November 20, 2012

KARIBUNI SANA NYASA, MLO WENYE VIRUTUBISHO VYA ASILI

                                                            KARIBUNI NYASA
Hilo tunaloweza kusema kuhusu wilaya ya Nyasa. Ni wakati wa kuburudika zaidi na kupata vyakula vyenye virubisho vya asili kama vinavyoonekana pichani.


SHULE YA MSINGI NDONGA YAHITAJI MATENGENEZO YA HARAKA SANA WILAYANI NYASA


Pichani ni wanafunzi wa shule ya msingi NDONGA. Shule hii ipo katika hali mbaya sana kutokana na wanafunzi kusomea kwenye majengo mawili ya shule hiyo ambayo yaliezuliwa na kubomoka kutokana na upepo mkali mapema mwaka jana(2011). 
Eneo la Ndonga linajulikana kutokana na kukabiliwa na upepo mkali sana hasa kipindi cha kiangazi na masika. tangu kuezuliwa kwa paa la shule hiyo wanafunzi wamekuwa wakisoma huku wakipigwa na jua kali kutokana na kutoezekwa. 
Wanafunzi kama wanavyoonekana pichani hawanjakingwa na jua hivyo kuzorotesha ufanisi wao maishani. Ni Jukumu la wakazi wa kijiji cha Ndonga, Uongozi wa kijiji, Tarafa, na Wilaya ya Nyasa kushughulikia suala hili. 
Hali kama hii haiwezi kwuachochea wanafuzni kuwa wavumbuzi au wenye kiu ya kupata elimu kama maeneo mengine yenye mazingira mazuri ya kusomea kama Shule ya msingi Mwongozo iliyopo mjini Liuli. 
Mazingira kama haya yanampa wakati mgumu sana mwanafunzi kuweza kufanikisha ndoto zake, ndio maana wengi wanaishia kuwa watoro shuleni. jambo jingine ni kwamba mazingira kama haya ynachochea wanafunzi kutoona umuhimu wa elimu kwani mazingira wanayotumia hayatoa motisha ya wao kupenda shule. 
Shime watu wa Ndonga, uongozi, tarafa na wilaya yote ya Nyasa, ni wakati wa kushughulikia hili kwa kupitia watu wote wanaohusika katika kuboresha elimu yetu. Hali hii inawarudisha nyuma wanafunzi na walimu wao. 
Ili kuondokana na ukosefu wa walimu katika shule nyingi za Wilaya ya Nyasa hatuna budi kuhakikisha tunatengeneza mazingira mazuri ya wanafunzi na watoto wetu.

Picha ya Jamii Forum, kwa hisani ya Weston Ndomba, Nyasa

November 15, 2012

NAFASI ZA KAZI, MWISHO NOVEMBA 29, 2012

SEKRETARIETI YA AJIRA NCHINI

INATANGAZA NAFASI ZA KAZI. Soma hapo JUU katika LINK

Details for TANGAZO LA KAZI Swahili 15 Novemba 2012


PropertyValue
Name:TANGAZO LA KAZI Swahili 15 Novemba 2012
Description:Mwisho wa kupokea barua za maombi ni Tarehe 29-Novemba-2012
Filename:TANGAZO LA KAZI Swahili 15 Novemba 2012.pdf
Filesize:180.32 kB
Filetype:pdf (Mime Type: application/pdf)
Creator:psrsweb
Created On:11/15/2012 11:57
Viewers:Everybody
Maintained by:Editor
Hits:863 Hits
Last updated on:11/15/2012 12:00
Homepage:

ELIMU NI UHAI, WATU WAPE ELIMU

Sehemu ya jengo la madarasa katika shule ya Sekondari Lituhi, mjini Lituhi. Kwa sasa hali ya mabadiliko imekuwa kubwa kutokana na shule hiyo kukabidhiwa kwa serikali ambapo mwanzoni ilikuwa ikimilikiwa na wazazi ambao waliamua kujenga sekondari hiyo kwa lengo la kuondokana na kero ya ukosefu wa elimu kwa watoto wao.

Hosteli za shule ya Sekondari ya Mbamba bay, mjini Mbamba Bay. Hatua hii itasaida kuondoa ukosefu wa mabweni katika shule nyingi za Kata katika wilaya ya Nyasa. Kwakuwa sekondari ya Mbamba Bay ni ya Kata basi inaweza kuchukuliwa kama mfano wa shule zingine ili kuondokana na kero mbalimbali za elimu na kuwafanya wanafunzi wasome kwa utlivu wakiwa na maeneo mazuri ya kusomea.
Jengo la madarasa matatu katika shule ya sekondari ya Linda iliyopo nje kidogo ya mji mkuu wa wilaya ya Nyasa, Mbamba Bay. Ujenzi wa madarasa hayo unatarajiwa kukamilika ifikapo mwanzoni mwa mwaka 2013. Ambapo Ujenzi wake ulianza katika mwaka fedha 2008/2009. Hii ni hatua nzuri ambayo inahitaji msukumu zaidi ili kukamilisha huduma za elimu kwa wakazi wa mji wa Linda na wilaya Nyasa kwa ujumla.


Madrasa ya shule ya sekondari ya Wukiro, iliyokarabatiwa kwa baadhi ya vifaa vya LCDGC, ambapo ukarabati katika majengo hayo haujakamilika. matarajio yake ni kukamilishwa mwanzoni mwa mwaka ujao 2013.

PICHA ZOTE NA HOOPS KAMANGA, Nyasa.