April 16, 2009

Yasinta+Wanablogu= MIMI NABISHA

Nilikuwa napitia mada mbalimbali ambazo nimezikosa tokana na kutokaa sana mtandaoni. Nimevutiwa na mada ya dada Yasinta kuhusu mapenzi. mada hiyo kilichonikuna ni maoni ya Prof. Mbele. kwamba tunatakiwa kutafakari kwa kina namna ambavyo tunaiga kila kitu. Kama ambavyo ameandika makala yake katika gazeti la KWANZA Jamii

Amejaribu kuhoji maendeleo ni nini na kwanini tunakubali kuitwa nchi zinazoendelea. Kimsingi kama ambavyo NABISHA kwamba magaidi pekee hawakulipua WTC mwaka 2001 bali kuna mambo yanaendelea.

Sasa katika maoni hayo nakubali kwamba yeye kama mimi nimekulia kijijini na nawaza kwa msingi wa kijijini, mtakumbuka niliwahi kundika kwamba ndege wangu amepotea. Hoja kuu ni yale yale ya kuonyeshana mbele za watu kwamba mnapendana, inawezekana kweli lakini sioni mantiki wala ulazima kama kuiga kila jambo toka kwa wazungu.

Nitaishi hivyo hata kama wapenzi wataona wamekutana mhafidhina kama rafiki zangu wanavyoniita daima. Kikubwa ni kwamba sisi kama binadamu lazaima tuwe na njia halisi za kuishi kama sisi. Lazima tukubaliane kwamba UTAMBUZI ni soma muhimu sana. ndiyo maana tunajiuliza sisi ni nani??????????? Ikiwa kama ambavyo dada Koero alivyosema kwamba siku hizi tunaiga kila kitu, nakubaliana naye akumbuke kwamba HAKUNA MTU ANAYEWEZA KUFANYA NGONO KIZUNGU au hakuna anayeweza kucheka kizungu bali utacheka kama wewe ulivyo siyo wao walivyo. Tabia hii ya kuiga kwamba ni lazima kama mwenzako anahuzuni kimapenzi umfariji imeshamiri lakini haina sababu za kutokea kwake zaidi ya kuiga tu. kuna mambo yanatia KINYAA namna ambavyo tunaiga. Naamini ipo siku tutaanza KUNYA, KUTAPIKA, KULEWA, KUOGA, KUKIMBIA kizungu tena kama akina BUSH, BLAIR nk.

Lakini msingi huo wa kuiga unatokana na HULKA ambayo tunajijengea kwamba kizazi chetu chenye kuhoji ukweli kinataka hata akiwa tegemezi kwa wazazi yaani awe na miaka 17 au 20 anataka kuleta boyfriend wake au girlfriend wake nyumbani kwa wazaziwe. AJABU hivi haya ndiyo mambo tunayoyataka au ni nini? Kuiga mambo ya kijinga kama hayo au kudai kwamba kumpenda mtu kwa dhati unapaswa kuonyesha hadharani huo ni UBATILI. Kumpenda mtu kwa dhati wala hakuambatani na KULAMBANA mitaani au kujidekeza eti uhudumiwe na mpenzio kwakuwa aonyeshe anakujali. Hivi unadhani kukujali kwa kuzoa matapishi ni lazima iwe mapenzini?? Usimfanye mtu kuwa kila kitu kwako maana siku akiondoka hutakiwa na kitu!!!

Nina mengi ya kuwajuza walimwengu, naweza kuongeza hata ujinga halafu nikashindwa kujieleza vema. HEKO mzee MBELE kwa kuonyesha uhalisia, ndiyo maana nahoji hata mantiki ya ndoa zilizopo hapa duniani kwa kisiingizo kwamba kilichofungwa na mungu binadamu asitenganishe halafu anayesema maneno hayo ni binadamu mwenzio ha ha ha ha ha ha ha ha nicheke mieeeeee.
Nini kudekadeka bwana, nini ulindwe na mwanaume bwana, jilinde mwenyewe, nini kufunguliwa mlango na mwanaume???? kwani wewe umekuwa kiwete??? nini kushikwa kiunoni bwana mbele za watu, kwani huko vyumbani hakutoshi????? kwani nini washkaji??? ha ha ha ha ha a ha ha ha nawaza tu
Msikilizeni sana EMINEM hasa pale asemapo katika wimbo wake wa JUST LOSE IT halafu niambieni yule jamaa kwanini alikuwa akiishi na vitoto ndani.

ha ha ha ha ha ha leo nimeamua kuwaza zaidi. haya mawazo tu wala msikasilike washikaji maana wakati mwingine NAFYATUKA na KUBWATA. ha ha ha ha ha ha ha ha ha ooooooooooiiiiiiiiiiioooooooooo ngoja nikavue mjanhahali ndo msimu wake huu bwana.
karibuni nyasa

HATIMAYE: Wamefika nyasa, wamefika Mbamba bay

Wamisionari,watawa au tuseme watu wa dini au vipi? lakini kumbuka usiwe na kicheko kile cha nyege za kutaka kujua kulikoni lakini tulia tu nikuhabarishe mambo ya nyasa. Chipole kuna sekondari inaitwa St Agnes ni shule ya watawa wale nadhani ni pamoja na wale wa Wabendictino wa Peramiho( dada Yasinta, sahihisha).

Wamekwisha kutua Mbamba bay na hii ndiyo hoteli yao ambayo inatwa MBAMBA BAY HOTEL. Nakumbuka yupo dada Anna pale tuliyecheza naye enzi za Mwalimu, enzi za wewe baba na mimi mama au vipi? lakini siku hizi najua amesahau hakumbuki shauri kavaa utawa jamani duuh!1 sasa habari yenyewe ndiyo hiyo kwamba wameanzisha hii hoteli au shirika la utawa ambalo ni shemu ya Chipole.
haya wageni na wwale wasiojua kuogelea na wanaogopa kama dada Yasinta(eti anaogopa mamba) Karibuni sana. tovuti yao http://www.chipolestagnes.org/ (kama sijakosea0.picha kwa hisani yao