YANAYOJIRI KWA WANYASA, MALAWI
WIKI hii ndugu zangu wa Malawi wana mjadala mzito, na majadala huo umedumu kwa majuma kadhaa kuhusiana na uamuzi wa serikali kukomesha suala la ndoa za mitala.
Serikali ya Malawi inadhamiri kupiga marufuku suala la ndoa za mitala katika jamii za nchini humo. Sijui zaidi ya hapo kuna nini ila kwa hakika hili ni suala la kuongelea kila mara kuhusiana na mwenendo wa binadamu.
Watetezi wa ndoa za mitala wanadai hiyo ni haki yao na kitendo cha serikali kuingilia kati kutaka kuwapiga marufuku kutooa wanawake zaidi ya mmoja au kuolewa na wanaume zaidi ya mmoja, ni kuingilia uhuru wao wa kuishi.
Tunakumbuka katika baadhi ya mila na desturi za India wanawake wanaweza kutoa mahali na kuoa, pia kutoa mahali ya kuolewa na zaidi ya wanaume wawili. Hivyo mwanamke ndiye anayepanga hilo, na kulichagua ni namna gani aishi na wanaume wake.
Ndoa za mitala kwa Malawi inaambana na mila na desturi ya makabila yao, kwa kiasi kikubwa kwao ndoa za aina hii ni fahali na kuonyesha ukubwa wa familia n.k, sifa moja kubwa ni kuzaa watoto wengi, na kuwaozesha endapo wapo wanawake au kuwa na watoto wengi na kusifiwa.
Mara nyingi wanawake katika jamii za kabila la Wanyanja na Wachewa hawana kauli sana kuhusiana na maisha ya ndoa hususan wale wanaoishi katika mazingira ya kitamaduni. Au kufanya uchaguzi wa kuolewa na mume gani
Maana wapo wengine nasema hawana utamaduni kwakuwa wanaishi katika mazingira ambayo ni vigumu kuyafafanua kwa utamaduni wao halisi(rejea jamii zilizozuka zamani huko Venice, Italia, na uchambuzi wa Karl Marx.
Hivyo wiki hili katika jiji la Blantyre mjadala siyo haba, na sijui mwelekeo wake utafikia wapi ila serikali imesisitiza kukomesha suala hilo.
Tukienda kwa kabila la Watumbuka, hali nayo siyo tofauti sana sawa na Wahyao.
Hili ni suala ambalo jamii nyingi za Malawi lineendekeza na kuamini kuwa ni uhalali wa maisha yao. Ni wazi wanaamuni kutokana na kurithi tangu enzi za mababu, lakini kama kuna umuhimu wa kuliendeleza ni vema kuangalia nafasi ya maisha halisi kuliko kushadadia tu.
Hata hivyo serikali imefafanua kwamba uwezekano wa kuenea maambukiz ya ukimwi kunatokana na ndoa hizi, inaelezwa wkamba wengi wanaolewa/kuoa kisha kuachwa/kuachana na kujikuta wakiwa wameathiriwa na magonjwa mbalimbali ikiwemo ukimwi.
Na zaidi inaelezwa kuwa kunakuwa na ongezeko la wajane au watu walioathiriwa kisaikolojia kutokana na ndoa hizo. Wengine ni mabinti wadogo ambao huozeshwa kulingana na mila na desturi.
Ni matumaini yangu Usia Nkhoma utachangia hapa, Vincent Kumwenda, Alley Kapito.... Lol! nchito ilipo bambo..... just for u Sophie Moyo.
TUJIULIZE
Ndoa za mitala ni hatari sana?
Kuna athari za ndoa za mitala?
serikali inaingilia uhuru wa kuishi?
Binadamu tunao uhuru kiasi gani?