February 07, 2008
Wanyasa kwa Samaki huwatoi kabisa,.. Hata wakiwa Ughaibuni..
Nilijikuta najiuliza hivi hawa wanyasa bila samaki ingekuwaje?Basi ni hivi nimepata waraka kutoka Ughaibuni,yaani dadangu huyu huko Ughaibuni anakwambia anakumbuka Magege yakiwekwa chumvi na pilipili pembeni we acha kabisa..Lakini usishangae nimepataje hii habari kwani utajua kuwa nipo hapa nyasa.Jibu ni ndiyo lakini nimeibukia hapa Mbinga hapa kama kawaida kudandia maisha.Dada anakumbuka samaki wa ziwa nyasa yaani njozi zote mambo ya nyumbani.Wanyasa, hebu soma sehemu ya ujumbe huu "Nimevutiwa na Blogu yako,mimi mnyasa yaani nakumbuka nilipokuja mwaka jana mwezi novemba nilipewa magege na chumvi kisha na pilipili yaani acha nijichane we acha tu nyumbani bwana".Mtoto wa kinyasa utamjua tu si unaona alivyochambua aina ya samaki hao? yani anajua viungo vyake na bila shaka liapewa samaki wa kuchomwa.Ukitaka kujua yuko wapi hebu peruzu jiografia nchi ya Sweden ilipo ndipo utajua ninachokisema.Dada yupo ughaibuni lakini hajasahau nyumbani {Tanzania}anakuja kutembelea,Je wengine mpo?Lakini ndugu yangu Ndesanjo anatembelea sana Jeff na wenzake.Mwenzetu anakumbuka samaki lakini amesahau dagaa,kambale,ntaka,mandongo,mbasa,ngogo n.k ndiyo nyasa hiyo watu wanaselebuka kwa raha kama dada yetu anavyoselebuka toka ughaibuni na samaki wa nyasa. Wanyasa kwa samaki huwatoi kabisa....yaani mpaka ughaibuni?
Madhumuni
habari,
kumbukumbu,
lundo
February 06, 2008
Fumbo katika Maisha kutoka Nyasa...
Jua limekuwa likitoka na kutua kila siku ya wiki iliyokwisha na litafanya hivyo hivyo katika wiki inayofuata.Mambo yataendelea hivyo bila kujali jinsi ninavyofanya au hata jinsi ninavyokuwa,Muda unapita na sote tunaona,wavivu kwa wachapakazi,wasiojali kwa wenye nidhamu hali kadhalika.Tunasimama katika mwanzo wa wiki hii,muda ambapo wiki mbili zinapokutana zinaweza kuleta harufu ya uchungu kwa baadhi yetu.
Uchungu wa kumbukumbu ya kushindwa kwa nyakati zilizopita,lakini pia inakuja na alama ya furaha kwetu sote kwa vile ni muda wa tumaini jipya linalofungulia mlango wa mafanikio mapya...Huu ni muda wa mafaniko mapya.
HEBU SASA TAFAKARI....Wiki iliyopita imepita,Hivi ilikuwa na maana gani kwangu?Inapokuja ilinikutaje?Na sasa imeniachaje?Na hapa inaanza wiki mpya nyingine.Je italeta nini au itaniletea nini?Hivi nitajisikiaje kadiri saa zake zitakapokuwa zinapita siku?Hayo yote ni fumbo kwangu kwa sasa....Hivi kila siku itakuwa na rangi gani?Na itaweka sura gani mbele yangu,kadiri nikitazama mshale wa saa ukisonga,hilo ni fumbo kwangu.
Uchungu wa kumbukumbu ya kushindwa kwa nyakati zilizopita,lakini pia inakuja na alama ya furaha kwetu sote kwa vile ni muda wa tumaini jipya linalofungulia mlango wa mafanikio mapya...Huu ni muda wa mafaniko mapya.
HEBU SASA TAFAKARI....Wiki iliyopita imepita,Hivi ilikuwa na maana gani kwangu?Inapokuja ilinikutaje?Na sasa imeniachaje?Na hapa inaanza wiki mpya nyingine.Je italeta nini au itaniletea nini?Hivi nitajisikiaje kadiri saa zake zitakapokuwa zinapita siku?Hayo yote ni fumbo kwangu kwa sasa....Hivi kila siku itakuwa na rangi gani?Na itaweka sura gani mbele yangu,kadiri nikitazama mshale wa saa ukisonga,hilo ni fumbo kwangu.
Madhumuni
amani na upendo,
falsafa,
Nyasa
Subscribe to:
Posts (Atom)