Jamani natumaini hamjambo woteeeeeee wa kijiwe cha maswali magumu. Nipo kamili tena nazidi kuwakilisha kama kawaida.
Nadhani wengine mlikuwa mnangoja kujua labda tulipiga gumzo gani na dada Yasinta. Bila shaka mambo ya wanablogu yanafurahisha sana na utamu wa mashairi kama kaka Fadhy poa sana.
Katika kupiga gumzo na dada Yasinta, kuna jambo amenifanya nitafakari sana na wakati mwingine huwa najiuliza nianze vipi.
Gumzo la kawaida kuhusu mambo ya teknolojia, blogu na maisha kama ilivyoblogu yake. Jambo lenyewe linahusu VITABU. Nilimkuta kashika kalamu ya wino anaandika, nikauliza kulikoni mwenzetu huchoki? Akatabasamu na kusema 'kutafakari jambo muhimu lazima uandike ukizingatia kuandika ni jambo muhimu pia". Hapo gumzo likazama kuhusu vitabu maana kama ajuavyo napenda kuandika vitabu kuhusu jamii yetu.
Nadhani wengine mlikuwa mnangoja kujua labda tulipiga gumzo gani na dada Yasinta. Bila shaka mambo ya wanablogu yanafurahisha sana na utamu wa mashairi kama kaka Fadhy poa sana.
Katika kupiga gumzo na dada Yasinta, kuna jambo amenifanya nitafakari sana na wakati mwingine huwa najiuliza nianze vipi.
Gumzo la kawaida kuhusu mambo ya teknolojia, blogu na maisha kama ilivyoblogu yake. Jambo lenyewe linahusu VITABU. Nilimkuta kashika kalamu ya wino anaandika, nikauliza kulikoni mwenzetu huchoki? Akatabasamu na kusema 'kutafakari jambo muhimu lazima uandike ukizingatia kuandika ni jambo muhimu pia". Hapo gumzo likazama kuhusu vitabu maana kama ajuavyo napenda kuandika vitabu kuhusu jamii yetu.
Lakini alikuja na swali hili: "Kwanini huandiki vitabu kama unaweza? Si ni jambo la kukaa na kutafakari tu kisha unaandika kwa uamkini?akaongeza, Au hakuna soko la Vitabu? Basi andika vitabu vya wototo, haiwezekani?"
sijui kama mnanielewa ninachotaka kukisema? Ni jambo la kujiuliza sna katika jamii zetu kwani waandishi wa vitabu wanapotea, wengi waliopo wanaandike vile ambavyo vinadumu kwa muda mfupi.
Ni vigumu kupata vitabu kama RAI YA JENERALI, MAKUADI WA SOKO HURIA achilia mbali vile vya Issa Shivji{mwaka jana katoa Pan africanism or Pragmatism?} kizuri. Kwa kweli dada Yasinta kanipandisha moli kama wamasai.
Ndiyo maana nilisema katika maoni yangu fulani kama Simon Kitururu anapaswa kuandika vitabu vya falsafa, Fadhy naye awe Shaban Robert wetu, mzee wa changamoto nye awepo, dada Koero kama vile kitabu cha THINK BIG{umekisoma?}, Bwaya, Kaluse, Kalama tuleteeni UTAMBUZI wenu jamani. Ni hayo tu


