February 24, 2008
SIMAMISHA.KILA KITU SOMA FALSAFA HII
"Elimu siyo shahada wala cheti,ni uwezo wa kuchambua,kufikiri kwa njia pana,kuwa mbunifu,kuuliza maswali,kuwa jasiri,kujiamini,kujua jinsi ya kujifunza zaidi,kupanga mambo vizuri,kupima,kuhoji,kuweza,kutatua matatizo ambayo hujawahi kukabiliana nayo".Vipi ndugu yangu Dada JANETI unaonaje hayo na ndugu yangu Dada SUZI pale chuo kikuu cha Mwalimu Nyerere unaonaje hii.Simamisha kila kitu kwani usiposoma basi unafukuzwa katika ulimwengu huu au kusoma blogu hii{natania}.kazi kwenu wanazuoni hasa Ndesanjo
February 23, 2008
Haa!!Kumbe Watawala wetu "VAYIVA?"
Jamani tusishangaane hapa,mbona hii hatari kwa wanyasa sisi?Yaani hawa viuongozi wetu "VAYIVA"? haya maajabu wala hawaoni noma!.Neno "VAYIVA" lina maana "WANAIBA",nimelitumia hili kustaajabishwa na hali ya majambazi wa wa nchi yetu ambao tumewapa mamlaka ya kutuongoza.Wezi wakubwa hawa na kikundi chao na wizi yaani "VAYIVA" hawana hata aibu halafu wanalilia kusikilizwa mbona makubwa.Huku nyasa wala hatuna habari lakini eti nimefika hapa Mbinga ndiyo napewa kale haotuba ka mnyakyusa aliyesoma kale karipoti kanakowataja wale wezi wetu.Yaani "VAYIVA"?..
February 21, 2008
LUNDU na LUNDO ni vijiji tofauti
Lundu ni kijiji kilichopo ukanda wa nyasa katika kata ya Mbaha,na kwa urahisi unaweza kufika kijiji hiki kwa kupitia Lituhi ama toka Mbinga kwa kupitia Ngumbo na maeneo yanayoweza kukurahisishia usafiri hususani wa meli kwa kupitia Mbamba bay au Itungi-kyela na kushuka bandari ya LUNDU.Ni kijiji ambacho Mimi nimetokea na kuishia mpaka sasa.LUNDO ni kijiji kilichopo kilometa chache sana toka mji wa Mbamba bay au kutoka mji wa Liuli.Ni kijiji ambacho kina sekondari na kumbukumbu ya kutunza wakimbizi wa Msumbiji kabla ya kurejeshwa mwaka 1995 baada ya vita vya wenyewe kwa wenyewe kwisha ambavyo RENAMO walipigana na wenzao wa FRELIMO.Ingawa vijiji hivi wilaya ya Mbinga lakini vinatofautiana na kwa herufi za mwisho tu,na Lundu ni kijiji kilichopo na uhusiano na vijiji vya mbali kidogo vya Manda.Sifa na tofauti yake ni kwamba Lundu ni bandari ndogo katika shughuli za usafiri katika ziwa nyasa na Lundo ni kumbukumbu ya wakimbizi,sekondari na mashamba makubwa ya kilomo cha mpunga na hata Rais Jakaya analijua hilo.
Subscribe to:
Posts (Atom)