September 27, 2007
Chiwindi Mpakani!!
CHIWINDI-hiki ni kijiji kilichopo katika mpakani mpakani mwa Tanzania kama unaelekea Msumbiji kupitia mwambao wa ziwa nyasas.kijiji hiki kinapokea nakukaribisha wageni wa aina mbalimbali ambao wengine huwa katika taifit mbalimbali juu ya maeneo haya au nchi kwa ujumla.Ni kijiji kinachotegemea uvuvi,biashara ambayo si kubwa sana,kilimo ambacho ni nguzo za maisha ya raia wake.Eneo hili lina barabara ambayo huwasasidia wakazi wake kusafiri umbali mfupi kwani linamatatizo ya kijiografia tokana na milima na mawe yanayozunguka kijiji hicho lakini ni kijiji chenye utulivu naraia wake wanamahusiano mazuri na jirani zao Msumbiji,hujaribu kushirikiana kimichezo,kitamaduni nakiuchumi kwani wanakaribiana sana.Lugha inatumika ni kiswahili na kinyanja(kinyasa) ambacho huzungumzwa pia nchini Malawi amabayo ianapakanana kiji hiki kupitia ziwa nyasa.Wakaazi wake pia hufanya safari mara kwa mara kwenda Malawi kani ni muda wa saa 1 kwa boti.Hapa ni mpakani kabisa hivyo pana shughuli za hapana pale na pana walinzi na usalama ka pande zote mbili yani Msumbiji na Tanznia.wakaazi wake wanapendana sanalicha ya kuwa nchi tofauti na wanashirikiana.
Madhumuni
chiwindi
September 23, 2007
Nyasa Na Mazingira Yake
Ukanda huu kama nilivyosema awali kwamba una mengi ya kujivuni licha ya ziwa hilo.
Eneo hilo lina shughuli nyingi tu ikiwemo kilimo,ufugaji,uvuvi ambao ndiyo nguzo.
Sasa ukanda huu una mambo ya kujivunia sana kwani hakuana matatizo ya njaa kwa wakazi wake hivyo ni maeneo yenye adhi nzuri na maandhari yenye kuvutia kwa wageni na wenyeji
pia bila kujali asili.Taratibu tuitaingia katika uchambuzi wa vijiji na miji midogo ya eneo hilo ambalo nisehemu kubwa inayounda jimbo la uchaguzi la Mbinga magharibi na wakazi wake ni wanyasa ambao mchanganyiko wake wengine ni kutoka Malawi au wenye asili ya huko lakini
raia wa Tanzania,kwani ukiuatilia asili yao wengi wanaishi nchini Malawi au kuna uhusiano
kati ya wanyasa wa Tanzania na wale wa Malawi licha ya ukaribu wao.
Eneo hilo lina shughuli nyingi tu ikiwemo kilimo,ufugaji,uvuvi ambao ndiyo nguzo.
Sasa ukanda huu una mambo ya kujivunia sana kwani hakuana matatizo ya njaa kwa wakazi wake hivyo ni maeneo yenye adhi nzuri na maandhari yenye kuvutia kwa wageni na wenyeji
pia bila kujali asili.Taratibu tuitaingia katika uchambuzi wa vijiji na miji midogo ya eneo hilo ambalo nisehemu kubwa inayounda jimbo la uchaguzi la Mbinga magharibi na wakazi wake ni wanyasa ambao mchanganyiko wake wengine ni kutoka Malawi au wenye asili ya huko lakini
raia wa Tanzania,kwani ukiuatilia asili yao wengi wanaishi nchini Malawi au kuna uhusiano
kati ya wanyasa wa Tanzania na wale wa Malawi licha ya ukaribu wao.
Madhumuni
Nyasa
Subscribe to:
Posts (Atom)