November 19, 2008

zana za kazi zipo mapumzikoni

November 18, 2008

zawadi ni zawadi usambe utajiri jamani


picha nzuri, niliahidi kuitolea zawadi. HABARI NDIYO HIYO.

November 17, 2008

kuvua dagaa usiku


dagaa wa ziwa nyasa ni watamu sana, wananoga mno, ukila unajiumauma tu hamu na kuzidi kunogea. SASA ukitazama picha hii utaona KARABAI zimefungwa mtumbwini, hapo ndipo kazi inafanyika kwani ukisha funga hivyo kazi inaanza kwenda kilindini na anyavu ya kuvulia kusaka kitoweo kunoga na utamu kuliko chochote..... ebu taja kitu kingine kitamu kuliko dagaa? najua utataja nanii....... nini ile ...... sijui ebu inaitwaje!!!! aahaa tuache, hayo. haya ndiyo mambo ya nyasa na zana zao

kazini hakuna matata

kuvua samaki ndiyo zetu, ni kazi zetu ni shughuli zetu wala hatuachi kufanya hivyo. KARIBUNI NYASA

November 15, 2008

hatuchoki tunataka haki sawa hapa siyo longolongo

SIWAOGOPI HAWA WENYE NYWELE NDEFU NA KUNENEPEANA KWA SHIBE ZAIDI, BALI NAWAOGOPA WANYONGE NA WENYE NJAA- Julius Caesar. Chuo kikuu kimefungwa shauri ya migomo ya kutoingia madarasani. Lakini hawa walionenepeana halafu wakashangilia kwa mikogo eti OBAM kashinda. Zinawatosha ninyi??? sheria za kikandamizaji ataondoa huyo? wizi wa mitihani ataondoa huyo kuweka meli za kuvulia samaki ataleta OBAMA, kwania ananihusu nini?? ninyi ndiyo milompigia kura??? mliomba kwa mungu, ina maana asingejaza fomu basi mungu angelimjazia ha ha ha ha ha ha ha ha

Chuo Kikuu sehemu ya Mlimani


Tanzani ni migomo, maandamano kila mara. Chuo kikuu kimefungwa na kampasi zake zote WANAFUNZI wamegoma. Tunahitaji mabadiliko siyo uongozi wa mazoea HAPA. UONGOZI UMEKWAMA, UMEELEMEWA WANABAKI KUONGEA MPAKA MKOROMEA YANAKAUKIWA MATE

November 13, 2008

kipindupindu kiingie ikulu


sikujua uchungu, sononeko la moyo
akili yagota kwangu, moyoni harijojo
ghadhabu yanisibu,adhuhuri si kikomo
dibaji ya nini,uchafu mitaani?

kila leo twaumwa,vichomi na kuhara
miili yatuuma,akili nayo yagoma
maji haba salama, twanywa ya visima
dibaji ya nini uchafu mitaani?

kipindupindu chapindua,kinyesi kuwa maji
mwili kukongoroka,acheni dhihaka jamani
kila leo twanya uharo, ikulu vipi?
dibaji ya nini,uchafu mitaani

kipindupindu ikulu,napenda kitinge
waharishe wakuu,nasi tupumzike
aghalabu isiwe vigumu, wanye uharo preeee
wakome na kuona mashudu,wanune au wacheke?
dibaji ya nini,uchafu mitaani

ngoja kipindupindu kiingie ikulu
ooooh alamsiki waungwana wema