July 17, 2010

NIKUPE NINI?

Nikupe nini ewe rafiki? Nifanye nini kwako rafiki mwema, usiyeficha msimamo wako na kukataa kile kisichokuwa chema? hakika wajua thamani ya urafiki, wajua thamani ya ukweli na upendo kwangu, Nitakupa nini rafiki yangu? Mangapi yangu yamesemwa na ukaambiwa lakini hujanificha?

Nifanye nini maana bado najiuliza kila siku? Najua tumetofautiana mara kadhaa lakini uzuri tunajadili yanakwisha. Najua habari kadhaa zangu umezipata na pengine unashindwa kunielewa misimamo yangu kadhaa. Lakini uzuri wajua tabia,mwenendo,misimamo,mitazamo na hadidu zangu za rejea.

NIKUPE nini ewe rafiki yangu? Sema sasa nijuwe maana kusubiri nishachoka nisije nikawa MVUMILIVU HULA MBOVU. Wajua ni kwanini tumekuwa hivi, wajua ni ukweli,bila simanzi, ni upendo na uwazi. Aaah! nitakupa nini ewe mwema. Naamini mungu ajua yakuwa twajua kwamba kiasi cha mambo tuyajuayo ni sehemu ya kujua tu ingawa pia hakutoshi kuyajua.

Asante rafiki kujibu hata maswali yaelekezwayo kwako lakini yanihusu mimi. Yote tisa naweza kukuita hakimu mzuri kwa kuhukumu vizuri  bila upendeleo Lol.... You know what it is rafiki. Daima umesimamia ukweli. Nakupenda sana rafiki yangu. Hivi ni nani atakaye tutenganisha? au huyu Mungu? ataweza kweli maana ananiogopa kila siku...... Lol

Napenda staili ya urafiki wetu mama, naamini ni ndugu sana kwa mengi mema. Zaidi nimeipenda picha inanikuna sana. JE URAFIKI UNASOMEWA DARASANI AU CHUO KIKUU? Thamani yeru ya urafiki ni pale tunapotazamwa kwa tofauti kumbe walaaaaaaa! Mungu mkubwa! THE SAME DRAMA

July 12, 2010

Wooh!! PALEPALE PALIPOUNGUA SHOKA NA MPINI UKABAKIA.........

Kama kuna kitu ambacho unakipenda halafu ukajikuta hutakiwi kukikosa utafanyaje jamani? Eti kuna umuhimu wa kususa kitu unachokipenda kweli? Au heshima unayompatia mtu inatakiwa iweje jamani? Maana mimi huwa naheshimu ninachokipenda na huwa natekeleza haswa. Mfano huu mpira uliokwisja jana hapa na kuona wachawi wanaowanga na nyungo kwa kutumia Pweza wametabiri mambo halafu wanaita utabiri wa kiteknolojia. Duh! ingekuwa afrika eti utamaduni wa kishenzi..... ha ha ha Nanyi ushenzi wenu ukae wapi jamani wazungu ninyi? Samahani kwa MCHARUKO huo.

Kombe limeisha, sasa nimerudi jamani yaani kikamilifu kidogo maana kuna mambo yanatakiwa yakamilike mwezi huu wote ndipo nitasema kweli kombe limekwisha sasa. Yaani RAHA kweli namshangaa rafiki yangu Yasinta anaangalia mpira kwa 'kubip' yaani haangalii kwa undani na umakini yeye anacheki kidogo na kuendelea na mengi Lol.... nitakucharikia aaaaah kumbe Erik amechukua tabia zako kidogo afadhali hii hajachukua mweeeee! WADAU wangu nimerudi,

WADAU wangu pale MKWAWA UNIVERSTY Francis Myale, Castro Tunuka na yoo man Jose a.k.a Jose, nimeipata barua pepe yako nitakupaisha mwana. Nilikuwa bizie na hii mipira ya JABULANI na mdogo wangu na rafiki yangu  Elvis Msigwa, utamwambia nini kuhusu soka huyu? Aaah mpira bwana mtamu usifananishe bwana. Yaani weka mahaba kando kabisa..... Mtani Fadhy a.k.a shemeji aaaaah ulipendeza kaptura lako a.k.a pensi naona shemeji anakaangiza kwelikweli yaani we acha tu. Kama kawaida Papaaa  yaani palipo ungua shoka na pini ukabakia........ PAMOKA DAIMA ++