August 23, 2010

MAISHA YAPO SAFARINI.......

Basi la Sumry sambamba na gari la mizigo
Pale maisha yanaomaanisha tunapambana kwa njia tofauti. Lakini kwanini tupambane na maisha wakati hatuishi ili kupambana?? Kwanini nitoe nafasi wakati hakuna anayenipa nafasi?? MAWAZO maisha SAFARINI....

LITEMBO

Nilifika hapo nikiwa mdogo enzi zile za homa ya Pumu. Lakini amini nakwambia nilipona kwa dawa za Mitishamba, na kwa urahisi iliyochanganywa na Asali. Hakika nawashukuru madaktari enzi zile, lakini sasa sina dalili za kahoma hako. niko CADANGA kama Hugo Chavez pale Venezuela, yaani NGANGARI

ANGALIA BONGO- anuani imebadilika

Kwa wale wapenzi wa blog ya dada Saraphina Peter, bila shaka mnampata vema. Kwangu mimi namnyaka vizuri tuuuuu. Sasa ANUANI ya Blog hiyo imebadilika. Zamani ulijua kufungua HIVI lakini kwa taarifa hapo hutaipata.
ANUANI mpya ambayo unapaswa kuisopma Blog yako ya Angalia Bongo uipendayo, BASI unatakiwa kuisoma HIVI hapa ndipo ANUNUANI sahihi.

August 20, 2010

Viongozi wa TUCTA kugombea Urais 2015 na 2020?

James Oliver Robertson, alipata kuandika hivi; ‘msingi wa kutafuta maisha na furaha kunataka mtu abadilike na wale wasiofanya hivyo wanabakia watu wa kusikitisha na kusikitikiwa,kuchekwa na kubezwa’(mwisho wa kunukuu).
Je usemi huu utatimia kwa uongozi wa shirikisho la vyama vya wafanyakazi nchini? Tujiulize swali hilo huku tukitambua kuwa waraka wa mkuu wa utumishi wa umma namba 1 wa mwaka 2000 na kanuni ya 65(1) ya kanuni za utumishi wa umma za mwaka 2003, watumishi wa umma hawaruhusiwi kufanya shughuli za siasa wakati wa saa za kazi na wakiwa kazini na kuajiriwa na chama cha siasa.
Isome Makala nzima, USIPITWE