April 03, 2013

GHASIA ZA TUNDUMA, HALI SIO NZURI SANA


Ghasia zinazoendelea katika mji wa Tunduma ulioko mkoani  Mbeya zimechochea uharibifu kijamii. Tunduma haiko katika hali nzuri.

Vurugu kama hizo ziliwahi kutokea mjini Mwanza na kuhusisha wamumini wa imani ya kikristo na Kiislamu. Mauaji yalitokea na serikali ilifanya juhudi kuwakamata wahusika.  

Hapa mwakilishi wa Blogu ya Lundunyasa, anaelezea kwa ufupi sana juu ya kile kinachoendelea mjini humo.

Ni kwamba inaelekea hotuba ya Rais Jakaya Kikwete kuhusu uchinjaji bado haijaeleweka, hivyo wakristo bado walikuwa na msuguano na wenzao juu ya nani achinje. 
Tamko la Polisi lilisema waislamu waendelee kuchinja sasa leo alfajiri vijana wa kikristo walienda machinjoni na kumgawia kichapo cha kutosha mchinjajiwa kiislam ambaye alifanikiwa kutoroka. 

Baada ya hapo wakristo nasikia ndiyo wakaanza hizo fujo ikiwemo pamoja na kufunga barabara, kuharibu msikiti, kubomoa nyumba ya polisi mmoja aliyejenga uraiani, wameandamana na biblia mikononi kudai haki ya kuchinja. 

Polisi wa Tunduma kazi imewaelemea na ikabidi nguvu itoke mkoani na RPC yupo huko sasa hivi. Juzi kanisani Padre mmoja alitoa kauli kuwa kama hawa watu wanataka kuchinja basi watuchinjie na kitimoto.

Kisa kikuu ni kwamba madalali wa mifugo wamegoma kupima nyama zinazochinjwa na wakristo, hivyo wakristo wanahoji kwanini iwe hivyo. Pia mtaani mabucha ya nyama zilizochinjwa na waislamu zimeganda hakuna wanunuzi.

Raia ilibidi wakimbilie mahakamani kwa kuona kwamba ndiyo sehemu pekee ya usalama kwao, hivyo ikalazimu mahakama kuhairishwa ili kuepusha balaa. Kale kamchezo kakuchoma matairi na kufunga barabara kakawa ndiyo mchezo wa kawaida.

KIM POULSEN ANASTAHILI MKATABA MNONO TAIFA STARS



Hivi karibuni kocha mkuu wa Taifa Stars, Kim Poulsen ametoa mipango mizuri kwa maendeleo ya soka. Kim ameliambia shirikisho la soka nchini kuwa anahitaji kuona kikosi cha timu ya taifa ya vijana Serengeti Boys ikishiriki michuano ya Ligi Kuu Tanzania Bara. 

Kocha Kim anasema, mpango wake ni kutaka kuona wachezaji hao wanakuwa wanacheza mechi za ushindani kwa kila wiki ya mwezi ili kuweza kujijenga kiushindani na kimbinu. Kwa mujibu wa kocha huyo, anasema kama wachezaji wa Serengeti Boys wataweza kucheza mechi moja kwa wiki, kisha wakafanikiwa kushiriki michuano yote ya Ligi Kuu basi hakuna shaka kabisa watakuwa kwenye ushindani mkali watakapopewa nafasi ya kuchezea timu ya wakubwa.
Kocha Kim anasema, wachezaji hao vijana wanatakiwa kuchezea timu ya taifa kwa muda kisha wakifikisha umri wa  kuvuka Serengeti Boys basi watarudishwa kwenye klabu zao ili kupisha wengine waweze kutumika katika kikosi hicho na kushiriki michuano ya Ligi Kuu Tanzania Bara.
Dhumuni la kocha huyo ni lilelile kuwafanya wachezaji wengi vijana wakipata nafasi na kucheza soka la ushindani wakati wote. Pia kocha Kim anakusudia kujenga kikosi bora cha miaka ijayo hivyo hakuna wasiwasi kuwa kati ya mwaka 2015 au 2017 tanzania inaweza kabisa kushiriki michuano ya Kombe la mataifa ya Afrika pamoja na kombe la dunia mwaka 2018 nchini Russia au 2022 nchini Qatar. 

Nilipotafakari programu hiyo upesi nikakumbuka namna kocha Marcio Maximo alivyoweza kuishirikisha timu ya taifa ya vijana kwenye michuano ya kombe la taifa ambalo linashirikisha mikoa yote ya jamhuri ya muungano wa Tanzania. Moja ya faida hizo ni kumjengea uwezo mshambuliaji wa TP Mazembe, Thomas Ulinwengu ambaye alishiriki kikamilifu kwenye michuano hiyo. 

Kwa wengine sasa wanaona Thomas Ulimwengu amekuwa mshambuliaji hatari na hodari zaidi, lakini njia alizopitia zimemjengea umakini na uhodari katika soka, ambako sasa anaweza kupambana na washambuliaji hatari klabuni kwake kama Kaluyituka, Given Singuluma, na wengineo. 

Kwa mtazamo wangu uamuzi wa kocha Kim kuliagiza shirikisho la soka nchini TFF kuhakikisha Serengeti Boys inashiriki mechi za Ligi Kuu Tanzania bara kuna lengo moja tu kuhakikisha anakuwa na kikosi imara zaidi cha timu ya taifa ya wakubwa(Taifa Stars). 

Ukiangalia rekodi za kocha Kim na namna anavyoweza kujenga kikosi chake katika timu ya taifa, hakika amekuwa kocha wa kipekee sana. nasema hivi sio kwasababu ya matokeo mazuri, bali muundo wake wa utendaji kazi na namna anavyoweza kutufahamisha makosa yetu kwa hekima. 

Kim anajua kabisa tulichokosa ni misingi ya soka la vijana kwahiyo anachofanya ni kuhakikisha tunakuwa na hazina ya kutosha katika soka la vijana kupitia timu ya taifa. Wakati Kim akisema hayo wenyewe tunafahamu kuwa tuna michuano miwili muhimu sana ambayo inawajenga vijana lakini bado haionekani kuwa imara kiushindani. Mfano michuano ya Copa cocacola na michuano ya Uhai. 

Hii ni michuano inayohusisha timu za vijana ambazo kwa namna moja ama nyingine zinapata faida, lakini hakuna mwendelezo wake. Kwahiyo kocha Kim amegundua moja ya sababu za kushindwa kuwa na mwendelezo ni gharama za uendeshajiu, kwahiyo anaamua kupunguza gharama hizo kwa kuitumia timu ya taifa ili iweze kusaidia kuzalisha wachezaji imara. 

Pia anaikumbusha TFF kuwa hakuna njia ya mkato kama inataka wachezaji wazuri zaidi ya kuwekeza ikibidi shirikisho lenyewe kuwa na kituo chake. Kwa mantiki hiyo badala ya kuwkusanya vijana huko mitaani na kuwapeleka uwanja wa Karume, kocha Kim anatumia timu ya taifa kama mahali pevu ambapo pataleta hamasa kwa vijana na kuongeza ujuzi wao kipindi wakirudi kwenye klabu zao. 

Pili, hii itazisaidia timu zetu kama Yanga na Simba ambazo mara nyingi zimekuwa zikisubiri wachezaji walioko timu ya taifa ndio wawasajili. Namna gani kocha Kim ataweza kuwaendeleza wachezaji watakaofanya vema kwenye kikosi cha Serengeti Boys? Hilo litateguliwa kwa kumuongezea mkataba mpya ambao utamfanya ajikite zaidi kutengeneza timu imara za timu za taifa akishirikiana na makocha wazawa. 

Nimalize kwa kusema, hakuna jambo baya kama tutaruhusu kuondoka kwa kocha Kim Poulsen wakati huu ambapo ametuonyesha falsafa bora kabisa ya soka letu. Ni vyema TFF na serikali zinaona umuhimu wa kuongeza mkataba mnono kwa kocha huyu. Muhimu tuache blah blah katika hili.

STRAIN THEOTY/CRIMENOLOGY VS UDINI NA DINI=CUHUMI?



Wataalamu kama Robert Merton waliwahi kusistiza umuhimu wa uhalifu katika jamii. Lakini kwa wataalamu hao hao wanasema, ikiwa njia za kujipatia pato zikibanwa au zikibinywa uhalifu ni kitu kinachochukua nafasi ambapo watu hutafuta pato kupitia njia zozote zile ikiwemo uhalfu. 
 
Wakasema kuwa kuna umuhimu wa uhalifu sababu unaileta jamii pamoja. Jamii inakuwa kwenye kutafuta njia mwafaka kumaliza uhalifu, lakini lazima jamii hiyo ijitolesheleze ndipo tunaweza kuufanya uhalifu kumalizika. .......

Naam kama nchi yenu haiongelei suala la ukuzaji uchumi, itaongelea nini? Kama tumeshuhudia watu kule Mwanza wanauana kisa HAKI YA KUCHINJA na kuvaa mavazi ya DINI kisha kumwaga damu, nini tafsiri yako? Je, umewaona wanaoshiriki zoezi la kuuana ni watu wa namna gani? ....je wale wanawezaje kuachwa katika faili la UCHUMI? Hatuna uchumi imara lakini hatutakiwi kuacha kutafuta UCHUMI imara.   

@Nakupenda sana nchi yangu TANZANIA. 

Hatutendi haki hata kidogo kutoandika 'aya' za uchumi wetu ambayo ndio msingi wa taifa letu na kumwachia Rais wetu Kikwete akihutubia mambo machache. Labda afadhali hayo machache kuliko kukosa kabisa. Kama tunataka kujenga utamaduni wa kutomwambia basi tunajenga taifa la watu wasioweza kufikiri au taifa la watu wanaopendelea mambo mepesi. 

Hatukatai kuona kuwa hotuba ya rais wetu haiwezi kuwaridhisha watu wote, lakini mimi naona kuna haja pia kuwakumbusha wale wote wanaohusika kuwa, wajaribu na waweze kufanya kitu ambacho kinaakisi jamii yao. Kama tunakubaliana kwamba uhalifu ni kitu kinacholeta jamii pamoja, na kwamba lazima jamii ijitosheleze basi yatupasa kujiuliza itajitosheleza katika lipi na kwanini? 

Lazima tumfanye rais wetu awe 'mgumu' kwa maana mtu 'mzito' kwa hoja nzito. Kwahiyo tusitegemee kuwa Rais anaweza kufanya hilo pekee bali lazima tusaidie, lazima kumfanya awe bora sababu ni mali yetu na tunajivunia yeye. Lakini kama kuna watu wanadhani kukosoa hotuba ya Rais ni dhambi ati sio saizi yetu hatuba budi kusema labda akina sisi tunaokosoa tumechanganyikiwa na tunakaribia kuchojoa nguo. 

Ni jambo baya sana tunapoona kila mtu anadhani waandishi wa hotuba ya Rais wanajua kila kitu. Lakini wanayo fursa ya kupata tafiti za kisasa za uchumi, makabrasha na kadhalika ili kuweza kuelezea jambo la msingi kuhusu hali ya maisha ya watu wetu. 

Ni vigumu sana kuamini kuwa Rais wetu anaandikiwa hotuba nusu, labda wenzetu walisahau, ila nakumbusha kama huijui jamii yako basi unaelekea kuchanganyikiwa. Turuhusu waandishi wa hotuba ya rais wawe hodari kwa kuwajengea hoja zenye maana sio kuwatusi. Tuwape nafasi ya kujisahihisha sababu wao sio miungu hata kidogo..

SERIKALI YASHIKILIA MSIMAMO SAKATA LA LOLIONDO



Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

SERIKALI     kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii imesema haitabidili kamwe  maamuzi iliyotoa kuhusu Pori Tengefu la Loliondo, mkoani Arusha na kuwataka wanaharakati wanaochochea mgogoro wa ardhi katika eneo hilo kuacha mara moja.

Tamko hilo la serikali, limekuja muda mfupi baada ya watu mbalimbali kutoa maoni yao kwenye mitandao na vyombo vya habari kwamba uamuzi wa
serikali kuhusu pori tengefu si sahihi.

Tamko la serikali lilitangazwa na Waziri wa Maliasili na Utalii, Balozi Khamis Kagasheki hivi karibuni kwamba, wameacha  kilomita za mraba 25,000 kwa ajili ya wananchi na serikali imechukua kilomita za
mraba 15,00 kwa ajili ya kutunza rasilimali za nchi.

Alifanya hivyo kwa kwa mujibu wa Sheria ya Wanyamapori Namba 5 ya Mwaka 2009, Sehemu ya 16 Vifungu Na. 4, 5 na 6 na kwamba muda mrefu viongozi wa wizara wamekuwa wakikutana na wananchi na viongozi wa mkoa wa Arusha na Wilaya ya Ngorongoro kujua kero zilizopo ili zitatuliwe na ndio imewezesha serikali kufanya uamuzi alioufanya.

"Ukweli ni kuwa Waziri Kagasheki alifuata sheria alipotoa tamko kuhusu kupunguza eneo la pori tengefu la Loliondo kwa mujibu wa sheria inayompatia waziri mwenye dhamana uwezo wa kupitia upya mapori tengefu na kufanya marekebisho mbalimbali muhimu kwa manufaa ya wananchi bila
kuathiri uhifadhi,"alisema George Matiko, ambaye ni msemaji wa wizara.

Katika taarifa kwa vyombo vya habari jana, Matiko alisema tamko lilizingatia tafiti mbalimbali ikiwemo utafiti wa  Taasisi ya Utafiti wa Wanyamapori (TAWIRI) na mapendekezo ya tume mbalimbali zilizoundwa kuchunguza mgogoro wa Loliondo ikiwemo ya Waziri Mkuu iliyoundwa mwaka juzi.

Aliongeza kuwa eneo la kilomita za mraba 1,500 litaendelea kumilikiwa na wizara kwa mujibu wa sheria na kwa kutambua kuwa ni sehemu ya mazalia ya wanyamapori, mapito ya wanyamapori na vyanzo vikuu  vya maji kwa hifadhi mbalimbali ikiwemo Serengeti.

Alisisitiza ardhi iliyobaki baada ya kuondoa eneo la pori tengefu la Loliondo itasimamiwa na vijiji kwa mujibu wa Sheria ya Ardhi ya Vijiji Namba 5 ya Mwaka 1999 na wananchi watawezeshwa ili waanzishe Eneo la Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori (WMA) katika ardhi hiyo kwa manufaa
yao.

"Tanzania inajali uhifadhi lakini pia inajali maslahi ya wananchi, ndiyo maana asilimia 25 ya eneo la nchi hii limehifadhiwa bila kuwepo migogoro. Hakuna migogoro kati ya wananchi na Serikali, kwa kuwa wananchi wanatambua umuhimu wa uhifadhi kwao na kwa vizazi vijavyo.

Ndiyo maana wananchi wanachangia kwa kiwango kikubwa katika kufanikisha uhifadhi,"alimaliza Matiko.

March 29, 2013

BREAKING NEWS: JENGO LA GHOROFA 16 LAPOROMOKA JIJI DAR ES SALAAM

Tunatoa pole kwa ndugu, jamaa, na marafiki wote walio kumbwa na kuanguka kwa jengo lenye gorofa 14 (Mtaa wa Morogoro, Dar-es-salaam) kwa namna moja au nyingine. Inasikitisha sana kwani vifo vingi vimetokea.    


Mtaa wa Mosque katikati ya jiji la Dar es salaam


BADO WATU WAPO ENEO LA TUKIO WAKIWEMO VIONGOZI WAKUBWA WA MKOA;ASILIMIA KUBWA YA WATU WAMEOKOLEWA HUKU VIFAA DUNI VYA UOKOAJI VIKIKWAMISHA KAZO HIYO;WATU KADHAA WANAHOFIWA KUFA JAPOKUWA SINA IDADI KAMILI


MAONI YA MHANDISI EGBART JEREMY KATIKA UKURASA WANGU WA FACEBOOK
anasema, matatizo kama haya yanachangiwa na ....

COLUM ZIMEFELI TATIZO LA WAKANDARASI ,NA WAMILIKI UNAWEZA KUKUTA KUNA KIBAO CHA KUTAMBULISHA KAMPUNI INAYOJENGA LAKINI KAMPUNI HAIPO WALA WATAALAM NI KIBAO TU KIPO LAKINI UJENZI UNAFANYWA NA MMILIKI WA JENGO. NI TANZANIA ZAIDI UIJUAVYO...... anaendelea kusema ....


NILIKUWA NAANGALIA KWENYE TV YA CHANEL TEN JINSI LILIVYO POROMOKA LIMESHUKA LOTE NIKAGUNDUA KUWA COLUMN ZIMEFELI KUBEBA MZIGO MZITO


March 28, 2013

KWETU PAZURI, KARIBU SANA NYASA

Ni pwani ya mji wa LIULI, unavyoonekana kwa uzuri. Karibu sana Nyasa, karibuni sana na kwetu pazuri.

MASANJA MKANDAMIZAJI APANIA TAMASHA LA "TUMAINI JIPYA"

Masanja Mkandamizaji


Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

MCHEKESHAJI maarufu na mwimbaji wa muziki wa Injili nchini, Emmanuel Mgaya, Masanja Mkandamizaji, amesema kuwa amejipanga imara kuhakikisha kuwa anafanya vitu vya aina yake katika onyesho la Tumaini Jipya, linalotarajiwa kufanyika mkoani Morogoro Machi 31, katika Uwanja wa Jamhuri na kushirikisha pia waimbaji mbalimbali nchini.
Akizungumza jijini Dar es Salaam, Masanja alisema kuwa amejiandaa vyema kutangaza neon la Mungu kwa kupitia kipaji chake cha uimbaji wa muziki wa Injili, akiamini kuwa afya yake itakuwa njema na kuimba pamoja na wadau wao katika onyesho hilo la Tumaini Jipya.
Alisema ingawa anatamba sana katika ulingo wa uchekeshaji kwa kuwa na aina ya uzungumzaji na kufurahisha watu wengi, lakini makali yake hayaelezeki katika uimbaji wa muziki wa injili.
“Nipo sawa kiafya na naamini Mungu atanibariki kila zuri kwa ajili ya kuimba pamoja kwenye tamasha hilo la Tumaini Jipya nikiwa na waimbaji wengine wenye makali ya aina yake.
“Itakuwa ni siku nzuri kwa siku ya Jumapili ya Machi 31 katika uwanja huo wa Jamhuri, hivyo naamini watu watakuja kwa wingi kulishuhudia neno likipenya masikioni mwao,” alisema Masanja Mkandamizaji.
Mbali na Masanja, wengine watakaofanya onyesho hilo ni pamoja na Martha Mwaipaja, Stara Thomas, Bahati Bukuku, Sifa John, Joseph Nyuki pamoja na vikundi mbalimbali vya kwaya vikitajwa kuwapo kwenye tamasha hilo la Tumaini Jipya litakaloanzia mkoani Morogoro.