January 15, 2013

MRADI WA MAJI KIJIJI CHA NG'OMBO WAKAMILIKA

Na Mwandishi  wetu, Ng'ombo
Wakazi zaidi ya 2450 wa kijiji cha Ng’ombo katika Kata ya Chiwanda wilayani Nyasa mkoani Ruvuma wameondokana na adha iliyokuwa ikiwakabili ya upatikanaji wa maji safi na salama baada ya kukamilika kwa ujenzi wa mradi wa maji kijijini hapo,

Akizungumza na Lundunyasa Network, Mhandisi wa Maji wa Wilaya hiyo Amos Mtweve alisema mradi huo ambao umejengwa kwa ufadhili wa UNDP kupitia Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira umegharimu jumla ya shilingi 298,346,700 na kwamba kuna vituo 23 ambavyo wakazi wa kijiji hicho watakuwa wakivitumia kupata maji.
Mhandisi Mtweve alisema kuwa kabla ya kujengwa kwa mradi huo wananchi walikuwa wakilazimika kutumia maji ya ziwa Nyasa kwa ajili ya kunywa, kupikia, na kuoga hali ambayo ilikuwa ikihatarisha usalama wa afya zao.
Alisema pamoja na changamoto mbalimbali zilizokuwa zikijitokeza wakati wote wa ujenzi wa mradi huo ikiwemo baadhi ya wananchi kutojitokeza kuchangia nguvu zao kama uchimbaji wa mtaro kwa ajili ya kulaza mabomba lakini bado mradi umekamilika kwa kwango kilichotakiwa.
“kukamilika kwa mradi huu kimsingi ni sifa kubwa kwetu kwani itawapa matumaini wafadhili wetu kufadhili miradi mingine hasa ikizingatiwa kuwa UNDP wamefadhili miradi michache ya maji hapa nchini ikiwemo huu wa kwetu,” alisema Mhandisi Amos Mtweve.

MIKOA YA MTWARA,LINDI NA RUVUMA TAFUTENI SULUHU KUFELI MITIHANI

Na Hamisi Magendela , Dar es Salaam
SIKU chache zilizopita wananchi wa mikoa ya kusini waliandamana kupinga uchimbaji wa bomba la gesi kutoka huko kwenda Dar es Salaam ambacho ingetumika kwa ajili ya kuzalisha umeme.
wanafunzi wakiwa darasani katika moja ya shule za msingi wilayani Nyasa
Umeme huo ambao ungezalishwa jijini Dar es Salaam ungetumika katika mikoa mbalimbali ya Tanzania hali ambayo inaaminika kuwa itasaidia kupungua ghalama za umeme na kufanya ukali wa maisha kupungua.
Sipingi mawazo yao kwani kila mmoja anafikilia kwa utashi wake japo ni vema wakaangalia faida kuliko na mafanikio yatakayopatika siku za usoni ikiwa gesi hiyo itasafilishwa kwa njia ya bomba kwenda Dar es Salaam.
Kikumbwa ambacho naweza kusema ni kwa wananchi wa mikoa ya kusini wanatatizo makubwa zaidi ya kuandamana kutaka manufaiko ya gesi wakati suala zima la elimu likiwa limewatupa mkono kiasi kwamba inatia simanzi kuona inashika nafasi 10 za mwisho katika ufauru wa matokeo ya kidato cha pili yalitangazwa juzi na Wizara ya Elimu na Mafunzo jijini Dar  es Salaam jana.
Licha ya kuwa ni aibu kwa wananchi pamoja na viongozi wa mkoa huo lakini naweza kusema kuwa ni kashfa ambayo katika miaka 50 ya Uhuru ijayo inatakiwa kufanyiwa kazi ili kuhakikisha wanapata elimu ya kutosha na kuondoka na ujinga wa kukosa elimu.
Ingekuwa vema zaidi badala ya kulalamikia kuhusu gesi wangepiga kelele kwa kukosa elimu bora kwa wanachi wengi wa mikoa hiyo hali inawafanya kukosa nafasi nzuri katika viwanda vinavyojengwa katika mikoa.
Kwa maana nafasi nzuri ya ajira itakuwa ikishirikiliwa na wageni ambao wana elimu ya kutosha ya kukidhi mahitaji ya kazi inayohitajika kwa wakati huo na kufanya wenyeji kufanya kazi za hali ya chini kila siku.
Pia wananchi wa mikoa ya kusini umefikia wakati wa kusimama kidete kuhakikisha fursa iliyotangazwa na Serikali kuwa kuanzia sasa hakutakuwa na mwalimu atakaepangiwa kazi mijini kwa wanaotoka vyuoni.
Kwa maana hiyo ikiwa viongozi wa mikoa hiyo wakitumia fursa hiyo kuwahamasisha wananchi wa kuzingatia elimu badala ya kung'ang'ani masuala ambayo kwa sasa hayasaidii sana katika miaka 50 ijayo.
Kusudio hilo la Serikali kupeleka walimu vijini linatokana na malalamiko kutoka sehemu hizo kuwa zimesahaurika kielimu kutokana na kukosa walimu wa kutosha hali inayofanya mikoa hiyo kushikia mikia katika matokeo ya mwisho kama ilivyo sasa kwa mikoa ya kusini.
Serikali kupitia Wizara ya Elimu ilisema lengo la kufanya hivyo ni kupata uwiano wa mwalimu mmoja kwa wanafunzi 10 hali itakayosaidia kunyanyua kiwango cha elimu katika mikoa iliyo pembezoni mwaka nchi.
Hivyo naamini fursa hiyo ikiwa itatumiwa vema na wananchi wa huko itafanya viwanda vinavyojengwa sasa katika mikoa hiyo wenyeji kunufaika kazi zaidi kuliko wageni ndio madhumuni makubwa ya baadhi ya wawekezaji.
Kwa maana wapo wanaotoa ahadi kuwa ikiwa viwanda vyao vitamalizika waajili wenyeji kwa asilimia zaidi ya 60, lakini ikiwa hali ya elimu itaendelea kuwa hivyo ni dhairi wageni watakuwa na nafasi kubwa kuliko wazawa.
Viongozi wa mikoa ya pembezoni mwa Tanzania ikiwemo ya kusini kazi kwenu kuhakikisha mnahamasisha wananchi wenu wanatumia fursa inayotolewa na Serikali kupeleka walimu vijijini inatumiwa vizuri na matunda yaonekana.
Pia kwa Serikali ni vema ikatambu kuwa si walimu pekee wanahitajika katika mikoa hiyo iliyo pembezoni mwa Tanzania bali vyenzo za kufundishi nazo ni muhimu, itakuwa haina maana kupeleka walimu bila ya vitendea kazi na kuwajengea miondo mbinu mingine ikiwemi malazi bora.
Kwani upo uhushuhuda kuwa walimu wengi wanakacha kwenda kufundisha vijini kutokana na kutopatiwa mahitaji muhimu ya kibinadamu ikiwemo usafiri, nyumba nzuri za kuishi na kuishi katika maboma.
 Maoni: 0782839898

January 12, 2013

WANAWAKE NA WANAUME: HAKI SAWA NA USOMI

Jackline Mluge, Finland

Na Jackline Mluge, Finland

WANAWAKE VIPI? katika ulingo wa ndondi kuna raundi 1 hadi 12. zamani wakati raundi moja kwenda nyingine inapokwisha, kuna wanaume walikuwa wamevishwa suti au mavazi safi kutangaza raundi inayokuja ni ya ngapi. 
SIKU hizi WANAWAKE wanatumika kutangaza raundi huku wakiwa wamevishwa vichupi, au mavazi ambayo yanaonyesha nusu uchi kabisa, wanatembea kwa mikogo sana. Nini hicho? 
Hapa bongo utaona WANAWAKE wanavaa visuluwali vya mazoezi na kugeza kuwa mtoko wa siku, wanasema fasheni. Kila sehemu ya mwili huonekana, kama minyama au kiuno maridadi na kadhalika. WANAWAKE mnajidhalilisha ama? naendelea ....
Sasa hivi wanawake wanafanya kazi zote ambazo wanaume wanafanya. Ilikuwa zamani lakini si kwa sasa ila wanaume ndio wanao ji dhalilisha kwa sasa unakuta dumezima lina baka mtoto.Mimi na pingana kabisa haki sawa kwa jinsia zote
simpenzi wa nguo fupi lakini nadhani kila mtu ana uhuru wa kuvaa anachotaka hiyo siyo kujidhalilisha. 
Na kuhusu kujiuza kuna wanaume wanajiuza kwa akina mama wenye pesa tena wanapanga mstari unachagua kama nguo, na sasa wanawake wanajibadilisha kuwa wanaume na wanaume wanajibadilisha kuwa wanawake. Hao wanafunzi wanaojiuza wamezoea kujiuza sisababu hawajapata mkopo- mfano nasoma chuo cha Afya napata hela kidogo kutoka serikalini lakini muda wangu wa ziada nafanya kazi ya fani ninayosomea au hata nyingine kujipatia hela za matumizi na wakati huohuo na soma. 
Naamini unapokuwa chuo si mtoto tena umefikia umri wa kujitegemea kiamawazo lakini nia aibu mtu mzima kufundishwa kuacha umalaya, Hebu niambie wakimaliza chuo wasipopata kazi watalalamika kazi hakuna ngoja tuendelee kujiuza. 
Limenisikitisha sana kuona watu wenye elimu bado wanakili za kulalamika kitu fulani badala ya kuchagua njia mbadala ya kutatua matatizo yao mfano mnaweza kuanzisha kuuza sambusa hostel unajipatia pesa tatizo la wasomi wa Tanzania mtu akifika chuo hataki kufanya kazi mbaya mbaya anataka kufanya kazi hiyo hiyo aliyosomea huku kuna watu wanasomea uanasheria au uganga nk lakini utakuta wanafanya kazi ya kuuza baa kipindi wanasoma wakijipatia hela za kujikimi na mtu aoni aibu.Tanzania ehiii amka sasa acheni porojo.

January 11, 2013

CCM IMERUHUSU YENYEWE KUKABWA KOO NA UPINZANI


Na Markus Mpangala, Dar es Salaam

Kuna dhana moja kwamba vyama vya upinzani ni uadui. Kimsingi jambo hilo sio kweli na lazima tukemee kuwa kazi ya vyama vya upinzani ni kuikumbusha serikali kupitia chama kinachotawala. Hivyo basi kazi ya serikali ya CCM ni kuhakikisha kuwa masuala ya msingi ndani ya nchi yanafanyika ipasavyo. 
Haiwezekani wapinzani wakaibuka tu kutoka porini na kuanza kupinga ama kulalamikia jambo fulani. Lazima wameketi chini na kuona namna ambavyo CCM inakosea na makosa hayo ni dosari tu ambayo inatakiwa kufanyiwa kazi. Vivyo hivyo kazi ya CCM sio kulalamika kuwa kwanini wapinzani hawashiriki kutatua kero ya nchi yetu. Kazi ya vyama vya upinzani ile kukosoa na kukishambulia CCM maana yake wanatimiza wajibu wa kuikumbusha serikali ya CCM kuwa kuna mahali hapaendi vizuri. 
Kwahiyo Kazi ya mpinzani ni kukupinga. Dosari yako ni faida kwake. Yapo maeneo ambayo vyama vyote vinapaswa kushirikiana, mathalani lile kongomano lililoandaliwa na ofisi ya msajili wa vyama vya siasa kuhusu ulinzi, usalama na demokrasia, mbali ya Chadema kususia. Lakini neno kubwa hapa ni kwamba mpinzani akiona dosari zako ndio kete yake ya kupata ushindi.  
Ukitaka mpinzani wako asipate kete ya ushindi hakika unaziba mianya yote ya kumfanya apate kete. kwanza, hakika Ilani ya chama chako inatekelezwa, ahadi zote zinatimizwa. njia mpya za uchumi zinavumbuliwa maana watalamu wapo. mkondo mpya wa kuibua maendeleo unatakiwa kupatikana, vivyo hivyo unapaswa kuelewa kuwa anayesababisha vyama vya upinzani kupata la kusema ni chama tawala chenyewe. 
CCM ikijikita kwenye shughuli za kutimiza maazimio yake kwa wananchi, sidhani kama ni vibaya. MTAJI KISIASA, inawezekana hata Mheshimiwa mbunge wa Nzega alipokemea kuhusu uchimbaji madini na kuhimiza watu kugoma ni MTAJI PIA. Sijui wanasiasa wetu wanatafsiri namna gani juu ya mtaji wa kisiasa. Na kugoma ilikuwa hatua ya mwisho pale Nzega mjini Tabora ili serikali isikilize kilio cha wachimbaji wadogo wa madini. MUHIMU; CCM timizeni mliyokusudia kwa maendeleo ya wananchi. do it all utaona kama akina sisi huku pembeni kama tutakosoa. Ni faida kwenu na kwa wananchi sisi.

WILAYA YA MBINGA YAENDESHA KAMPENI YA UPANDAJI MITI

Ambroce Nkwera, Mbinga
Na Ambroce Nkwera, Mbinga

Wilaya ya Mbinga imeendendelea na kampeni kubwa ya upandaji miti kwenye maeneo mbalimbali ya wilaya hii. Hatua hii inalenga kulinda na kuhifadhi mazingira ya wilaya Mbinga ikiwemo kupambana na mabadiliko ya tabia nchi. Wananchi mbalimbali walijumuika katika kapeni hii ambayo imewahusisha watu wa kada mbalimbali, maofisa wa serikali na asasi binafsi wilayani hapa.
Wananchi wamehimizwa sana umuhimu wa kupanda miti kila wanapokata na hata pale wasipokata. kwa mujibu wa azimio la Halimashauri ya Wilaya Mbinga, kila mwananchi anataiwa kushiriki ikiwa sehemu ya mipango ya maendeleo ya uchumi kwa kulinda mazingira ya wilaya hii. mwandishi wa Habari hizi amefanikiwa kupata miti 700 ambayo amefanikisha kusafirisha hadi kijiji cha Mkali kilichopo katika wilaya ya Nyasa kwa lengo la kuendeleza kampeni ya kupanda miti. 
Kwa mujibu wa ratiba ya kampeni ya upandaji miti, itapita katika vijiji mbalimbali vinavyounda wilaya ya Mbinga huku uwezekano wa kampeni hizo kuhamia wilaya ya Nyasa ni mkubwa. Ikumbukwe kuwa wilaya ya Nyasa ni mpya ikwia bado inategemea watendaji kutoka wilaya ya Mbinga, hivyo kampeni hizo zitakwenda sambamba na uhamasishaji wa utunzaji mazingira kwa wilaya ya Nyasa ili kuepuka ukame unaoweza kutokea. Kampeni hii imevutia wengi na wananchi wamepanda miti ya kutosha.
Kulikuwa na mkakati wa upandaji miti na bado unaendelea, awamu ya kwanza waliotesha miti laki nne(400,000) yote wakawagawi wananchi bure na ikaisha awamu ya pili ndio hii, pia wamegawa miti karibu laki moja(100,000) na imeisha. Wananchi wameitikia mwito huu kwa ari kubwa sana. Tumegundua kuwa wananchi walikuwa wakikosa msukumo hivyo hatua hii imesaidia zaidi kufanikisha kusambaza habari za utunzaji wa mazingira kwa maendeleo yao.
Mipango mingine juu ya kusambaza na kuelimisha umuhimu wa upandaji miti inaendelea hapa Mbinga, huku halmashauri ya Wilaya kwa kushirikiana na baraza la Madiwani na wabunge wake kuhakikisha mpango huu unakwenda safi na kuboresha mazingira. Aidha, tunatarajia mpango huu utafikishwa hadi wilaya ya Nyasa kama ilivyokusudiwa ili kukabiliana na ukame, pamoja na kuhifadhi mazingira. Tunawakaribishana wana Mbinga wote kutimiza ajenda hii ya kutunza na kuendeleza mazingira ili yawe bora kwa afya bora. Hilo litasaidia kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi.

UCHAWI: DHANA INAYOANGAMIZA JAMII YETU



Na John Chitanya, Nyasa

Mei 4, 2012 yalifanyika maandamano makubwa sana katika wilaya mpya ya Nyasa iliyogawanywa kutoka wilaya ya Mbinga. Nyasa ni wilaya ni kiserikali, lakini katika Tume ya Taifa ya Uchaguzi inafahamika kama jimbo la Mbinga Magharibi. Maandamano yaliyofanyika yalilenga kuishinikiza serikali kumruhusu Mganga wa Kienyeji apewe  kibali cha kufanya kazi yake ya kuwaumbua wachawi wilayani hapa.
Maandamano yale yalionyesha na televisheni ya TBC1  wakazi wa mji wa Kilosa nje kidogo ya mji mdogo wa Mbamba Bay, kwa hakika ilikuwa fedheha kubwa kwa wananchi wa ukanda wa ziwa Nyasa na maeneo mengine yanayounda wilaya hiyo kwa upande wa mashariki ambayo yanakaliwa na jamii ya Wamatengo.
Kwa mtazamo wangu kama kuumbuana na kushika uchawi  wameshikana sana,  sasa tunataka maendeleo sio kuimba nyimbo za wachawi kuwanyima maendeleo baadhi ya watu.  
Watu wengi wanaamini kuwa kuna kasoro pale inapotokea jambo fulani likawa baya, basi linazungumzwa kuwa linatokana na kurogwa na wachawi.
Mganga wa kienyeji
Niliwahi kushuhudia tukio moja kwa moja ya familia iliyokuwa ikiendesha kikao cha kifamilia, kwamba binti mmoja wa shule ya msingi alishindwa kusoma na kuandika hivyo walipanga kwenda kwa Mganga wa Kienyeji ‘kumfungua” kwa madai alifungwa na watu wabaya(wachawi) asiweze kujua kusoma na kuandika.
Hakika suala hilo lilileta mtafaruku kwa wale waliofanikiwa kwenda shule, wakadai kuwa hilo ni suala la mwanafunzi mwenyewe wala halina uhusiano na kufungwa kwa misingi ya uchawi. Lakini ilishikiliwa uchawi ndio umemfunga binti yule. Hadi naandika makala hii juhudi za kumfikisha mwanafunzi yule kwa Mganga wa kienyeji zilikuwa zimesimishwa ila sina shaka zitaendelea kwani nia yao ipo na wanaonekana kuamiani sana uchawi umetumika kwa binti yule.
Matukio ya uchawi yamekuwa yakitangazwa sana hata wakati uchaguzi unapofanyika, kwani wagombea mbalimbali wanadaiwa kuwategemea waganga wa kienyeji, wapiga ramli na kuamua hatima ya harakati zao. Kwenye michezo ya mpira wa miguu na mingine suala la uchawi limekuwa likichukua nafasi kubwa bila kutegemea sayansi ya kuleta mafanikio.
Hatua za vigogo kuhangaika na kuwategemea waganga wa kienyeji inaleta ujumbe kuwa jamii yetu inakabiliwa sana na janga la uchawi na kutoamini nguvu zilizomo kwenye akili na miili yetu.
Leo hii ni vigumu kufanya jambo la maajabu kwa kutohusisha uchawi. Hapa ndipo mimi siku zote huamini mapinduzi ya maendeleo ya wilaya ya Nyasa na yale yenye kasumba za kutegemea wachawi yanapaswa kuanzia katika fikra zetu. Tuna mambo mengi ya kuyafanyia maandamano katika nchi hii, mfano umeme, bandari, barabara isiyoisha na mengine mengi, lakini wananchi wameshikilia na kuamini kuwa uchawi umesababisha wawe na maisha duni.
Hata hivyo tukio la mji wa Kilosa, waliohamasishwa mapema mwezi Mei, ili Mganga wa kienyeji kutoka Tanga walikamatwa na mamlaka zinazohusika. Mganga huyo alihamasisha vijana wa Mbamba Bay wafanye fujo kushinikiza apewe kibali ili atoe uchawi kwenye nyumba za watu, basi wale vijana wakavunja ofisi za serikali na kuchoma moto, huku  wakalazimisha kila familia kuchangia shilingi 5000.
Mamlaka zinazohusika zilifanikiwa kuzima jaribio hilo, na kuwakamata baadhi ya vijana waliohusika. Baadhi ya vijana yao ni mabinti watatu waliokamatwa kwa kosa la kuandamana bila kibali na kufanya vurugu, walishikiliwa mjini Kilosa, Mbamba Bay. Tukio hilo linaturejesha kwenye mjadala hivi masuala ya uchawi yanachukuliwaje kama turufu ya kufanya uhalifu au uvunjifu wa amani? Uchawi umekuwa ukizungumziwa sana katika jamii zetu.
Wafanyabiashara wanategemea uchawi, watu wa kawaida wanategemea uchawi, ina maana hata masuala yenye kuhitaji utaalamu yamepewa dhana ya uchawi. Jamii yetu imeshikilia dhana ya uchawi kama nyenzo ya kupata mafanikio. Wengi hushikilia sana kupiga ramli, wamekuwa wakishindwa kujielemisha na kupata ufumbuzi wa matatizo ya familia na jamii huku wakiamini matukio hayo yanatokana na uchawi. 
Idadi ya wapiga ramli nayo inaongezeka kila kukicha. Ulimwengu unatuacha nyuma, na kila mwenye mafanikio maishani anaweza kutazamwa kwa namna mbili; mosi aliiba mahli na pili amefanya uchawi. Hakuna watu wanaoamini kuwa juhudi hizo zimefanywa na mhusika. Kuna masimulizi mengi sana kwa wana jamii ya wilaya ya Nyasa kuhusiana na uchawi. Magari yakipinduka husemwa uchawi, hakuna anayesema kuwa barabara ni mbovu, wote husikilia uchawi.
Kuna mambo mengi yanatisha na bila juhudi za serikali kusambaza elimu kila jambo lingeonekana kwua uchawi. Na serikali yetu haiamini uchawi hivyo ni kosa la mtu kufanya fujo kama vijana wale kwa kisingizio cha uchawi. Sio hapa tu, hata Afrika Kusini, aliyekuwa kocha wa timu ya taifa ya nchi hiyo, Pits Mosimame aliwahi kukaririwa na vyombo vya habari akijibu swali kwanini Bafana Bafana haijashinda mechi nyingi tangu achukue madaraka.
Naye  alijibu kwa urahisi kuwa shirikisho la soka la Afrika Kusini halijamlipa Sangoma (mganga wa kienyeji) tangu michuano ya kombe la dunia. Hali hiyo inaonyesha namna gani jamii imetawaliwa na uchawi. Kila kitu tunachofanya kinaonekana kimetokana na uchawi. Wachawi wamekuwa vikwazo kwenye mafanikio ya jamii yetu.
Dhana hii ya uchawi itaendelea kutuangamiza ikiwa juhudi za makusudi hazitachukuliwa. Kwa mtazamo wangu, naona uchawi ni sumu kali sana, lakini kama uchawi wa kisayansi basi nitasema kila nchi inao uchawi.
Nasema kila nchi inao uchawi kwa maana ya kisayansi kutokana na mila na desturi za nchi hiyo. Ujerumani walileta utabiri wa Pweza Paul, akatabiri ushindi kwa wahispania. Nao ni uchawi kama wapiga ramli za kisayansi sio mazingaombwe. Zipo nchi zinatumia uchawi wa kisayansi kwa njia ya maneno hususani katika dini,  “kuapishwa” au “kusimikwa”, kinachotendeka ni uchawi, ni mila na desturi za nchi husika na tamaduni zao. Mikoa ya kanda ya ziwa inakabiliwa na dhana hii ya uchawi imesababisha hofu kwa ndugu zetu albino, na wazee wenye macho mekundu. Wazee hao huuawa kwa kisingizio eti wachawi. Nionavyo uchawi uliosababisha watu wa mji wa Kilosa waandamane mapema mwezi Mei mwaka huu ni sumu kali sana, na kawaida sumu haiwezi kutibu ugonjwa mwingine, kwani huua.

John Chitanya ni mwandishi na mwalimu wa Miracle Center, mjini Songea. Niandikie: 0718 005557

NIDHAMU YA WALIMU WETU KAMA WANAMUZIKI WA BONGOFLEVA


Na John Chitanya, Nyasa
Naandika baada ya kufanya ziara fupi kutembelea shule ya sekondari ya Monica Mbega iliyopo Kata ya Mbaha katika Tarafa ya Ruhuhu. Nilianza safari yangu katka kijiji cha Lundu kuelekea Mbaha, ambapo umbali wake ni kilimita 1, niliwasili shuleni hapo yapata saa asubuhi.
Lengo la safari hiyo ni sehemu ya mkakati wa kutembelea shule zote za Kata katika Tarafa ya Ruhuhu, kisha shule za Tarafa ya Ruhekei kwenye wilaya mpya ya Nyasa. Nilipowasili shule hapo nilikusudia kuangalia mazingira ya shule na namna gani walimu wa shule hiyo wanavyowasilia katika uwajibikaji wao kwa wanafunzi na namna gani wanafunzi wanawajibika kwa walimu wao ili kujenga nidhamu na mafanikio ya shule.
Nidhamu baina ya mwalimu na mwanafunzi ndio msingi mkuu wa kulefa mafanikio ya shule yoyote.
Mpaka naondoka shuleni hapo saa moja na nusu sikufanikiwa kumuona mwalimu yeyote hata wa zamu hakuwepo, mazingira ya wanafunzi nao wapo kama wapo msibani hakuna shughuli za usafi wa mazingira. Nilijaribu kumhoji mmoja wa wanafunzi kama wamefanya ‘roll call’, nikaambiwa muda bado haujafika. Wakati huo ilikuwa saa moja na robo. Mpaka muda huo nilikuwa na wanafunzi wasiozidi 50.
Wanafunzi wa shule ya msingi Mango, wilayani Nyasa. 
Picha kwa Hisani ya Tanzglo
Na kati yao hapakuwa na mwenye saa. Picha hiyo unatarajia patakuwa na hali nzuri kimasomo, wajibu na nidhamu kati ya mwalimu na mwanafunzi? Kwahiyo hali nzuri ya kitaaluma kwa shule kama hiyo sio jambo linaloweza kutokea, kwa vile mwanafunzi hurithi tabia za wakubwa naamini wanafunzi watakuwa katika hali gani kitabia na kitaaluma toka kwa walimu hao? Kama mwalimu ni mvivu kuwahi shule unatarajia atapanda mbegu gani kwa wanafunzi wake? Nilipojaribu kutaka kujua kama walimu wanakaa mbali na maeneo ya shule niliambiwa wote wanakaa ndani  ya mita 100 toka shuleni hapo. Je unatarajia nini kwa shule kama hiyo?
Nilifanya ziara hiyo kwakuwa mwezi wa pili nilikuwa katika kikao cha tathmini ya matokeo ya mitihani ya taifa kwa kidato cha pili na nne. Nilienda kwa niaba ya mzee kwa wanafunzi. Katika matokeo ya kidato cha pili walikuwa wanafunzi sio chini ya 47, lakini waliovuka wastani ni wanafunzi watatu tu. Katika matokeo ya kidato cha nne hawakuzidi wanafunzi 37, lakini waliopata vyeti kwa daraja la nne kwa pointi  29-33 ni wanafunzi 6 pekee na wanafunzi waliobaki walifeli.
Wakati ule mkuu wa shule alijitetea kwenye kikao cha tathmini kuwa shule haikuwa na walimu  wa kutosha kwani walikuwa watatu tu. Kwa sasa shule hiyo ina walimu 8 bado hawatoshi. Kama walimu 8 hawafiki darasani kwa muda mwafaka wakiwa walimu 20 itakuwaje hali ya shule hiyo? Sitakosea nikisema walimu hao ipo siku watafika shuleni saa sita mchana kwa kufuata muda wa vipindi vyao tu? Leo nimekumbuka msemo wa walimu  wa siku hizi  ni walimu wa bongofleva wanafika shuleni wamevaa suluali za jeans. Na wao wanajitetea kuwa ualimu sasa sio wito bali kazi, na kama wito ulikuwa zamani sana. Sijui, natafakari tu.

•    John Chitanya, ni mwandishi na mwalimu wa Miracle Center iliyopo Songea. Maoni: 0718 005557