Nilikwisha kueleza kwamba kipindi hiki siyo kizuri kwa wale wasiozoea usafiri wa meli shauri ya dhoruba kali. Sasa kuna dhoruba ambayo kwa wale wasoizoea wanaweza kujikuta akisafiri kama yupo rumande. Dhoruba ni kali sana kipindi hiki hadi mwishoni mwa mwezi septemba kwahiyo wanaweza kutumia magari kwa barabara za Mbamba bay au ile ya jijini Mbeya
August 28, 2008
kumbukumbu tena
Nilikwisha kueleza kwamba kipindi hiki siyo kizuri kwa wale wasiozoea usafiri wa meli shauri ya dhoruba kali. Sasa kuna dhoruba ambayo kwa wale wasoizoea wanaweza kujikuta akisafiri kama yupo rumande. Dhoruba ni kali sana kipindi hiki hadi mwishoni mwa mwezi septemba kwahiyo wanaweza kutumia magari kwa barabara za Mbamba bay au ile ya jijini Mbeya
Madhumuni
kumbukumbu,
maisha,
Nyasa,
zana
Karibuni nyasa
jionee fahari,nyasa nakupenda sana. kuna yeyote ana hoja kwamba hii siyo hali halilisi ya nyasa?jieleze
Madhumuni
Hisia za moyo,
maisha,
mapumziko
Mv Ilala kazini
ukija mbamba bay unaweza kwenda Malawi kwa kutumia meli hii hata kama una mizigo mikubwa kiasi gani.Kwa ile Mv Mtendele inashindwa kutia nanga shauri ya bandari yetu mbamba bay ni ndogo
August 27, 2008
Pekupeku
Ndiyo sijaiba wala sikuruhusiwa kuitumia picha hii lakini imenikumbusha mbali sana. Kaka yangu Mbilinyi kaanza mazoezi ya kutembea pekupeku,yaani wakati ule ukijifanya unavaa kandambili basi huonekana ufahari sana. jamani kutembea pekupeku hapa nyasa ni kama utamduni na maisha yenyewe lakini tunaulamba suti nakadhalika
Madhumuni
kumbukumbu,
maisha
August 23, 2008
Haya tena kama kawaida wanyasa
najua wengine mmenuna eti kisa sijablogu kwa wiki kadhaa,jamani ni majukumu haya kuvua samaki kwahiyo tuliondoka kijijini kwetu kwenda vijiji vya mbali kuvua samaki kwahiyo hata muda wa kwenda mbinga mjini ikawa ngumu sanna.Eti leo hata dada Janeth kaandika ujumbewa hasirakwanini sijablogu na nimeweka picha zamani sana.Niliomba msamaha lakini inaonekana hana raha na kasi ya kublogu siku hizi.Haya kama kawaida wanyasa nipo tena. sijasahau kuna habari ya kutembea peku hebu isome hapo kaka Mbilinyi
Madhumuni
kumbukumbu,
Nyasa,
zana
Subscribe to:
Posts (Atom)