July 15, 2008
ujumbe wa leo
'Utii bila uhuru ni utumwa'
July 14, 2008
uzuri wa nyasa?ngoja nikuambie
Kumbukumbu + Nyasa + Uzuri
Wapi pale,ni pwani ya mbamba bay au unaonaje mwenzangu.Tazama hii picha halafu ninong'oneze asisikie yule Yasinta wa Ughaibuni...itakuwa varangati...uatajuaje kama natania.Ni mbamba bay pwani ya ziwa nyasa
Madhumuni
amani na upendo,
uzuri
July 13, 2008
Asante Yasinta kwa kumbukumbu
Madhumuni
kumbukumbu,
Nyasa,
ughaibuni
July 12, 2008
Jioni Njema Nyasa
July 11, 2008
Panaitwaje Vile? Lundu
Hapa ni moja ya maeneo ya Lundu yaani hapa ndipo ukurasa mkuu wa maisha yangu ulipo.Hapa ukitazama unaona mlima huo,halafu uapnde wa kushoto ndiko uelekeo wa bandari ya Lundu ilipo.Mv Iringa na Mv Songea hutia nanga hapo,hapaonekani yaani ni kushoto zaidi kwahiyo picha ilitaka mlima.Ni ukurasa mkuu wangu wa maisha,mwone mnyasa yupo kazi na zana
July 10, 2008
Siyo Uvuvi pekee .....hata usafi pia
Ukanda wa ziwa nyasa unategemea sana maji ya ziwa nyasa kwa matumizi ya nyumbani.Wengi wamenufaika na ziwa hili kwani maeneo mengi hayana maji ya safi ya bombani.Achila mbali maeneo ya kama Mba Bay,Lundo,Chinula,Liuli na Lituhi lakini maji kwa maeneo mengi ni suala sugu.Kwa mbali wanaonekana watu wakifanya usafi wa nguo zao.Lakini yule mbunge wake sijui anafanya nini kila siku anatetea chama chake cha majambazi
July 09, 2008
kumbukumbu Profesa Chachage S Chachage
"Laiti kama wahenga waliomwaga damu yao takatifu katika vita ya ukombozi ya Majimaji wangalifufuka leo na kuwasikia wajukuu wakiusifia ubeberu na ukoloni mamboleo,bila shaka wangewakana na kulaani kwamba huu sio uzao wao"........"Utii bila uhuru ni utumwa" Jamani leo ni kumbukumbu ya mwanafalsafa wa kitanzania ambaye alifariki julai 9 2006.leo ni miaka miwili kamili tangu alipofariki.Tafura kitabu chake maridadi cha MAKUADI WA SOKO HURIA. Unajua kama mzee mkapa yule rais aliyestaafu alimchukia sana Chchage?Huyu alikuwa katika sayansi ya siasa UDSM-mlimani.Hayo ni moja ya maneno yake,huyu jamaa alikuwa kiboko waulize watawala wa enzi za mkapa.Mungu amlinde daima
Madhumuni
kumbukumbu,
maisha,
siasa.
Nimesahau!Ah Nyasa pale.....
Subscribe to:
Posts (Atom)




