October 31, 2008

kuweni makini na usafiri wa meli kipindi hiki

nilisema awali kwamba katika miezi ya julai hadi katikati ya novemba ni kipindi cha dhoruba katika ziwa nyasa kwahiyo wale wasio na uzoefu wa safari za meli wanapaswa kuelewa hili ili watumie safari za magari. kwasasa dhoruba ni kubwa si kidogo tazma hiyo picha vema.

Je mungu alituumba majuha?

hivi kweli mungu alituumba waafrika kuwa majuha? soma hapa www.raiamwema.co.tz katika safu ya fikra mbadala ya Mwanafalsafa Ayoub Rioba. Namwita Mwanafalsafa kwa vigezo vyangu kwani ni muumini wa fikra zake kama ilivyo kwa Jenerali Ulimwengu na wengine

tunaweza kutunza mazingira yetu siyo samaki tu

October 29, 2008

natabasamu jamani RAHA za hapa nyasa

tazama tabasamu hilo linavyoukita. tabasamu linakuita bila kinyongo. kaja huyu je wewe uliye jirani? karibu nyasa

Raia mwema: muungwana ni vitendo

WATU WANGU, WADAU WANGU, WAPENDWA WANGU= AMANI IWE NANYI.

Nawashukuru nyote mnaonisoma na kuniunga mkono. Lakini pia niwashukuru hawa waliopo ughaibuni kwa kutumia muda wao kunipa pongezi, ingawa ni muda mrefu. Leo nasema ASANTENI SANA.
1. JOSEPH MBELE, www.josephmbele.blogspot.com & www.africonexion.com
2. RAITON MBELE www.raitonambele.blogspot.com
3. ROBERT NGALOMBA.

NAWASHUKURU SANA KWA KUNIFUATA KATIKA BLOGU YANGU. wote mnaonisoma nawapenda sana. Na ikiwa unadhani nimesahau jina lako basi naweka ................................... jaza jina lako. Au vipi waungwana!
PAMOJA DAIMA!!!!!

unatupenda au unatutega? nunua moja basi!!

je unafikiria nini unapowaona watoto kama hawa wanafanya hivi? Je katika maisha yako ulikwisha kufanya jambo hilo? Nini maoni yako?

October 28, 2008

unanipenda?? unanitega?? Je hivi utaweza??

ukinipenda haya utaweza? au unanitega kwamba unanipenda? aaa karibuni sana yaani bado tupo tupo sana nyasa, bado tupo tupo kwanza.

usafiri upo usihofu

tafadhali ukiwa na njaa kali toa taarifa

October 25, 2008

raha+utamu+upendo= nyasa

karibuni lakini wale walevi hatuwataki dada Yasinta na mwenzake kaka Simoni. sharti mje mnywe komono na pombe zote za huku lakini hizo za mujini hatuzitaki

karibuni Chinula jamani

yaani raha sana karibuni. WEKEZA SASA MKOA WA RUVUMA USINGOJE

vijana wapya Jamani wapeni moyo.

Inaonekana kama nimekuwa mvivu kuhusu blogu siku hizi, lakini amini nawaambia siyo ila mambo ya hapa na pale kuvua samaki kuogelea sana mpaka machp yawe mekundu kama wale mabibi wa shinyanga halafu mseme uchawi.
Kuna vijana wapya nawasaka wamekuja katika blogu jamani. Kazi yangu nyingine sasa ni kuhamasisha kuanza blogu kwahiyo msione kimya. He waangalieni hawa vijana ambao nimefanikiwa kuendeleza kazi za Ndesanjo Macha

www.kambilisports.blogspot.com
www.shamakala.blogspot.com

wapeni moyo, nafanya juhudi kubwa kuhamasisha kuhusu blogu