December 03, 2008

nawapenda Kingoli na Litumbandyosi, lakini poleni

Mvua kubwa iliyoambatana na upepo makali imeleta maafa makubwa katika kijiji cha KINGOLI kata ya LITUMBANDYOSI iliyopo wilaya ya MBINGA. Upepo huo umeezua mapaa ya nyumba TISA. Akizungumza kwa masikitiko Afisa mtendaji wa kijiji hicho Aloyce Nchimbi alisema mvua hiyo ilinyesha kwa zaidi ya saa moja na kusababisha baadhi ya wanafunzi wa shule ya msingi KINGOLIkutokuwa na mahali pa kusomea.
Mvua hiyo iliambatana na upepo mkali imeezua MADARASA MAWILI ya shule ya KINGOLI na NYUMBA mbili za WALIMU pamoja na majengo mawili ya ZAHANATI ya kijiji hicho
Mkuu wa wilaya ya MBINGA Amina Masenza amesema kamati ya kushughulikia tukio hilo imeundwa na itafanya kazi mara moja

NB; waungwana poleni watani zangu na watu wangu wa mkoa wetu PAMOJA DAIMA

nimeirejesha tena hii kumbukumbu


nimeipenda hii picha, sijui labda naifikiria sana na kuyaelewa mazingira yetu ya hapa nyasa. Lakini kuna jambo nalifikiria kuhusu mazingira haya na nyuso za wavuvi wenzngu.Waangalie vema unaelewa nini??

December 01, 2008

mauzo ya kondomu

Mara nyingi napenda habari mpya zenye vituko ambavyo vinanipa kazi ya kutafakari lakini sipendi vituko au habari za kunichosha ingawa sichoki mwili akili inagota.

SASA: Mauzo ya Kondomu huko Korea yamepnda sana tokana na watu hususani vijana wadogo kujihusisha na utamu wa ngoma ya kikubwa NGONO. Mauzo hayo ni kwa mujibuwa Dk Janet Hyde aliyefanya utafiti katika jamii za watu wa Korea toka chuo kikuu cha Wiscons. Anasema wingi wa Runinga, pamoja na mhusiano mabaya ya wazazi majumbani ni mambo ambayo yanaaminika kuchochea vitendo vya ngono kwa vijana wa umri mdogo.

Wengi wanaangalia vipindi ambavyo vinaashiria au kupandisha mzuka kama siyo midadi ya ngono na hawavai kondomu. Lakini hivi karibuni utafiti unaonyesha kondomu inanunuliwa sana tu ili kujiburudisha na majambozi ya kiutamu utamu!!!! Vijan wengi ni wale wadogo wenye umri wa miaka 13 na 15 ambao anadai wameshafanya ngono kama siyo kufaidi utamu huo katika umri mdogo. Mauzo yameongezeka sana kipindi hiki kuliko ilivyokuwa awali:Na maadili yamekuwa mabaya sana siku hzi huko KOREA

HIVI ndivyo vituko, lakini nafikiri unaweza kuwaza jambo. JE JAMII ZA KITANZANIA ZIPO VIPI? VIPI WALE WAPUMBAVU WANAODAI UTANDAWAZI huku hawana lolote katika utandawazi wenyewe? Je utandawazi hauna maadili? PAMOJA DAIMA!!!!!!

zawadi yako dada YASINTA

Ngoja nikupe zawadi nzuriiiiii sana dadangu kwani umenifanyia kazi nzuri katika blogu yangu. Hebu tazama hapo hilo ua vipi, ni kwaajili yako dada Yasinta na familia yenu yote.ASANTE.

November 30, 2008

usafiri wetu niyo huu

November 27, 2008

unapofurahia kunywa, ujue na kushughulika

naam mambo shughuli za kulima kahawa. hapo ni suala la kukausha si mnajua tunakausha kwa njia za asili au mnafanyaje ninyi.