July 21, 2010

KARIBUNI NYASA- jamani!

Ukitokea kijiji cha Mbaha kuelekea Ndumbi utakutana Pwani hizi zinazokuonyesha uelekeo wa Lituhi.
Hapa unaona mlima kwa mbaliiiiii, ambako ndiyo Lituhi. Lakini ardhi iliyoingia ziwani inaitwa Folk Land ni eneo la Lituhi. Pna historia sana hapa kwa uvuvi wa MBASA
Karibuni

MAKALA MPYA; TANZANIA; Azimio la Arusha na miluzi ya ubepari

TANZANIA; Azimio la Arusha na miluzi ya ubepari (1)

Nmesoma mara nyingi hoja za madai kwamba sera za Ubepari ni nguzo ya uchumi wa dunia. Katika kupitia hoja hizo, nakubaliana nao kwa kiwango fulani lakini iko haja ya kuchanganua zaidi na namna ya kuinua kiwango cha hoja zao. Dai lao la kukumbatia ubepari linatokana na mfumo wa soko huria uliobuniwa na kupigiwa mbiu sana na Adam Smith ambaye aliandika katika kitabu chake cha Wealth of the Nation.

Baada ya kukaa kimya kwa kipindi kirefu licha ya kushawishiwa na wale wanaoniamini kuwa ninaweza kuzichambua sera hizo- nilipanga kunyamaza na kuangalia mustakabali wa uchumi wa dunia. Niliamini muda utasema, na sasa nimeamua kusema kwamba Miluzi mingi ya Ubepari inampoteza Mbwa mwelekeo’. ...................

                   Usipitwe, isome yote

MAKALA MPYA; Je Waafrika tunapenda sana ngono?

Je Waafrika tunapenda sana ngono?


MWAKA 2003, katika Gazeti la The Guardian la Uingereza, Mwanasafu wake Hanif Kureishi alipata kuandika ‘Huwezi kujua kamwe uliyoyatamka yataleta maana gani kwako mwenyewe au kwa mtu mwingine ama ulimwengu wa maneno utakayoyaumba utakuwaje. Lolote lile laweza kutokea. Tatizo la kukaa kimya ni kwamba tunajua nini kitatokea’.(mwisho wa kunukuu).
                      
                       usipitwe, isome

HARUNA MOSHI YUKO SAHIHI?

Ukiniambia nimlaumu HARUNA MOSHI kuamua kuondoka nchini Sweden katika klabu ya Gefle nitakwambia, kosa lake ni lipi? Ukiniambia alikuwa akilipwa kwanini kaondoka nitakwambia acha afanye anachoona bora. JE YUKO SAHIHI AU HAYUKO SAHIHI?

July 17, 2010

NIKUPE NINI?

Nikupe nini ewe rafiki? Nifanye nini kwako rafiki mwema, usiyeficha msimamo wako na kukataa kile kisichokuwa chema? hakika wajua thamani ya urafiki, wajua thamani ya ukweli na upendo kwangu, Nitakupa nini rafiki yangu? Mangapi yangu yamesemwa na ukaambiwa lakini hujanificha?

Nifanye nini maana bado najiuliza kila siku? Najua tumetofautiana mara kadhaa lakini uzuri tunajadili yanakwisha. Najua habari kadhaa zangu umezipata na pengine unashindwa kunielewa misimamo yangu kadhaa. Lakini uzuri wajua tabia,mwenendo,misimamo,mitazamo na hadidu zangu za rejea.

NIKUPE nini ewe rafiki yangu? Sema sasa nijuwe maana kusubiri nishachoka nisije nikawa MVUMILIVU HULA MBOVU. Wajua ni kwanini tumekuwa hivi, wajua ni ukweli,bila simanzi, ni upendo na uwazi. Aaah! nitakupa nini ewe mwema. Naamini mungu ajua yakuwa twajua kwamba kiasi cha mambo tuyajuayo ni sehemu ya kujua tu ingawa pia hakutoshi kuyajua.

Asante rafiki kujibu hata maswali yaelekezwayo kwako lakini yanihusu mimi. Yote tisa naweza kukuita hakimu mzuri kwa kuhukumu vizuri  bila upendeleo Lol.... You know what it is rafiki. Daima umesimamia ukweli. Nakupenda sana rafiki yangu. Hivi ni nani atakaye tutenganisha? au huyu Mungu? ataweza kweli maana ananiogopa kila siku...... Lol

Napenda staili ya urafiki wetu mama, naamini ni ndugu sana kwa mengi mema. Zaidi nimeipenda picha inanikuna sana. JE URAFIKI UNASOMEWA DARASANI AU CHUO KIKUU? Thamani yeru ya urafiki ni pale tunapotazamwa kwa tofauti kumbe walaaaaaaa! Mungu mkubwa! THE SAME DRAMA