi kali sana hii na naipendamno na kuiamini na ikiwa andhani ni utoto mwanangu ameumia sana.Maana walijisifia kwamba wanapendana mno kumbe ni kiini macho...mara leo namba ninayopigiwa....mpigaji haongei...mara...niwekewe sauti ya zima moto mara..... lakini sijibu kitu.....yaani ni "dirty off you shoulder" ....ukurasa mwingine .....,,.,,..,,n.k
Hivi kwanini YASINTA umefanya hivyo?kwanini unachukulia maisha kama mbio za vijiti? maana mbio hizo ukichoka bora kujitoa kuliko kujifanya kinara huku uhai unatoweka.
bado kauli niliyoambiwa mwaka 2000 naikumbuka kwamba...."mwongoze mwanamke mkiwa barabarani.." yaani sikuelewa ila siku hizi nimebaini kumbe ni kujifanya unampenda sana msichana basi umkumbatie hadharani yaani popote...sijui kupigana mibusu......na nini...sijui barabarni...n.k .. hadharani nayo ni njema au vipi maana kijana sijui kitu waungwana,yaani siyajui hayo toto lililozoea kuvua samaki na kuogelea na watalii waliokuja ziwa nyasa enzi za mapadre wa kizungu(wa kikoloni) we aah acha tu.
Nilishasema kwamba ndugu yangu mimi ni mtu sahihi,lakini kazi bure wanapenda kuvinjari na maisha ya kwenye runinga za kimagharibi..lakini kijana sijui hayo si kwa ujinga bali msimamo,hoja n.k. Huyu binti ananifanya niwaze wasichana wote kama ni majeruhi wa maisha yaani hawana kile wanachoamini katika mahaba yao(samahani najua si wote).Yaani angejua sasa ninavyo watazama wasichana kwa jicho la pembeni nikiamini kuwa siku yoyote yatatokea kama ya WTC huko marekani,yaani nakimbia kama mbio za akina mzee Bayi.
Yaani naogopa kuelekeza mawazo haya na mtazamo wangu juu ya masuala haya tena basi bali ni kujibisha katika shughuli zangu ikiwemo kuandika porojo zangu katika anuani hii,bora kuliko kumtaka mtu ambaye haoni umuhimu wa kutakiwa na asiyemtaka.Hivi kwanini alifanya hivyo au wasichana wanapenda sana kubembelezwa? aaaaahhh hapa najua si hivyo ila nauliza tu.wala sijui kubembeleza ndio nini jamani...
Basi ndio hivyo nimeamua kuwa na maarifa mapya,mtazamo mpya,fikra mpya,mapinduzi mpya, sitaki kupoteza muda wa kuinua maisha yangu kama alivyotuasa 2PAC.Wasomaji niacheni nizungumze kama mwndawazimu maana huyu dada hajui kama mimi nilikuwa namhitaji sana na nadhani ipo siku atatambua kwamba aliyekuwa akimhitaji ni mimi,potelea mbali sasa nimefunga masikio nasaka fikra mpya kutoka sayari mpya na siyo dunia tena labda wasizaliwe na mwanzo wa HAWA na ADAMU.aaaaaaaaaaaaaaaaaaahhhhhhh...acheni nicheke...ooooooiiiiiih
Si mkwara bali akiona hapa aone kama sitanii kitu nimekuwa mwanaharakati wa mapinduzi ya kweli hakuna muda wa kuzubaa tena.
Pole kwa kunifuatlia sana lakini huyu binti naamini ninaweza kuonana naye muda wowote ila tatizo ni mitazano tu,yupo anajidai anakamua kitabu cha sheria za shahada huko.......na naamini kwamba ananiheshimu kama ninavyomheshimu kama wanadamu wengine.
kila la heri kwa maisha yake hayo....lakini kwanini alifanya hivyo?alidanganya kwamba aliyeongea nami katika simu ni waubani wake wakati naitambua sauti ile,hata hivyo mtu aliye karibu yake anashindwa kuniambia ukwEli kwa kuwa anajua sina muda wa kuujua UKWELI HUO TENA kwani nimeshaujua na sihitajiki kuujua zaidi bali.......
KWAHERI.......
Subscribe to:
Posts (Atom)

