tunavua hivi na tunafanya hivi kama tupendavyo. kazi ipooooooooo
December 30, 2008
wazee wa kazi ndiyo zetu
Madhumuni
kumbukumbu,
Nyasa,
zana
December 29, 2008
nini msingi wa IMANI?
Nilidhani sitoweza kublogu karibuni sababu ya HAMU ya kumngoja dadangu Yasinta, lakini naona kama nilivyosema kwamba blogu ni kitulizo cha moyo wangu. Najua dada Yasinta akija mambo poa.
LAKINI
Baada ya kusoma mambo kadhaa kuhusu imani zetu, nimeona niwasilishe swali katika kijiwe chetu cha MASWALI MAGUMU- Yasinta, Bwaya, Mzee wa changamoto, Simon,Kaluse,Fadhy, Fita,Mzee wa taratibu,Kalama,Markus na sasa dada Koero.
Swali hili linatokana na hoja za dada Koero Mkundi kwamba biblia ilikosewa na maoni yake kuwa hakulenga kuuponda ukristo, sawa nakubali! hasa baada ya mimi kuhoji mantiki ya injili kadhaa kuachwa ikiwemo ya 'bikira' maria.
LABDA
nilikosea kuhoji lakini nimefurahi sasa dada Koero kutukumbusha mambo kadhaa kuhusu imani. Mimi naona tujadili hili suala kwani hata kama tunajiona tunapoteza muda lakini lazima tujadili, lazima tujiulize kuhusu imani hizi za mashariki ya kati.
Swali lenyewe.
Je unaweza kuikana NAFSI yako katika mwenendo wako wa maisha?
Je unaweza kukubali kwamba unaongozwa na IMANI ya dini kuliko IMANI yako katika nafsi yako?
Je kwanini walisema uikane nafsi yako?
Je iwapo tunaamini kuwa kilichoandikwa ndicho, mbona kuna utamaduni wa maeneo yao husika?
Je tunaongozwa maisha yetu kwa IMANI ipi?
Je twaenenda kwa IMANI au kwa kuona?
Je nafsi zetu hazina imani thabiti?
BASI unajua nilitaka tu kijiwe cha MASWALI MAGUMU tujumuike kufundishana haya mambo hasa mimi nisiyejua kitu kwani nimekulia na kulelewa na wamisionari na kuwa na ndoto ya upadre LAKINI ikayeyuka. kwanini? kuusaka ukweli? Labda waafrika hawakuwa na IMANI ndiyo maana twaenenda kutoka mashariki ya kati.
mmmm labda nimechanganykiwa kidogo au?
LAKINI
Baada ya kusoma mambo kadhaa kuhusu imani zetu, nimeona niwasilishe swali katika kijiwe chetu cha MASWALI MAGUMU- Yasinta, Bwaya, Mzee wa changamoto, Simon,Kaluse,Fadhy, Fita,Mzee wa taratibu,Kalama,Markus na sasa dada Koero.
Swali hili linatokana na hoja za dada Koero Mkundi kwamba biblia ilikosewa na maoni yake kuwa hakulenga kuuponda ukristo, sawa nakubali! hasa baada ya mimi kuhoji mantiki ya injili kadhaa kuachwa ikiwemo ya 'bikira' maria.
LABDA
nilikosea kuhoji lakini nimefurahi sasa dada Koero kutukumbusha mambo kadhaa kuhusu imani. Mimi naona tujadili hili suala kwani hata kama tunajiona tunapoteza muda lakini lazima tujadili, lazima tujiulize kuhusu imani hizi za mashariki ya kati.
Swali lenyewe.
Je unaweza kuikana NAFSI yako katika mwenendo wako wa maisha?
Je unaweza kukubali kwamba unaongozwa na IMANI ya dini kuliko IMANI yako katika nafsi yako?
Je kwanini walisema uikane nafsi yako?
Je iwapo tunaamini kuwa kilichoandikwa ndicho, mbona kuna utamaduni wa maeneo yao husika?
Je tunaongozwa maisha yetu kwa IMANI ipi?
Je twaenenda kwa IMANI au kwa kuona?
Je nafsi zetu hazina imani thabiti?
BASI unajua nilitaka tu kijiwe cha MASWALI MAGUMU tujumuike kufundishana haya mambo hasa mimi nisiyejua kitu kwani nimekulia na kulelewa na wamisionari na kuwa na ndoto ya upadre LAKINI ikayeyuka. kwanini? kuusaka ukweli? Labda waafrika hawakuwa na IMANI ndiyo maana twaenenda kutoka mashariki ya kati.
mmmm labda nimechanganykiwa kidogo au?
Madhumuni
falsafa,
kumbukumbu,
maisha
December 27, 2008
karibu nyumbani Yasinta, nina HAMU
duuuh unajua kwanini huwa naandika sana kuhusu huyu mtu? usiulize wewe pigia tu mistari au vipi. Ni jambo jema sana kukukaribisha tena nyumbani,kunyumba, hakika ni raha sana. Nashukuru pia kwa muda wote ambao umetumia katika shajara/blogu yako maana kuna kipindi ulikuwa katika mawazo sana kama siyo MAWAZONI, ndiyo maana nilisema nitafungua MASHTAKA iwapo ungeacha kublogu. Leo nafarijika namna unavyofanya kazi njema na kuibua mada motomoto ambazo hufikirisha. Hata hivyo naamini kutokuwapo kwako hewani ni kwa muda mfupi nina hakika na naamini utarejea tena baada kula DAGAA NYASA weeeeeeee karibu kunyumba bambu likolo la manyungu, mbulika, magege,kitimoto,ULANZI, komoni, myakaya na mambo mengi sana. Karibu nyumbani jamani maskani palipali pa mfaranyaki au kubombambili mmmm kuruhuwiko kwa Matetereka? haha ha ha nina raha sana maana nyumbani ni nyumbani, wale DAGAA wamefanya kazi sana maana najua mate yamekujaa mdomoni leo. KARIBU NYUMBANI dada Yasinta lakini kumbuka mashtaka yangu ukiacha kublogu tu yapo palepale!!! Erik a.k.a spite boy + Camilla a.k.a baby boom karibuni nyumbani. PAMOJA DAIMA
Madhumuni
amani na upendo,
maisha,
Nyasa,
ughaibuni,
urafiki
Dada KOERO karibu ndani !!
Jamani eeeeeeeeeeh, sina neno ila karibu sana tena sana dada KOERO, hakika tutajenga mnara katika miamba. hakuna jambo rahisi kama kuifanya nafsi ifurahia kile unachokiona kinafaa daima. Ni jambo ambalo kila mtu anaweza kulitenda ikiwa tu anaongozwa na dhamira imara lakini ni uwezo wa kuyabadili mazingira yetu kwa wakati wetun ndiyo huu ni WAKATI WETU, TUNAWEZA HAYA TWENDA NA DADA KOERO. KARIBU NDANI katika SHAJARA wengine mnasema BLOGU poa tu.Ni mimi Markus Honorius Mpangala mvuvi wa nyasa na mnyasa wa nyasa.
December 25, 2008
wanablogu karibuni ndani
aaah si mmezoea kwenda disko, gesti ******, baa, kilabuni na mambo kadhaa kuhusu raha zetu? jamani siye tunawakaribisha hapa, ndiyop starehe zetu hizi na kipindi hiki cha sherehe za kila mwaka. wanashajara za mtandaoni karibuni ndani. Lakini kama huwezi sema tukusaidie
Madhumuni
kumbukumbu,
maisha,
Nyasa,
uzuri
December 24, 2008
waambie ROHO yangu nzuri, AMA ZANGU AMA ZAO
nashangaa wananichukia bila sababu, sijawatendea madhambi lakini wananitumia ujumbe wa simu wataniua, eeeh ongezeni juhudi sitoacha kundika kile ninacho amini tena mimi mfuasi wa MALCOM X, kwangu Martin Luther King jr siyo shujaa! naamini hivyo licha ya kukubali umahiri wake, napenda ukali wa X kwani unaonyesha msimamo siyo kupewa sifa za upole na ustaarabu, waambie ROHO ni nzuri kuliko picha. Sijawatendea madhambi nashangaa wana chuki, wanataka kunihukumu, wamefanya kikao cha kumaliza roho yangu, nasema niueni anza hata sasa mimi sitishwi kwa ujumbe mfupi wa maneno ya simu eti sitowezi kuzuia kifo, eti wataniua kwsababu zao sijui nilichowakosea lakini SITISHWI na mtu yeyote wambie AMA ZANGU AMA ZAO hiki ni kima changu ama chao iwe mtaani maskani au mahali popote pale, kwani dunia nzuri kama picha hii hutoa taswira upendo na nafasi zetu. Waambie upendo wangu haupo kwa maadui, ndiyo kwani naogopa KUFA labda sijazaliwa waambie tena na tena ukiona uzuri na upole wa picha hii utadhani hakuna SHARI. Anzeni basi, kwani HATARI KITU GANI?
kazi+kumbukumbu
ninakumbuka enzi zile tukilima mpunga, ekari kibao na shangazi yangu pale Ngindo, yaani ilikuwa tka asubuhi saa moja hadi saa kumi na moja jioni. Duuh kwa mwendo wa kuchoka na kulegea kila kitu. nipumue siku hizi huuuuuuuuuuuuuuuuuu nalima kwa kompyuta
Madhumuni
kumbukumbu,
mila na desturi,
Nyasa,
zana
Subscribe to:
Posts (Atom)