Gumzo lilikolea si haba, tukajiburudisha kwa utani wa hapa na pale. Lakini jambo la msingi ni matumizi ya blogu katika kuelemisha na kuwa na marafiki zaidi. Sasa gumzo lilipokolea ilibidi mambo ya teknolojia yaanze kujadiliwa. Mosi ilikuwa huduma poa ya NeoWORX Widgets.
Huduma hii inakuwezesha mambo mengi ikiwemo kujua idadi ya watembeleaji, hali ya hewa, picha na mambo mengine. Hii inamaana pamoja na Free NeoCounter (wageni wanaoitembelea blogu yako), NeoBoard, NeoEarth (hali ya hewa ya mahali unapotaka), NeoPod, NeoFlags( ukipenda bendera mbalimbali ziwepo katika blogu yako), NeoPlanet (mambo ya sayari) na NeoKube.
Huduma hizo ni pamoja na zile za malipo na za bure, sasa kama tunavyojua kwamba blogu zetu zinazidi kupewa kipaumbele kwani zote hizi nia yao ni kuboresha zaidi. Sasa gumzo na mseto wa mazungumzo ilikuwa huduma hizi, lakini binafsi bado najifunza hazijakaa kwenye medulla sawasawa ndiyo maana kuna NeoCounter pekee. Basi bwana Klayson akahoji huduma za bure huzipendi, ikabidi nimweleze mimi bado najifunza hizo kwahiyo polepole.
Mambo ya blogu zetu siku hizi ni mengi huduma ni nyingi mno ambazo Wanablogu inabidi tuzitumie, pia ipo ya Feedbliz , hii ni huduma ambayo kila unachoandika unawatumia wasomaji katika akaunti zao, hivyo wao huingia moja kwa moja kukuta mjadala uliowasilishwa au habari/picha. Hata hivyo ahadi zetu ni kwamba huduma hizi tutaweza kuzitumia iwapo tutajipa muda kuzielewa umuhimu wake. Blogu ni mambo yanayokwenda na mabadiliko sana kwani tayari wataalamu wamebaini siyo upepo wa kupita. Kivumbi cha Gaza blogu zimeweka video, picha na habari motomoto ambazo hutumiwa na mashirika kama BBC, DW, AP, Skynews n.k jamani blogu ni teknolojia ambayo sijui magazeti itakuwaje tuendako maana Thomas Friedman anasemaje katika kitabu chake 'The World is Flat', yanawezekana, AMKA anza WEWE ili tuibadili jamii. Gumzo lilikuwa tamu sana aiseh
January 17, 2009
Mseto,Teknolojia na Yasinta+Klayson
Madhumuni
amani na upendo,
kumbukumbu,
soga,
ughaibuni,
zana
January 12, 2009
nakumbuka sana mambo haya
Huwa nawaona wengi wakiwa katika mazingira haya hapa kwetu nyasa, huwa nakumbuka mengi nikiona namna hii. Nayakumbuka aina ya maisha niliyokulia na kushuhudia mambo haya. Nilidhani ni kawaida lakini siku hizi huwa naumia sana kumbe haikuwa kwaajili yao bali sote bila kujali nasaba zetu. Nawaza sana Lakini sijui jawabu lake labda kuna siku nitawasaidia. Nimeirudisha picha baada ya kujaribu kutafakari ni picha ipi bora kwangu kwa mwaka 2008. Nimeichagua hii nimekulia mazingira ya aina hii hapa kijijini kwetu Lundu maeneo ya nyasa.
January 11, 2009
CO.MMENTS + BLOGLINES= mambo mapya
Jana niliandika kuhusu huduma ya Aggregators/Bloglines kisha nikasema unaweza kurahisisha mambo kwa huduma hizo. Lakini nikatoa anuani ya kusoma zaidi mambo hayo ya www.mwongozo.wordpress.com Sasa leno niseme hii CO.MMENTS na BLOGLINES pia. Huduma ya CO.MMENTS ni tamu sana, nayo inakuletea habari mpya kuhusu maoni uliyoyaacha mahali/katika blogu uliyoacha MAONI.
Huduma hii inachofanya ni kukupa taarifa mpya toka sehemu ulizoacha maoni, mfano umetembelea blogu ya Koero kisha ukaacha maoni wakati huohuo unataka kujua wasomaji au wanablogu wengine watasema nini juu ya maoni uliyotoa, kawaida unachofanya ni kurudi pale ulipoacha maoni ya wengine kuendeleza mjadala.
CO.MMENTS inakusanya maoni yote mapya toka mijadala unayoshiriki na kukuletea katika akaunti yako. Kwetu TZ tunajua baadhi yetu tunategemea huduma za kulipia kwahiyo suala la MUDA ni muhimu sana, kwani unaweza kutembelea blogu 25 halafu hazina mambo mapya.
Huduma ya CO.MMENTS na BLOGLINES zinakusaidia kukusanya habari mpya na MAONI mapya toka kwenye idadi yoyote unayotaka hata 100 na kukuletea katika ukurasa mmoja.
Sasa hii huduma ya CO.MMENTS inakupatia fursa ya kujua blogu zote ulizopitia na kuacha MAONI wapo wasomaji au wanablogu wamechangia, kwahiyo maoni yao yanakuwa yanakusubiri uyasome ili kuendeleza mjadala.
Binafsi nimejaribu hiyo, na napata taarifa za maoni katika akaunti yangu kila ninapoacha maoni mapya katika blogu yoyote, na nimeanzia kwa dada Koero na mengine nitayapata. NB: ili kujiunga na huduma hii unajiunga na BLOGLINES kwa urahisi hapa www.mwongozo.wordpress.com nyingi sana kuhusu huduma hizo.
Huduma hii inachofanya ni kukupa taarifa mpya toka sehemu ulizoacha maoni, mfano umetembelea blogu ya Koero kisha ukaacha maoni wakati huohuo unataka kujua wasomaji au wanablogu wengine watasema nini juu ya maoni uliyotoa, kawaida unachofanya ni kurudi pale ulipoacha maoni ya wengine kuendeleza mjadala.
CO.MMENTS inakusanya maoni yote mapya toka mijadala unayoshiriki na kukuletea katika akaunti yako. Kwetu TZ tunajua baadhi yetu tunategemea huduma za kulipia kwahiyo suala la MUDA ni muhimu sana, kwani unaweza kutembelea blogu 25 halafu hazina mambo mapya.
Huduma ya CO.MMENTS na BLOGLINES zinakusaidia kukusanya habari mpya na MAONI mapya toka kwenye idadi yoyote unayotaka hata 100 na kukuletea katika ukurasa mmoja.
Sasa hii huduma ya CO.MMENTS inakupatia fursa ya kujua blogu zote ulizopitia na kuacha MAONI wapo wasomaji au wanablogu wamechangia, kwahiyo maoni yao yanakuwa yanakusubiri uyasome ili kuendeleza mjadala.
Binafsi nimejaribu hiyo, na napata taarifa za maoni katika akaunti yangu kila ninapoacha maoni mapya katika blogu yoyote, na nimeanzia kwa dada Koero na mengine nitayapata. NB: ili kujiunga na huduma hii unajiunga na BLOGLINES kwa urahisi hapa www.mwongozo.wordpress.com nyingi sana kuhusu huduma hizo.
Subscribe to:
Posts (Atom)