Mara ngapi umesoma kitabu au mahali ambapo panakupatia jawabu ambalo linaleta ukakasi kwako? Unaweza kufikiria lakini kama huwezi kufikiria basi jaribu kunisoma halafu fikiria kisha jipe jawabu kamili uone ukweli ulivyo.
1. Usiwe mwadilifu kupita kiasi unaweza kuwa mkiwa bureee maana mungu mwenyewe inadaiwa alisema hilo. Na kwakuwa kuna watu wanaamini kuwa dini za ukristo na Uislamu ni mwisho wa yote, hawajipi muda kuhoji, kwanini dini hizo za jamaa kutoka mashariki ya kati ambapo mmoja alikuwa akivaa misalaba mikubwa na mwingine alikuwa akifuga ndevu na kupka hina. Mbona kuna Wabudha, wahindu n.k angalia usiwe mwadilifu kupita kiasi.
2. Usiamini kitu chochote kwasababu tu kinasemwa na mtu mwenye busara. Pima mambo yako ewe mwanadamu usikubali tu kama ilivyo ndivyo bali unavyoamini ndivyo.
3.Usiamini kitu chochote kwasababu tu watu wengi wanaamini. Ndiyo maana sitaki kusikia dini ambazo zimejaa vimelea bya kutohojiwa, ambazo zinasadikisha ati ilikuwa lazima watakao hoji na wapingaji ukristo. Nimelelewa katika msingi wa dini zenyewe lakini ninachokiona katika ulimwengu wenyewe nashangaa tu. Kwani lile sanamu la mwanamke aliyepanda mnyama aliyepo pale nje ya bunge la ulaya ni nini kama siyo ushetani kwa mujibu wa UFUNUO WA YOHANA? soma tuulewe vema. Si mnadanganya na dini zenu kuwa Obama alikosea kuapishwa? wadanganyeni haohao ili mnyasa nisalie kuamini vile ambavyo naamini.
4.Usiamini kitu chcochote kwasababu tu vitabu vya kale vimeadnika. Yako mengi tu, mbona tunadanganywa Nostrodamus alitabiri vita vya dunia vya 3, alitabiri kuzaliwa kwa Adolfu Hitler na mengine mengi kama mapinduzi ya Ufaransa....lakini hatusemi kuhusu Mysters School ya Freemasons ambazo zilimfindisha kufundisha ushetani wake.
5 Usiamini jambo lolote kwasababu tu vitabu vitakatifu vimeandika. Hapo mie simo lakini unaamini kuwa simulizi za mambu wa mashariki ya kati ni chanzo cha kuwepo wa sisi. Alaah kumbe ilikuwaje aliyeletwa kwaajili ya Babeli na wayahudi akawa wa dunia nzima? Na historia ya Roma inaweza kunisadikisha kwamba niamini ndivyo ilivyo nisadiki tu bila kuhoji? Niamini anayekupiga kwenzi akuchape na mitama?
6. Amini jambo kwasababu wewe mwenyewe umelipima na ukaliona liko sahihi.
Ndiyo maana nasimimia hoja kwamba sihitaji kanisa wala msikiti wowote, sihitaji mchungaji wala ninachokiandika sikitumikii nakitumikia tangu mwaka 1996 hadi leo hii. Je unafikiri dini yako ni bora kuliko ya mwenzio? Unafikiria kanisa lako ni bora kuliko la mwenzio? Unafikiri sadaka yako ni bora kuliko ya mwenzio?
November 17, 2009
FIKIRIA SANA, USIAMINI SANA, AMUA WEWE
Madhumuni
falsafa
November 15, 2009
HIVI PUNDE:.....kikao cha NYAZODE kimemalizika
Baada ya kutoka likizo mara vyuo vilipofungwa kwa muhula wa kwanza kumaliza. Na sasa kukiwa kumeshaanza muhuala mwingine hatukupata muda wa kuongea wala kujadili kwa kina kuhusu mradi wetu wa NYAZODE. Lakini leo hii jumapili HIVI PUNDE kumemalizika kikao hicho cha kwanza na maazimio kadhaa kupitishwa.
Mradi huu kwa hakika ukikamilika utawezesha wale walalahoi wenzetu wa nyasa kuamka wakiwa neema nzito maishani mwao. Ni hivi punde tumekamilisha masuala kadhaa muhimu ambayo yatawezesha mustakabali mzima wa NYAZODE.
Sasa mradi unapiga hodi katika ofisi ya Mbunge wa jimbo la Mbinga magharibi bwana John Komba ili apate taarifa maridhawa kuhusu mradi wenyewe. Na vilevile wazee kama Profesa Mihanjo, hivi punde atapewa maazimio na kuweza kufanya kile ambacho wengi hawakutarajia kufanywa na kundi hili la wazee wa nyasa. Ni hivi punde tu kumemalizika kikao hicho.
ASANTE KWA UHUDHURIAJI WENU NA KARIBUNI S ANA NYASA.
Mradi huu kwa hakika ukikamilika utawezesha wale walalahoi wenzetu wa nyasa kuamka wakiwa neema nzito maishani mwao. Ni hivi punde tumekamilisha masuala kadhaa muhimu ambayo yatawezesha mustakabali mzima wa NYAZODE.
Sasa mradi unapiga hodi katika ofisi ya Mbunge wa jimbo la Mbinga magharibi bwana John Komba ili apate taarifa maridhawa kuhusu mradi wenyewe. Na vilevile wazee kama Profesa Mihanjo, hivi punde atapewa maazimio na kuweza kufanya kile ambacho wengi hawakutarajia kufanywa na kundi hili la wazee wa nyasa. Ni hivi punde tu kumemalizika kikao hicho.
ASANTE KWA UHUDHURIAJI WENU NA KARIBUNI S ANA NYASA.
Madhumuni
Hisia za moyo,
kumbukumbu,
maisha,
Nyasa
November 11, 2009
VITUKO VYA WANYASA NA SANAMU LA ASKARI DAR ES SALAAM
Nakumbuka nikiwa mdogo, simulizi za snamu la skari huyu zilinitihs akuona mji huu siyo wa kuishi. Nakumbuka waliowahi kufika huko Dar es alaam wakisifia na kutisha kuhusu mji wenyewe. Nakumbuka wengine waliwahi kusimulia kuwa hapo zamani kulikuwa na mzee fulani MNYASA aliwahi kukaa hapo kwa kuombeleza asamehewe makosa yake kwani hakujua kama anavunja kanuni za mji.
Na kosa lenyewe lilikuwa kushangaa ghorofa zilizojipanga katikati ya mji tangu alipokuwa akiishi Upanga. Na kwakua alikuwa mgeni basi aliamua kujipa jukumu la kuyajua mazingira kwakuwa alizowea mji kiasi chake. Basi akaijikuta maefika katika sanamu la askari huyu, mzee wa watu akapiga magoti kuomba msamaha sana kwa makosa ya kushangaa majumba makubwa watu wanaishi angani kama FIDEGE tena wale mbayuwayu...nawapenda sana hawa ndege.
Mzee huyo inasemekana alilia kwa nguvu zote kwa kudhani atasamehewa kosa la kushangaa majumba makubwa, yenye watu wasiotosheleza ubongo hadi wakawa walarushwa wakubwa na kuita TAKRIMA. Basi mzee huyo akaangua kilio hapo lakini hakuna aliyejali sana kuhusu hilo kwani alidhaniwa kua ni kichaa tu.
Lakini kama ujuavyo wabongo kwa kunusanusa udaku wakamsogelea mzee wa kinyasa na kumhoji inakuwaje anaongea na sanamu kwani amekuwa kichaa? Lakini mzee akasisitiza kuwa askari yule amemweleza atamdhuru kwanini ameshangaa maghorofa wakati anajua yanalipiwa? watu wakacheka inasadikika hivyo, wakamweleza huyo askari ni samanu tu hivyo kumtaka arejee nyumbani, ndipo mzee alikubalina lakini kwa sharti la kusindikizwa.
Alipotoa rai hiyo basi waungwana wakafanya hivyo hadi mtaa wa Undali na akaonyesha anapoishi kisha wenyeji wakajitokeza. Ndipo ikaulizwa kulikoni? Mzee akasimulia kisa na kudai jamaa wamemwokoa.... hee wenyeji wakaangua kicheko ikawa usiku ikawa mchana ......simulizi zimeendelea vizazi hadi vizazi vya mzee wa Lundunyasa alisimuliwa.....na hapo kale alikuwa akikataa kuja mji huu sababu hiyo ingawaje baadaye alikubali tu shauri ya elimu siyo sababu ya askari sanamu. Na akitimiza agano mzee wa Lundunyasa lazima arejee agano lake la nyasa. Vituko vya wanyasa na sanamu hilo jamani nilikuweo enzi hizo wakitusimulia yatokanayo
Madhumuni
falsafa,
familia,
kumbukumbu,
maisha,
soga
Subscribe to:
Posts (Atom)