June 09, 2008

Hapa Kazi tu Hakuna Kuremba

Nakumbuka niliweka picha ya aina hii hapa bloguni.Lakini naona huu ni mwendelezo wa Wanyasa katika shughuli za kuinua uchumi wetu.Sifa ya kwanza ya wanyasa ni kazi,huwezi kuolewa kama mwanamke hujui kazi,mwanaume anakamilika kwa kuonyesha uwezo wa kufanya kazi.Wamo au unasemaje?

June 08, 2008

Hatujashindwa Tunasonga Mbele kama Hivi...

Ni kweli Timu yetu ya Taifa imefungwa jana na Timu ya Cape Verde bao moja, lakini haimaanishi kwamba tumeshindwa,tutashangilia na kujionea fahari ya timu yetu yaTaifa 'TAIFASTARS' kama hivi,tena kwa moyo mmoja,upendo mmoja,amani moja na juhudi Moja wala siyo The Philosophy Of loser.Tunaimanai na Maximo Wetu tuna imani na kila mchezaji kwani hao ndiyo mtaji wetu wa kuelekea kuwa na kina Zidane wetu,saa zaja,wakati waja twende pamoja jumamosi tukawashangilie kaka zetu vijana wenzetu dhidi ya kina Eto'o wa Kameruni.....Twende pamojaaaa iwe kwa upendooooo .....marafiki zaidiiiiiii..

Janeti na Hamu ya Njika kusoma Blogu

Kuna jamaa hapa ananitazmasana sijui anashangaa nini.Labda tokana na kasi yangu ya kundika hapa bloguni.Lakini namfahamu sana huyu jamaa unajua jina lake nani?nimemkumbuka umeona jina la mtu mwenye hamu ya kublogu hapo juu?Ndiye huyo anaitwa Njika Clara ni ndugu yangu,basi leo nimemnogesha kublogu nakwambia amebaki kutola mate tu jinsi anavyonogea mmm halafu ananiudhi amshika shavu sijui anamanaa gani.Najua hapa akitoka hapa nyasa anahamu ya kwenda kumtembelea shangazi yake mtaa fulani najua anafuata samaki tu si unajua wanyasa kitoweo chao.uache hilo,kuna mwingine tazama jina lake mwanzo "Janeti" basi jana kasoma blogu ya nyasa hii mpaka akakasirika kisa wivu eti wanyasa wanajidai na blogu yao.Haa nikammwambia mbona nawe mnyasa?akaniambia haijalishi ila wanyasa tunaringia kublogu.Lakini akamaliza kwamba hata yeye Blogu hii inamhusu shauri ye mnyasa.Basi huyu Njika anasoma blogu hii naona mpaka njaa inamuuma sijui hajala..ebu mtazama huyo hapo pembeni anakunja ndita sababu gani?.Mmmmm timu yetu ya taifaimefungwa na CapeVerde bao moja jana mmmm inauma sana

June 06, 2008

Wanyasa Tumuombe mungu Tushinde

Huyu ndiye Mrisho Ngasa (mwenye jezi ya bluu)ambaye tutamkosa katika mechi ya Jumamosi hii tarehe7/6/2008 nchini Cape Verde katika mechi ya kuwania kufuzu kwa kombe la dunia.Tutamkosa sana kwani mechi iliyopita hakuacheza baadaya kuumia nyonga mazoezini.ni mchezaji mahiri na mwenye msaada mkubwa kwa timu licha ya umri mdogo alionao.Tuloge na kuwanga kichawi kinyasanyasa

Timu Ya Taifa Imeondoka Leo

Timu ya taifa imeondoka leo kwenda nchini Cape Verde kwa mechi ya kuwania kufuzu kwa kombe la dunia.Hapa ni sehemu ya mashabiki wakishangilia timu ya taifa katika mechi dhidi ya Malawi iliyofanika hivi karibuni

June 05, 2008

Lizombe Limeumana hapa utasema nini

Usistaajabu kwani nimeondoka kidogo nyasa na kuingia mjini hapa na kukutana na picha hii muhimu sana kwa watu wa Ruvuma na wanyasa wote.Sina mengi ila tumshukuru kaka Richard Mwakienda kwa picha hii

June 04, 2008

Mwenye Mwanya aje,Washashi wanamtaka

kama una mwanya njoo nyasa utakutana na washashi pale Matema Beach nje kidogo ya bandari ya Itungi.N wengine ninawajua...unataka nikutajie?Sitaji mapaka unipe kwanza rushwa si unajua siku hizi rushwa ni kama kulamba asali,utamu ukizidi sana....natania bwana washashi wapo kibwena

Wanacheza,wanaselebuka na kuvinjari

sina maneno hapo,umenuna?kazi kwako ukiwa unakasirika mara nyingi utazeeka lakini ukicheka sana picha itapotea...polepole basi karibu nyasa hata kimyakimya

Mshashi Anavinjari Nyasa

Inaelekea huamini kama nyasa Washashi wanakuja kuselebuka..Bisha na hii.Halafu kuna jamaa anapenda sana kupingapinga mambo sasa nampa ngumi ya tumbo,sikio na mbavuni aaah samahani nilisahau bado sijapona ile ngumi ya ukutani ya yule jamaa.Hebu mwangalie Bibie huyo,anakukuna sana?eeeeh usije ukatangaza ndoa..wala sihusiki,lakini ananiambia anataka mvulana mwenye mwanya,je unao?

Ghorofa hilo! Wivu wa nini,Unacheka una Mwanya?

hapo sina hata maelezo ila wanyasa wanajua umuhimu wa kupumzika ndiyo maana wakajenga ghorofa hilo limegharimu hela nyingi sanajumlisha na za wale wezi wa wa benki kuu na yule Rais mwizi aliyemaliza muda wake mwaka 2005!unamjua?aakaa mie simjui nasikia alikuwa kibaka sana.unacheka,unaringa una mwanya....???

Unaonaje hapo?

Boti siyo mpaka uende ughaibuni,hata kwetu zipo waulize Litumbandyosi watakwambia,alikini usiniulize mimi mji huu uko wapi.Hebu tazama paleeeeeeee kuna dada mmoja hivi anapajua yule pale mtaa wa ruhuwiko bloguni bonyeza atakujibu

Wamo,Siyo Samaki pekee

kama unafikiri wanyasa wanachokiweza ni kuvua samaki na kujua majiraya kutega nyavy zao basi hujakosea ila hujui nini kinachoendelea hapo.Tazama wanaume wakiwa mzigoni wamekaza viuno,meno,miguu mpaka ngozi hakuna masihara hapo utaumia.kwanza inabidi uwe umeshiba sahani kama tano za ugali wa muhogo ikiwa wewe ni mgeni,lakini wenyewe ni nguvu za asili wale hawajui kwendaklabu za mazoezi kama huko mijini kwenu wanaogopa kansa shauri ya kutu za vyuma.

MV Songea inaingia Moja ya Vituo vyake Nyasa

Huna haja ya kuhofu,utamu wa nyasa ndiyo huuuuuuu.Ona watu wanangojea usafiri wao waupendao.

Tazama Uzuri wa Nyasa Yetu, Mazingira yetu

Nilipoandika kwamba mazingira safi,kama mlidhani nacheza basi mmenoa.Nyasa ndiyo jioni hapo uzuri unajionyesha wenyewe.Kwa mara ya kwanza nilipoitazama picha hii nikajiuliza swali moja.Kwanini yule rafiki yangu Christine wa Bavaria alilia na kugomea kuondoka Lundu pale ufukweni?Lakini nilipata swali la pili,kwanini wazazi wake waliamua kuwapo pale kwa masaa matano?,Sasa majibu nayapata kwamba ile kauli ya rafiki yangu yule kwamba "hapa naona nimependa upendo wangu wote,natamani ningelikuwapo kila siku,hakuna baridi kama kwetu,joto siyo kali ni la wastani haliumizi.Mbona hamchangamkii hii hali?lakini kifupi ni eneo zuri,nakuahidi Markus nitafika peke yangu mara nyingine bila hawa wazazi ambao wananilinda kama mtuhumiwa".Sikuwa na majibu ya haraka,na ingawa hajafika tangu mwaka 2003 lakini nimeamua kweka mtandaoni utamu wa nyasa kama huu,kwa yeyote ahayehusika karibuni nyasa

June 03, 2008

Washashi Nao Wamegota Nyasa

Naona nisiandike mengi,kwani nianchofanya ni kutoa ushuhuda wa "Karibuni Nyasa' ona Washashi nao wamegota.Washashi ni wazungu si unajua lugha za maeneo ya kizungu kwa vijana.Hatushangai tunajiunga nao tu...

Hawa Nao Wamo ......karibuni Nyasa

hapa ni Matema beach pembeni ya mji wa Kyela.Kuna ufukwe mzuri sana yaani ukanda wa ziwa hili ni utamu sana,Huyu Mshashi naye yumo katika kujiburudisha.Kairibuni nyasaaaaaa

Kitoweo.....Habari ndiyo hiyoooooooooo

Nashindwa hata kuongeza maneno mengi,jamani nyasa ni zaidi ya mnavyofikiri,Hivi niseme nini ili watu wapete kunielewa na nifanye nini ili niweze kuinua maisha ya nyasa...njoooooni muone....huyu samaki maarufu kwa jina Lingova ila wakiwa mengi tunasema Mangova.Aina ya Samaki hawa hupatikana zaidi nyakati za masika kwani ndiyo uzao wao hushamiri na kuenea zaidi.Picha hii kwa hisani ya rafiki zangu wapo pale Monkey Bay Malawi walinikuna sana waliponitumia nami naiweka hapa

Yule Mapunda Mpishi wa Kwenye Meli

Huyu ni mpishi wa shibe zetu ndani ya Mv Songea analonga na Mshashi.Yaani Mshashi hapo kagota hana mikogo shauri mambo ya nyasa siyo mchezo,Hebu waone wanavyoringa ndani ya Mv Songea hawana hata hofu juu ya Meli.Ziwa nyasa usafiri wa kutosha kama huu watu wa aina mbalimbali toka ughaibuni wanafurahia nyasa kazi kwako...mmmh usije najisifia kwa Washashi yaani wanyasa tuna ukarimu na msimamo hapo mshashi lazima adumishe nidhamu hakuna kuleta zake maana wanyasa kwa ngumi huwatoi si unajua kazi zao za uvuvi na kina dada mahiri na wakakamavu

Niambie Mnyasa Mwenzangu Maana Hawaamini

Tazama kwa umakini halafu jiulize wapi hapo....jibu ni Nyasa yetu ndugu

HataUsiku Kwa Mnyasa ni Uvuvi Tu

Watu hawachoki,samaki ni watamu hakika jionee mwenyewe wanaume wa kinyasa kazini.

Na Usafiri ndiyo Huo........ karibuni Nyasa

Hii ni Mv Songea ni meli ya kuaminika sana wala usihofu kama hayo magaro yenu ambayo ajali ni kama amri za usafiri wenyewe.Hii ni meli kubwa katika ziwa nyasa upande wa Tanzania.Na ile ndogo inaitwa Mv Iringa.Hapo ipo kazini na bila shaka kina Mzee Bukuru wapo ndani.Imenikuana sana Nyasa,yaani hii ni ari ya zamani,kasi ya zamani na nguvu za zamani...au unasemaje dadangu hapo ruhuwiko ya ughaibuni

Mnyasa Nimetua Chinula Wageni Mnasemaje hapo

Naam ndiyo nyasa yetu hiyo.Hapa ni barabara ambayo inakwenda moja kwa moja mpaka mji wa Mbamba Bay ambao ni mji mashuhuri sana katika ukanda wa nyasa una bandari nzuri sana,ingawaje sijaandika kuhusu sifa zake lakini polepole tutafika tu.Hapa ni maeneo ya kijiji cha Chinula pembeni ya mji wa Mbamba Bay.Angali nyumba zetu wala sina hamu na maisha yenu huko mijini.Usicheke basi kwani hatuna uhai?