Na Mwandishi Wetu, Mbinga
Miongoni mwa mabadiliko makubwa ya ufugaji wa nyuki ni ile hatua ya watu kuamua kujitoa kwa dhati kabisa kupata mafunzo ya ufugaji wa nyuki. Wengi tumezoea kuona njia za zamani ambazo zinawafanya baadhi ya watu wasio watalaamu kuelezea kuwa wanasumbuliwa na ufugaji wa nyuki pamoja na ulinaji asali kwa ujumla.
Lakini kijana Ernest Ndonde kutoka Lundu alifanya mazungumzo na Lundunyasa Network, kuelezea juu ya utaalamu wake aliopata huko Mpanda wa kufuga nyuki.
Yeye anasema wka sasa anakaribia kuanzisha mradi wa ufugaji nyuki katika kijiji cha Mbaha ambacho ni kipo jirani kabisa na kijiji cha Lundu, katika tarafa ya Ruhuhu wilayani Nyasa. Ernest Ndonde aliamua kuchukua ujuzi wa kufuga nyuki wka njia za kisasa kutokana na mahitaji na mabadiliko ya namna ya kulina asali na wateja wake.
Pia alichukua njia hiyo kuwa moja ya utaalamu ambao anaufanyia kazi katika maeneo mbalimbali ambayo wateja huhitaji mafunzo ya ufugaji nyuki kwa njia za kisasa. Akiwa mjini Mbinga alisema, "Niliamua kuchukua mafunzo hayo ili kufanya kazi hiyo kwa njia za kuboresha maisha ya watu na binafsi. Naelewa ufugaji wa nyuki haufanywi kwa njia za kisasa lakini sasa nina utaalau huo nitafanya na kila mmoja kulingana na mahitaji yake na popote nchini".
Kwa mujibu wa bwana Ndonde ni kwamba ameona kuna haja ya kuwekeza kupitia ufugaji wa nyuki kuliko wote kutegemea upande mmoja ambao kwa kiasi fulani unazorotesha mahitaji na kuinuka kiuchumi kwa baadhi ya vijana.
Lundunyasa Network ilimuuliza kama yuko tayari kufanya kazi za watu wengine ambao watahitaji utaalamu wake, yeye alisema haya, "Utaalamu wangu ninaufanya kwa yeyote anayehitaji. Jambo muhimu ni makubaliano ambayo yanaleta faida kwa pande zote, hivyo sote tutaweza kuinuka kiuchumi kwa kuifanya kazi kwa ufasaha zaidi.
Alisema pia kwa wale wanaohitaji huduma zake za kutoa mafunzo ya ufugaji wa nyuki kwa njia za kisasa wanaweza kuwasiliana naye kwa simu; 0759 965843, 0777665843, 0684965843 au 0655965843 au wka barua pepe; ernestndonde@ymail.com. Naam na Lundunyasa Network inamtakia kila la heri katika utaalamu wake huu mpya ili aweze kusaidia watanzania wanaopendelea kufugaji nyuki na wale wanaotarajiwa kufuga nyuki hapo baadaye.


