Jana nilikuwa katika msafara wa mgombea urais kwa tiketi ya CHADEMA. Nilikuwa nasoma sana saikolojia za mashabiki wake na wanachama wake pia. nilikuwa nawasoma sana kadiri muda ulivyokuwa unakwenda.
Kwa hakika binafsi namkubali sana Dr Slaa, na ninaumia sana kwa hatua yake ya kugombea urais badala ya kujenga kwanza ngome huku chini(bungeni). hata angegombea udiwani, mimi naamini tunajenga mzizi, lakini hakuna jinsi ni lazima tukubali wakati unakwenda na sasa ni miaka takribani 17 tangu kuanza vyama vingi.
Hata hivyo natambua sisi watanzania ni WANAFIKI.... sitanii na wala situkani..... naamini Dr Slaa kwa jinsi anavyoendesha mambo ndani ya bunge na namna anavyowasilisha tafiti zake. Nasema anastahiki kwenda Magogoni huku bloggers tukipiga jaramba pale Luthuli.
Je tumejiandikisha kupiga kura?(unafiki wa kwanza), je tumeweka dhamira ya kumchagua Dr Slaa(unafiki wa pili). Mimi nitamchagua, na wewe anza sasa.....
swali linabaki Je Dr Slaa ataweza?




