nimeamua kujipendelea ndugu yangu.Wahenga walinena raha jipe mwenyewe mwanakwetu.Wacha nijipendelee kwani wao wakiweza wananini hata sisi tushindwe tunanini,wasalimie wote masela wangu TKZee,Mandoza,Mina Nawe kule bondeni kwa Nelson Mandela na midundo yao ya Kwaito inanikuna sana.Mmmh najua dada Yasinta ameshaweka kanda kuanza kucheza Kwaito maana anazipenda mno jasho linamtoka kila siku kunengua kwaito!! aaah wapi raha tu,yote yatimilike ndani ya muda huu,eee bwana muda bado unaruhusu!!Karibuni nyasa
August 09, 2008
Ni upendeleo au nini jamani....aa wapi
nimeamua kujipendelea ndugu yangu.Wahenga walinena raha jipe mwenyewe mwanakwetu.Wacha nijipendelee kwani wao wakiweza wananini hata sisi tushindwe tunanini,wasalimie wote masela wangu TKZee,Mandoza,Mina Nawe kule bondeni kwa Nelson Mandela na midundo yao ya Kwaito inanikuna sana.Mmmh najua dada Yasinta ameshaweka kanda kuanza kucheza Kwaito maana anazipenda mno jasho linamtoka kila siku kunengua kwaito!! aaah wapi raha tu,yote yatimilike ndani ya muda huu,eee bwana muda bado unaruhusu!!Karibuni nyasa
August 08, 2008
uzuri,utulivu,nyasa
August 04, 2008
gumzo,michapo na mseto
nashangaa hata sijui nataka kuandika nini lakini najikuta nataka kuandika.Ngoja kwanza,kuna kitu kinanifurahisha sana halafu sikijui sawasawa lakini najiona nina furaha toka jana niliofanya.Haa utashangaa eti sikijui huku nakifanya-ngoja ni hivi nahisi naandika lakini sijui naadika nini ambacho wanyasa wenzeangu wanafurahia. Nilikuwa mbinga juzi bwana nikaona jinsi watani wangu wamatengo wanavyochakarikia samaki,yaani wanahaha wananunua pale karibu na kituo cha mabasi katika soko la samaki.Aise niliwaona wanahangaika na kusukumana kisa kitoweo toka nyasa.Hivi najieleza vizuri kweli?unanielewa mnyasa mwenzangu?Nimekumbuka tena wenzenu huku nyasa sasa ni kula mpuchulela/kisamvu,kuoposha mandongo/kula mlenda,chaina bila kusahau mangatongo/eti wengine waita mbegu za upupu kazi kwenu.Huu ni msimu wa samaki kupotea shauri ya kuogopa kwisha(natania)naona kila mtu anahaha kupata japo kidogo mpuchulela.Mmh ni hivi nimepata kitabu kile cha 'makuadi wa soko huria' kiliandikwa na porofesa/profesa chachage chachage.unajua wanyasa kuatmka profesa ni kazi nzito sana?wao huita porofesa au yule osama wanaita usama/hosama.Unaielewa au nianze upya?Nahisi sijui kujieleza vizuri sijui nimepagawa na nini lakini najua kitabu hiki kinanikuna sana nasoma hadi maandishi yafutike yote.Mmm ngoja hivi kuna sababu ya watu kublogu?aah bora uniue kabisa kuliko kunizuia kublogu aise patachimbika yaani hapatoshi na mwendo wa kutunisha misuli tu. Ngoja nikomee hapa na michapo ya mseto
Madhumuni
falsafa,
maisha,
mila na desturi
Subscribe to:
Posts (Atom)
