November 23, 2008

karibu tunakula, sijui utakifurahia chakula chetu..

hebu tazama nyuso za walaji hawa, watazame kwa umakini kisha sema mwenyewe wapo katika hali gani. Kuna jambo unalojifunza? Inakufikirisha kidogo? Tunahitaji kuanza upya mapinduzi? JIKOMBOE SASA, UHURU DAIMA.

November 21, 2008

alaah kumbe wavuvi nao wanaofisi zao, kumbeeee


mnyasa naye yupo

November 20, 2008

Mwl Klayson karibu sana Nyasa


Nasema sana KARIBU NYASA

November 19, 2008

zana za kazi zipo mapumzikoni

November 18, 2008

zawadi ni zawadi usambe utajiri jamani


picha nzuri, niliahidi kuitolea zawadi. HABARI NDIYO HIYO.

November 17, 2008

kuvua dagaa usiku


dagaa wa ziwa nyasa ni watamu sana, wananoga mno, ukila unajiumauma tu hamu na kuzidi kunogea. SASA ukitazama picha hii utaona KARABAI zimefungwa mtumbwini, hapo ndipo kazi inafanyika kwani ukisha funga hivyo kazi inaanza kwenda kilindini na anyavu ya kuvulia kusaka kitoweo kunoga na utamu kuliko chochote..... ebu taja kitu kingine kitamu kuliko dagaa? najua utataja nanii....... nini ile ...... sijui ebu inaitwaje!!!! aahaa tuache, hayo. haya ndiyo mambo ya nyasa na zana zao

kazini hakuna matata

kuvua samaki ndiyo zetu, ni kazi zetu ni shughuli zetu wala hatuachi kufanya hivyo. KARIBUNI NYASA