December 26, 2007

NYASA;krisimasi,furaha,burudani na uhai wa wanyasa

Naam nilikuwa katika kijiji lundu kujionea burudani na furaha ya kusherehekea krisimasi ambayo bila shaka ni ni wakati wa wazazi,watoto,ndugu,jamaa na marafiki kujumuika katika simu hii ambayo hupatika mara moja kwa mwaka pale wakristo wanapokumbuka siku ya kuzaliwa Yesu krsito.Ni kawaida yangu kutulia katika siku za aina hii lakini nilishindwa kutulia ilibidi nijiulize nitaandika nini nikifika Mbinga asubuhi hii maana wenzenu mambo ya mtandao haya mapaka tusafiri kidogo ndipo tuandika katika blogu namna hii.Naam nimekuwa katika mzunguko mkali wa siku hiyo ya krisimasi ili kujionea burudani,furaha na uhai wa wanyasa katika maisha yao lakini nikaona sisi bina damu tuna kawaida ya kusahau matatizo siku kama hizi maana nikaona hata wale maadui wanakumbatiana kwa wema kuikumbuka siku ya mwokozi wao.Asubuhi hii ikawa balaa maana kuna jamaa alikwenda kuvua samaki hivyo nimemwahidi kwenda kupata japo kitoweo kumbe mwenzie naondoka zangu kusafisha macho mjini Mbinga angalu nione wamjini wanaburudika vipi hata siku kama ya leo.Nimekuta watu wamelewa,wanatapika hovyo,mara mafumanizi na uchafu kibao na nikaambiwa na mwenyeji wangu kuwa kuna mwanamke mmoja kafumaniwa na kijana wa kinyasa mtaa wa Flastoo.Hapo nikaguna huyu mnyasa yuko hai kweli? nikambiwa wanyasa wana mbio katika hatari maana jamaa kachia mbio kuokoa uhai wake....si unajua fumanizi za wenyemali.Sasa badala ya furaha,burudani na uhai wa wanyasa jamaa kasafiri hadi hapa mjini halafu anajiona wa leoleo na vihela mbuzi vyake akakoswakoswa na wenye uchu wa kutanya uhai wa wenzie na bahati yake kwa wanyasa kuwa mbio kali ni sifa moja ya uhai wako nyakati za hatari.Ndiyo wanyasa wa mbio za ajabu mithiri ya swali mbugani.Lakini baada ya kuandika hapa mjini katika blogu hii natarajia niende zangu kijiji maana jamaa akija nadhani ataghadhibika kwani nimeahidi kununua samaki wake ili apate pesa za kuburudika na furaha ya familia maana jana kalewa mipombe halafu kasahau familia lakini kaahidi leo ni burudani ya familia yote sasa watoto wako juu kwelikweli maana wanataka kuonyesha uwezo wao wa kuburudika. mapumziko mema,watu wote wa ughaibuni maana najiuliza hivi Ndesanjo anasoma habari za wanyasa kweli?vipi kaka Jeff,DaMija,Michuzi na kitoto pale London?sijui lakini polepole,KARIBUNI NYASA!

December 22, 2007

Likwilu,Kilosa,Mtipwili na mengineyo

Naam kamanilivosema inabidi kuangali kwa uchache baadhi ya maeneo nyeti ya ukanda waziwa nyasa lakini nimeona kilasehemu ipewe nafasi yake.Likwilu na Kilosa ni vijiji vinavyopakana au tunaweza kusema kwa Likwilu ni mtaa mkubwa ndani ya kijiji cha Kilosa kwani umekuwa maarufu katika maeneo hayo huku ukikiacha nyuma kijiji halisi cha Kilosa.Maeno haya kama ilivyo mengine yanatawaliwa na mashamaba makubwa ya kilimocha mpunga ambacho ndiyo uti wamgongo wa maeneo hayo.Hata hivyo kijiji cha kilosa kinapakana kwa kiasi kikubwa na mji mdogo wa Mbamba Bay ambako ndiyo kama makazi makuu ya watuwa maeneo hayo.Shughuli kubwa ni kilimo,uvuvi,biashara na maeneo ya historia.Kilosa ni mahali ambapo miaka ya kale ilikuwa kituo kikuucha kufundishia vijana JANDO na UNYAGO ambapo hadi leo kuna majengo na maeneo yaliyowazi ambayo yalikuwa yakifanyika shughuli hiyo.Watu wengi wamekuja kujionea historia hiyoya mababu wa kale katika kijiji cha kilosa na vitongoji vyake kwani pamekuwa mahali muhimu katika kazi ya kumbukumbu za watu wa kale.Eneo kubwa la kijiji hiki ni tambarare hali inyowafanya watu wake kuishi kwa amani bila kuwapo na hofu ya wanyama wa porini ambaoni hatari wapendao kuishi karibu na milimani.Usafiri hupatikana kwa uhakika.Pia watu wa maeneo haya huwa na mawasiliano makubwa na watu wa nchini MALAWI kama nilivyoainisha mwanzo.Mawasiliano ya karibu yapo katika miji ya NKATA BAY,MZUZU,LIKOMA NSISI na mengineyo ambayo hufikiwa na wakazi hawa.