June 15, 2008

Rais Anapo Blogu,Wewe Unangoja Nini?

Mwanzo sikuamamini kabisa kwani niliambiwa na rafiki yangu kwamba kuna myasa mmoja palejirani yetu naye anablogu yake.Nikauliza huyuhuyu Rais Bingu wa Mutharika tunayemfahamu?Basi nikamtumia swali hilo rafiki yangu yule Chikoko Cryton wa Malawi pale nikamwuliza hilo...akanitumia anauani hii..

http//;www.Bingu-Mutharika-nts.blogspot.com

June 14, 2008

Maximo AKimwelekeza Jambo Shabani Nditi

Wacheaji wote wa taifa stars nawapenda sana lakini aina ya uchezaji wa Shabani Nditi unanikuna sana yaani najihisi kama nipo katikati nakula ugali wa muhogo na samaki pembeni halafu kuna mtu ananisumbua lakini kwa kunifurahisha...yani we acha hebu mwangalie anavyomsikiliza kocha wa timu ya Taifa yetu Marcio Maximo yaani rahaaaaaaa nicheke nina mwanya?

Tulimwomba Mungu Atulinde kama Hivi

Hivi wachezaji wetu walivyomwomba mungu awalinde shauri ya kuwakilisha taifa dhidi ya kameruni leo jumamosi

Twende Pamoja!!! Hivi ndivyo Walivyoshangilia Leo Dhidi ya Kameruni

Pamoja na uwezo wetu mdogo wa soka lakini tumewaonyesha Kameruni tunajua maana ya soka ....kama hivi kwa umoja wetu

Toka Nyasa Mpaka Ughaibuni

Ni uzuri wa nyasa.Ebu tazama kizazi cha nyasa hiki kutoka ughaibuni.Hapo toka kushoto Philo,dada Yasinta{yule wa blogu ya Ruhuwiko},Eric na Camilla ee bwana wamependeza au?hata kama hutaki hii ndiyo nyasa ucheke una mwanya?njoo nyasa jionee

June 13, 2008

Ile Nafasi Ya Kazi Imepata Mwenyewe..

Unakumbuka lile tangazo la nafasi ya kazi hapa nyasa?Lisome.Ingawa sikupata ruhusa ya kumtangaza lakini huu ndiyo ukweli kwamba ile kazi imempata mwenye ujuzi wa kutosha kwani vielelezo alivyonavyo hakukuwa na haja ya kungojea wengine.Lakini pamoja na wale wasiochaguliwa katika nafasi hiyo tunaomba wasisite kuomba tena pindi watakapoona tangazo lingine la kazi kwani tunahitaji wafanyakazi wengi.Kwani nafasi hii ni ya juu zaidi na mshindi wetu anavigezo na utaalamu wa hali juu hivyo jamani...pigeni makofi tafadhali....eeh makofi tafadhali....aaahaa samahani siyo kutwangana makofi bali ni kushangilia kwa pongezi kwa mshindi wetu.Jina lake ni......naomba uje hapa mbele ujitambulishe mwenyewe......makofi tafadhali.......makofi....makofi....makofi tafadhali....