TAMU ni yenye ladha ya sukari ambayo huridhisha kinywani. Ingawa vipo vitu vitamu vya kuhisia ambavyo havihitaji vipitie KINYWANI. Vitu VITAMU vipo vingi sana duniani. Havina hesabu. Vipo vinavyokolea UTAMU wake kwa kupikwa ama kuchemshwa au hata kukaangwa. Navyo huwa VITAMU, vipo vya kukorogwa kuchanganywa na kughushiwa ili UTAMU unoge. Kazi hiyo hufanywa na sisi binadamu wenye akili na busara. Lakini viumbe wengine wakiwemo wanyama, ndege, na wadudu husaidia kuifanya kazi hiyo adhimu wakati mwingine bila wao kujua.
VITAMU huwa VITAMU.
Lakini VITAMU viongozavyo na ambavyo huvivumilia vinaporishai katika GEGO na FIZI za kinywa ni asali. Lo masalaleee!! Huu ni UTAMU ulioje wa asali? Sijui unatoka wapi?. Sio wa kukaangwa wa kughushiwa. UTAMU wa maumbile. UTAMU huo wa asali si bure, umefanyiwa kazi kubwa. Haushuki duniani kama mvua Wapo wenyewe ambao wanatengeneza. Ni viumbe kama sisi waitwao NYUKI. Hivi huo UTAMU WA MAUMBILE Upoje??? mbona NYUKI wanatupatia UTAMU mpaka WARINA ASALI wasitake kujua mtengenezaji??
December 09, 2008
heee!!! warina asali nao !!!!!
Najua unanogea+mate yanatoka=urudi nyumbani
najua kabisa unanogea, najua nakupatia HAMU. maana najua bila hamu huwezi kukumbuka kitu. Hawa siyo sawa na dagaa kigoma wanaochacha kama wa enzi zile za KIGONSERA a.k.a CAIGO BOYS, umenisoma kaka Mtanga ha ha ha ha Nina HAMU ndiyo ndiyo maana nakwambia haya. Watazame walivyoanikwa mchangani vizuri halafu unapata NG'ONDA upo hapo. RUDI NYUMBANI ha ha ha ha ha
Madhumuni
maisha,
mila na desturi,
Nyasa,
urafiki,
wageni
December 08, 2008
aaaah!! nina HAMU !!!
Nina hamu sana unajua? Nina hamu ndiyo maana nakwambia nina hamu mpaka nashindwa kujizuia. Nina hamu mpaka nataka kulia. Si hamu nyingine bali ya kukusalimia MAMBO? aaaaaah umnielewa huna hamu ya DAGAA wewe?
Madhumuni
kumbukumbu,
mila na desturi,
Nyasa
kazi+juhudi+ubunifu+mapenzi=MAISHA
maisha tu haya kama utapenda nunua tu utakuwa umenisaidia sana maana mwanangu namsomesha kwa kutegemea hii kazi yangu. Nahiheshimu sana. Ni kama anasema hivyo
Madhumuni
maisha,
mapenzi,
mila na desturi,
wageni,
zana
December 06, 2008
njoo unangoja nini, mwenzio nafaidi
Madhumuni
amani na upendo,
maisha,
Nyasa
maandalizi ya Noeli, karibu
Madhumuni
kumbukumbu,
Nyasa,
ughaibuni,
urafiki,
wageni
December 05, 2008
alaaah! sina kipaji cha kupenda, sikujua hayo
Aghalabu ni ningelijua lakini hakika sijijui labda kwakuwa sijui ndiyo maana nipo hivi. Nakupenda ndiyo maana nilikuja mbele ya wazazi wako, ingawa hawajui wanajua sisi tunafahamiana na marafiki. Sasa kivipi ilikuwa vile jakamoyo ukaijenga ulikuwa ukighadhibika? mbona hukusema, ingawa mara chache ulinena? hukusema kama unajua sina kipaji cha kupenda sasa mbona najua hilo kama sina kipaji? Poa sina simile wala sipigi kite kwani najua WARINA asali hawajui utengenezaji wake, wao HURINA tu hawajui mweka SEGA ni nani. Sasa najua sina kipaji cha kupenda unatakaje? nitembee kama nani, niige za ughaibuni hapana! tena thubutu bwana. Sasa nifanyeje ingawa najua kwamba unanipenda lakini ile tarehe milele sitoisahau daima itakaa moyoni kama simanzi ulotaka kunipa. Dunia ni nini? mbona wanipa majonzi huku wajua nakupenda? Nashukuru umenisamehe lakini swali langu, KUMBE SINA KIPAJI CHA KUPENDA? alaah kwanini hukuninong'oneza? mbona ulikuwa kimya ukadai wanipenda, nashangaa hata mungu anatakaa kujifanya muumini wakati una zigo la madhambi? au kujiona bora mapenzini, acha dhihaka, kweli ndivyo nilivyoumbwa siwezi kujibadili au nisake kipaji kama RONALDINHO maana wahenga walisema WA MBILI HAVAI MOJA au tusemeje AOMBAYE KIGAE AWE NA CHAKE? sijui ila asante kunisamehe ingawa niliuchukia mwezi Novemba. Alaaah kumbe sina kipaje cha kupenda?????
Madhumuni
burudani,
kumbukumbu,
maisha,
mapenzi,
urafiki
December 04, 2008
kwa watu wangu wa BIA na ULANZI
naam kwa watu wa toka nyasa mpaka mjini, wote mliopo juu na chini ujumbe utafika. wale wangu wa BIA kaka Simon na dada Yasinta yaani wapenda BIA naona huu ulaji ndiyo zenu sana? ha ha ha najua wanywaji hapa kwetu wanaita KAPILI hasa wale samaki waitwao NTAKA na vipande vya KAMBALE. ooooh kuna wale wapenzi wa kufakamia misosi ya kwenye sherehe basi hii ni ZAWADI yenu ila wale wanywa BIA wangojee yao.
December 03, 2008
nawapenda Kingoli na Litumbandyosi, lakini poleni
Mvua kubwa iliyoambatana na upepo makali imeleta maafa makubwa katika kijiji cha KINGOLI kata ya LITUMBANDYOSI iliyopo wilaya ya MBINGA. Upepo huo umeezua mapaa ya nyumba TISA. Akizungumza kwa masikitiko Afisa mtendaji wa kijiji hicho Aloyce Nchimbi alisema mvua hiyo ilinyesha kwa zaidi ya saa moja na kusababisha baadhi ya wanafunzi wa shule ya msingi KINGOLIkutokuwa na mahali pa kusomea.
Mvua hiyo iliambatana na upepo mkali imeezua MADARASA MAWILI ya shule ya KINGOLI na NYUMBA mbili za WALIMU pamoja na majengo mawili ya ZAHANATI ya kijiji hicho
Mkuu wa wilaya ya MBINGA Amina Masenza amesema kamati ya kushughulikia tukio hilo imeundwa na itafanya kazi mara moja
NB; waungwana poleni watani zangu na watu wangu wa mkoa wetu PAMOJA DAIMA
Mvua hiyo iliambatana na upepo mkali imeezua MADARASA MAWILI ya shule ya KINGOLI na NYUMBA mbili za WALIMU pamoja na majengo mawili ya ZAHANATI ya kijiji hicho
Mkuu wa wilaya ya MBINGA Amina Masenza amesema kamati ya kushughulikia tukio hilo imeundwa na itafanya kazi mara moja
NB; waungwana poleni watani zangu na watu wangu wa mkoa wetu PAMOJA DAIMA
Madhumuni
familia,
kumbukumbu,
maisha,
urafiki,
wageni
nimeirejesha tena hii kumbukumbu

nimeipenda hii picha, sijui labda naifikiria sana na kuyaelewa mazingira yetu ya hapa nyasa. Lakini kuna jambo nalifikiria kuhusu mazingira haya na nyuso za wavuvi wenzngu.Waangalie vema unaelewa nini??
Madhumuni
kumbukumbu,
Nyasa
Subscribe to:
Posts (Atom)
