January 18, 2013

NIMEBOBEA KATIKA UFUGAJI WA NYUKI KWA NJIA ZA KISASA-ERNEST NDONDE

Na Mwandishi Wetu, Mbinga

Miongoni mwa mabadiliko makubwa ya ufugaji wa nyuki ni ile hatua ya watu kuamua kujitoa kwa dhati kabisa kupata mafunzo ya ufugaji wa nyuki. Wengi tumezoea kuona njia za zamani ambazo zinawafanya baadhi ya watu wasio watalaamu kuelezea kuwa wanasumbuliwa na ufugaji wa nyuki pamoja na ulinaji asali kwa ujumla. 
Lakini kijana Ernest Ndonde kutoka Lundu alifanya mazungumzo na Lundunyasa Network, kuelezea juu ya utaalamu wake aliopata huko Mpanda wa kufuga nyuki. 
Yeye anasema wka sasa anakaribia kuanzisha mradi wa ufugaji nyuki katika kijiji cha Mbaha ambacho ni kipo jirani kabisa na kijiji cha Lundu, katika tarafa ya Ruhuhu wilayani Nyasa. Ernest Ndonde aliamua kuchukua ujuzi wa kufuga nyuki wka njia za kisasa kutokana na mahitaji na mabadiliko ya namna ya kulina asali na wateja wake. 
Pia alichukua njia hiyo kuwa moja ya utaalamu ambao anaufanyia kazi katika maeneo mbalimbali ambayo wateja huhitaji mafunzo ya ufugaji nyuki kwa njia za kisasa. Akiwa mjini Mbinga alisema, "Niliamua kuchukua mafunzo hayo ili kufanya kazi hiyo kwa njia za kuboresha maisha ya watu na binafsi. Naelewa ufugaji wa nyuki haufanywi kwa njia za kisasa lakini sasa nina utaalau huo nitafanya na kila mmoja kulingana na mahitaji yake na popote nchini". 
Kwa mujibu wa bwana Ndonde ni kwamba ameona kuna haja ya kuwekeza kupitia ufugaji wa nyuki kuliko wote kutegemea upande mmoja ambao kwa kiasi fulani unazorotesha mahitaji na kuinuka kiuchumi kwa baadhi ya vijana. 
Lundunyasa Network ilimuuliza kama yuko tayari kufanya kazi za watu wengine ambao watahitaji utaalamu wake, yeye alisema haya, "Utaalamu wangu ninaufanya kwa yeyote anayehitaji. Jambo muhimu ni makubaliano ambayo yanaleta faida kwa pande zote, hivyo sote tutaweza kuinuka kiuchumi kwa kuifanya kazi kwa ufasaha zaidi. 
Alisema pia kwa wale wanaohitaji huduma zake za kutoa mafunzo ya ufugaji wa nyuki kwa njia za kisasa wanaweza kuwasiliana naye kwa simu;  0759 965843, 0777665843, 0684965843 au 0655965843 au wka barua pepe; ernestndonde@ymail.com. Naam na Lundunyasa Network inamtakia kila la heri katika utaalamu wake huu mpya ili aweze kusaidia watanzania wanaopendelea kufugaji nyuki na wale wanaotarajiwa kufuga nyuki hapo baadaye.

January 15, 2013

MRADI WA MAJI KIJIJI CHA NG'OMBO WAKAMILIKA

Na Mwandishi  wetu, Ng'ombo
Wakazi zaidi ya 2450 wa kijiji cha Ng’ombo katika Kata ya Chiwanda wilayani Nyasa mkoani Ruvuma wameondokana na adha iliyokuwa ikiwakabili ya upatikanaji wa maji safi na salama baada ya kukamilika kwa ujenzi wa mradi wa maji kijijini hapo,

Akizungumza na Lundunyasa Network, Mhandisi wa Maji wa Wilaya hiyo Amos Mtweve alisema mradi huo ambao umejengwa kwa ufadhili wa UNDP kupitia Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira umegharimu jumla ya shilingi 298,346,700 na kwamba kuna vituo 23 ambavyo wakazi wa kijiji hicho watakuwa wakivitumia kupata maji.
Mhandisi Mtweve alisema kuwa kabla ya kujengwa kwa mradi huo wananchi walikuwa wakilazimika kutumia maji ya ziwa Nyasa kwa ajili ya kunywa, kupikia, na kuoga hali ambayo ilikuwa ikihatarisha usalama wa afya zao.
Alisema pamoja na changamoto mbalimbali zilizokuwa zikijitokeza wakati wote wa ujenzi wa mradi huo ikiwemo baadhi ya wananchi kutojitokeza kuchangia nguvu zao kama uchimbaji wa mtaro kwa ajili ya kulaza mabomba lakini bado mradi umekamilika kwa kwango kilichotakiwa.
“kukamilika kwa mradi huu kimsingi ni sifa kubwa kwetu kwani itawapa matumaini wafadhili wetu kufadhili miradi mingine hasa ikizingatiwa kuwa UNDP wamefadhili miradi michache ya maji hapa nchini ikiwemo huu wa kwetu,” alisema Mhandisi Amos Mtweve.

MIKOA YA MTWARA,LINDI NA RUVUMA TAFUTENI SULUHU KUFELI MITIHANI

Na Hamisi Magendela , Dar es Salaam
SIKU chache zilizopita wananchi wa mikoa ya kusini waliandamana kupinga uchimbaji wa bomba la gesi kutoka huko kwenda Dar es Salaam ambacho ingetumika kwa ajili ya kuzalisha umeme.
wanafunzi wakiwa darasani katika moja ya shule za msingi wilayani Nyasa
Umeme huo ambao ungezalishwa jijini Dar es Salaam ungetumika katika mikoa mbalimbali ya Tanzania hali ambayo inaaminika kuwa itasaidia kupungua ghalama za umeme na kufanya ukali wa maisha kupungua.
Sipingi mawazo yao kwani kila mmoja anafikilia kwa utashi wake japo ni vema wakaangalia faida kuliko na mafanikio yatakayopatika siku za usoni ikiwa gesi hiyo itasafilishwa kwa njia ya bomba kwenda Dar es Salaam.
Kikumbwa ambacho naweza kusema ni kwa wananchi wa mikoa ya kusini wanatatizo makubwa zaidi ya kuandamana kutaka manufaiko ya gesi wakati suala zima la elimu likiwa limewatupa mkono kiasi kwamba inatia simanzi kuona inashika nafasi 10 za mwisho katika ufauru wa matokeo ya kidato cha pili yalitangazwa juzi na Wizara ya Elimu na Mafunzo jijini Dar  es Salaam jana.
Licha ya kuwa ni aibu kwa wananchi pamoja na viongozi wa mkoa huo lakini naweza kusema kuwa ni kashfa ambayo katika miaka 50 ya Uhuru ijayo inatakiwa kufanyiwa kazi ili kuhakikisha wanapata elimu ya kutosha na kuondoka na ujinga wa kukosa elimu.
Ingekuwa vema zaidi badala ya kulalamikia kuhusu gesi wangepiga kelele kwa kukosa elimu bora kwa wanachi wengi wa mikoa hiyo hali inawafanya kukosa nafasi nzuri katika viwanda vinavyojengwa katika mikoa.
Kwa maana nafasi nzuri ya ajira itakuwa ikishirikiliwa na wageni ambao wana elimu ya kutosha ya kukidhi mahitaji ya kazi inayohitajika kwa wakati huo na kufanya wenyeji kufanya kazi za hali ya chini kila siku.
Pia wananchi wa mikoa ya kusini umefikia wakati wa kusimama kidete kuhakikisha fursa iliyotangazwa na Serikali kuwa kuanzia sasa hakutakuwa na mwalimu atakaepangiwa kazi mijini kwa wanaotoka vyuoni.
Kwa maana hiyo ikiwa viongozi wa mikoa hiyo wakitumia fursa hiyo kuwahamasisha wananchi wa kuzingatia elimu badala ya kung'ang'ani masuala ambayo kwa sasa hayasaidii sana katika miaka 50 ijayo.
Kusudio hilo la Serikali kupeleka walimu vijini linatokana na malalamiko kutoka sehemu hizo kuwa zimesahaurika kielimu kutokana na kukosa walimu wa kutosha hali inayofanya mikoa hiyo kushikia mikia katika matokeo ya mwisho kama ilivyo sasa kwa mikoa ya kusini.
Serikali kupitia Wizara ya Elimu ilisema lengo la kufanya hivyo ni kupata uwiano wa mwalimu mmoja kwa wanafunzi 10 hali itakayosaidia kunyanyua kiwango cha elimu katika mikoa iliyo pembezoni mwaka nchi.
Hivyo naamini fursa hiyo ikiwa itatumiwa vema na wananchi wa huko itafanya viwanda vinavyojengwa sasa katika mikoa hiyo wenyeji kunufaika kazi zaidi kuliko wageni ndio madhumuni makubwa ya baadhi ya wawekezaji.
Kwa maana wapo wanaotoa ahadi kuwa ikiwa viwanda vyao vitamalizika waajili wenyeji kwa asilimia zaidi ya 60, lakini ikiwa hali ya elimu itaendelea kuwa hivyo ni dhairi wageni watakuwa na nafasi kubwa kuliko wazawa.
Viongozi wa mikoa ya pembezoni mwa Tanzania ikiwemo ya kusini kazi kwenu kuhakikisha mnahamasisha wananchi wenu wanatumia fursa inayotolewa na Serikali kupeleka walimu vijijini inatumiwa vizuri na matunda yaonekana.
Pia kwa Serikali ni vema ikatambu kuwa si walimu pekee wanahitajika katika mikoa hiyo iliyo pembezoni mwa Tanzania bali vyenzo za kufundishi nazo ni muhimu, itakuwa haina maana kupeleka walimu bila ya vitendea kazi na kuwajengea miondo mbinu mingine ikiwemi malazi bora.
Kwani upo uhushuhuda kuwa walimu wengi wanakacha kwenda kufundisha vijini kutokana na kutopatiwa mahitaji muhimu ya kibinadamu ikiwemo usafiri, nyumba nzuri za kuishi na kuishi katika maboma.
 Maoni: 0782839898

January 12, 2013

WANAWAKE NA WANAUME: HAKI SAWA NA USOMI

Jackline Mluge, Finland

Na Jackline Mluge, Finland

WANAWAKE VIPI? katika ulingo wa ndondi kuna raundi 1 hadi 12. zamani wakati raundi moja kwenda nyingine inapokwisha, kuna wanaume walikuwa wamevishwa suti au mavazi safi kutangaza raundi inayokuja ni ya ngapi. 
SIKU hizi WANAWAKE wanatumika kutangaza raundi huku wakiwa wamevishwa vichupi, au mavazi ambayo yanaonyesha nusu uchi kabisa, wanatembea kwa mikogo sana. Nini hicho? 
Hapa bongo utaona WANAWAKE wanavaa visuluwali vya mazoezi na kugeza kuwa mtoko wa siku, wanasema fasheni. Kila sehemu ya mwili huonekana, kama minyama au kiuno maridadi na kadhalika. WANAWAKE mnajidhalilisha ama? naendelea ....
Sasa hivi wanawake wanafanya kazi zote ambazo wanaume wanafanya. Ilikuwa zamani lakini si kwa sasa ila wanaume ndio wanao ji dhalilisha kwa sasa unakuta dumezima lina baka mtoto.Mimi na pingana kabisa haki sawa kwa jinsia zote
simpenzi wa nguo fupi lakini nadhani kila mtu ana uhuru wa kuvaa anachotaka hiyo siyo kujidhalilisha. 
Na kuhusu kujiuza kuna wanaume wanajiuza kwa akina mama wenye pesa tena wanapanga mstari unachagua kama nguo, na sasa wanawake wanajibadilisha kuwa wanaume na wanaume wanajibadilisha kuwa wanawake. Hao wanafunzi wanaojiuza wamezoea kujiuza sisababu hawajapata mkopo- mfano nasoma chuo cha Afya napata hela kidogo kutoka serikalini lakini muda wangu wa ziada nafanya kazi ya fani ninayosomea au hata nyingine kujipatia hela za matumizi na wakati huohuo na soma. 
Naamini unapokuwa chuo si mtoto tena umefikia umri wa kujitegemea kiamawazo lakini nia aibu mtu mzima kufundishwa kuacha umalaya, Hebu niambie wakimaliza chuo wasipopata kazi watalalamika kazi hakuna ngoja tuendelee kujiuza. 
Limenisikitisha sana kuona watu wenye elimu bado wanakili za kulalamika kitu fulani badala ya kuchagua njia mbadala ya kutatua matatizo yao mfano mnaweza kuanzisha kuuza sambusa hostel unajipatia pesa tatizo la wasomi wa Tanzania mtu akifika chuo hataki kufanya kazi mbaya mbaya anataka kufanya kazi hiyo hiyo aliyosomea huku kuna watu wanasomea uanasheria au uganga nk lakini utakuta wanafanya kazi ya kuuza baa kipindi wanasoma wakijipatia hela za kujikimi na mtu aoni aibu.Tanzania ehiii amka sasa acheni porojo.