December 10, 2008

wanablogu karibuni ndani

jamani wana-shajara za mtandaoni karibuni ndani. atakayepuuzia shauri yake. karibuni sana, mambo ndiyo hayo

kwa kweli nakupenda sana

nina HAMU ndiyo maana nakambia nakupenda sana NYASA. Gego na Fizi zinakupenda sababu ya utamu. angalia picha hiyo kwa umakini halafu niambie kama hutamani kweli!!! mmm nakupenda saaaaaana nyasaaaaaaa. karibuni

December 09, 2008

heee!!! warina asali nao !!!!!

TAMU ni yenye ladha ya sukari ambayo huridhisha kinywani. Ingawa vipo vitu vitamu vya kuhisia ambavyo havihitaji vipitie KINYWANI. Vitu VITAMU vipo vingi sana duniani. Havina hesabu. Vipo vinavyokolea UTAMU wake kwa kupikwa ama kuchemshwa au hata kukaangwa. Navyo huwa VITAMU, vipo vya kukorogwa kuchanganywa na kughushiwa ili UTAMU unoge. Kazi hiyo hufanywa na sisi binadamu wenye akili na busara. Lakini viumbe wengine wakiwemo wanyama, ndege, na wadudu husaidia kuifanya kazi hiyo adhimu wakati mwingine bila wao kujua.
VITAMU huwa VITAMU.
Lakini VITAMU viongozavyo na ambavyo huvivumilia vinaporishai katika GEGO na FIZI za kinywa ni asali. Lo masalaleee!! Huu ni UTAMU ulioje wa asali? Sijui unatoka wapi?. Sio wa kukaangwa wa kughushiwa. UTAMU wa maumbile. UTAMU huo wa asali si bure, umefanyiwa kazi kubwa. Haushuki duniani kama mvua Wapo wenyewe ambao wanatengeneza. Ni viumbe kama sisi waitwao NYUKI. Hivi huo UTAMU WA MAUMBILE Upoje??? mbona NYUKI wanatupatia UTAMU mpaka WARINA ASALI wasitake kujua mtengenezaji??

Najua unanogea+mate yanatoka=urudi nyumbani

najua kabisa unanogea, najua nakupatia HAMU. maana najua bila hamu huwezi kukumbuka kitu. Hawa siyo sawa na dagaa kigoma wanaochacha kama wa enzi zile za KIGONSERA a.k.a CAIGO BOYS, umenisoma kaka Mtanga ha ha ha ha Nina HAMU ndiyo ndiyo maana nakwambia haya. Watazame walivyoanikwa mchangani vizuri halafu unapata NG'ONDA upo hapo. RUDI NYUMBANI ha ha ha ha ha

December 08, 2008

aaaah!! nina HAMU !!!

Nina hamu sana unajua? Nina hamu ndiyo maana nakwambia nina hamu mpaka nashindwa kujizuia. Nina hamu mpaka nataka kulia. Si hamu nyingine bali ya kukusalimia MAMBO? aaaaaah umnielewa huna hamu ya DAGAA wewe?

kazi+juhudi+ubunifu+mapenzi=MAISHA

maisha tu haya kama utapenda nunua tu utakuwa umenisaidia sana maana mwanangu namsomesha kwa kutegemea hii kazi yangu. Nahiheshimu sana. Ni kama anasema hivyo

December 06, 2008

njoo unangoja nini, mwenzio nafaidi

wageni tu jamani hata wenyeji poa karibuni. haya mwangalie na huyu naye

maandalizi ya Noeli, karibu

kambale bwana, unakumbuka utamu wake? kwa wale wasiomla poleni huyo ndiyo kambale toka BABU hadi Mjukuu wanakula. ERIK UMEWAHI KULA KAMBALE WEWE? mwambie mama asiwe na roho mbaya hivyo akutafitie huko Uswidi , mkikosa njoeni nyasa