November 09, 2012

WADAU WA MAENDELEO YA WILAYA YA NYASA WAJADILI MUSTAKABALI WA WILAYA YAO

 MICHAEL NCHIMBI akandika kwenye mtandao wa Facebook kuhusu Wilaya ya Nyasa. Kupitia mtandao wa NYASA akasema kuwa; .... "Jamani hivi Nyasa hakuna matatizo yoyote yale ya kijamii? Sababu ndugu Komba(John) mbunge wa jimbo la Nyasa hajawahi kusimama Bungeni tangu lianze tarehe 30 kueleza matatizo ya wananchi wa Nyasa"! 
 
 Mbunge wa Jimbo la Mbinga Magharibi, Kapteni John Komba akifungua Zahanati ya Tumbi, wa kwanza kulia ni Katibu wa CCM Wilaya ya Mbinga Anastia Amasy 

 WADAU WAKACHANGIA YAFUATAYO;

1. JOSEPH NDOMONDO ... akasema, "Huyo mtu vijana wenye mtazamo tulimkataa, But(lakini) CCM, pesa ya wananchi na akina mama wakinyasa ndiyo waliyompa nafasi tena. Kwahiyo hata hajasimama bungeni hiyo imekula kwetu. Kwahiyo guys(vijana) tuwaelimishe wamama(wanawake) wapendwa wa Nyasa ili Nyasa iwe mfano 2015 tumbwage. But i'm not interested with political now. Pamoko kwa sana ila mje Nyasa siyo kwenye Facebook tuuu@Joe.

2. JAMES ZOTTO, akasema haya ........ " Kwani ni lazima aongee kila Bunge?"

3. MAURICE NCHIMBI ... akachangia pia, " Acha siasa bwana Zotto kwani Bunge lililopita aliongea nini..."

4. JAMES ZOTTO, 
 Akarejea tena kuchangia  ..."Aliongea mpaka wetu na Malawi na Huduma za Jamii lakini wanaomlaumu John Komba ni wanafiki sana maana wao ndio wa kwanza kumpigia debe na kumchagua. Kwani alichaguliwa na nani? Je, nani alijitolea kutoa elimu kwa wapiga kura na kuwafahamisha wanyasa kuwa tunataka mabadiliko? Si Komba tu, ni mfumo mzima umedorora! Labda hapa nitaeleweka, nitagombea 2015, Mtanisapoti?

5. MARKUS MPANGALA, ..... 
 Nami nikajongea na kusema haya ..."Kaka James Zotto, kabla hujagombea una kazi kubwa ya kufanya naomba hilo wazo sogeza hadi 2020. Nadhani sasa tushughulikie hili unalofanyia kazi sasa na mengineyo. Suala la John Komba kutoongea jamani inabidi tujiulize nani KERO ipi inatakiwa kuzungumziwa na hatua gani zilichukuliwa ama zinafanyiwa nini. Binafsi kuna juhudi zinanifurahisha sana ndio maana nazijaza kwenye blog hata kama ni kidogo lakini zinaleta matumaini. Mimi natamani ELIMU na AFYA ziwe kipaumbele. Je, mbunge wetu anaweza kufanya kila kitu kuhusu Nyasa? Na kila jambo linategemea Bunge? Kama tulivyo na desturi yetu ya kujitolea kwa maendeleo yetu Wanyasa, naomba tudumishe hilo. Kaka Hoops Kamanga ananipa mengi na kuelewa Nyasa inaelekea wapi. Nina miaka mitano mbele naamini Nyasa itakuwa na fursa nyingi mno na habari za Dar es salaam syndrome zitaanza kutoweka angalau kidogo. 

6. HOOPS KAMANGA, 

Naye akachangia haya, ..............." Markus lazima tukubali kuwa vijana na wasomi wa leo tuna tatizo la kulalamika pengine bila hata kujifikirisha nn kiini cha ttz kumlaumu komba kuwa haongei bungeni ni kutojua kinachoendelea nyasa jamaa ana influnce kubwa sana kwenye hii serikali nyasa hv leo kuna miradi mikubwa ya maendeleo ambayo hatukuwahi kuiona kwa serikali hii ya ccm sion mwakilishi atakaeisaidia nyasa zaidi ya huyu kuna haja gani kuongea bungeni wakat ukipeleka kimemo kwa waziri unatekelezewa hv mnajua nani ali push ishu ya wilaya mpya na mwez ujao halmashauri inaanza.....kwa nafasi zetu tuanze ss kurudisha fadhila nyasa napendekeza tuanzishe online harambee tukusanye fedha kila baada ya miezi 3 au 6 tuanze kuwanunulia wadogo zetu vitabu nawasilisha.

November 07, 2012

WAZEE WA KYELA WATOA USHAHIDI KUHUSU MGOGORO WA ZIWA NYASA



Wazee wanaoishi pembezoni mwa Ziwa Nyasa, Wilaya ya Kyela, mkoani Mbeya, wameunga mkono hoja ya serikali kwamba, mpaka wa Tanganyika na Malawi, upo katikati ya ziwa hilo, wakisema ndivyo walivyoelezwa na wazee wao walipokuwa vijana.

Walisema hayo mbele ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe, alipokutana nao ili kupata ushahidi kuhusu mpaka halali wa nchi hizo.

Waziri Membe akiongea na wazee wa Kyela katika ziara yake ya kuzungumza na wazee kuhusu mipaka ya Ziwa Nyasa. Picha: Subi Sabato/Wavuti

Mzee Edwin Kasirati (75) alisema alizaliwa na kulikuta ziwa hilo na wakati wakiwa vijana walielezwa na wazee wao kuwa mpaka wa Tanganyika na Malawi ni mto Songwe, ambao unaingia ndani ya Ziwa Nyasa.
Alisema mwaka 1961 Wamalawi wenyewe walikiri kwamba, mpaka ni katikati ya ziwa na mto Songwe.
Mzee Michael Mwang’onda (70) alisema tangu wakiwa wadogo walikuwa wakielezwa na wazee wao kwamba, mpaka wa Tanzania (wakati huo Tanganyika) ni huo huo uliopo katikati ya ziwa kama ilivyo na  wameendelea kuulinda hadi sasa.
Alisema wanavyoelewa ni kwamba, Tanzania ndiyo inayomiliki eneo kubwa la ziwa hilo linalofikia theluthi mbili ya ziwa lote na Malawi wanalo eneo dogo ikilinganishwa hata na Msumbiji.
Mwang’onda alisema kama ni kulalamika, basi wangelalamika wananchi wa Msumbiji, ambao ndio wanafuatia kwa kumiliki eneo kubwa la ziwa na wala siyo Malawi.

wazee wa Kyela wakimsikiliza waziri Membe
Alisema hivi karibuni ziwa hilo limepanuka na kumega eneo lao, akidai kuwa hata makaburi ya mababu zao hivi sasa yamefunikwa na maji umbali wa zaidi ya kilometa mbili ndani ya ziwa Nyasa, hivyo haiwezekani ziwa lote ni mali ya Malawi. 
Katika safari yake ya kukusanya ushahidi, tayari Waziri Membe amekwishapita katika mikoa ya ya Ruvuma, hususan wilayani Mbinga na Mbeya katika wilaya ya Kyela, ambako alikutana na wazee mbalimbali na kuzungumza nao.
Awali, akizungumza na Kamati ya Ulinzi na Usalama Mkoa wa Mbeya, Waziri Membe alisema serikali haitarudi nyuma kushugulikia mgogoro wa mpaka baina yake na Malawi ndani ya ziwa hilo na kwamba, inataka kufikia mwaka 2015 suala hilo liwe limepata ufumbuzi.
Alisema licha ya Serikali ya Malawi kusuasua kuhudhuria vikao vya kuzungumzia mgogoro huo, Serikali ya Tanzania haitalifumbia macho suala hilo kabla ya kulipeleka katika Mahakama ya Kimataifa (ICJ).

wavuvi wakivua samaki katika ziwa Nyasa
Akiwa wilayani Kyela, Waziri Membe alizungumza na wananchi wa Kata ya Katumba Songwe na Matema akiwataka waendelee kuishi kwa amani na utulivu na asitokee mtu kwenda kuwatisha na kuwadanganya kwamba kuna hatari yotote katika mpaka huo.
Alisema serikali inalitambua tatizo hilo na inalifuatilia kwa makini ili kulipatia ufumbuzi na ndio sababu hivi sasa yeye anakwenda kwa wananchi na kuzungumza na wazee kwa nia ya kupata ushahidi utakapelekea kupata suluhu.
Alisema hata Rais Kikwete alitoa kauli ya kuwaahidi Watanzania kwamba, kabla ya kumaliza uongozi wake anahitaji suala hilo liwe limepata ufumbuzi ili wananchi wa eneo hilo waendelee kuishi bila wasiwasi, kwa amani na utulivu.
Aliwahakikishia wananchi hao kuwa hata kama suala hilo litapelekwa ICJ, lazima Serikali ya Tanzania itashinda kutokana na ushahidi unaotolewa na wazee katika maeneo mbalimbali anakopita. CHANZO: SOMA ZAIDI, HABARI ZINGINE SOMA HAPA KUHUSU NYASA NA WAZEE WA KYELA

CHANZO: HABARI NA EMMANUEL LENGWA
CHANZO: NIPASHE

UJENZI WA MACHINJIO MBINGA NA SOKO LIWETA


Katika kuboresha huduma za jamii, kuna mengi huwa yanafanyika. Miongoni mwake ni kujenga Machinjio yenye ubora na mazingira salama kwa afya za wanadamu. Wilaya ya Mbainga imefanikiwa kujenga machinjio katika eneo la mbinga mjini. Machinjio hii itasaidia kuondokana na mazingira duni ya kuchinjia wanyama mbalimbali wanaopelekwa sokoni kuuzwa. Picha ya chini inaonyesha sehemu ya kusafishia utumbo katika Machinjio hayo mjini Mbinga.


Picha ya chini: eneo la Machinjio hayo, mjini Mbinga. Kama tulivyoeleza awali kuwa machinjio hii itawanufaisha sana wafanyabishara wa nyama na watumiaji kutokana na ubora uliopo, kulingana na kanuni za AFYA.

UJENZI WA SOKO
Ujenzi wa Soko la Kijiji cha Liweta. Ujenzi huo upo katika awamu ya kwanza. Unatarajiwa kukamilika mapema mwakani ili kuhakikisha wakazi wa kijiji hicho wanaweza kuwa na Soko lenye kiwango kizuri baada ya kutokuwepo kwa Soko kwa muda mrefu. ni njia moja wapo ya kuweka mazingira safi na kuwawezesha wauzaji wadogowadogo kuuza bidhaa zao katika mazingira mazuri.