nilipotea kidogo, lakini nilikabiliwa na kikao kizito na muhimu zaidi kuhusu NYASA. Nambukuka mwanzoni mwa mwaka huu mzee wangu Profesa Joseph L.Mbele alinishauri kuhusu kuandika kitabu kuhusu nyasa. Nililipokea wazo lake kwa mikono miwili huku rafiki yangu koero akisisitiza jambo hilo.
Hata hivyo naweka wazi kwasasa kuna kikao kizito kuhusu nyasa, kikao ambacho kinaendeshwa na wanafunzi wa vyuo vikuu ambao wametoka katika ukanda wa nyasa. Kikao hicho kinazungumziaq maendeleo ya maeneo hayo na namna ya kuanzisha umoja ambao utawezesha jamii za nyasa kielimu,siasa, na uchumi. Jambo hili nashukuru linafanyika huku wazo la mzee Mbele likiwa mezani kwangu.
Jumapili iliyopita kulikuwa na kikao hicho, tulijaribu kuweka ama kuorodhesha kero na mambo mazuri ambayo nyasa tunayo na tunaweza kuwafaidisha wakazi wake. kikao hicho naweza kukiita NYASA DEVELOPMENT ORGANISATION. ni wazo ambalo tumeamua kwa moyo mmoja kujitolea kwa kuanzisha kikundi hiki kwa nia ya kuendeleza wananchi wa amaeneo yetu.
Kikao hiki cha kwanza kimefanyika huku wahudhuriaji wake ni BARAKA WANDAWANDA, HELLEN LOCHI. LAWRENCE EMANUEL, BONIFACE MNDALA, EMMANUEL NAMINGA, RICHARD MWANJA, VENANT KATOPOLANGA, SIMON HARRISON, FRANK NDOMBA, FRANK MAPUNDA, na LIBADA MAPUNDA pamoja na MARKUS HONORIUD MPANGALA.
Sisi siyo mwsho bali wenzetu wengine walikabiliwa na majukumu ya chuo, kwahiyo tunaamini kikao kijacho cha jumapili wiki hii kitakwenda katika mpangalio uleule. jitihada ni kubwa na ari yetu ni kubwa sana kwani kikundi hiki kinaundwa na vijana ambao wastani wa umri wetu ni chini ya 25. Tumedhamiria na tunahakika lengo letu litafanikiwa.
Mipango yetu ikiwa katika njia sahihi nitawahabarisha zaidi ili mjue dhamira yetu watoto wa kinyasa kuwa tunataka kufanya nini katika ukanda wetu na watu wetu. Kundi hili linakaribisha mwanachama yeyote ambaye anaweza kukiboresha na kusaidia mambo mbalimbali hususan mchango wa mawazo ambao ni muhimu sana. Vilevile ingawa ni suala binafsi sana lakini nawaomba Raiton Mbele(Ukraine), Robert Ngalomba(UK) na mzee wangu Mbele kuwa mchango wenu ni muhimu sana. Yasinta Ngonyani(sweden) nawe pia tunaamini kuwa upo pamoja nasi. Pia Mzee wangu Prof Mbele ningependa na nitakupendekeza uwe mlezi wetu iwapo nafasi itakuruhusu kwani mchango wako ni muhimu sana. Jumapili iyajo(juma hili) tunakikao cha pili ili kufikia maazimio yetu.
Tunakaribisha kila ya aina ya mawazo yenu wanablogu wote bila kujali ukanda wala mahali ulipotolea bali tunachofanya ni kujaribu kuwezesha jamii zetu. Sasa ninajikita katika kujitolea kwa jamii rasmi bila malipo. Tunawakaribisha sana nyasa.
May 21, 2009
Kikao cha Dharura kuhusu NYASA
Madhumuni
amani na upendo,
habari,
kumbukumbu,
Nyasa,
urafiki
May 16, 2009
HAPPY BIRTHDAY MARKUS II
Nawashukuru wanablogu wenzangu, nawashukuru kwa kila namna yaani hadi chozi linadondoka, nawakumbuka zaidi ninyi kwani mnanifanya nijue kwamba wapo watu wanaonijali zaidi. Koero Mkundi uko wapi mziwanda wangu?, u hali gani huko mafichoni??????
Amini upendo mtamu
kama salamu tamu
kwakoFadhy wangu
Wanipa hamu hamu
Mtanga wangu, asante daima
Uso wapwita chozi,rabana ajua
Nionacho, u mwanamalenga
Hakika nakusujudia
Dhima yako idumu,milele
Maisha yangu kama tetere
Naishi bila kelele,nisonge mbele
U wapi koero wangu
U wapi pacha wangu
Kilio waona humu?
Nione kwa tonge au saumu.
Asante Changamoto, nipo mjini
jogoo la shamba mie,siwiki mjini
mtandaoni nipo,mjini nyingi dili
asilani sitokwacha,niamini
Nawasalimu kwa hamu
sina simile wala gubu
Nawapenda ninyi,mdumu
sijafunga kufuli,mlango u wazi
Jasho la majukumu, lakula muda bloguni
Wape hi Marekani na mashariki ya mbali
Waambie bongo twaishi mambo ni shwari
Asante Yasinta,kwa siku yangu
Kumbukumbu najivunia wangu
Usijali tupo sawi,tudumu
Asantedada weshi, ukarimu udumu
Usumbufu ulokubali,kunikirimu
Ahadi yetu itadumu,daima idumu
mungu mkubwa waungwana
Nimetembelea maduka ya vitabu pale Afrikasana kwa dada Weshi Lema kisha akanipeleka Mikocheni pale mtaa wa Regent, nikajipatia kitabu cha "PESA NA MAWE" kitabu kizuri nimekipenda, nashukuru kwa wote mliopo nami kwa kila dakika, kaka Simon mkodo Kitururu naamini tuko pamoja daima.
Nawashukuru nyote nawapendeni sana, hata kama sijakutaja najua hapa ................................. utaandika jina lako.
Dada Yasinta kwa kila dakika ya kunijulia hali na kujua siku yangu nashukuru sana. Digna, Manka na wengine. Nawapenda sana, upendo utadumu kama samaki na maji ingawa malaria yalinisumbua lakini sikuacha kwenda dukani kujinunulia kitabu. nitaandika kile nilichojifunza baada ya kwenda katika maduka hayo na ukweli wetu watanzania.
Madhumuni
amani na upendo,
kumbukumbu,
ughaibuni,
urafiki,
uzuri
Subscribe to:
Posts (Atom)