January 01, 2009

20009+ YASINTA+ Wanablogu


2009 Pamoja daima.Wanablogu wote Nawatakieni mafanikio mema zaidi.Na kudumisha maendeleo ya Blogu zetu.Nimefurahi zaidi kwani jana nilikuwa na mwanablogu dada Yasinta,na kupiga gumzo la hapa na pale.Anatuandalia kitu kingine;tanzaniaresan2009.blogspot.com
NAWATAKIA SAFARI NJEMA.
ZIDUMU BLOGU ZETU na WANABLOGU DAIMA

2009 amani iwe nanyi kama MZEE WA CHANGAMOTO

Amani Heshima na Upendo kwako ndugu. Natumai kuwa u-mwema na unamalizia mwaka vema. Basi napenda kuchukua nafasi hii kukushukuru kwa mchango wako wa namna moja ama nyingine katika nyanja hii ya blog. Uwepo wako ni muhimu sana na kwa hakika tunajifunza mengi. Natumani (pamoja na wana-changamoto wote) kuwa mwaka ujao utakuwa mwema zaidi na tutaendelea vema katika ile nia ya KUIELIMISHA, KUIBURUDISHA NA KUIKOMBOA JAMII YETU kwa kadri ya uwezo wetu.
Heri ya mwaka mpya wa 2009 toka CHANGAMOTO YETU BLOG.

Salamu zako zipo http://changamotoyetu.blogspot.com/2008/12/happy-new-year-bloggers.html

"www.changamotoyetu.blogspot.com"

December 31, 2008

Wanaopuuza shauri yao


nimesoma maoni ya Koero katika shajara/blogu ya Bwaya kuwa wapo wanaotazama blogu kama upuuzi. Nimefarijika kuona dada Koero kawagundua watu hawa lakini anawashangaa wanasoma mambo ambayo wanasema ni upuuzi. Namshukuru kwa kuwabaini LAKINI naomba uwaaambie blogu siyo upepo wa kupita, hii ni hatu nyingine zaidi ya kusoma magazeti na kuangalia luninga. Hapa hatuhitaji wahariri wakuu wala waandamizi bali nidhamu imejenngwa na mtu mwenyee. Kwa hakika watu tunajikuta tunafanya mambo ya ajabu lakini kujipa muda angalau kufanya jambo linalokufanya uwe bize na kuepusha porojo za hovyo LAKINI watu wengine hawaelewi. Jamani nia yangu ni kwamba pamoja na kwamba wanasema ni upuuzi ambao wanausoma lakini wajue kuwa blogu siyo upepo. Nashukuru dada Koero amegundua hilo maana kuna watu ukiwaeleza hili jambo wanaona kama ujinga fulani, eeeeh shauri yao wanaopuuza tunajua hawaamini kuwa wasomaji wanaweza kuwa wahariri na wahariri wanaweza kuwa wasomaji. Hivi huamini tunaishi zama zingine za teknolojia? Wape maneno yao dada Koero asante kwa kutukumbusha wanaopuuzia blogu/shajara shauri yao.

December 30, 2008

wazee wa kazi ndiyo zetu

tunavua hivi na tunafanya hivi kama tupendavyo. kazi ipooooooooo

December 29, 2008

nini msingi wa IMANI?

Nilidhani sitoweza kublogu karibuni sababu ya HAMU ya kumngoja dadangu Yasinta, lakini naona kama nilivyosema kwamba blogu ni kitulizo cha moyo wangu. Najua dada Yasinta akija mambo poa.

LAKINI
Baada ya kusoma mambo kadhaa kuhusu imani zetu, nimeona niwasilishe swali katika kijiwe chetu cha MASWALI MAGUMU- Yasinta, Bwaya, Mzee wa changamoto, Simon,Kaluse,Fadhy, Fita,Mzee wa taratibu,Kalama,Markus na sasa dada Koero.
Swali hili linatokana na hoja za dada Koero Mkundi kwamba biblia ilikosewa na maoni yake kuwa hakulenga kuuponda ukristo, sawa nakubali! hasa baada ya mimi kuhoji mantiki ya injili kadhaa kuachwa ikiwemo ya 'bikira' maria.

LABDA
nilikosea kuhoji lakini nimefurahi sasa dada Koero kutukumbusha mambo kadhaa kuhusu imani. Mimi naona tujadili hili suala kwani hata kama tunajiona tunapoteza muda lakini lazima tujadili, lazima tujiulize kuhusu imani hizi za mashariki ya kati.

Swali lenyewe.
Je unaweza kuikana NAFSI yako katika mwenendo wako wa maisha?
Je unaweza kukubali kwamba unaongozwa na IMANI ya dini kuliko IMANI yako katika nafsi yako?
Je kwanini walisema uikane nafsi yako?
Je iwapo tunaamini kuwa kilichoandikwa ndicho, mbona kuna utamaduni wa maeneo yao husika?
Je tunaongozwa maisha yetu kwa IMANI ipi?
Je twaenenda kwa IMANI au kwa kuona?
Je nafsi zetu hazina imani thabiti?

BASI unajua nilitaka tu kijiwe cha MASWALI MAGUMU tujumuike kufundishana haya mambo hasa mimi nisiyejua kitu kwani nimekulia na kulelewa na wamisionari na kuwa na ndoto ya upadre LAKINI ikayeyuka. kwanini? kuusaka ukweli? Labda waafrika hawakuwa na IMANI ndiyo maana twaenenda kutoka mashariki ya kati.
mmmm labda nimechanganykiwa kidogo au?

December 27, 2008

karibu nyumbani Yasinta, nina HAMU

duuuh unajua kwanini huwa naandika sana kuhusu huyu mtu? usiulize wewe pigia tu mistari au vipi. Ni jambo jema sana kukukaribisha tena nyumbani,kunyumba, hakika ni raha sana. Nashukuru pia kwa muda wote ambao umetumia katika shajara/blogu yako maana kuna kipindi ulikuwa katika mawazo sana kama siyo MAWAZONI, ndiyo maana nilisema nitafungua MASHTAKA iwapo ungeacha kublogu. Leo nafarijika namna unavyofanya kazi njema na kuibua mada motomoto ambazo hufikirisha. Hata hivyo naamini kutokuwapo kwako hewani ni kwa muda mfupi nina hakika na naamini utarejea tena baada kula DAGAA NYASA weeeeeeee karibu kunyumba bambu likolo la manyungu, mbulika, magege,kitimoto,ULANZI, komoni, myakaya na mambo mengi sana. Karibu nyumbani jamani maskani palipali pa mfaranyaki au kubombambili mmmm kuruhuwiko kwa Matetereka? haha ha ha nina raha sana maana nyumbani ni nyumbani, wale DAGAA wamefanya kazi sana maana najua mate yamekujaa mdomoni leo. KARIBU NYUMBANI dada Yasinta lakini kumbuka mashtaka yangu ukiacha kublogu tu yapo palepale!!! Erik a.k.a spite boy + Camilla a.k.a baby boom karibuni nyumbani. PAMOJA DAIMA

Dada KOERO karibu ndani !!

Jamani eeeeeeeeeeh, sina neno ila karibu sana tena sana dada KOERO, hakika tutajenga mnara katika miamba. hakuna jambo rahisi kama kuifanya nafsi ifurahia kile unachokiona kinafaa daima. Ni jambo ambalo kila mtu anaweza kulitenda ikiwa tu anaongozwa na dhamira imara lakini ni uwezo wa kuyabadili mazingira yetu kwa wakati wetun ndiyo huu ni WAKATI WETU, TUNAWEZA HAYA TWENDA NA DADA KOERO. KARIBU NDANI katika SHAJARA wengine mnasema BLOGU poa tu.

Ni mimi Markus Honorius Mpangala mvuvi wa nyasa na mnyasa wa nyasa.