Nikupe mchapo? Wanawake nao WAMO sijui ndiyo wanaume tumewajuza au la. Wenyewe wanasema hakuna wanaume waoaji siku hizi. Lakini ukiwauliza wanasema wanaume ni kama mbwa eti tunawinda sana akina dada duh!
Duh! huku wenyewe wakishikiria nadharia yao kuwa siku hizi lazima uwe na wanaume (wapenzi) wawili (nazungumzia wale wasio na ndoa). Mmoja wanampenda sana na wapili wanamgeuza machimbo ya Mwadui-Shinyanga. Wanamchimba dhahabu halafu yule wa kwanza ananufaika shauri mwanamke anampatia mavuno ya mwadui.
Eti! weee! Markus utanipeleka wapi wakati unafikiria maisha? Unajua wazee hawana noma yaani ukitaka mkwanja wanakata tu, si unamuona yule nanii alikuwa anataka kununua gari?.....nikajibu namfahamu.... ' sasa sikiliza kile kibabu pale kilikuwa kikimtaka... akamweleza mbona mwenzangu una gari nami nataka lakini nina hela kidogo niongezee basi?
Duuh! kile kibabu kikasema nitakupa milioni tano na hizo 15 tafuta mwenyewe.
Aisee! basi yule dada alikuwa na mpenzi wake akampa habari ya kununua gari, jamaa anazo bwana akamwongezea milioni 5. Unaona? lakini nakwambia kile kibabu kimesotea 'kupata' tena 'kikapewa' siku moja tu, si unajua anaye mtu wake? kwahiyo inabidi kuwa na wawili ili mambo yakae sawa!
Wee mngoni, mmm tena mnyasa utanipeleka wapi wewe? acha bwana tafuta maisha Markus usihangaike nasi, wazia maisha kakangu eeeehee! Siku hizi wanawake tunao wapenzi wawili wawili ili kuweka 'mambo sawa', maana maisha yenyewe haya mmmm, utawehuka achana na soga zetu nenda ukasoma magazeti na vitabu vyako sivipendi kabisa halafu wewe mwanaume muda wote vitabu, ungekuwa 'wangu' nakwambia 'utapata' hivyo vitabu na magazeti nyooo lionee ha ha ha ha ha ha ha ha.
Mnyasa nikasema! Eee wala waungwana kumbe wanawake wamo! hamuogopi ukimwi ninyi? eeeeh kwaheri waungwana
January 08, 2009
Wanawake nao WAMO!!!
Maisha! maisha! maisha
Duhh! jamani wakati fulani pale mji wa Mzuzu-Malawi, nilijiuliza mambo kadhaa kuhusu maisha yetu. Samahani usiwaambie uhamiaji kama situmii pasipoti wala mayai visa, maana wale ni ndugu zetu bwana tunalonga kinyanja na kuingia kwa mitumbwi poa. Haya maisha ya Bongo na kule naweza kusema aheri kwetu japo kwa sumuni. Jamani nakumbuka baadhi ya vijiji au mitaani tu wapo wanaoamini Wabongo maisha tunapeta, lakini sote tunajua kinachoendelea. Sasa kwa kawaida huwa najiuliza sana maisha yetu hapa kijijini Lundu na haya ya ndugu zangu wa damu kule Mzuzu na maeneo mengine! Jamani maisha! maisha! maisha! maisha! maisha! maisha!January 07, 2009
Koero: Maoni yako yananitekenya sana
Rafiki yangu anisomaye sana kaanieleza dada Koero kaweka maoni matamu sana, yanahuzunisha na kufikirisha sana. Nisomapo maoni yako dada Koero yananitekenya sana najiuliza maswali kadhaa ikiwemo Je tutaweza kuibadilisha jamii hii? Je tutaweza kuwafanya watu watamani kusoma vitabu? Nikamkumbuka rafiki yangu Ezdeny Jumanne aliwahi kuweka vijisenti katika kitabu cha How to be Brilliant, akakisahau mahali ambapo alikaa binti fulani lakini wala hakushughulika mpaka tuliporejea na kukitwaa kisha kumweleza mbona anaacha japo hela ya soda? akastaajabu, tukamwonyesha vile visenti akajilaumu sana na kusema kwa utani 'ningejua nakwambia msingekikuta' ..... lakini rafiki yangu Ezdeny Jumanne akasema 'ukitaka kuficha hata hela tu, basi weka kitabuni mbongo hatajua kabisa" Maneno haya yananikumbusha maneno ya kaka Bwaya na wengine LAKINI maoni ya dada Koero yamenitekenya sana na kukumbuka miswada yangu ya 1. LAZIMA UNIOE na 2. TAIFA MOJA, MTAZAMO MMOJA? jamani nimeona niyaweke maoni yake hapa bila kuhariri lolote, nimeyapenda yananigusa kila kona ya mwili DUUH!!!!
Koero Mkundi said...
Kuandika vitabu sawa, lakini wasomaji wapo?
T
atizo ninaloliona ni kwamba watanzania hawapendi kusomavitabu, naomba nikiri hilo, ajitokeze mtu anibishie.
sisi tumekuwa ni jamii ya kupiga majungu, fitna, uwongo, kusengenyana na kuhujumiana.
Tumekuwa ni wavivu wa kufikiri, na hatuko tayari kuongeza maarifa, utakuta mtu kama amesomea mambo ya sheria au udaktari basi yeye na taaluma yake hiyo hiyo hahitaji kuongeza chochote wala kusoma maarifa ya wengine ili kupanua wigo wake wa uelewa, hana muda huo, sana sana labda atazungumzia siasa basi kamaliza.
magazeti yanayopendwa ni ya udaku yale ya hard news hayananafasi na ndio maana yanachechemea, watu hawataki kuyasoma.
Ndio sababu waandishi wengi mahiri hawaandiki tena.
Wako wapi kina Kajubi Mukajanga, Elvis Musiba, Penina Mhando, na wengine nimewasahau.
nashukuru baba yangu alitujengea utamaduni wa kupenda kusoma vitabu mbali mbali bila kuchagua.
06 January, 2009
Koero Mkundi said...
Kuandika vitabu sawa, lakini wasomaji wapo?
T
atizo ninaloliona ni kwamba watanzania hawapendi kusomavitabu, naomba nikiri hilo, ajitokeze mtu anibishie.
sisi tumekuwa ni jamii ya kupiga majungu, fitna, uwongo, kusengenyana na kuhujumiana.
Tumekuwa ni wavivu wa kufikiri, na hatuko tayari kuongeza maarifa, utakuta mtu kama amesomea mambo ya sheria au udaktari basi yeye na taaluma yake hiyo hiyo hahitaji kuongeza chochote wala kusoma maarifa ya wengine ili kupanua wigo wake wa uelewa, hana muda huo, sana sana labda atazungumzia siasa basi kamaliza.
magazeti yanayopendwa ni ya udaku yale ya hard news hayananafasi na ndio maana yanachechemea, watu hawataki kuyasoma.
Ndio sababu waandishi wengi mahiri hawaandiki tena.
Wako wapi kina Kajubi Mukajanga, Elvis Musiba, Penina Mhando, na wengine nimewasahau.
nashukuru baba yangu alitujengea utamaduni wa kupenda kusoma vitabu mbali mbali bila kuchagua.
06 January, 2009
Madhumuni
falsafa,
kumbukumbu,
urafiki
January 06, 2009
Vipi unatuonaje, angalia tena
kama napumzika na kazi ya uvuvi yaani unajipa maraha kama haya! taratiiiiiiiiibu kinyasa nyasa siyo mchezo mambo haya.
Madhumuni
kumbukumbu,
mila na desturi,
uzuri,
zana
January 05, 2009
Gumzo letu na dada Yasinta
Jamani natumaini hamjambo woteeeeeee wa kijiwe cha maswali magumu. Nipo kamili tena nazidi kuwakilisha kama kawaida.
Nadhani wengine mlikuwa mnangoja kujua labda tulipiga gumzo gani na dada Yasinta. Bila shaka mambo ya wanablogu yanafurahisha sana na utamu wa mashairi kama kaka Fadhy poa sana.
Katika kupiga gumzo na dada Yasinta, kuna jambo amenifanya nitafakari sana na wakati mwingine huwa najiuliza nianze vipi.
Gumzo la kawaida kuhusu mambo ya teknolojia, blogu na maisha kama ilivyoblogu yake. Jambo lenyewe linahusu VITABU. Nilimkuta kashika kalamu ya wino anaandika, nikauliza kulikoni mwenzetu huchoki? Akatabasamu na kusema 'kutafakari jambo muhimu lazima uandike ukizingatia kuandika ni jambo muhimu pia". Hapo gumzo likazama kuhusu vitabu maana kama ajuavyo napenda kuandika vitabu kuhusu jamii yetu.
Nadhani wengine mlikuwa mnangoja kujua labda tulipiga gumzo gani na dada Yasinta. Bila shaka mambo ya wanablogu yanafurahisha sana na utamu wa mashairi kama kaka Fadhy poa sana.
Katika kupiga gumzo na dada Yasinta, kuna jambo amenifanya nitafakari sana na wakati mwingine huwa najiuliza nianze vipi.
Gumzo la kawaida kuhusu mambo ya teknolojia, blogu na maisha kama ilivyoblogu yake. Jambo lenyewe linahusu VITABU. Nilimkuta kashika kalamu ya wino anaandika, nikauliza kulikoni mwenzetu huchoki? Akatabasamu na kusema 'kutafakari jambo muhimu lazima uandike ukizingatia kuandika ni jambo muhimu pia". Hapo gumzo likazama kuhusu vitabu maana kama ajuavyo napenda kuandika vitabu kuhusu jamii yetu.
Lakini alikuja na swali hili: "Kwanini huandiki vitabu kama unaweza? Si ni jambo la kukaa na kutafakari tu kisha unaandika kwa uamkini?akaongeza, Au hakuna soko la Vitabu? Basi andika vitabu vya wototo, haiwezekani?"
sijui kama mnanielewa ninachotaka kukisema? Ni jambo la kujiuliza sna katika jamii zetu kwani waandishi wa vitabu wanapotea, wengi waliopo wanaandike vile ambavyo vinadumu kwa muda mfupi.
Ni vigumu kupata vitabu kama RAI YA JENERALI, MAKUADI WA SOKO HURIA achilia mbali vile vya Issa Shivji{mwaka jana katoa Pan africanism or Pragmatism?} kizuri. Kwa kweli dada Yasinta kanipandisha moli kama wamasai.
Ndiyo maana nilisema katika maoni yangu fulani kama Simon Kitururu anapaswa kuandika vitabu vya falsafa, Fadhy naye awe Shaban Robert wetu, mzee wa changamoto nye awepo, dada Koero kama vile kitabu cha THINK BIG{umekisoma?}, Bwaya, Kaluse, Kalama tuleteeni UTAMBUZI wenu jamani. Ni hayo tu
January 03, 2009
Mandhari na Maudhui
Uzuri, Maudhui na Mandhari ya maeneo ya milima ya kaskazini mwa mbamba bay. yaani toka maeneo ya Kilosa, Matenje, Kwambe, Ng'ombo, Chamate, Linda, na mengineyo. Miinuko na vilima
Subscribe to:
Posts (Atom)