November 21, 2008

alaah kumbe wavuvi nao wanaofisi zao, kumbeeee


mnyasa naye yupo

November 20, 2008

Mwl Klayson karibu sana Nyasa


Nasema sana KARIBU NYASA

November 19, 2008

zana za kazi zipo mapumzikoni

November 18, 2008

zawadi ni zawadi usambe utajiri jamani


picha nzuri, niliahidi kuitolea zawadi. HABARI NDIYO HIYO.

November 17, 2008

kuvua dagaa usiku


dagaa wa ziwa nyasa ni watamu sana, wananoga mno, ukila unajiumauma tu hamu na kuzidi kunogea. SASA ukitazama picha hii utaona KARABAI zimefungwa mtumbwini, hapo ndipo kazi inafanyika kwani ukisha funga hivyo kazi inaanza kwenda kilindini na anyavu ya kuvulia kusaka kitoweo kunoga na utamu kuliko chochote..... ebu taja kitu kingine kitamu kuliko dagaa? najua utataja nanii....... nini ile ...... sijui ebu inaitwaje!!!! aahaa tuache, hayo. haya ndiyo mambo ya nyasa na zana zao

kazini hakuna matata

kuvua samaki ndiyo zetu, ni kazi zetu ni shughuli zetu wala hatuachi kufanya hivyo. KARIBUNI NYASA

November 15, 2008

hatuchoki tunataka haki sawa hapa siyo longolongo

SIWAOGOPI HAWA WENYE NYWELE NDEFU NA KUNENEPEANA KWA SHIBE ZAIDI, BALI NAWAOGOPA WANYONGE NA WENYE NJAA- Julius Caesar. Chuo kikuu kimefungwa shauri ya migomo ya kutoingia madarasani. Lakini hawa walionenepeana halafu wakashangilia kwa mikogo eti OBAM kashinda. Zinawatosha ninyi??? sheria za kikandamizaji ataondoa huyo? wizi wa mitihani ataondoa huyo kuweka meli za kuvulia samaki ataleta OBAMA, kwania ananihusu nini?? ninyi ndiyo milompigia kura??? mliomba kwa mungu, ina maana asingejaza fomu basi mungu angelimjazia ha ha ha ha ha ha ha ha

Chuo Kikuu sehemu ya Mlimani


Tanzani ni migomo, maandamano kila mara. Chuo kikuu kimefungwa na kampasi zake zote WANAFUNZI wamegoma. Tunahitaji mabadiliko siyo uongozi wa mazoea HAPA. UONGOZI UMEKWAMA, UMEELEMEWA WANABAKI KUONGEA MPAKA MKOROMEA YANAKAUKIWA MATE