October 14, 2008

kama ninge...... kama ningekuwa Nabii Mwalimu Nyerere

wale wanaoabudu dini zao wana manabii wao. Nami sioni soni kukuita Nabii wa kweli kwa imani ya kiafrika wala iyo wale waliozaliwa mashariki ya kati. Mungu wetu yu pamoja nawe. kama ningekuwa wewe .........
wamatengo hamyambu yambu

October 12, 2008

hamu+utamu+uzuri+utulivu=nyasa

smaki aina ya ngorokoro
korido za Mv Ilala ambayo hufanya safari zake toka Malawi-Tanzania. hii ni mali ya Malawi na yapili kwa ukubwa baada ya Mv Mtendele

October 11, 2008

ufukweni kijijini kwetu LUNDU

hapa ni kijijini kwetu LUNDU. halafu ukiangalia nembo ya LUNDU upande wa kulia utaona watu wanafurahi sana ni utundu mdogo. sasa hapa ndiyo kwangu yaani kijiji nilichozaliwa.karibuni msije mkaja na pombe hatutaki

ni maisha tu kwani nani anajali hali hii

mafisadi nao wanatumalizia kitoweo cha maendeleo

October 09, 2008

habari ndiyo hiyo

hapa hakuna la mnadi swala wala sauti za kanisa, mchezo ni kujiburudisha, mchezo kufurahi yanini kujibana wakati muda wenyewe robo eti tutakwenda peponi mmmm

October 08, 2008

Labda leteni huku nyasa

sijaomba picha hii, lakini poa tu. Kuna jamaa walevi wanapenda sana hivi vitu. wengine wakunywa eti kupoteza mawazo. ebo nani kakwambieni mawazo yanapotezwa? mnajidanganya,mkipoteza mtapata wapi mengine. ndiyo nimechukua hapo bloguni Ruhuwiko kwa wanywa ulanzi na chimpunu(natania). jamani ukitaka kuwa na urafiki bora nami ni vema ukatofautisha haya makopo na nami. kama unasema unataka kupiga gumzo nami hakikisha pembeni hakuna makopo kama hayo. hata kama iwe mnasema 'mtoko' au 'matembezini' nakwambia nakuachia mtoko wako ukiniletea hayo makopo kama vipi kunywa kwa muda wako kisha harufu yako usilete kwangu au vipi waungwana. Unajua nini hapa nyasa hakuna, kwahiyo washamba tumekuwa wengi nasikia ukinywa tu unakufa. Kuna daktari mmoja alipogundua kwamba nina damu nyingi aliniuliza eti kama nakunywa pombe nusura nimzabe kibao, nikamwambia akome na akomae au vipi. karibuni nyasa lakini ONYO usije na hayo makopo ni haramu

maswali magumu

Mwanablogu Yasinta Ngonyani aliandika kuhusu yeye katika blogu yake. Ilikuwa Agosti 23, 2008 kwamba udadisi kwake ni sehemu ya maisha, akaongeza kwamba katika hali hiyo amejikuta amepoteza baadhi ya marafiki hasa wale wasiopenda maswali yake yaani walikuwa wakikerwa na maswali yake. Mimi sijui walikerwa kwasababu gani, wao wanajua. Sasa mimi namfahamu kiasi dadangu Yasinta, jamani hapo ni kiboko ya maswali yaani jamaa anauliza maswali mpaka unaona hee huyu vipi? Ukweli mmoja ya waathirika ya maswali yake ni Mnyasa hapa lakini kawaida ya Mnyasa ni uvumilivu na utulivu ndiyo uliobaini kwamba uulizwaji kwake maswali ni njia yake ya uwasilishwaji wa urafiki tofauti na wengine walivyokuwa wakidhani. Jamani dadangu anamaswali mpaka unaweza kuungua utadhaniumeunguzwa na moto. Sasa huwa najiuliza vipi mjomba wangu Erik na Camilla watakuwaje? nikajikuta nimegota,nimeishiwa maneno ya kuwatabilia. Lakini maswali yake yanakufanya muda wote uwe unafanya kazi ya kujibu na usipojibu heee umemkimbia au la. Jamani mimi nilivumilia na nimekubali kwamba kama alivyoandika ni kawaida yake kwahiyo naona poa tu. Habari ndiyo hiyo, kublogu/kuandika unachopenda

mwanamke auawa kwa kupigwa shoka

Na HAPPY KULANGA, SONGEA.

Watu wawili wameuawa kikatili katika matukio mawili tofauti yaliyotokea wiki jana.Kamanada wa polisi Falhum Mshana alisema jana kwamba katika tukio la kwanza agnes Kabanda aliuawa kwa kukatwa na shoka kichwani na hawara yake aliyehamika kwa jina la Ally Makinda. Kamanda huyo alisema tkio hilo lilitokea oktoba 3 saa 3:15 usiku katika eneo la Majengo Kisiwani ambako Makinda alimkata mpenzi wake shoka na kukimbia.

Taarifa z akufa zilitolewa na Hassan Salum(28) mkazi wa majengo C ambaye alikuwa akipita nyumbani kwake na kuona mwili wa marehemu ukiwa katika uwanja wa nyumba ya Makinda. Alisema chanzo cha mauaji ni ugomvi uliokuwepo baina ya marehemu na mtuhumiwa, ingawa alisema hadi sasa polisi bado hawajui ugomvi huo ulisababishwa na nini. Lakini uchunguzi unaendelea.

Pili, KILOSA MBAMBA BAY.
MkaZi wa Kilosa katika mji wa Mbamba bay Meshack Ngalima(62) amefariki dunia baada ya kudondokewa na mwembe aliokuwa akiuka. Tukio hilo lilitokea oktoba 3 saa 5 asubuhi mwaka huu. Meshack alifariki muda mfupi baada ya kufikishwa katika kituo kidogo cha afya Mbamba bay alikopelekwa na mdogo wake kwa ajili ya matibabu.