October 01, 2008

zana za kazi hizi

Mitumbwi imetu;lizana baada ya kazi yake

September 29, 2008

kama... kama ... kama nini?

aaaaaah acha niseme bwana kwani huwa siataki ushahidi mwenzenu bali naweka tu hapa mjionee ninayoyaona miye.mengine niliyaona kale lakini nilikuwa haifadhi bila kujua wapi nitaweka lakini shajara zinarahisisha mambo kama hivi. Hivi ni kama... kama.. kama nini? eti unaonaje?

September 27, 2008

SONGEA LEO HII ; Afungwa maisha kwa kulawiti

IMEANDIKWA NA HAPPY KULANGA,
SONGEA


Mkazi wa kijiji cha Mageuzi Mlilayoyo wilayani Songea Vijijini bwana Maneno Katuna(24) amehukumiwa kifundo na mahakama ya wilaya ya Songea baada ya kukiri kosa la kumlawiti mtoto wa darasa la kwanza wa shule ya msingi Mageuzi mwenye umri wa miaka 8. Mwendesha mashtka Inspekta Patrius Mlowe alieleza mbele ya hakimu wa mahakama hiyo Joseph Emmanuel Foyo kuwa mtuhumiwa alitenda kosa hilo Septemba 16 mwaka huu asubuhi kwa kumlaghai mtoto huyo kuwa anataka kumpa Chai. Aliiambia mahakama kuwa baada ya mtoto huyo kuingia ndani alimvua nguo na kuanza kumwingilia kinyume na maumbile na kumsababishia maumivu makali hata akshindwa kutembea. Alisema mtoto huyo aligundulika na wasamaria waliokuwa wakipita jirani na nyumba hiyo walimwona mtoto huyo akilalamika kutokana na maumivu makali aliyokuwa ameyapata. Mshtakiwa baada ya kusomewa shtaka lake alikiri kosa na kuiomba mahakama imsaidie kwa maelezo kuwa umri wake kuwa mdogo na anahitajika katika ujenzi wa taifa. Hata hivyo madai yake yalitupiliwa mbali na hakimu Fovo ambaye aliamua kumhukumu kwenda jela maisha yake yote,akisema adhabu hiyo ni fundisho kwa watu wengine wenye tabia kama hiyo.

kwa wanaotaka kwenda majuu - III

kila la heri mnaotaka kwend majuu ila mjue wala sichukii na wala sina kinyongo. Msidhani nawaonea wivu kwani najua kimsingi wivu humuua mtu mjinga. Mbinu za kutaka misaada na yale ya BRAIN DRAIN saswa tu hakuna maneno msidhani nawashambulia.Sina uuwezo wa kuwashambulia mimi binadamu mwenye nafasi ndogo katika maisha yako.Ninachosisitiza ni kwamba nenda ughaibuni kwa mipango,jiandae,kuwa mkamilifu,soma tamaduni zao,kuwa mwangalifu,amini kwamba mipango,jiwekee malengo huko uendako,usidanganyike na wapenzi/mapenzi/mpenzi..lakini kuwa makini kwa kila hatua.

September 26, 2008

uzuri+utulivu = wageni mnakaribishwa

pwani ya ziwa nyasa/ufukweni karibuni nyasa

nchuwa/bao.........................jaza jina unalolijua

kwa wanaotaka kwenda majuu - II

Awali nilikuwa sielewi kwanini hawa watu wangu wanataka kuondoka nchini mwetu, lakini baadaye nilipokuwa Uchina na bwana Mao rais wa pale nilielewa sababu zao kwani nilikutana nao wataalamu wetu walioondoka Tanzania. Walinieleza sababu zao zenye maana kabisa,nikaelewa kwamba wanamipango mizuri. ...hata hivyo nikawaambia msisahau nyumbani jamani si mnajua kule mmewaacha ndugu zenu. kumbukeni hata sisi tulisomeshwa na mkoloni halafu tukapambana naye kwahiyo hata ninyi mnaweza kupambana nami kama sifanyi yale yanayowapendeza,huo ni utumiaji wa elimu. Sasa mkiondoka hawa wasiojua kitu watapambana vipi,watanitikisa vipi wakati siwaogopi. Lakini vijana wetu wakifundishwa kwenda mahala bila mipango,kuondoka kinyemela kwa ahadi za watu wasiowajua wala utamaduni wao,nadhani taifa litaaibika sana. Mnamwachia Mwl.NYERERE kupamba na umasikini kwani yeye ndiye aliwaletea? Haaa(kicheko). Lakini ninyi watu lazima mfikiri siyo kuhubiri tu maghorofa ya ulaya na amerika hapa..hayakuja bure shauri yenu....na...na ....na elimu yenu bado mnawapatia kila jambo hawa ndugu zetu...(wazungu).Msidhani kwamba mnyasa ninaandika mambo gani..kwani naona ile kasi ya kutaka kuishi majuu kwa kusingizia kusoma na wengine kutafuta kazi imezidi sana.Wabongo hayo maneno ni ya huyu mzee pichani JULIUS KAMBARAGE NYERERE.kama siku ya mwisho kuwepo duniani ningelikuwa naye,ningelimuomba kichwa chake yaani ubongo wake tu basi. Lakini kama kweli tunadhani elimu bora iko huko ughaibuni,elimu yetu airekebishe nani? tukisha soma huko basi tunaomba kazi hukohuko tena kufagia n.k baada ya hapo unarudi bongo unalalamika mbona hali haibadiliki? eboo! huna adabu akubadilishie nani wakati ulipomaliza shule hukurudi kuibadilisha si ulikwenda kuishi na yule Mwenyekiti wa Marais waongo duniani Joji Kichaka? Natumia lugha kali bila kutumia tafsida ili mpate ghadhabu na kuongeza juhudi. Mungu akupe hekima Ndesanjo Macha, Fred Macha nipo nanyi daima.Jikomboe. Uhuru daima

September 25, 2008

kwa wanaotaka kwenda majuu


Usitoke katika nchi yako kama hujui unakokwenda. Huna mpango,hiyo ilikuwa moja ya nguzo zangu za kuandika TWENZETU ULAYA kuwaonya wenzangu kuondoka bila mpango
. Hayo ni maneno ya mzee wangu Fred Macha mtu ambaye sikosi kusoma kazi zake iwe katika magazeti au vitabu. Vijana wengi Bongo tuna ndoto za kwenda Ulaya,lakini nami nawaonya ikiwa umeshindwa kuweka maisha yako vizuri hapa basi usitajie kufanya hivyo ughaibuni,wengi wanadanyika na picha z akwenye filamu na majumba makubwa kana kwamba ughaibuni kuna mazuri zaidi. Lakini hatujiulizi haya mazuri yanakujaje. Enyi wenye ndoto za mchana kwamba mnakwenda ughaibuni kusoma,hivi manajua kwa undani nini kinachofanyaika katika za wenzenu? hivi digrii tu mtu anaitafuta ughaibuni wakati tuna vyuo vingi hapa Tanzania. Tena ni afadhali ukaenda nchi zilizopo ndani ya bara la Afrika kwwani zinafanana isipokuwa Afrika kusini ambako mambo ni kama huko ulaya. Tafuteni kitabu cha MPE MANENO YAKE kilichoandikwa na mzee huyu kwani ni mkusanyiko wa mambo yaliyotokea mahali alimoishi. au soma mohajiano/habari nzima hapa; bongocelebrity.com/.../kwa-kina-na-freddy-macha

makosa+urafiki+kumbukumbu+msamaha


Ngoja niandike kwanza leo. Yasinta Ngonyani ni dada yangu,rafiki yangu na mtu wangu wa karibu.Lakini katika kipindi chote hiki nadhani mnaelewa watu wakiwa marafiki wema hushauriana kupiga gumzo na mseto wa michapo n.k. Nimeamua kuandika kwasababu najua nilimkosea rafiki yangu mnyasa mwenzangu,mngoni mwenzangu,mtanzania n.k hata hivyo nadhani hakuna matata. Ila nasema kweli dada Yasinta nimeamua kuandika hapa ingawa najua utaniuliza busara zangu kwani yalikuwa masuala ya kirafiki na binafsi zaidi,lakini ujue mwenzio wala hata moyo hauridhiki najihisi kukosea. Kwahiyo naomba nisamehe 7mara 777. nafikiri unajua kwamba utasema hakuna kosa lakini nakupenda sana dadangu nikikosea nisahihishe mdogo wako mimi kwani naamini una mengi uliyoyaona kukukuta. Kwani historia yako inanipa uchungu inanikumbusha namna ambavyo sijafaidi raha za wazazi sababu ya shule yaani tangu darasa la sita nipo mbali na wazazi kwahiyo wakati mwingine naona siitendei haki nafsi yangu. Salamu kwa shemeji,mjomba wangu Eric na Camilla waambie msameheni anayejuta. Unajua kwamba kuna wakati sitendi kama ninavyopaswa lakini nashukuru kama unaelewa kwamba mdogo wako nipo katika hali gani. idumu blogu ya ruhuwiko. Amina