September 15, 2009

KARIBUNI NYASA, KARIBUNI SAMAKI

Basi nikamwambia unataka kufahamu chakula nikipendacho zaidi? Hakuna kingine zaidi ya UGALI WA MUHOGO kwa smaki aina ya KAMBALE.... nikaona anacheka,,,, tena kwa harara utadhani amekamata lile jani au ile pombe mashuhuri hapa nyasa ya Myakaya. ha ha ha ha basi nikamkumbusha wale samaki aina ya MAGEGE nikamwambia utaniambia nini masika ifikapo? Nikajikumbusha raha za mji wangu niupendao wa LUNDU, nikamwambia naridhika na kutulia sana nikiwa hapa, nikamweleza zaidi kuwa labda anipeleke MBEYA mahali pengine ninapopapenda zaidi... halafu na pengine ni pale jijini LILONGWE kule kwa asili ya akina MPANGALA, kwa wajomba na mababu zetu, napazimia sana napahusudu sana mahali pale, vipi ile klabu ya soka ya Sivo service United huishangilii wewe?

Mi naihusudu bwana, si unaona ilivyojipangia mikakati? Halafu siku ile pale ulinizome ilipofungwa na MTL Wanderers, we haya tu bwana...... eti akacheka kwa mikogo ati. Ngoja na Mbinga magharibi sasa kuna mchakato wa kuifanya Mbinga magharibi kuwa wilaya rasmi.

Najua watagombania kati ya LIULI, MBAMB BAY na LITUHI wapi waweke makao makuu. Maana hata wiki jana nilikuwa na rafiki yangu kipenzi Raymond Ndomba..... kijana mcheza soka ninayemshangaa.... anaweza kucheza namba yoyote utakayo mpanga uwanjani tangu golikipa hadi winga wa kushoto....lakini shule imemfanya awekeze huko.......na sasa anawania kupata nini kile kinaitwa MASTERS. Huyu alinidokeza kuwa wazo la makao makuu la Wilaya Mbinga magharibi litakuwa shubiri maana kila mji unapenda iwe hivyo...nadhani LIULI wanaweza kupendelewa eti ni katikati ya wilaya yenyewe.

Tuache hayo, twende katika samaki wetu hawa watamu sana na adhimu duniani. Ni nyasa bwana wapi kwingineko utakako pata samaki hawa, ha ha ha ha raha sana. KARIBUNI NYASA, KARIBUNI SANA lakini neno langu siyo sheria au vipi waungwana? Pendaneni kwa mpango!

NKATA BAY: Bandari salama, lakini.....

Ha ha ha ha ha ha! Nayakumbuka niliyopita hadi kufikia uamuzi wa kuomba mnisamehe niliowakosea. Najua mapitio yale yalikwaza ndiyo maana simulizi ni nyingi hadi zikanifikia.........au vipi Babu? ha ha ha Pouwa ha ha ha ha ha ndiyo maana nimesema sina elimu ya FALAKI! Eeeehh! najua hayanihusu, nisielewe sana bureeeee!!!!!

Nkata Bay ni moja ya bandari iliyopo kaskazini kabisa mwa Malawi, ukiangalia pichani unaona Mv Ilala ikiwa bandarini. Kwa maana hiyo basi unaweza kujenga picha fulani kuwa ni eneo ambalo halina bandari nzuri ama kubwa kama ya Mtwara ama Lindi. Ni kweli, nilifika bandarini hapo kwa mara ya kwanza 1999 na mara ya pili ilikuwa mwaka 2oo1. Wakati huo tuliambiwa marekebisho makubwa yanakuja kwajili ya kuboresha huduma zake.

Hii ilitokana na suala la biashara kati ya TZ na Malawi. Lakini wakti huo kulikuwa na uongozi wa Rais Muluzi ambaye siyo siri aliwapenda na kuwapendelea sana waTZ, hilo lipo wazi kabisaaaaaaa. Lakini baada ya kuingia Rais Bingu wa Mutharika, mwanablogu mahiri tu ingawa ni mwanasiasa nakiongozi wa nchi, upendeleo ule umetoweka na hata wafanya biashara waliokuwa wakitumia sana usafiri wa meli wamepungua kama siyo kwisha.

Mv Ilala ni kubwa sana, kuna wakati kulikuwa na matatizo kwani bidhaa zilikuwa adimu huku meli likiwatia nanga Mbamba Bay ikiwa na mzigo kidogo. Hii yote ni kwasababu ya ujio wa Rais mwanablogu Bingu wa Mutharika. Simlaumu kwa lengo lake la kujenga uzalendo wa nchi yake.

Nkata Bay tatizo lake ni swa na pale bandari ya Manda, kwani kwa mujibu wa wachunguzi inadaiwa kuwa kuna miamba mingi chini ya maji-na sifa yake kubwa ni kina kirefu. Kwa uapnde wa TZ tunaringa kwa kuwa na maziwa mengi, lakini Malawi wanalitumia ziwa hilo kwa umakini sana, ukifika pale bandari ya Chilumba wanavua kwa zana za kisasa, na sheria kuhusu uhai wa samaki unalindwa sana.
Wavuvi wameelimishwa ipasavyo wanaelewa umuhimu wa kutunza mazingira na kuvua samaki bora.

Nkata Bay ni pazuri kama mji na bandari inapswa kuwa nzuri zaidi licha ya uzuri, changamoto kubwa kwetu ni TZ ni kuiboresha bandari ya Mbamba Bay au Liuli maana ile ya Chiwanda tuliambiwa mbali na hakuna kina kirefu, kweli nimeshuhudia hali ile na kuna upepo mkali sana ukielekea kijiji cha Kwambe ambapo ni jirani tu na Chiwanda. Bandari nzuri...lakini Rais Bingu apunguze "kuwafukuza" wabongo...... ila anatufukuza kwa kuwawezesha wamalawi...ndiyo hapo changamoto yetu ilipo.