Pamoja na harakati au mchakamchaka wa maisha na shule kunibana kwa mitihani miiiiiiiiingiiiiii, lakini sijaweka kando jambo hili. Ninaye mkononi Yasser Arafat nakula nondo zake, najielimisha. Lakini bado kitabu cha Prof Mbele ninahamu nacho sana tena sana.Sasa nadhani mambo ya mzee wangu Freddy Macha na semina za ujuzi zimekwisha, nimefaidika nimejifunza, tunmeongea mengi, tukafurahi na kupiga gumzo la hapa na pale. Vilevile mkononi ninaye TOM CLANCY katika THE CARDINAL OF THE KREMLIN. haya msije mkasema nimeacha kuvua samaki na kuvamia kusoma. Mimi na samaki ni kama mizizi na ardhi. KOERO mwana wa MKUNDI upo hai au umekumbwa na KIDELI maana siku hizi duuuh! haya mambo ya aiseh! ha ha ha ha
