May 24, 2009

NYASA DEVELOPMENT ORGANISATION

Nilikuwa nimebanwa kidogo na semina za Freddy Macha, nikashindwa kuandika hapa, lakini nashukuru mungu nimerudi tena.
Ndugu zangu kimsingi jumuiya yetu hii ya Nyasa development organisation inaundwa na sisi vijana ambao kwa wastani kwa umri ni chini ya 27, tupo katika masomo tofauti kuanziia sheria, siasa, ustawi wa jamii, elimu, sanaa, kompyuta, na mambo mbalimbali yanayohusu elimu yetu.


Mradi huu ni ubunifu wetu kwamba kwa kiasi gani tunaweza kuibadili hali ya nyasa au maeneo yaliyopo katika jimbo la mbinga magharibi? hili lilikuwa swali kubwa sana kwetu, lilikuwa jukumu ambalo kama wanadamu tunapaswa kukabiliana nalo. kundi letu linaundwa na wanafunzi toka chuo kikuu cha dodoma, dar es salaam, IFM, na vingine vingi tu. kwani dhamira yetu ni kuwakusanya wenzetu ambao hawakuhudhuria awali tunaamini kuwa mchango wao ni muhimu sana,


Leo ni kikao cha pili, mazimio yatafikiwa na nitayaweka hapa. Tukumbuke huu ni mradi wa kujitolea, tumeamua kutumia nafasi tuliyopewa katika elimu na nchi yetu ili kuyabadili mazingira yetu. Mara nyingi namkumbuika sana Ndesanjo Macha, huwa nasisistiza kuwa ukitaka kuleta mapinduzi katika nyanja za kimaendeleo basi anza mwenyewe kwa kubadili sura ya mtaa wenu. Hilo ndilo lengo letu sisi vijana, maana tunaamini ni jukumu letu kuyaweka mapinduzi ya maendeleo katika ukanda wetu na hakika tuna dhamira kubwa sana, pia blogu yangu itakupasha mambo yote yanapohusu mradi huu na ikibidi kuanzisha blogu nyingine kama kutakuwa na umuhimu huo tutafanya hivyo mara mradi huu ukikaa ukiwa katika mhimili wake.


Nashukuru maoni ya mzee wangu Prof Mbele, kwa hakika umenipa faraja kubwa na kuona kwamba wapowatu wanaojali hali za wengine katika maisha. TUMEAMUA KWA DHATI, NA LEO HII NINAVYOANDIKA HAPA KUNA KIKAO KINGINE ILI KUIPANGA MIKAKATI ENDELEVU. tunakaribisha mawazo yenu ni muhimu sana.
kama unapenda kuwasiliana moja kwa moja na kiongozi wetu AMBROCE NKWERA, simu yake ni hii hapa 255-712514078, mawasiliano mengine tutayaweka hapa au niandikie katika barua pepe, lundunyasa@yahoo.com au jikomboe@gmail.com .
Leo ni kikao cha pili saa tisa katika ukumbu wa NewVenus pale mtaa wa Relini Tataba jirani na ofisi za gazeti la Mwananchi. KARIBUNI

May 21, 2009

Kikao cha Dharura kuhusu NYASA

nilipotea kidogo, lakini nilikabiliwa na kikao kizito na muhimu zaidi kuhusu NYASA. Nambukuka mwanzoni mwa mwaka huu mzee wangu Profesa Joseph L.Mbele alinishauri kuhusu kuandika kitabu kuhusu nyasa. Nililipokea wazo lake kwa mikono miwili huku rafiki yangu koero akisisitiza jambo hilo.

Hata hivyo naweka wazi kwasasa kuna kikao kizito kuhusu nyasa, kikao ambacho kinaendeshwa na wanafunzi wa vyuo vikuu ambao wametoka katika ukanda wa nyasa. Kikao hicho kinazungumziaq maendeleo ya maeneo hayo na namna ya kuanzisha umoja ambao utawezesha jamii za nyasa kielimu,siasa, na uchumi. Jambo hili nashukuru linafanyika huku wazo la mzee Mbele likiwa mezani kwangu.

Jumapili iliyopita kulikuwa na kikao hicho, tulijaribu kuweka ama kuorodhesha kero na mambo mazuri ambayo nyasa tunayo na tunaweza kuwafaidisha wakazi wake. kikao hicho naweza kukiita NYASA DEVELOPMENT ORGANISATION. ni wazo ambalo tumeamua kwa moyo mmoja kujitolea kwa kuanzisha kikundi hiki kwa nia ya kuendeleza wananchi wa amaeneo yetu.

Kikao hiki cha kwanza kimefanyika huku wahudhuriaji wake ni BARAKA WANDAWANDA, HELLEN LOCHI. LAWRENCE EMANUEL, BONIFACE MNDALA, EMMANUEL NAMINGA, RICHARD MWANJA, VENANT KATOPOLANGA, SIMON HARRISON, FRANK NDOMBA, FRANK MAPUNDA, na LIBADA MAPUNDA pamoja na MARKUS HONORIUD MPANGALA.

Sisi siyo mwsho bali wenzetu wengine walikabiliwa na majukumu ya chuo, kwahiyo tunaamini kikao kijacho cha jumapili wiki hii kitakwenda katika mpangalio uleule. jitihada ni kubwa na ari yetu ni kubwa sana kwani kikundi hiki kinaundwa na vijana ambao wastani wa umri wetu ni chini ya 25. Tumedhamiria na tunahakika lengo letu litafanikiwa.

Mipango yetu ikiwa katika njia sahihi nitawahabarisha zaidi ili mjue dhamira yetu watoto wa kinyasa kuwa tunataka kufanya nini katika ukanda wetu na watu wetu. Kundi hili linakaribisha mwanachama yeyote ambaye anaweza kukiboresha na kusaidia mambo mbalimbali hususan mchango wa mawazo ambao ni muhimu sana. Vilevile ingawa ni suala binafsi sana lakini nawaomba Raiton Mbele(Ukraine), Robert Ngalomba(UK) na mzee wangu Mbele kuwa mchango wenu ni muhimu sana. Yasinta Ngonyani(sweden) nawe pia tunaamini kuwa upo pamoja nasi. Pia Mzee wangu Prof Mbele ningependa na nitakupendekeza uwe mlezi wetu iwapo nafasi itakuruhusu kwani mchango wako ni muhimu sana. Jumapili iyajo(juma hili) tunakikao cha pili ili kufikia maazimio yetu.
Tunakaribisha kila ya aina ya mawazo yenu wanablogu wote bila kujali ukanda wala mahali ulipotolea bali tunachofanya ni kujaribu kuwezesha jamii zetu. Sasa ninajikita katika kujitolea kwa jamii rasmi bila malipo. Tunawakaribisha sana nyasa.