December 04, 2012

HAPA NA PALE WILAYANI NYASA

Shamba la Mtama na mikorosho la shule yya sekondari ya Lituhi

Shamba la Mpunga lililolimwa katika vyanzo vya Maji kwenye kijiji cha Mkako.

Bomba la mradi wa Maji Kindimba Juu.

KUITWA KWENYE USAILI DESEMBA 6&7

WALIOOMBA KAZI KATIKA SEKRETAIETI YA AJIRA NCHINI.

SOMA HAPA ....

December 02, 2012

TAARIFA KWA WAWEKEZAJI WAPYA KATIKA KILIMO CHA MITI YA MBAO, KARATASI NA NGUZO.

Fresh Farms & Tours (T), biashara tanzu ya Anesa Co.,Ltd (Nyaluke Business Empire); inayojishughulisha na upandaji, utunzaji na uendelezaji wa mashamba ya miti ya mbao, karatasi na nguzo-mkoani Iringa. Pia inahusika na uvunaji na usambazaji wa mazao ya miti, (mbao na nguzo za umeme) sambamba na ufugaji.
Fresh Farms ilianzisha programu maalumu, mapema mwaka jana; inayolenga kuwawezesha watanzania wengine kuwekeza katika kilimo cha miti kwa urahisi. Tayari makumi wa watanzania wamechangamkia fursa hii. Fresh Farms & Tours (T) tunapenda kuwaarifu wale wote wenye nia ya kuwekeza nasi; KWAMBA kuanzia tar 1, Feb, 2013 kutakuwa na mabadiliko ya bei na gharama za uendeshaji kwa mashamba ya miti. Mashamba tunayoyauza laki sita kwa sasa; bei mpya itakuwa milioni moja; na yale tunayouza laki nane gharama yake itakuwa milioni moja na nusu.
Bei hizi hazitawaathiri wateja wa awali na wale ambao wamekwisha wasilisha oda zao. Fresh Farms & Tours (T) tunaendelea kuboresha huduma, taarifa na usaidizi kwa wote wanaowekeza nasi. Kabla ya mwisho wa mwaka huu; tutazindua tovuti maalaumu itakayobeba taarifa za uwekezaji katika kilimo na ufugaji; pia kila anaewekeza nasi atapata nafasi ya kufungua akaunti yake katika tovuti hiyo; na akaunti hiyo itamwezesha kufuatilia mwenendo wa mashamba yake popote alipo duniani. Fresh Farms & Tours (T)-GREENING THE WORLD AND FEEDING PEOPLE. (C) Anesa Co., Ltd

November 28, 2012

LIULI YAHIFADHI HISTORIA YA JIWE LA POMONDA

Jiwe la Pomonda
Miongoni mwa miji muhimu katika wilaya ya Nyasa ni mji wa Liuli. Mji huu unayo bandari muhimu ambayo hutumiwa na meli zinazofanya safari katika ziwa Nyasa kwa upande wa Tanzania. meli za Mv Iringa na Mv Songea zimekuwa zikitia nanga katika bandari hiyo ikiwa ni sehemu ya kukuza uchumi, usafirishaji bidhaa na kadhalika. 
Katika rekodi za kihistoria kuna mengi ya kukumbukwa katika mji wa Liuli, lakini jambo muhimu ni kuwepo kwa Jiwe hilo ambalo linalinganishwa na sura ya binadamu. Ukkchunguza jiwe hilo utaona linafanana kidogo au kuwa na maumbile fulani yenye sura ya binadamu. 
Ni historia nzuri na tamu kwa wakazi wa nyasa na vitongoji vyake. Jiwe hilo lipo karibu kabisa na Bandari ya Liuli ambapo kila abiria au msafiri yeyote anapotumia bandari hiyo ataweza kuliona. Ni moja ya vivutio vya Utalii katika mji wa Liuli. KARIBUNI WATALII, KARIBUNI LIULI kujionea mengineyo.

WARAKA KUTOKA MJINI LAHTI NCHINI FINALND


Na JACKLINE MLUGE-AUTIO, LAHTI-FINLAND

Wakati wote tunafikiria kuwa wenzetu wazungu wanapesa nyingi sana na ndio maana wanatusaidia. Lakini ukweli si kama wanapesa ila wana moyo wakufanya hivyo, ninasababu za kusema hivyo kwa sababu roho inaniuma kuona kuwa kuna baadhi ya watu ambao huwatesa watoto bila sababu ya msingi. Kila kukicha ukisoma katika magazeti mbalimbali ya Tanzania utakuta habari mbalimbali ambazo zinahusiana na kuteswa kwa watoto. Swali najiuliza kama kweli unamchukua mtoto wa mwezango kwa lengo la kumsaidia iweje leo umtese.
Kuna wangapi ambao wana moyo wa kuwatunza watoto wa wenzaao bila kuwatesa ni wakati umefika sasa Watanzania kuweza kubadilika ikiwa una mchukua mtoto wa mwenzako kwa lengo la kumtunza basi mtunze kweli na sivinginenvyo. Kuna usemi usemao kutoa ni moyo na si utajiri. Seija Saarikoksi Silvola ambaye ni  mama mwenye umri wa miaka 65 amebahatika kupata mtoto mmoja.
Jackline Mluge-Autio, akiwa na Mama Seija Saarikoksi nchini Finland.

Unaweza kujiuliza kwanini nimeamua kuandika makala hii? Nimeandika kwa nia ya kutoa changamoto kwa watanzania wenzangu kuweza kusaidia watu wengine hata kama tuna watoto zetu lakini pia kama unauwezo wa kusaidia inabidi tuweze kusaidia. Mara ya kwanza Seija, kufika bara la Afrika aliposhinda zawadi ya tiketi ya kwenda nchi ya kama unavyojua kwa mara ya kwanza kufika Afrika aliweza kuvutiwa na ukarimu wa watu ambao kwa nchi kama ya Finland ukarimu ni kitu kigumu sana.
Jackline Mluge-Autio akiwa na rafiki zake.
Mwaka 2007 alienda Tanzania na shirika la Settlement na baadhi ya wafini ambao walienda kutengeneza shule ya msingi Pekomisegese iliyopo mkoa wa Morogoro. Nakumbuka mwaka huo, mimi nilikuwapo ingawa sikuweza kukaa kwa muda mrefu kutokana na masomo. Tulikuwa tunalala kwenye mahema. Wafini walikuwa wanafanya kazi kwa kushirikiana na wakazi wa Pekomisegese. Na weza kutoa pongezi zangu na shukrani zangu kwa wakazi hao wa Pekomisegese kwani waliweza kushirikiana kwa hali na mali kwa kujitolea kuweza kujenga shule ambayo leo hii watoto wanaweza kukaa darasani na kujisomea.
Jackline akiwa na wanafunzi wenzake.
Mwaka 2009-2010 Seija na baadhi ya wafini walienda kujitolea kujenga shule ya msingi Pinda iliyopo Mgeta mkoa wa Morogoro. 2011-2012 shule ya msingi Tandale. Mbali na kujitolea kujenga shule pia Seija ana watoto zaidi ya kumi ambao anawasidia kwa hela yake mwenyewe bila kutegemea NGO. Ana wasidia kwa kuwalipia ada za shule na kuwanunulia vifaa vya shule. Sio kwamba eti Seija ni tajiri , la hasha ni ana moyo. Ikiwa mtu kutoka mbali anaweza kutusaidia je sisi wenyewe tunashindwa najua kabisa kuna mashirika ambayo yanasaidia watoto lakini pia mtu mmoja mmoja tunaweza kujitolea na kuwasaidia watoto wetu wa tanzania wenzetu bila kujali kabila au dini.  Kumsaidia mtu si mpaka umjue.