Jana niliandika kuhusu huduma ya Aggregators/Bloglines kisha nikasema unaweza kurahisisha mambo kwa huduma hizo. Lakini nikatoa anuani ya kusoma zaidi mambo hayo ya www.mwongozo.wordpress.com Sasa leno niseme hii CO.MMENTS na BLOGLINES pia. Huduma ya CO.MMENTS ni tamu sana, nayo inakuletea habari mpya kuhusu maoni uliyoyaacha mahali/katika blogu uliyoacha MAONI.
Huduma hii inachofanya ni kukupa taarifa mpya toka sehemu ulizoacha maoni, mfano umetembelea blogu ya Koero kisha ukaacha maoni wakati huohuo unataka kujua wasomaji au wanablogu wengine watasema nini juu ya maoni uliyotoa, kawaida unachofanya ni kurudi pale ulipoacha maoni ya wengine kuendeleza mjadala.
CO.MMENTS inakusanya maoni yote mapya toka mijadala unayoshiriki na kukuletea katika akaunti yako. Kwetu TZ tunajua baadhi yetu tunategemea huduma za kulipia kwahiyo suala la MUDA ni muhimu sana, kwani unaweza kutembelea blogu 25 halafu hazina mambo mapya.
Huduma ya CO.MMENTS na BLOGLINES zinakusaidia kukusanya habari mpya na MAONI mapya toka kwenye idadi yoyote unayotaka hata 100 na kukuletea katika ukurasa mmoja.
Sasa hii huduma ya CO.MMENTS inakupatia fursa ya kujua blogu zote ulizopitia na kuacha MAONI wapo wasomaji au wanablogu wamechangia, kwahiyo maoni yao yanakuwa yanakusubiri uyasome ili kuendeleza mjadala.
Binafsi nimejaribu hiyo, na napata taarifa za maoni katika akaunti yangu kila ninapoacha maoni mapya katika blogu yoyote, na nimeanzia kwa dada Koero na mengine nitayapata. NB: ili kujiunga na huduma hii unajiunga na BLOGLINES kwa urahisi hapa www.mwongozo.wordpress.com nyingi sana kuhusu huduma hizo.
January 11, 2009
CO.MMENTS + BLOGLINES= mambo mapya
January 10, 2009
Aggregators+Bloglines =vikusanya habari
AGGREGATORS: ni moya teknolojia tunazoziita teknolojia za kutunza muda. Vikusanya habari vinatunza muda kwa kutuwezesha kujua BLOGU zipi zimeandika habari mpya/mambo mapya badala ya kuzitembelea BLOGU moja moja. Inawezekana pia ukatumia vikusanya habari kupata habari toka katika tovuti mbalimbali za habari na siyo BLOGU pekee.
Huduma ya AGGREGATORS ni kama huduma ya BLOGLINES, inachofanya ni kukusanya habari toka kwenye blogu mbalimbali unazozipenda na kuzileta katika ukurasa mmoja.
KAWAIDA; ukitaka kusoma blogu upendeleayo unachofanya ni kuzitembelea kwa kuandika anuani zake.
Lakini unaweza kutembelea blogu 10 halafu hazina habari mpya. Sasa hii BLOGLINES inakuletea mambo mapya yaliyoandikwa katika blogu uzipendazo. Fungua blogu yako ingia halafu bonyeza LAYOUT ili kuongeza ukurasa mwingine uupendao. Utaona orodha ya kurasa ambazo ungependa ziwepo, ndipo utakuta BLOGLIST bonyeza halafu utaona neno ADD kisha andika blogu unayoipenda kusoma habari zake. Sasa hapo kichwa cha habari kimeandikwa MY BLOGLIST unaweza kubadili kama ambavyo nimefanya, mfano: mimi nimeandika kikusanya habari(tazama kulia kwa blogu yangu).
Unaweza pia kusoma hapa; www.mwongozo.wordpress.com
NB ukiwa na tatizo, ni vema tukatafutana ukipenda, napatikana Sinza Kijweni ofisi za New Habari house siku za jumamosi ni poa sana
Huduma ya AGGREGATORS ni kama huduma ya BLOGLINES, inachofanya ni kukusanya habari toka kwenye blogu mbalimbali unazozipenda na kuzileta katika ukurasa mmoja.
KAWAIDA; ukitaka kusoma blogu upendeleayo unachofanya ni kuzitembelea kwa kuandika anuani zake.
Lakini unaweza kutembelea blogu 10 halafu hazina habari mpya. Sasa hii BLOGLINES inakuletea mambo mapya yaliyoandikwa katika blogu uzipendazo. Fungua blogu yako ingia halafu bonyeza LAYOUT ili kuongeza ukurasa mwingine uupendao. Utaona orodha ya kurasa ambazo ungependa ziwepo, ndipo utakuta BLOGLIST bonyeza halafu utaona neno ADD kisha andika blogu unayoipenda kusoma habari zake. Sasa hapo kichwa cha habari kimeandikwa MY BLOGLIST unaweza kubadili kama ambavyo nimefanya, mfano: mimi nimeandika kikusanya habari(tazama kulia kwa blogu yangu).
Unaweza pia kusoma hapa; www.mwongozo.wordpress.com
NB ukiwa na tatizo, ni vema tukatafutana ukipenda, napatikana Sinza Kijweni ofisi za New Habari house siku za jumamosi ni poa sana
January 08, 2009
Wanawake nao WAMO!!!
Nikupe mchapo? Wanawake nao WAMO sijui ndiyo wanaume tumewajuza au la. Wenyewe wanasema hakuna wanaume waoaji siku hizi. Lakini ukiwauliza wanasema wanaume ni kama mbwa eti tunawinda sana akina dada duh!
Duh! huku wenyewe wakishikiria nadharia yao kuwa siku hizi lazima uwe na wanaume (wapenzi) wawili (nazungumzia wale wasio na ndoa). Mmoja wanampenda sana na wapili wanamgeuza machimbo ya Mwadui-Shinyanga. Wanamchimba dhahabu halafu yule wa kwanza ananufaika shauri mwanamke anampatia mavuno ya mwadui.
Eti! weee! Markus utanipeleka wapi wakati unafikiria maisha? Unajua wazee hawana noma yaani ukitaka mkwanja wanakata tu, si unamuona yule nanii alikuwa anataka kununua gari?.....nikajibu namfahamu.... ' sasa sikiliza kile kibabu pale kilikuwa kikimtaka... akamweleza mbona mwenzangu una gari nami nataka lakini nina hela kidogo niongezee basi?
Duuh! kile kibabu kikasema nitakupa milioni tano na hizo 15 tafuta mwenyewe.
Aisee! basi yule dada alikuwa na mpenzi wake akampa habari ya kununua gari, jamaa anazo bwana akamwongezea milioni 5. Unaona? lakini nakwambia kile kibabu kimesotea 'kupata' tena 'kikapewa' siku moja tu, si unajua anaye mtu wake? kwahiyo inabidi kuwa na wawili ili mambo yakae sawa!
Wee mngoni, mmm tena mnyasa utanipeleka wapi wewe? acha bwana tafuta maisha Markus usihangaike nasi, wazia maisha kakangu eeeehee! Siku hizi wanawake tunao wapenzi wawili wawili ili kuweka 'mambo sawa', maana maisha yenyewe haya mmmm, utawehuka achana na soga zetu nenda ukasoma magazeti na vitabu vyako sivipendi kabisa halafu wewe mwanaume muda wote vitabu, ungekuwa 'wangu' nakwambia 'utapata' hivyo vitabu na magazeti nyooo lionee ha ha ha ha ha ha ha ha.
Mnyasa nikasema! Eee wala waungwana kumbe wanawake wamo! hamuogopi ukimwi ninyi? eeeeh kwaheri waungwana
Duh! huku wenyewe wakishikiria nadharia yao kuwa siku hizi lazima uwe na wanaume (wapenzi) wawili (nazungumzia wale wasio na ndoa). Mmoja wanampenda sana na wapili wanamgeuza machimbo ya Mwadui-Shinyanga. Wanamchimba dhahabu halafu yule wa kwanza ananufaika shauri mwanamke anampatia mavuno ya mwadui.
Eti! weee! Markus utanipeleka wapi wakati unafikiria maisha? Unajua wazee hawana noma yaani ukitaka mkwanja wanakata tu, si unamuona yule nanii alikuwa anataka kununua gari?.....nikajibu namfahamu.... ' sasa sikiliza kile kibabu pale kilikuwa kikimtaka... akamweleza mbona mwenzangu una gari nami nataka lakini nina hela kidogo niongezee basi?
Duuh! kile kibabu kikasema nitakupa milioni tano na hizo 15 tafuta mwenyewe.
Aisee! basi yule dada alikuwa na mpenzi wake akampa habari ya kununua gari, jamaa anazo bwana akamwongezea milioni 5. Unaona? lakini nakwambia kile kibabu kimesotea 'kupata' tena 'kikapewa' siku moja tu, si unajua anaye mtu wake? kwahiyo inabidi kuwa na wawili ili mambo yakae sawa!
Wee mngoni, mmm tena mnyasa utanipeleka wapi wewe? acha bwana tafuta maisha Markus usihangaike nasi, wazia maisha kakangu eeeehee! Siku hizi wanawake tunao wapenzi wawili wawili ili kuweka 'mambo sawa', maana maisha yenyewe haya mmmm, utawehuka achana na soga zetu nenda ukasoma magazeti na vitabu vyako sivipendi kabisa halafu wewe mwanaume muda wote vitabu, ungekuwa 'wangu' nakwambia 'utapata' hivyo vitabu na magazeti nyooo lionee ha ha ha ha ha ha ha ha.
Mnyasa nikasema! Eee wala waungwana kumbe wanawake wamo! hamuogopi ukimwi ninyi? eeeeh kwaheri waungwana
Maisha! maisha! maisha
Duhh! jamani wakati fulani pale mji wa Mzuzu-Malawi, nilijiuliza mambo kadhaa kuhusu maisha yetu. Samahani usiwaambie uhamiaji kama situmii pasipoti wala mayai visa, maana wale ni ndugu zetu bwana tunalonga kinyanja na kuingia kwa mitumbwi poa. Haya maisha ya Bongo na kule naweza kusema aheri kwetu japo kwa sumuni. Jamani nakumbuka baadhi ya vijiji au mitaani tu wapo wanaoamini Wabongo maisha tunapeta, lakini sote tunajua kinachoendelea. Sasa kwa kawaida huwa najiuliza sana maisha yetu hapa kijijini Lundu na haya ya ndugu zangu wa damu kule Mzuzu na maeneo mengine! Jamani maisha! maisha! maisha! maisha! maisha! maisha!January 07, 2009
Koero: Maoni yako yananitekenya sana
Rafiki yangu anisomaye sana kaanieleza dada Koero kaweka maoni matamu sana, yanahuzunisha na kufikirisha sana. Nisomapo maoni yako dada Koero yananitekenya sana najiuliza maswali kadhaa ikiwemo Je tutaweza kuibadilisha jamii hii? Je tutaweza kuwafanya watu watamani kusoma vitabu? Nikamkumbuka rafiki yangu Ezdeny Jumanne aliwahi kuweka vijisenti katika kitabu cha How to be Brilliant, akakisahau mahali ambapo alikaa binti fulani lakini wala hakushughulika mpaka tuliporejea na kukitwaa kisha kumweleza mbona anaacha japo hela ya soda? akastaajabu, tukamwonyesha vile visenti akajilaumu sana na kusema kwa utani 'ningejua nakwambia msingekikuta' ..... lakini rafiki yangu Ezdeny Jumanne akasema 'ukitaka kuficha hata hela tu, basi weka kitabuni mbongo hatajua kabisa" Maneno haya yananikumbusha maneno ya kaka Bwaya na wengine LAKINI maoni ya dada Koero yamenitekenya sana na kukumbuka miswada yangu ya 1. LAZIMA UNIOE na 2. TAIFA MOJA, MTAZAMO MMOJA? jamani nimeona niyaweke maoni yake hapa bila kuhariri lolote, nimeyapenda yananigusa kila kona ya mwili DUUH!!!!
Koero Mkundi said...
Kuandika vitabu sawa, lakini wasomaji wapo?
T
atizo ninaloliona ni kwamba watanzania hawapendi kusomavitabu, naomba nikiri hilo, ajitokeze mtu anibishie.
sisi tumekuwa ni jamii ya kupiga majungu, fitna, uwongo, kusengenyana na kuhujumiana.
Tumekuwa ni wavivu wa kufikiri, na hatuko tayari kuongeza maarifa, utakuta mtu kama amesomea mambo ya sheria au udaktari basi yeye na taaluma yake hiyo hiyo hahitaji kuongeza chochote wala kusoma maarifa ya wengine ili kupanua wigo wake wa uelewa, hana muda huo, sana sana labda atazungumzia siasa basi kamaliza.
magazeti yanayopendwa ni ya udaku yale ya hard news hayananafasi na ndio maana yanachechemea, watu hawataki kuyasoma.
Ndio sababu waandishi wengi mahiri hawaandiki tena.
Wako wapi kina Kajubi Mukajanga, Elvis Musiba, Penina Mhando, na wengine nimewasahau.
nashukuru baba yangu alitujengea utamaduni wa kupenda kusoma vitabu mbali mbali bila kuchagua.
06 January, 2009
Koero Mkundi said...
Kuandika vitabu sawa, lakini wasomaji wapo?
T
atizo ninaloliona ni kwamba watanzania hawapendi kusomavitabu, naomba nikiri hilo, ajitokeze mtu anibishie.
sisi tumekuwa ni jamii ya kupiga majungu, fitna, uwongo, kusengenyana na kuhujumiana.
Tumekuwa ni wavivu wa kufikiri, na hatuko tayari kuongeza maarifa, utakuta mtu kama amesomea mambo ya sheria au udaktari basi yeye na taaluma yake hiyo hiyo hahitaji kuongeza chochote wala kusoma maarifa ya wengine ili kupanua wigo wake wa uelewa, hana muda huo, sana sana labda atazungumzia siasa basi kamaliza.
magazeti yanayopendwa ni ya udaku yale ya hard news hayananafasi na ndio maana yanachechemea, watu hawataki kuyasoma.
Ndio sababu waandishi wengi mahiri hawaandiki tena.
Wako wapi kina Kajubi Mukajanga, Elvis Musiba, Penina Mhando, na wengine nimewasahau.
nashukuru baba yangu alitujengea utamaduni wa kupenda kusoma vitabu mbali mbali bila kuchagua.
06 January, 2009
Madhumuni
falsafa,
kumbukumbu,
urafiki
January 06, 2009
Vipi unatuonaje, angalia tena
kama napumzika na kazi ya uvuvi yaani unajipa maraha kama haya! taratiiiiiiiiibu kinyasa nyasa siyo mchezo mambo haya.
Madhumuni
kumbukumbu,
mila na desturi,
uzuri,
zana
January 05, 2009
Gumzo letu na dada Yasinta
Jamani natumaini hamjambo woteeeeeee wa kijiwe cha maswali magumu. Nipo kamili tena nazidi kuwakilisha kama kawaida.
Nadhani wengine mlikuwa mnangoja kujua labda tulipiga gumzo gani na dada Yasinta. Bila shaka mambo ya wanablogu yanafurahisha sana na utamu wa mashairi kama kaka Fadhy poa sana.
Katika kupiga gumzo na dada Yasinta, kuna jambo amenifanya nitafakari sana na wakati mwingine huwa najiuliza nianze vipi.
Gumzo la kawaida kuhusu mambo ya teknolojia, blogu na maisha kama ilivyoblogu yake. Jambo lenyewe linahusu VITABU. Nilimkuta kashika kalamu ya wino anaandika, nikauliza kulikoni mwenzetu huchoki? Akatabasamu na kusema 'kutafakari jambo muhimu lazima uandike ukizingatia kuandika ni jambo muhimu pia". Hapo gumzo likazama kuhusu vitabu maana kama ajuavyo napenda kuandika vitabu kuhusu jamii yetu.
Nadhani wengine mlikuwa mnangoja kujua labda tulipiga gumzo gani na dada Yasinta. Bila shaka mambo ya wanablogu yanafurahisha sana na utamu wa mashairi kama kaka Fadhy poa sana.
Katika kupiga gumzo na dada Yasinta, kuna jambo amenifanya nitafakari sana na wakati mwingine huwa najiuliza nianze vipi.
Gumzo la kawaida kuhusu mambo ya teknolojia, blogu na maisha kama ilivyoblogu yake. Jambo lenyewe linahusu VITABU. Nilimkuta kashika kalamu ya wino anaandika, nikauliza kulikoni mwenzetu huchoki? Akatabasamu na kusema 'kutafakari jambo muhimu lazima uandike ukizingatia kuandika ni jambo muhimu pia". Hapo gumzo likazama kuhusu vitabu maana kama ajuavyo napenda kuandika vitabu kuhusu jamii yetu.
Lakini alikuja na swali hili: "Kwanini huandiki vitabu kama unaweza? Si ni jambo la kukaa na kutafakari tu kisha unaandika kwa uamkini?akaongeza, Au hakuna soko la Vitabu? Basi andika vitabu vya wototo, haiwezekani?"
sijui kama mnanielewa ninachotaka kukisema? Ni jambo la kujiuliza sna katika jamii zetu kwani waandishi wa vitabu wanapotea, wengi waliopo wanaandike vile ambavyo vinadumu kwa muda mfupi.
Ni vigumu kupata vitabu kama RAI YA JENERALI, MAKUADI WA SOKO HURIA achilia mbali vile vya Issa Shivji{mwaka jana katoa Pan africanism or Pragmatism?} kizuri. Kwa kweli dada Yasinta kanipandisha moli kama wamasai.
Ndiyo maana nilisema katika maoni yangu fulani kama Simon Kitururu anapaswa kuandika vitabu vya falsafa, Fadhy naye awe Shaban Robert wetu, mzee wa changamoto nye awepo, dada Koero kama vile kitabu cha THINK BIG{umekisoma?}, Bwaya, Kaluse, Kalama tuleteeni UTAMBUZI wenu jamani. Ni hayo tu
Subscribe to:
Posts (Atom)