Hivi mnajua utamu wa dagaa wa ziwa nyasa?Hamjawahi kula?Mnagoja nini?Sijui niseme nini,kama mashtaka nipo tayari kuzikwa hai kutetea nyasa.Nilikuwa najiuliza hawa jamaa{baba zangu} niwakaribishe vipi,nilikuwa nahoji kwanini Mwalimu wangu wa blogu hajanisapoti toka nimwambie nimeanza kublogu?Nikajiuliza mbona siku hizi hajibu hata waraka pepe wangu?Lakini alisema mambo mengi huwa anazidiwa nitamsamehe.Lakini sijawahi kumwambia mzee wangu Fred kama ninablogu yangu,halafu juni 12 mwaka huu pale kwa Weshi Lema TPH nimenunua kitabu chake kile kinaitwaje?...Ebu dada Yasinta nikumbushe hapo Sweden hujapata?aaaah kinaitwa MPE MANENO YAKE.Kuna visa vitamu sana kwenye hiki kitabu.Sasa nikajiuliza nifanye nini mimi mvuvi wakati kila siku nabanwa na ratiba za kuvua dagaa,mandongo,kambale,mbelele,vituwi,ngorokoro,pelege n.k nitaweza kuwasiliana na wazee wangu hawa?Mmmh kwanza yule mzee Fred siku hizi amebadilisha anuani yake sijui kwanini au wanamghasi wale majambazi wa mtandaoni?Ndesanjo naye kila siku warsha,makongamano, juzi pale nimemwona kwenye ile dokumentari nilipoenda pale Mbinga mjini{mwenzenu kublogu mpaka nifike mbinga}.Sasa nitamwambia nini au nilalamike kama wale wezi wa richmondi na yule mzee mamvi anayejidai kulilia 'natural justice' samahni nilitajiwa hilo neno hata sijui sheria mimi.Basi ni hivi karibuni nyasa wazee wangu Ndesanjo Macha na Fred Macha mle dagaa kama hawa...tunawaandalia ugali wa muhogo....mtamu sana...
June 26, 2008
Ndesanjo Macha na Fred Macha Karibuni Nyasa
Hivi mnajua utamu wa dagaa wa ziwa nyasa?Hamjawahi kula?Mnagoja nini?Sijui niseme nini,kama mashtaka nipo tayari kuzikwa hai kutetea nyasa.Nilikuwa najiuliza hawa jamaa{baba zangu} niwakaribishe vipi,nilikuwa nahoji kwanini Mwalimu wangu wa blogu hajanisapoti toka nimwambie nimeanza kublogu?Nikajiuliza mbona siku hizi hajibu hata waraka pepe wangu?Lakini alisema mambo mengi huwa anazidiwa nitamsamehe.Lakini sijawahi kumwambia mzee wangu Fred kama ninablogu yangu,halafu juni 12 mwaka huu pale kwa Weshi Lema TPH nimenunua kitabu chake kile kinaitwaje?...Ebu dada Yasinta nikumbushe hapo Sweden hujapata?aaaah kinaitwa MPE MANENO YAKE.Kuna visa vitamu sana kwenye hiki kitabu.Sasa nikajiuliza nifanye nini mimi mvuvi wakati kila siku nabanwa na ratiba za kuvua dagaa,mandongo,kambale,mbelele,vituwi,ngorokoro,pelege n.k nitaweza kuwasiliana na wazee wangu hawa?Mmmh kwanza yule mzee Fred siku hizi amebadilisha anuani yake sijui kwanini au wanamghasi wale majambazi wa mtandaoni?Ndesanjo naye kila siku warsha,makongamano, juzi pale nimemwona kwenye ile dokumentari nilipoenda pale Mbinga mjini{mwenzenu kublogu mpaka nifike mbinga}.Sasa nitamwambia nini au nilalamike kama wale wezi wa richmondi na yule mzee mamvi anayejidai kulilia 'natural justice' samahni nilitajiwa hilo neno hata sijui sheria mimi.Basi ni hivi karibuni nyasa wazee wangu Ndesanjo Macha na Fred Macha mle dagaa kama hawa...tunawaandalia ugali wa muhogo....mtamu sana...
Madhumuni
amani na upendo,
siasa
June 22, 2008
Eti Huo Ni Unyanyasaji Kwa Wanawake...?
Mimi sijui ndiyo maana nimeuliza wanazuoni mnisadie kwani hapa nyasa naona ni hali ya kawaida mwanamke kubeba mzigo wa kuni kama huu.Pengine wenzetu mnaweza kujua nini maana ya unyanyasaji kwani kwetu nyasa tunasikia tu kitu kama hicho lakini hatukijui tunaomba kufunzwa.Huyu mama kabeba kuni{HANJU}kwa ajili ya shughuli za nyumbani n.k Je huo ni unyanyasaji kwa wanawake?mjadala....
Madhumuni
liuli,
mila na desturi,
Nyasa
Unakumbuka Pale Liuli....Pomonda?
Ndiyo hapo sasa.Hapa ni Liuli katika ghuba yake ile pale bandarini halafu ukiangalia kwa mbele kuna mawe.Pale ni mahala maarufu sana panaitwa POMONDA,pale ni mahali ambapo kuna saini ya David Livingstone enzi za ukoloni.Tazama vizuri kuna kama vivuli hivi....hayo ni mawe ndugu.kumbukumbu za wakoloni na mambo yao.
Madhumuni
kumbukumbu,
liuli,
Nyasa
Uhondo Wa Kambale Huo Hapo
Madhumuni
mila na desturi,
Nyasa
June 20, 2008
Afya Njema Nyasa
Nakumbuka kuna wakati jamaa mmoja aliwahi kunieleza kwamba mwili haujengwi kwa matofali,sikumwelewa shauri nilikuwa sipendi tabia yake ya kula vitu vingi bila ustaarabu.Basi nilipokutana na akina mama hawa nikasema......kama siyo kuishi nyasa nitaishi wapi?Wakacheka na kusema kama ninataka ndizi niseme.... Nikashangaa kwani nilikuwa nasifia nyasa wao wanasema nichukue ndizi.Mwingine akaongeza kwa kauli ileile ya yule jamaa kuwa mwili haujengwi kwa matofali.Nikaelewa,kisha nikapewa mkungu wa mmoja.Nikasema AFYA NJEMA NYASA.tukaagana nikiwa tayari nimewapiga picha hii.Imekukuna sana?Yaani mimi hunitoi hapo.... haya tuanze kushindana kula hizo ndizi..
Madhumuni
falsafa,
familia,
mila na desturi
Asubuhi Njema Na Kujipatia Kitoweo
Tunachangamka kama hivyo ili kujipatia kitoweo kwani samaki ndiyo nguzo yetu kuu.Njoo usikubali kuhadithiwa
Madhumuni
Hisia za moyo,
zana
Kuipenda Kazi Ndiyo Msingi Wa Maendeleo
Sema unaloweza lakini kwetu nyasa hapa hakuna swala la kulalamika kwamba hakuna ajira kama hao watu wa mjini.Nani atakufundisha kupenda kazi yako kama huijali na kuiheshimu.Mwangalie anavyotoa msuli wa kujituma katika kazi.Hii picha imenikuna sana,nimetabasamu sana wakati naweka kwani kuna jamaa hapa anachungulia ninavyoandika na kuiweka anashindwa kuniuliza.Lakini akiuliza tu nitamwambia amesahau kama yupo nyasa nini?Niseme nini jamani......
Mama Kabeba Kitoweo.... Nyasa
Ebu angalia tabasamu lake halafu niambie nimwambie akutayarishie nini.Wala usihofu kila kitu kipo sawa.Karibuni nyasa.Najua tayari njaa imeshakukaba shauri hao samaki wanakukuna sana.Andaa ugali wako wa muhogo halafu itazame picha hii lakini kwa wanyasa hakuna kuangalia picha bali wanakula kitoweo kamili.Usiogope muombe tu wala wanyasa siyo wachoyo
Madhumuni
chiwindi,
kumbukumbu,
Nyasa
Subscribe to:
Posts (Atom)