Na JACKLINE MLUGE-AUTIO, LAHTI-FINLAND
Wakati wote tunafikiria kuwa wenzetu wazungu wanapesa nyingi
sana na ndio maana wanatusaidia. Lakini ukweli si kama wanapesa ila wana moyo wakufanya
hivyo, ninasababu za kusema hivyo kwa sababu roho inaniuma kuona kuwa kuna
baadhi ya watu ambao huwatesa watoto bila sababu ya msingi. Kila kukicha ukisoma katika magazeti mbalimbali ya Tanzania
utakuta habari mbalimbali ambazo zinahusiana na kuteswa kwa watoto. Swali najiuliza kama kweli unamchukua mtoto wa mwezango kwa
lengo la kumsaidia iweje leo umtese.
Kuna wangapi ambao wana moyo wa kuwatunza watoto wa wenzaao
bila kuwatesa ni wakati umefika sasa Watanzania kuweza kubadilika ikiwa una
mchukua mtoto wa mwenzako kwa lengo la kumtunza basi mtunze kweli na
sivinginenvyo. Kuna usemi usemao kutoa ni moyo na si utajiri. Seija
Saarikoksi Silvola ambaye ni mama
mwenye umri wa miaka 65 amebahatika kupata mtoto mmoja.
Jackline Mluge-Autio, akiwa na Mama Seija Saarikoksi nchini Finland.
Unaweza kujiuliza kwanini nimeamua kuandika makala hii?
Nimeandika kwa nia ya kutoa changamoto kwa watanzania wenzangu kuweza kusaidia
watu wengine hata kama tuna watoto zetu lakini pia kama unauwezo wa kusaidia
inabidi tuweze kusaidia. Mara ya kwanza Seija, kufika bara la Afrika aliposhinda
zawadi ya tiketi ya kwenda nchi ya kama unavyojua kwa mara ya kwanza kufika
Afrika aliweza kuvutiwa na ukarimu wa watu ambao kwa nchi kama ya Finland
ukarimu ni kitu kigumu sana.
Jackline Mluge-Autio akiwa na rafiki zake.
Mwaka 2007 alienda Tanzania na shirika la Settlement na
baadhi ya wafini ambao walienda kutengeneza shule ya msingi Pekomisegese
iliyopo mkoa wa Morogoro. Nakumbuka mwaka huo, mimi nilikuwapo ingawa sikuweza kukaa
kwa muda mrefu kutokana na masomo. Tulikuwa tunalala kwenye mahema. Wafini walikuwa wanafanya
kazi kwa kushirikiana na wakazi wa Pekomisegese. Na weza kutoa pongezi zangu na shukrani zangu kwa wakazi hao
wa Pekomisegese kwani waliweza kushirikiana kwa hali na mali kwa kujitolea
kuweza kujenga shule ambayo leo hii watoto wanaweza kukaa darasani na
kujisomea.
Jackline akiwa na wanafunzi wenzake.
Mwaka 2009-2010 Seija na baadhi ya wafini walienda kujitolea
kujenga shule ya msingi Pinda iliyopo Mgeta mkoa wa Morogoro. 2011-2012 shule ya msingi Tandale. Mbali na kujitolea
kujenga shule pia Seija ana watoto zaidi ya kumi ambao anawasidia kwa hela yake
mwenyewe bila kutegemea NGO. Ana wasidia kwa kuwalipia ada za shule na kuwanunulia vifaa
vya shule. Sio kwamba eti Seija ni tajiri , la hasha ni ana moyo. Ikiwa mtu kutoka mbali anaweza kutusaidia je sisi wenyewe
tunashindwa najua kabisa kuna mashirika ambayo yanasaidia watoto lakini pia mtu
mmoja mmoja tunaweza kujitolea na kuwasaidia watoto wetu wa tanzania wenzetu
bila kujali kabila au dini.
Kumsaidia mtu si mpaka umjue.