December 14, 2008

kumbikumbi+joto+pangaboi =MAPENZI

Utamu wa raha ni heshima, upendo na amani. Wawili huwa kama kumbikumbi na wengine hujiona kama JOTO na PANGABOI. Ndiyo Joto hupozwa na Panagaboi. Na yule umpendaye hakuna MWISHO haijalishi kama yuko mbali,karibu,jirani. Utamu wa roho na kupenda kwa moyo heshima ni kigezo kwani hata MOYO wako hunena kwa raha. Nikupe nini mziwanda wangu, KUMBIKUMBI wangu au nifanye nini ewe PANGABOI wangu? Moyoni najua naumia lakini naamini hakuna mwisho kwani NAKUPENDA. Najua kila MAWIO na MACHWEO hakuna MWISHO wa Penzi letu. Niambie basi nifanye nini,nikupe nini je niandike ujumbe mfupi kwako kila sekunde?Basi nina JOTO nawe ndiwe PANGABOI wangu nipulizie upepo nipe ubaridi ili nipunguze HARARA, wajua naandika huku nina simanzi? wajua kama ninasambaratika? Ooooooh nipe JOTO nikupe PANGABOI. Njoo basi tuongozane kama KUMBIKUMBI na MAPENZI yetu yadumu. HAKUNA MWISHO WA PENZI.
Akupendaye mnyasa mvuvi mahiri, mkulima satadi na mtafuta FARAJA kwako. MWAAAAAAAAAAAAAAAH
mimi Markus Mpangala wa kijijini.

NB; Asante dada Yasinta kwa Picha hii. PAMOJA DAIMA!!

hureeeeeee ayeyaaaaaah

ebwana ndiyoooooo, kichapo walichopata Sudan nyumbani kao hawata kisahau kwani ni jambo wanalolishangaa Tz kuibuka kinara. Mabao 2-1 ugenini mbona SHWANGA TU

December 13, 2008

njoo jiunge nasi, usihofu


kwani unatuonaje, angalia tulivyopendeza na tuna furaha kani vipi unashaka gani nasi. Tunafurahi kama tunavyotuona. Lakini hatuna uhakika siku ya kesho itakuwaje na tutakuwaje.

December 10, 2008

wanablogu karibuni ndani

jamani wana-shajara za mtandaoni karibuni ndani. atakayepuuzia shauri yake. karibuni sana, mambo ndiyo hayo

kwa kweli nakupenda sana

nina HAMU ndiyo maana nakambia nakupenda sana NYASA. Gego na Fizi zinakupenda sababu ya utamu. angalia picha hiyo kwa umakini halafu niambie kama hutamani kweli!!! mmm nakupenda saaaaaana nyasaaaaaaa. karibuni

December 09, 2008

heee!!! warina asali nao !!!!!

TAMU ni yenye ladha ya sukari ambayo huridhisha kinywani. Ingawa vipo vitu vitamu vya kuhisia ambavyo havihitaji vipitie KINYWANI. Vitu VITAMU vipo vingi sana duniani. Havina hesabu. Vipo vinavyokolea UTAMU wake kwa kupikwa ama kuchemshwa au hata kukaangwa. Navyo huwa VITAMU, vipo vya kukorogwa kuchanganywa na kughushiwa ili UTAMU unoge. Kazi hiyo hufanywa na sisi binadamu wenye akili na busara. Lakini viumbe wengine wakiwemo wanyama, ndege, na wadudu husaidia kuifanya kazi hiyo adhimu wakati mwingine bila wao kujua.
VITAMU huwa VITAMU.
Lakini VITAMU viongozavyo na ambavyo huvivumilia vinaporishai katika GEGO na FIZI za kinywa ni asali. Lo masalaleee!! Huu ni UTAMU ulioje wa asali? Sijui unatoka wapi?. Sio wa kukaangwa wa kughushiwa. UTAMU wa maumbile. UTAMU huo wa asali si bure, umefanyiwa kazi kubwa. Haushuki duniani kama mvua Wapo wenyewe ambao wanatengeneza. Ni viumbe kama sisi waitwao NYUKI. Hivi huo UTAMU WA MAUMBILE Upoje??? mbona NYUKI wanatupatia UTAMU mpaka WARINA ASALI wasitake kujua mtengenezaji??

Najua unanogea+mate yanatoka=urudi nyumbani

najua kabisa unanogea, najua nakupatia HAMU. maana najua bila hamu huwezi kukumbuka kitu. Hawa siyo sawa na dagaa kigoma wanaochacha kama wa enzi zile za KIGONSERA a.k.a CAIGO BOYS, umenisoma kaka Mtanga ha ha ha ha Nina HAMU ndiyo ndiyo maana nakwambia haya. Watazame walivyoanikwa mchangani vizuri halafu unapata NG'ONDA upo hapo. RUDI NYUMBANI ha ha ha ha ha