September 01, 2007

Uwongo si Mzuri..

Kuna jamaa hapa kanichezea sana,yaani nilijikuta natamani kumeza samaki mbichi kabisaa,unajua ni samaki gani 'mbasa'.Usishangae kwani huwezi kula samaki mbichi mpaka achomwe au kupikwa?

Jamaa kaniahidi kuniletea kitabu fulani hapa lakini matokeo yake hajaonrkana kwa kinyume na muda tulioahidiana wa saa 4,yaani nimengojea hadi saa 5 kasoro hivi jamaa haonekani.Aaaa nikaona huu sasa ni ujuha ngoja niongee na watu hapa kidogo lakini sina hasira naye kabisaa moyo uko safiiii....lakini si vizuri kudanganya kama masikini wa siasa na dhiki za siasa au vipi
u kwa vile mimi napenda sana vitabu na anajua kwamba nachukia sana uwongo...ananifanyia kusudi.

Aaa ndio huyu sasa anakuja huku mimi naandika waraka huu,eti anasoma..jamani ananikaripia,kwani mikono yake.....haya leta kitabu we' mbuni mnyasa feki maana jamaa anajiita mnyasa kumbe ....

August 31, 2007

Barua Ya Sekunde Moja

Jana nilikuwa karibu naandika ujumbe kwa watu mbali mtandaoni,lakini nakuambia nilistajabu mtu ninayemwandikia alikuwa kakaa karibu na kompyuta yake bwana naye akaanza kujibu hapo hapo wakati mimi nilikuwa naamini naandika barua ili nijibiwe kama ilivvyo posta mara anuani,kulamba stempu,kushika wino,kununua karatasi n.k

Acha bwana Fred Macha akajibu hapo hapo,ee nikashangaa mzee wangu kumbe yupo nami muda huu toka London.yaani kaacha kulicharaza gita halafu anapiga gumzo hapa? Gumzo hilo si lile la kulonga kimahaba "chat" katika mtandao bali unaandika barua kama unamwandikia baba,mama,kaka,dada,binamu n.k huku ukikaa miezi sita au wiki kadhaa kusubiri majibu,lakini jana nikajibiwa kwa sekunde moja.Yaani ilikuwa saa moja na dakika tano usiku halafu kanifahamisha kwamba yeye pale London ni saa 11 jioni yaani walikuwa wajidai mitaani tu huku wabongo tunajificha ndani kuogopa wakora...kisha kuamka siku inayofuata kwenda kutafuta mkate.

acha kabisa barua za sekunde moja hizi

Haya Wananchi Kazi Kwenu

Ndiyo wananchi sasa kazi kwenu maana kila kukicha serikali yenu inataka kuwahudumia kwa njia bora.sasa ni zamu yenu kuwahudumi wakuu na mamwinyi ukijumlisha na mabwanyenye.

Tovuti ya wananchi ndiyo hiyo ipi hewani msipotoa maoni kazi kwenu,lakini kweli maoni haya yatamfika mkuu wenu,msihofu kila kitu anakijua sana tu.hakuna haja ya kushangaa,toeni hoja,dukuduku,ushauri,na kila kitu chema kwa nchi yenu kwa kuwahudumua wote eehh sasa ingieni katika tovuti hii

www.wananchi.go.tz

Da' Maria karibu

Kupiga gumzo mtandaoni ni raha sana,basi jana nikaanza kuandika ujumbe kwa dada Maria Mtawali..sijui yuko wapi siku hizi hasemi mahali alipo labda ananiogopa.Nikawa naandika ujumbe kadhaa kwa ajili yake...mara nikakuta ujumbe unaoniuliza 'nyasa' ni nini? halafu...'wewe ni mnyasa?' duuh! kufikia hapo nikaona sasa dadangu amenikuana sana anaponiuliza kuhusu nyasa.

Ndiyo..tunavua samaki aina tofauti,kwanza hata wengine hawajui hata nikisema samaki ndio nin..si hiyo misangara yenu ila mandongo,kambale,ngorokoro n.k au waulize wale wazungu kule Liuli wanafanya nini,kisha njoo makao makuu yangu hapa LUNDU niambie unataka samaki wa aina gani au unataka mihogo ya kutafuna ambayo huko ughaibuni wengine wanasikia tu hewani.

Lakini dada maria miye ni toto la kinyasa yaani usijaribu yaani nakupenda nyasa kwangu hapa,kwani nguvu za kukaa katika kompyuta wananipa wao.Jana nilikula sana samaki kutoka mtera halafu nikabeza hawana hata harara kwa mwenye njaa.
Da' maria mi ndio mwenyewe nipo nimetulia nakukaribisha.....njooooo...katika darasa la Ndesanjo hili tujidai mpaka basii

Upweke mmhh

Jamani wakati mwingine huwa najichekea peke yangu au nikimwona mtu ninaye mfahamu huu napenda sana utani matokeo yake naambiwa nina tatizo la kisaikolojia.Hivi unajua kwanini?. Mara nyingi nakuwa mpweke sana yaani napenda kuwa sehemu tulivu mno.

Huwa naongea peke yangu mara nyingi tu huku nikitoa nafasi kwa ubongo wangu kufanya kazi sawa sawa si unajua tena mambo ya kuvua samaki nyavu inapaswa kuwa salama muda wote..
Acha bwana yaani najiona bonge la mjanja nikiwa pekee halafu nikikutana na washkaji naambiwa oooo nina ugonjwa sijui nini huko...

Hivi unavyonitazma kweli unaweza kuamini eti nina unini sijui.. ...sawa lakini napanga mikakati ya kuikamata nchi yaani kuwa rais halafu Ndesanjo anakuwa waziri mkuu,kisha Fred Macha naye anakamata wizara ya utamaduni..ili acharaze vyema gitaa lake...aaa sijashau bwana Michuzi anakama wizara ya sheria ili asiibiwe tena wahuni toka Nigeria maana wataiba hata *****za ndani jamani si fujo hizo hebu lete fimbo jamaa kaandika neno la minyotanyota kibao hapa nani huyu alaa.

August 29, 2007

Furaha Ni Kitu Adimu

Wengi tunadhani furaha ni kumiliki magari,wanawake wazuri,wanaume wazuri,kazi nzuri,nguo nzuri n.k lakini hawataji hasa kwanini mtu ajisikie furaha.

Furaha si kitu cha kuuzwa ma kununuliwa kama peremende kamwe furaha hailazimishwi bali huja kama anayehiotaji yupo sawa na kweli anahitaji furaha.Furaha si kwenda kanisani kupayuka,kulia,kuogopa mungu atakufa hivyo,kuogopa vifo n.k lakini fauraha haiji kama hitaki kuwa na furaha yenyewe.

Tujiulize kwanini leo Bili Geti anaamua kusaidia watu wa hali chini ambao wanadai kuwa ni masikini wakati ana mapesa,magari,mke mzuri,kampuni za mitaji mikubwa n,k lakini ameamua kusaidia watu wengine.Baaada ya kujikombea feza hizo kwa faida yeye anaamua kutoa bure kwa wengine ingawa suluhisho la kuondokana na hali ngumu si kutoa feza na magari.

Amkeni acheni ujuha,furaha ni kitu ambacho kila mwanadamu anakitegemea kwa mwingine,huwezi kuwa na furaha bila wanadamu wengine,acha rushwa,ubinafsi wape nafasi wngine nao wakupe furaha ya maisha wala haihitaji kununua dawa za kupata furaha kama huko kwa akina joji kichaka wanavyofanya.Furaha ni kitu adimu sana hakiji kwa kutumia nguvu nyingi au mapesa.

Mtabaki Na Labda Hivyo Hivyo

Hivi mbona watu hatujui siku zetu zilivyo hapa duniani?mbona kila raia ana hamu za kijinga hivyo?.

Utakuta kiongozi anahutubia raia wake huku akijifanya anauchungu na hali zao ngumu kumbe anaomba apewe nafasi ampeleke kimada wake ughaibuni kwenda kuzubaa na kushangaa shangaa na kuzunguka kama tiara.halafu akirejea anakuta raia wake wanazidi kuteketea na hali ngumu ya maisha,mwishowe nabaki na labda mungu,labda mizuka na nini uji**** mwingi tu.

Kujali maisha ya wengine hakuhitaji gharama au kuwa tajiri na kumiliki kampuni kama mabwanyenye au mabepari uchwara.hakuhitaji kuwa na mapesa mengi ambayo haywezi kukufanya kama ulivyo.
hivi labda sijui,huenda...m.k hazitaisha bila kutumia muda wetu kupanga huruma na raha kwa wengine.

Acheni Dhihaka

Kama hasira ni mbaya basi bora ziendane na tukio halisi,na kamwe siwezi kuacha hasira za na uchungu moyoni kama TUPAC SHAKUR,BOB MARLEY,J.K NYERERE n.k kwani kama watu hawa walipigani kuondoa unyonge wetu,halafu sisi kwa kujifanya kuja tunakaribisha tena unyonge ambao wenzetu walipigani uondolewe.

Yaani hatuna jeuri kabisa,kila kukicha eti lazima kuongea kiingereza au kuheshimu lugha hiyo kwa kuwa ya kimataifa,hivi mataiafa gani?.Ninaposoma vitabu vilivyoandikwa kwa lugha ya kiswahili nafarijika na kujihoji kwamba hivi wanaojifanya wasomi leo mbona hata msamiati mmoja wa kiswahili hawajui?Ilikuwaje Biblia ikatafsiriwa kwa kiswahili na kueleweka namna ile?

Mbona kamusi yetu ina maneno mengi tu yanayoashoria kwamba tuko zama sahihi ikiwa tutaamua kutumia lugha yetu? kwani maneno mengi ya kiingereza mbona yanatokana na lugha ya ya kikabila iliyozungumzwa zamani ya kibritaini pale visiwani uingereza halafu leo tunasema ya kimataifa na kimawasiliano.Kwani kiswahili si lugha ya kimawasiliano,acheni dhihaka nyie ****** wana wa kizazi cha wajivuni mbona wazee wetu waliamini miaka hii ndiyo ya kuruhusu lugha yeu kwani wakati ule walibanwa nbavu na hao wanaofanana na rangi ya ngozi ya nguru****?

Hisia toka moyoni;wakati ndio huu.Daahhh! nilitamani kutwanga ngumi mtumbwi wa mvuvi mmoja juzi baada ya kujidai anayajua maneno ya akina blea.lakini nikaona hii mbaya nikatulia na ghadhabu zangu na kumwambia acha dhihaka ndugu yangu mbona Wachina wanaongea kikwao na wanafanikiwa?

Tunadharau kiswahili..

Niliposoma makala inayozungumzia kiswahili katika gazeti moja leo hii baada ya kuingia toka kijijini Lundu,nilikuta natamani kutwanga ngumi ukutani,nilahamanika ile mbaya kwani nikaona watu wote hapa wilayani Mbinga kama vimulimuli.Makala inazungumzia namna Watanzania tunakidharau na kuona kiswahili kama lugha isiyo ya kisomi,ya kishenzi,mbovu,haina maana n.k

Lakini ukitazama hao wanaojiita wasomi eti kwa kuwa wanajua maneno kadhaa ya lugha ya kikoloni ni majuha na watumwa namba moja kuliko wale wasiosoma hapa ulimwenguni.Kwani utawakuta wakiamini eti Kiingereza ni lugha ya kuwasiliana! heee sasa kiswahili ni lugha ya kufanya nini nyiwe watumwa?,Usomi gani hata matumizi ya lugha yenyewe yanwashinda halafu muwe wajivuni?

Wengine hata sarufi maumbo,miundo,na matamshi hawajui matokeo yake hujifanya eti wanashindwa kuongea vyema kiswahili au nini sijui huko, yaani ******** hamna adabu kabisa hivi mnafikiri usomi ni kuja kiingereza na kubetuanetua midomo kama joji kichaka? mlaani***tena mpotee kabisa.

Usomi gani wa kuwa mambumbumbu wa wa lugha yako ya asili,usomi gani huu kama si mauaji ya fikra.Ndio maana tunasema kwamba eti wasomi wa siku hizi hakuna kitu,hivi mnadhani ni nini kama si hiyo lugha yenu ya midabwada.Wengine eti hujifanya kuongea na kuchanganya maneno ya kiingereza na kiswahili.Hilo nasema mko*** kabisa,mtaendelea na utumwa huku wenzenu wakitamani lugha hii ingekuwa yao maana wanaiendeleza sana.

August 26, 2007

:Kushushwa hadhi maana yake nini?

Karibuni Nyasa: Kushushwa hadhi maana yake nini?

Haya wamekwenda kuagua Buzwagi.

Inawezekana kama mzaha lakini ndiyo ukweli wenyewe maana kila siku ni za magonjwa tu.
ziara imekuwa zogo,inafunika kile kinachozungumzwa na kilichosababisha jamaa kuondolewa kule kijiweni kanda ya kati.

Kuna matatizo kule hivyo inaonyesha bora kwenda kuagua ili angalu kuponya na kuzimisha moto wa wenyewe na kuwaonyesha meno 32 na kwa vyovyote wasahau kwa vijijengo vyao vya laki moja kama viota vyipwa baada ya kuondolewa kwenye makasri yao ya maana.
salamu zao haa nilipo ni mbali na mako yetu,kwasabau huku nyasa tumezoea kuvua samaki mfano ngorokoro,perege,mandongo,kambale,mbasa,manswena,ntaka n.k.
lakini tunashukuru tunashiba sijui hao wenzetu huko Buzwagi washiba hivyo vijumba vyao maana naona kila siku natumiwa taarifa huku kijijini kwangu na marafiki waliopo mjini eti jamaa wamejengewa viota ili wahame na mali itegulishwe uchumi. samahani huku kwetui tunakula hata mlenda,kisamvu,matembele lakini hatuna dhahabu sijui ingekuwaje;maana wanyasa ninavyowajua! wangewangiwa kama huko kwenye madini?