May 29, 2010

SAFARI NJEMA DADA Diesmal

Kwanza nashukuru kunitumia picha hii baada ya kutua mjini Mbinga. Nadhani umekumbuka Frankfurt au uwongo ha ha ha na kiswahili chako kibovu eti 'nim'pika mbinga' badala ya kusema 'nimefika mbinga'. Usijali kazana safari ni ndefu hadi kuifikia Litembo dada halafu unasema una usongo wa kujimwaga kwetu nyasa.

Haya yangu mie macho tu, nakusubiri kwa hamu nadhani umeiona Mbinga sasa kazana tu mana hapo ndipo palipo nikuza na kunijuza ukiacha nyasa kwetu. Safari njema.

Hey mnasemaje kikwetu Diesmal? ha ha ha ha nimekumbuka ile lugha ngumu mweeeeeeeeeee, ha ha ha ha haya najaribu
   Gut sein reise madchen, i liebe du Diesmal......
           Ein kind bekommen....... lol

Diesmal natisha siku hizi naijua hii lugha, ha ha ha ha ha ha kideuctland chenu siyo? nami nimo eboooo! Dada Yasinta upo hapo? toto linajimwaga nyasa,litembo,kindimba na kadhalika, hebu mtakie safari njema au? Lol

May 27, 2010

HAPO VIPI?

May 26, 2010

WASOMI WETU, WANALILIA UPONYAJI!

Na: Albert Sanga, Tumaini University, Iringa

Nimeamua kuandika makala hii baada ya kutafakari kwa kina swali ambalo liliulizwa na kijana wa kitanzania kupitia katika mtandao wa internet. Kijana huyu anayefahamika kwa jina la Raymond Magambo, ni mwanafunzi wa shahada ya sayansi ya kompyuta Chuo Kikuu Cha Dodoma; anamiliki blogu inayofahamika kwa jina la {raymagambo.blogspot.com}. katika moja ya kurasa za blogu yake ameuliza swali lifuatalo “are the university students in Tanzania well prepared to bring changes in the country? Why?” tafsiri ya Kiswahili ya swali hili ni “Je wanafunzi wa vyuo vikuu katika Tanzania wanaandaliwa vema kuleta mabadiliko nchini? Kwa nini?”.

Kwa bahati nzuri sana ninamfahamu vema huyu kijana Raymond Magambo kwa sababu nilisoma naye kidato cha tano na sita pale Ilboru Sekondari. Ni moja ya vijana ambao wamekuwa na ndoto za kuona wanafanya vitu vya tofauti na vyenye historia za pekee katika dunia hii.

Vijana wa jamii kama ya Raymond Magambo hakika ndio wanaohitajika sana katika kuleta mabadiliko kwa jamii hasa ya kitanzania. Ukiona kijana kama huyu angalau anahoji uthamani na uwezo wa elimu anayoipata basi uwe na uhakika kuwa kuna mambo anatamani yafanyike katika namna fulani ambayo ni nzuri zaidi. Hawa ni watu ambao mimi nawaita “wanamapinduzi wa kutuokoa katika utumwa tuliouridhia”

May 23, 2010

HAPO NDIPO PENYE AKILI,HEKIMA?

"Hapa ndipo penye hekima. Yeye aliye na akili na ahesabu ya mnyama huyo, maana ni hesabu ya kibinadamu. Na hesabu yake ni mia sita sitini na sita(666). UFUNUO 13, 18."

Nina hakika msomaji hili siyo jambo geni kwako. Nasadiki kwa dhati kuwa wale waumini wa dini hii wataweza kutupatia tafsiri kamili juu ya mambo hayo, Tunaambiwa 666 ni hesabu ya kibinadamu zaidi na mwenye akili na aihesabu hiyo kama ilivyo katika UFUNUO wa Yohana.

Namba 666 inahusishwa na ishara za siri za aliyekuwa mfalme wa Rumi NERO CALUDIUS CAESAR AUGUSTUS GERMANICUS(37-68). 666 ni tarakimu inayohusishwa na utumwa wa mwanadamu na maangamizi kwake. 666 imetamkwa katika kitabu cha 11 na cha 66 cha Biblia. Cha 11 ni wafalme na cha 66 ni Ufunuo.

Kitabu cha 11 cha Biblia ni 1 wafalme 10; 14, Namba 666 kinasema hivi "Basi uzani wa dhahabu iliyomfikia Suleimani mwaka mmoja ndio talanta mia sita sitini na sita(666). Pia katika kitabu cha Mambo ya nyakati 9;13, ufunuo 13;48. Katika kitabu cha Ezra 2;13 kunatamkwa namba hii 666.

Biblia inavitabu 66 na 666. Hesabu toka Mwanzo hadi ufunuo. Je maana nyingine ufunuo ni mwisho? Ufunuo unafunua nini? Nafsi za Yakobo zilikuwa 666? soma mwanzo 46;26. Kwanini mwanamke wa kiisrael alipangiwa siku 66? soma Mambo ya Walawi 12;5.

Nini maana ya WWW(world wide website)? kwa maana kwa wagiriki W ni sawa na 6 ambayo warumi kwa kirumi ni VI, lakini huita I sawa na 1, V sawa na 5, X sawa na 10 na L ni sawa na 50. Je W ambayo ni 6, inamaana ya 666? Namba hiyo inaleta utata pia katika bunge la ulaya mbona kiti namba 666 hakikaliwi wakati kuna 667 na 665 ambavyo hutumika? Je ni bunge la kishetani ama Biblia iliandaliwa na watu maalumu?

WASHINGTON DOME
ujenzi wake ulikamilika mwaka 1884, una urefu wa futi 555. Ukikokotoa futi 555, utapata inchi 666. Je ni namba 666? Hii inaleta maana gani kwetu na wale waumini wafia dini? Je tunafikiri kwa bidii?

SARAFU YA EURO
Ina nyota 6, fito 6 zimeshika nyota. Julai 20, 1999 bunge la kwanza lilifanyika. Likachagua mwanamke aliyepanda mnyama kama ishara yao. soma UFUNUO 17;3, unaeleza sanamu la mwanamke lililojengwa katika bunge la ulaya mjini Brussels Ubelgiji.

Stemp ya 100 ya EU inafanana na sanamu hiyo. Pia umechorwa katika jengo la Brussels. Hii ni imani gani au ni za mwenyezi mungu? Sarafu mpya ya ulaya ina alama ya mwanamke aliyeketi juu ya mnyama. Je ni maagizo ya mola? Je Yohana anatufunulia mwisho wa dunia au kizazi cha shetani?

Halafu wanazindua biblia yenye lugha 66(?) unajua maana yake katika imani yako? Unadhani Mungu anahuruma sana? Nani alimwumba shetani?
TAFAKARI SANA.