Uzuri, Maudhui na Mandhari ya maeneo ya milima ya kaskazini mwa mbamba bay. yaani toka maeneo ya Kilosa, Matenje, Kwambe, Ng'ombo, Chamate, Linda, na mengineyo. Miinuko na vilimaJanuary 03, 2009
Mandhari na Maudhui
Uzuri, Maudhui na Mandhari ya maeneo ya milima ya kaskazini mwa mbamba bay. yaani toka maeneo ya Kilosa, Matenje, Kwambe, Ng'ombo, Chamate, Linda, na mengineyo. Miinuko na vilimaJanuary 01, 2009
20009+ YASINTA+ Wanablogu
2009 Pamoja daima.Wanablogu wote Nawatakieni mafanikio mema zaidi.Na kudumisha maendeleo ya Blogu zetu.Nimefurahi zaidi kwani jana nilikuwa na mwanablogu dada Yasinta,na kupiga gumzo la hapa na pale.Anatuandalia kitu kingine;tanzaniaresan2009.blogspot.com
NAWATAKIA SAFARI NJEMA.
ZIDUMU BLOGU ZETU na WANABLOGU DAIMA
Madhumuni
Hisia za moyo,
kumbukumbu,
maisha,
mapumziko,
mila na desturi,
urafiki,
zana
2009 amani iwe nanyi kama MZEE WA CHANGAMOTO
Amani Heshima na Upendo kwako ndugu. Natumai kuwa u-mwema na unamalizia mwaka vema. Basi napenda kuchukua nafasi hii kukushukuru kwa mchango wako wa namna moja ama nyingine katika nyanja hii ya blog. Uwepo wako ni muhimu sana na kwa hakika tunajifunza mengi. Natumani (pamoja na wana-changamoto wote) kuwa mwaka ujao utakuwa mwema zaidi na tutaendelea vema katika ile nia ya KUIELIMISHA, KUIBURUDISHA NA KUIKOMBOA JAMII YETU kwa kadri ya uwezo wetu.
Heri ya mwaka mpya wa 2009 toka CHANGAMOTO YETU BLOG.
Salamu zako zipo http://changamotoyetu.blogspot.com/2008/12/happy-new-year-bloggers.html
"www.changamotoyetu.blogspot.com"
Heri ya mwaka mpya wa 2009 toka CHANGAMOTO YETU BLOG.
Salamu zako zipo http://changamotoyetu.blogspot.com/2008/12/happy-new-year-bloggers.html
"www.changamotoyetu.blogspot.com"
December 31, 2008
Wanaopuuza shauri yao

nimesoma maoni ya Koero katika shajara/blogu ya Bwaya kuwa wapo wanaotazama blogu kama upuuzi. Nimefarijika kuona dada Koero kawagundua watu hawa lakini anawashangaa wanasoma mambo ambayo wanasema ni upuuzi. Namshukuru kwa kuwabaini LAKINI naomba uwaaambie blogu siyo upepo wa kupita, hii ni hatu nyingine zaidi ya kusoma magazeti na kuangalia luninga. Hapa hatuhitaji wahariri wakuu wala waandamizi bali nidhamu imejenngwa na mtu mwenyee. Kwa hakika watu tunajikuta tunafanya mambo ya ajabu lakini kujipa muda angalau kufanya jambo linalokufanya uwe bize na kuepusha porojo za hovyo LAKINI watu wengine hawaelewi. Jamani nia yangu ni kwamba pamoja na kwamba wanasema ni upuuzi ambao wanausoma lakini wajue kuwa blogu siyo upepo. Nashukuru dada Koero amegundua hilo maana kuna watu ukiwaeleza hili jambo wanaona kama ujinga fulani, eeeeh shauri yao wanaopuuza tunajua hawaamini kuwa wasomaji wanaweza kuwa wahariri na wahariri wanaweza kuwa wasomaji. Hivi huamini tunaishi zama zingine za teknolojia? Wape maneno yao dada Koero asante kwa kutukumbusha wanaopuuzia blogu/shajara shauri yao.
December 30, 2008
wazee wa kazi ndiyo zetu
Madhumuni
kumbukumbu,
Nyasa,
zana
December 29, 2008
nini msingi wa IMANI?
Nilidhani sitoweza kublogu karibuni sababu ya HAMU ya kumngoja dadangu Yasinta, lakini naona kama nilivyosema kwamba blogu ni kitulizo cha moyo wangu. Najua dada Yasinta akija mambo poa.
LAKINI
Baada ya kusoma mambo kadhaa kuhusu imani zetu, nimeona niwasilishe swali katika kijiwe chetu cha MASWALI MAGUMU- Yasinta, Bwaya, Mzee wa changamoto, Simon,Kaluse,Fadhy, Fita,Mzee wa taratibu,Kalama,Markus na sasa dada Koero.
Swali hili linatokana na hoja za dada Koero Mkundi kwamba biblia ilikosewa na maoni yake kuwa hakulenga kuuponda ukristo, sawa nakubali! hasa baada ya mimi kuhoji mantiki ya injili kadhaa kuachwa ikiwemo ya 'bikira' maria.
LABDA
nilikosea kuhoji lakini nimefurahi sasa dada Koero kutukumbusha mambo kadhaa kuhusu imani. Mimi naona tujadili hili suala kwani hata kama tunajiona tunapoteza muda lakini lazima tujadili, lazima tujiulize kuhusu imani hizi za mashariki ya kati.
Swali lenyewe.
Je unaweza kuikana NAFSI yako katika mwenendo wako wa maisha?
Je unaweza kukubali kwamba unaongozwa na IMANI ya dini kuliko IMANI yako katika nafsi yako?
Je kwanini walisema uikane nafsi yako?
Je iwapo tunaamini kuwa kilichoandikwa ndicho, mbona kuna utamaduni wa maeneo yao husika?
Je tunaongozwa maisha yetu kwa IMANI ipi?
Je twaenenda kwa IMANI au kwa kuona?
Je nafsi zetu hazina imani thabiti?
BASI unajua nilitaka tu kijiwe cha MASWALI MAGUMU tujumuike kufundishana haya mambo hasa mimi nisiyejua kitu kwani nimekulia na kulelewa na wamisionari na kuwa na ndoto ya upadre LAKINI ikayeyuka. kwanini? kuusaka ukweli? Labda waafrika hawakuwa na IMANI ndiyo maana twaenenda kutoka mashariki ya kati.
mmmm labda nimechanganykiwa kidogo au?
LAKINI
Baada ya kusoma mambo kadhaa kuhusu imani zetu, nimeona niwasilishe swali katika kijiwe chetu cha MASWALI MAGUMU- Yasinta, Bwaya, Mzee wa changamoto, Simon,Kaluse,Fadhy, Fita,Mzee wa taratibu,Kalama,Markus na sasa dada Koero.
Swali hili linatokana na hoja za dada Koero Mkundi kwamba biblia ilikosewa na maoni yake kuwa hakulenga kuuponda ukristo, sawa nakubali! hasa baada ya mimi kuhoji mantiki ya injili kadhaa kuachwa ikiwemo ya 'bikira' maria.
LABDA
nilikosea kuhoji lakini nimefurahi sasa dada Koero kutukumbusha mambo kadhaa kuhusu imani. Mimi naona tujadili hili suala kwani hata kama tunajiona tunapoteza muda lakini lazima tujadili, lazima tujiulize kuhusu imani hizi za mashariki ya kati.
Swali lenyewe.
Je unaweza kuikana NAFSI yako katika mwenendo wako wa maisha?
Je unaweza kukubali kwamba unaongozwa na IMANI ya dini kuliko IMANI yako katika nafsi yako?
Je kwanini walisema uikane nafsi yako?
Je iwapo tunaamini kuwa kilichoandikwa ndicho, mbona kuna utamaduni wa maeneo yao husika?
Je tunaongozwa maisha yetu kwa IMANI ipi?
Je twaenenda kwa IMANI au kwa kuona?
Je nafsi zetu hazina imani thabiti?
BASI unajua nilitaka tu kijiwe cha MASWALI MAGUMU tujumuike kufundishana haya mambo hasa mimi nisiyejua kitu kwani nimekulia na kulelewa na wamisionari na kuwa na ndoto ya upadre LAKINI ikayeyuka. kwanini? kuusaka ukweli? Labda waafrika hawakuwa na IMANI ndiyo maana twaenenda kutoka mashariki ya kati.
mmmm labda nimechanganykiwa kidogo au?
Madhumuni
falsafa,
kumbukumbu,
maisha
Subscribe to:
Posts (Atom)
