May 14, 2013

TUMEAMUA KUJIRIDHISHA NA FEDHA ZA “UWONGO”!


 Na: Albert Sanga, Iringa.

Nianze kwa kuwasalimu wasomaji wa safu hii ya Anga za Uchumi na Biashara, ambayo haikuwa hewani kwa takribani wiki saba. Sababu kubwa iliyonifanya nikatoweka safuni ni msiba niliokuwa nao baada ya kufiwa na binti yangu wa kwanza na wa pekee, Faith, aliyekuwa na umri wa takribani mwaka mmoja.
Katika juhudi na mahangaiko ya kuokoa uhai wake, binti yetu alifariki katika hospitali ya Mtakatifu Kizito iliyopo Mikumi wilayani Kilosa. Msiba huu uliniachia uchungu na majonzi makubwa mno kiasi ambacho akili, moyo na morali vilitoweka kabisa na isingekuwa rahisi kumudu tafakari pana zinazoijaza safu hii.
Nimekuwa na uzoefu (kiasi Fulani) wa kumudu majanga, mitikisiko na mikasa ya kibiashara; lakini lilipokuja suala la kupoteza mtu muhimu kama mwanangu, hakika nilijikuta ni mgeni kabisa wa kuhimili mtikisiko wa msiba huu.
Matakwa yetu na maombi yetu yalikuwa ni kupona kwa binti yetu, lakini Mungu aliamua kuutwaa uhai wake. Tunamshukuru na kumtukuza Mungu kwa yote tuliyopitia nasi tunajua Mungu anabaki kuwa Mungu hata kama hakujibu tulivyotaka.
Kipekee kabisa ninatumia fursa hii kuwashukuru makumi ya wasomaji wa safu hii kutoka maeneo mbalimbali nchini ambao, baada ya kuona sionekani walinitafuta na kutaka kujua kulikoni? Mbarikiwe sana mliotutumia rambi rambi za fedha na salamu za faraja.
Ijapokuwa sikuaga wakati napotea safauni lakini sisiti kupiga mbiu inayoashiria kuwa nimerejea. Yapo mambo mengi ambayo tutaendelea kushirikishana yahusianayo na ustawi wetu kiuchumi, kiujasiriamali na kibiashara. Kwa kuwa leo ndio kwanza ninarejea, nitachambua kiunaga ubaga namna utamaduni wa watu kupenda fedha kuliko thamani ya walivyonavyo; jinsi unavyourubuni uchumi wetu.
Ni vema tukajikumbusha historia ya namna fedha zilivyoanza kutumika katika maisha ya wanadamu. Hapo zamani kulikuwa kukifanyika biashara ya ubadilishanaji wa vitu kwa vitu (barter trade). Ilikuwa kwamba mtu awapo na ng’ombe basi atabadilishana na mwenye chumvi, vivyo hivyo kwa mwenye mahindi anaweza kubadilishana na mwenye nguo.
Kadiri mfumo huu ulivyoendelea ikaonekana suala la kubeba vitu na kuzunguka navyo ili kutafuta wa kubadilishana nae ni usumbufu na lina ugumu mkubwa wa kuoanisha hayo mahitaji. Wakati mwingine mwenye ng’ombe anapohitaji chumvi halafu mwenye chumvi akawa hayupo tayari kupokea ng’ombe; basi hakuna biashara itakayofanyika na hivyo mwenye ng’ombe anakwama kupata chumvi.
Katikati ya mfumo huu kukaja kuibuka matumizi ya vito vya thamani (mfano dhahabu, pembe za thamani, chuma na madini mengine); kama viambata vya kubadilishia bidhaa (media for exchange). Hapa ilikuwa kwamba, mkulima anapovuna mahindi yake, pengine gunia kumi,  anayachukua mahindi hayo  na kuyapeleka kwa hao wanaotengeneza vito vya thamani, kasha anapewa idadi ya vito vya thamani vinavyolingana na thamani ya mahindi yake. Huu ndio ulikuwa mwanzo wa hiki tunachokiita fedha.
Hata hivyo baada ya muda kupita ikaonekana kuna upungufu katika uthamanishaji wa vito vya thamani na bidhaa wanazozalisha watu. Ndipo kukatokea watu ambao walikuwa kama wahakiki wa thamani ya vitu, mali ama bidhaa alizonazo mtu.
Hapa ilikuwa hivi; mkulima anapolima na kupata mahindi yake, pengine tuseme gunia kumi, alikuwa anayapeleka mahindi hayo eneo maalumu ambapo wanamtunzia. Wale wenye ile stoo (eneo alipotunzia), walikuwa wanaandika karatasi (kibali) linaloonesha kuwa mkulima A anamiliki magunia kumi ya mahindi yaliyopo stoo B.
Kwa hiyo mkulima alikuwa hana tena sababu ya kutembea na magunia ya mahindi kumtafuta mwenye chumvi; badala yake alitembea na lile karatasi kiasi kwamba anapofika kwa mwenye chumvi anampa lile karatasi na kupewa chumvi.
Yule aliyempa mkulima chumvi ataenda kule kwenye stoo (iliyotunza mahindi) na kuchukua mahindi yanayolingana na thamani ya chumvi aliyompa mkulima; kasha lile karatasi analiacha pale stoo. Hizi stoo zilikuwa ndio chimbuko la benki tunazoziona hadi sasa nay ale makaratasi yaliyokuwa yanaandikwa na wenye stoo ndio chimbuko la hizi noti tulizonazo hadi leo.
Hii ina maana mfumo wa mabenki na fedha ulitokea ili kuwe na haki, usawa na ukweli. Mkulima mwenye magunia kumi ya mahindi ni lazima apewe karatasi (fedha) inayoonesha kweli anamiliki hayo magunia kumi na si vinginevyo. Kama huyu mkulima akipewa karatasi inayoonesha anamiliki magunia kumi ya mahindi wakati hajapeleka chochote kule stoo ingekuwa ni kumrubuni, kumdhulumu na kumlaghai Yule mwenye chumvi.
Hii ni kwa sababu mwenye chumvi atakapoletewa lile karatasi na mkulima (aliyedanganya) ataitoa chumvi yake; lakini atakapoenda kule stoo ataambiwa hapa hakuna magunia ya hayo mahindi yanayoonekana kwenye karatasi uliyotuletea!
Baadae sana jukumu hili la kuandika (kuchapisha) haya makaratasi (fedha) yanayoonesha fulani kazalisha nini kilichopo wapi, likachukuliwa na mamlaka za kiserikali zilizokuwa zinasimamia jamii mbalimbali. Hivyo ikawa mkulima akizalisha mahindi yake anapewa karatasi lake (fedha), vivyo hivyo kwa mfugaji anapofuga na kuongeza mifugo na mjenzi anapojenga jengo. Kila mtu katika jamii alikuwa anashika fedha inayoonesha thamani halisi ya kile alichozalisha katika uchumi.
Kwa jinsi hii, tunaona kuwa, fedha katika uhalisia wake ni matokeo ya uzalishaji anaoufanya mtu katika uchumi.  Fedha sio mafanikio, isipokuwa ni utambulisho wa mafanikio. Utajiri wa mkulima hauwi katika yale makaratasi aliyoyashika (fedha) isipokuwa utajiri wake unakuwa kwenye yale magunia aliyoyazalisha. Thamani ya mwalimu haitakiwi kupimwa kwa kiwango anacholipwa isipokuwa kwa maarifa aliyoyazalisha kwa wale anaowafundisha.
Lakini katika jamii na nchi yetu sasa, watu wamekuwa wanathamini fedha kuliko uzalishaji. Watu wanapenda kupata fedha hewa! Ndio maana wanataka kuonekana ni matajiri wakati hakuna lolote walilozalisha katika mfumo wetu wa uchumi. Tunapokuwa na jamii inayothamini fedha kuliko uzalishaji; maana yake ni kuwa tuna jamii inayopenda kurubuni, inayopenda mikato-mikato, uwongo-uwongo na unyonyaji kwa wengine.
Kwa mizania ya uchumi ni kuwa moja ya sababu za mfumuko wa bei ni uwepo wa ujazo mkubwa wa fedha katika uchumi usiolingana na uzalishaji (uzalishaji mdogo). Kinachotokea ni kuwa fedha zinakuwa nyingi na bidhaa ni chache.
Wale walioshika fedha wanaanza kugombania zile bidhaa chache zilizopo; kinachotokea? Watu wanapandishiana “dau”, mwenye nguvu ananunua na mnyonge anabaki kulalamika. Matokeo? Ndio tunasikia vitu vinapanda bei kwa kasi kubwa.
Unapoona madalalai wamejaa mtaani, ambapo kila unachotaka kununua wapo katikati, ujue kuna ulaghai unafanyika kiuchumi. Ikiwa ninataka kununua nyumba na mwenye nyumba anaeuza namfahamu, dalali wa nini hapo katikati? Kwa kuwa tumeshauzoea mfumo wa udalali, ninaenunua nyumba ya milioni 25 ninalazimika kulipa milioni 30 ili dalali apewe milioni 5 yake.
Kiuchumi ni kwamba tunakuwa tumempa dalali milioni 5 za uwongo kwa sababu hakuna uzalishaji wowote alioufanya; ingawa “kijamii” tutamuona anamiliki utajiri wa milioni tano! Dalali anapoichukua ile milioni 5 na kwenda kwa mkulima kununua mahindi, unakuwa ni ulaghai kiuchumi.
Ni ulaghai kwa sababu hela ile (milioni 5) imechapishwa wakati hakuna uzalishaji katika uchumi. Kesho na keshokutwa mkulima anapotaka kuitumia ile milioni 5 kununua pembejeo anajikuta haitoshi tena (imeshuka ama kupoteza thamani) kwa sababu ni ya uwongo!
Sina ugomvi na madalali na wala siwachukii; isipokuwa tunatakiwa tuwatumie madalali pale tu panapokuwa na ulazima na ikiwa kweli uwepo wao unazalisha thamani “halisi” ya gharama wanazotaka. Madalali ni mfano mmoja tu lakini ulaghai wa kupata fedha pasipo uzalishaji upo katika mazoea mengi mno.
Kahaba anapodai malipo ya elfu 50, ni nani anaekuwa amethibitisha kiuchumi ya kuwa huduma yake ina thamani hiyo? Mfanyakazi wa serikali anapotaka asilimia kumi (10%) ili kutoa tenda kwa upendeleo, ni uzalishaji gani ameufanya kiuchumi? Mfanyakazi anapolilia mshahara mkubwa pasipo kuongeza tija kiuzalishaji, anatutakia nini kiuchumi kama sio balaa?
Uchumi wetu hauwezi kusonga mbele kwa kiwango kizuri ikiwa tunaendekeza kupata fedha na utajiri usiolingana na uzalishaji tunaoufanya katika uchumi. Hakuna fahari ya mtu kujiridhisha na utajiri ama mafanikio ya fedha yaliyopatikana kiujanja-ujanja, kimteremko-teremko na kiusanii-sanii.
 stepwiseexpert@gmail.com

May 12, 2013

MY OBJECTION TO JOHN KOMBA AND ALEX SHAURI FOR THE 2015 ELECTION. LAKE NYASA IS NOW A DISTRICT AND JOHN KOMBA IS ITS MP.



 
BY DK. James Zotto, University of Dar es Salaam

I have not seen any substance since he entered the office rather than pomposity.
It is this time, after 8 years in the office that he comes to full people to 'discuss' what he and his incumbents have already dictated! He never tolerated to receive criticisms. To me, he represents his own interests.

I was irritated by his pronouncement that before him, the lake Nyasa people never saw a car and that kids wondered his! FOOLISH! What does a car mean? Has he bought one for them? Since I was born, I saw cars in my mother village, Liuli. I was taken to and from school by mission cars! The civilization of U.M.C.A in the lake corridor cannot be ignored. There have been cars before I was born. This guy doesn't suit us.

Alex Shauri! Still not matured in thinking, and does not represent people of the lake.  Learning from his father, former Bishop Shauri of the Anglican Church-Ruvuma Diocese, whose Cathedral is located in my my village. He is my neighbour as well. It is him who, in essence, is the cause of the crisis of OUR DIOCESE TODAY. 

EXAMPLES ARE MANY. He used a lot of money and projects for his own interests. He commended the current bishop who, in hearts of the many, was not our choice let alone God's! Computers were stolen by his General secretary and sold to malawi. My father, poor fellow, then Chief accountant was held responsible for the acts the bishop and his G. secretary benefited. I am not convinced if Alex did not benefit from the misconducts of his dady!

For Marx, A CLASS REPRODUCES ITSELF! Alex is from that clergy! No hope! We need a courageous, visionary and revolutionary person-new blood-young.  Lets prepare ourselves against these people.

KAMARA KUSUPA: MWAFRIKA ALIKUWA WA KWANZA KUWASILI MAREKANI KABLA YA CHRISTOPHER COLUMBUS

Na Markus Mpangala, Dar es Salaam
HIVI karibuni nilipata fursa ya kumhoji mwandishi wa kitabu cha ‘Kumrudisha Mwafrika kwenye Asili yake: Mradi mgumu kuliko yote,’ Mwinjilisti Kamara Kusupa.
Haya ndiyo mazungumzo yetu ambayo bila shaka yatawanufaisha Watanzania kufahamu nini maana na asili ya Afrika kwa ujumla wake na maisha halisi ya bara letu.
SWALI: Niliwahi kusoma vitabu vyako viwili, “Maisha yangu Gerezani”, baadaye kile cha “Hii ndiyo Tanzania tunayoitaka”. Kuna tofauti gani kati ya vitabu hivyo na hiki cha sasa?
KUSUPA: Tofauti ipo, sababu kile cha kwanza niliongelea maisha ya gerezani na namna vijana wanyonge wanavyoteseka. Wengine wanakosa utetezi na wengine hawana msaada wa kisheria na wapo wanaogandamizwa.
Nikiwa na Mzee Kusupa
Halafu kuna wale wanaosota miaka mingi bila kesi zao kutatuliwa. Kitabu changu cha pili kimeongelea suala la nchi yetu ya Tanzania, kwamba tunataka iweje na iongozwe vipi katika kutafuta katiba mpya. Naizungumzia Tanzania ya wakoloni, baada ya ukoloni, kipindi cha Nyerere na baada ya Nyerere. Halafu nimeongelea hili suala la vyama vingi vya siasa. Lakini kitabu hiki kipya namtazama Mwafrika na matatizo yake yanayomsonga kila kukicha bila ufumbuzi huku akiwa tegemezi. Mwafrika ambaye hajachukua nafasi kuyachukua mazuri ya mababu wa asili yake.
SWALI: Lakini maandiko ya namna hii yako mengi hapa nchini na kote Afrika kwa ujumla kuhusiana na Mwafrika. Wapo Watanzania ambao wameandika vitabu kuelezea matatizo ya Afrika, mfano Dk. Malima Bundara aliandika, “Waafrika ndivyo Tulivyo”. Je, wewe unazungumzia nini kwenye hiki kitabu kipya?
KUSUPA: Nakiri yapo maandiko mengi kuhusiana na Waafrika. Yapo maandishi kama ya akina Cheikh Anta Diop (Senegal), Dk. Elly Kamugisha (Tanzania), Franz Fanon (Algeria), Julius Nyerere, Leopold Senghor (Senegal), Ali Mazrui, Marcus Garvey, Nelson Mandela na wengineo.
Lakini jambo kubwa lililokuwa likijadiliwa ni nani hasa huyu Mwafrika. Lakini wakasahau kuwa Mwafrika huyu ana asili zake, hizo ndizo ninazoongelea kwenye kitabu hicho kipya.
SWALI: Unakubaliana na mahitimisho mengi ya wasomi wa Afrika kuhusu Mwafrika ni nani na anaweza kurudi kwenye asili yake kwa njia gani?
KUSUPA: Wengi wanakubaliana kwamba Mwafrika ni mtu mweusi, hivyo kuwatenga Waarabu, Wahindi, Wazungu na Waberiberi ambao kimsingi nao wamejikuta wakiwa wamezaliwa katika bara ya Afrika hivyo hawawezi kutengwa.
Kwa mfano; msomi Dk. Harrith Ghassany alipata kuandika nini asili ya Afrika. Kwa utafiti wake akaelezea kuwa asili ya Afrika ni kutoka kule Tunisia.
Dk. Harrith alisema hayo kwenye kitabu chake cha “Kwaheri Uhuru, Kwaheri Ukoloni: Zanzibar na Mapinduzi ya Afrabia.” Yote haya yanatuletea swali la msingi Mwafrika huyu ni nani?
Hata hivyo dunia imebadilika na kila kona inatusaidia kujua nini hasa kinachopaswa kusemwa kwa dhati na moyo safi kwa nyakati za sasa na baadaye. Kuna Wazungu wamezaliwa Afrika Kusini, Tanzania na wengine nchi nyingine za Afrika.
Je, hawa watakwenda wapi ikiwa hawajui asili zao au mahali walikoanzia zaidi ya kujikuta wakiwa katika nchi wanazoishi. Ni kama ambavyo Waafrika walioko Ulaya, Amerika na Asia wanavyojiuliza ni namna gani wataweza kurudi Afrika ambako hawajui waanzie wapi.
Ni vigumu leo kumwelezea Jesse Jackson, Mohamed Ali warudi Afrika kutoka Marekani. Ni vigumu vile vile kumweleza Lennox Lewis wa Uingereza arudi barani Afrika.
Ni vigumu kumwambia Danny Jordan wa Afrika Kusini kwamba uchotara wake sio kitu arudi kwenye asili ya makaburu Uholanzi na kwingineko. Au ni vigumu kumwambia Hellen Zille, mwenyekiti wa chama cha upinzani cha Democratic Alliance (D.A) pale Afrika Kusini na gavana wa jimbo la Cape Town, kwamba arudi kwa wazungu wenzake.
SWALI: Unadhani hilo linatokana na uhusiano wa Waafrika na wageni, ndio kiini cha Mwafrika kurudi kwenye asili yake?
KUSUPA: Kwanza niseme hii ni moja ya mabadiliko makubwa ya mipaka ya nchi ambayo imeshindwa kuzuia uhusiano wa wanadamu kutoka nchi moja hadi nyingine au kutoka jamii ya nchi moja kwenda jamii ya nchi nyingine.
Leo Mwafrika anaweza kuzaa na Mchina au Mkorea hivyo ni vigumu mtoto atakayezaliwa kutotambuliwa kuwa Mwafrika, na kuangalia asili. Lakini wapo watu wanaojaribu kujiuliza ni namna gani wanaweza kuwakumbusha Waafrika wenzeo kuwa Mwafrika alikuwa na asili yake.
Hata kwenye dini, Waafrika wanazo. Ukisema Waafrika hawana dini nitakuambia soma maandiko ya Mchungaji Blacid Temple kwenye kitabu chake cha “Bantu Philosophy”, kwa hiyo ushahidi wa asili zetu upo kidini, kisiasa na kiuchumi.
Propaganda iliyohubiriwa kwa nguvu na pia kufundishwa na elimu ya kikoloni ni kwamba Mwafrika ameanza kuwa na dini baada ya ujio wa Waarabu na Wazungu barani Afrika.
Baada ya kazi ni gumzo
Kwa mfano; katika Afrika ya Mashariki, Uislamu uliingizwa katika karne ya nane na wafanyabiashara kutoka Ghuba ya Uajemi (leo tunaita Iran), hao wafanyabiashara wa kiajemi ndio walioitia jina la Dar es Salaam mji maarufu wa Tanzania lenye maana ya mbingu ya amani.
SWALI: Je, ni kweli kwamba kabla ya ujio wa wafanyabiashara wa kiajemi, Waafrika wa eneo hili hawakuwa wakimwabudu Mungu?
JIBU: Narudi kama nilivyoeleza mwanzoni, Waafrika walimjua Mungu wa kweli, walimwabudu na kuishi kulingana na miongozo yake. Ushahidi wa kuonyesha Mwafrika aliabudu Mungu kabla ya ujio wa Uislamu na Ukristo ni uwepo wa majina yanayoendana na masuala ya kiroho na ibada.
Lakini tunapokuja kwenye eneo linalohusu mambo ya kiroho, maneno kama ibada, Nnungu, Mungu, Mulungu, Ngai, Nkoyi, Kyala, Malaika na Banzelu neno kutoka lugha ya Kilingala lenye maana ya viumbe weupe wanaong’ara  ni udhihirisho wa kwamba Mwafrika  alimjua Mungu na alikuwa na mawasiliano naye.
Katika somo hili tunajadili kwa ufupi juu ya Uislamu, Ukristo, Ubuntu na dini ya asili iitwayo Alabba ndani ya kitabu nimeeleza sana hili.
SWALI: Mwafrika haonekani kutajwa kwamba mmoja wa watu waliowahi kuishi au kufika Marekani kabla ya ukoloni. Labda tuseme Latini Amerika yote kusini na kaskazini. Lakini tunashuhudia Waafrika wengi wakiwa huko na baadhi ya mila na desturi zao zinalingana na Waafrika wa bara la Afrika. Kwa nini?
KUSUPA: Kwanza niseme wanaoeneza kuwa Mwafrika hakuishi Marekani kabla ya biashara ya utumwa hawako sahihi, au kule Latini Amerika. Kuna sababu nyingi, lakini kubwa ilianzia kwa Columbus.
Mwafrika alikuwa wa kwanza kuwasili Marekani kabla ya Christopher Columbus, hata ukisoma maandiko yenye ushahidi yaliandikwa na Profesa Ivan Sertima kwenye kitabu chake "THEY CAME BEFORE COLUMBUS". Hizo  'voyage' mbalimbali za Christopher Columbus zimejaa mengi ya kushangaza na kwa nini yanachukuliwa kuwa kama yalivyo au ukweli wenyewe? Waafrika wanayo mengi hayakuandikwa vizuri.
SWALI: Kwa hiyo una maana kwamba ndani ya Kumrudisha Mwafrika kwenye Asili yake: Mradi mgumu kuliko yote umeelezea nyongeza yake na hali halisi ya Mwafrika na asili zake, ukizingatia dhana ya uhai pia?
KUSUPA: Kwanza tunaangalia sisi Waafrika ni nani na asili yetu ikoje, hicho ndio kiini. Dhana ya uhai inakuwa kubwa na inachukua mkondo mkubwa pia, hivyo basi kitabu cha KUMRUDISHA MWAFRIKA KWENYE ASILI YAKE; MRADI MGUMU KULIKO YOTE nimeleta baadhi ya majibu ya maswali ambayo kila mara watu wanajiuliza.
Nimeelezea kuanzia kwenye dini, siasa, utamaduni, na mengine mengi kuhusu Afrika, nimeelezea mengi kwamba kuna makosa kadhaa yanafanyika ni vigumu kuizungumzia Afrika kama wanazuoni Ali Mazrui wanaoitazama Afrika kichotara.
SWALI: Unazungumzia Afrika ya kichotara, una maana gani hasa?
KUSUPA: Hakuna wakati wowote katika historia ya dunia na maisha ya mwanadamu kiujumla, ambapo Afrika imeacha kuhusiana na watu kutoka nje ya bara hili, hivyo nazungumzia Afrika na Wageni kutoka Ulaya, Amerika na Asia. Tangu awali na baada ya Kristo watu kutoka nje wamekuwa wakiingia Afrika kwa sababu moja au nyingine.
Katika mada hii ya Afrika na wageni, tunazungumzia wageni wa aina tatu kutoka nje ya bara la Afrika. Tunajadili juu ya Afrika na wafanyabiashara kutoka mabara mengine ya Asia, Ulaya na Arabuni, Afrika na waeneza dini kutoka nchi za ulaya magharibi na Afrika na Wazungu wa  magharibi waliojifanya wavumbuzi yaani wale wachoraji wa  ramani za kuonyesha mito mikubwa, milima mirefu na maziwa.
Tunajadili juu ya Afrika na tamaduni za kigeni, Afrika na dini za kigeni na mwisho tunajadili juu ya Afrika na tawala za kigeni ikiwa ni pamoja na mifumo inayoendelea kutumika hadi sasa kuongoza maisha ya Waafrika.
Kila jamii imekuwa kwenye asili yake na inakuwa vigumu kurudi kwenye asili yake. Tujiulize je, dini za Waafrika ni zipi? Mfumo wa utawala wa Waafrika ni upi?
Msingi wao na dhana ya uhai vikoje? Uhusiano wao na jamii za nje ukoje? Je, Mwafrika ataepuka dhahama ya mabadiliko ya kijamii duniani? Je, Mwafrika ataweza kurudi katika asili yake?
Nadhani ni moja ya mambo ya kusisimua na hakika yatakuwa na hamasa kwa wasomi mbalimbali na wananchi wengine. Kikubwa tuseme kama kweli tutaweza kurudi kwenye asili yetu au ni mradi mgumu?
SWALI: Katika kitabu chako umegusia suala la muungano wa bara Afrika?
KUSUPA: Hilo nimezungumzia kwa kina. Nimeanza toka kwenye utumwa, ukafuatia ukoloni na baadaye utawala wa chama kimoja au udikteta wa chama kimoja.
Hatimaye Afrika imeletewa utandawazi unaoyafanya mataifa yenye nguvu yawe dikteta wa kudumu wa kuzilazimisha nchi za Afrika kujiendesha sawa na watakavyo wao.
Afrika iligawanywa vipande vipande na kuitwa majina mapya na wakoloni, lakini pia wakoloni hao wakati wanachora na kuweka mipaka yao ya kufikirika, ndipo waafrika tulipogawanywa na kutenganishwa na kupewa utambulisho mpya wa kuitwa Watanganyika, Wakenya, Waganda, Wakongo, Wanyarwanda, Warundi, Warhodesia, Wamozambiki, Wanigeria, Wakameruni, Waghana, Wasenegali, Wamali, Waliberia, Wasealeoni, Wanamibia, Waangola, Wasudan, Wasomalia, Waethiopia n.k.
Wakati wakoloni wanaigawa Afrika na kuweka mipaka yao mipya tofauti na ile mipaka ya asili iliyokuwa inatambuliwa na wenyeji, pia waafrika walitenganishwa na kuumbiwa hisia mpya. Mpaka wa kutenganisha nchi na nchi nyingine uliweza kupita katikati ya eneo moja na kuwafanya watu wa kabila moja au ukoo mmoja kuwa na uraia wa nchi mbili tofauti. Hivyo Afrika lazima iungane.
SWALI: Nashukuru kwa kushirikiana katika fursa hii. Naamini Watanzania watanufaika kutoka katika maandiko yako mazuri ya kitabu chako.
KUSUPA: Karibu wakati mwingine, ninyi vijana mnatakiwa kujua zoezi jipya la Afrika kuwa na mipaka mipya lilimpa Mwafrika hisia mpya na utambulisho mpya. Nitafanya mhadhara UDOM kuelezea hilo Mungu atujalie. Kwa hiyo lazima tujirudishe kwenye asili zetu.
Baruapepe; mwanazuoni27@gmail.com

UDINI, UGAIDI MPAKA KUZIBA PANCHA ZA MITIHANI

Na Markus Mpangala, Dar es Salaam

Ulianza UDINI. Tukaambiwa chama fulani cha siasa ni cha kidini. Baadaye tukaelezwa kuwa kinafadhili au kutunza magaidi hapa nchini. Tukaambiwa wanaleta visu, silaha na kadhalika. Baadaye tukaambiwa chama fulani ni cha waumini wa dini fulani. Yalikuwepo mwaka 1995. Yakawepo mwaka 2000. Yakaongezwa mwaka 2005. Yakarutubishwa mwaka 2010 kwamba chama fulani cha waumini fulani. Sasa Bungeni tunasikia na kuambiwa chama fulani ni Magaidi. Halafu wale wa chama hicho nao wanasema chama fulani ni Magaidi.
Ndugu zangu, kuchanganyikiwa huku na hitilafu ya kijamii ilisababishwa na watu. Ni watu waliopika kwa juhudi UDINI. Wakapika kwa maarifa na jasho la kipumbavu. Baadaye wameanza kupikana kwa UGAIDI bungeni. Hili suala lilianza zamani sana juu ya Magaidi hapa kwetu (tukumbuke zama za uongozi wa mzee wetu Omar Mahita). 

Sote kinachotokea tunakiona, na tunalaghaiwa sana sababu tumekubali kulaghaiwa. Hakuna njia ya mkato kwamba kuchanganyikiwa huku kwa jamii yetu na kile kilichosababisha kufutwa kwa mitihani ya kidaoto cha nne, nadhani nako ni kuchanganyikiwa kulekule. Yaani tumejikuta tumechanganyikiwa kiasi ambacho hata binadamu aliye mbele yako ni adui bila kujua sababu zako za kufikiria yeye ni adui. 

Mapishi ya kuwagawa wananchi wa Tanzania yapo mengi na kwa kila namna. Sote tunashuhudia hili kila kona na hakuna aliye tayari kukiri kuwa alihusika ama yeye ndiye mhusika. Serikali inawalaumu wananchi wake, hali kadhalika Wananchi wanailaumu serikali yao. Chama tawala wanawalaumu vyama vya upinzani, hali kadhalika vyama vya upinzani wanakilaumu chama tawala.
Idara za serikali zinawaambia watu na kuwatisha kuwa wakijadili uchochezi watakamatwa. Mimi nasema hatukufikia kujadili fikra za kichochezi hivi hivi kama sio kujilemeza na kutawaliwa kwa njia ambazo zinaleta ukakasi.
Wimbo wa uchochezi ni matokeo ya kujaribu kufifisha fikra huru zenye kujadili mambo ya msingi, maana kinachofanywa ni kujumuisha sote tumekuwa wachochezi. Daima utawala mbovu husingizia na kulaumu kuwa kuna watu wachochezi, na mwishowe kila mara kazi yake ni kujitetea kila uchao. Hakika tumechanganyikiwa mno. 

Leo hii tumeruhusu watu wajione waathirika wa masuala ya kufikirika. Leo tumeruhusu kugombana sababu ya kuchinja. Leo tunagombana sababu ya imani za dini. Leo tunatishia uhai na kuitana majina mabaya ndani ya Ukumbi wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Spika wetu mheshimiwa naye anasikia kauli chama fulani cha kigaidi na mlalamikiwa naye anakuja juu akisema chama fulani ni magaidi. 

Malumbano haya yanapoachiwa kwenye jengo la Bunge nadhani watu huku pembeni wanaendelea kulishwa kwamba tishio letu ni ugaidi na sio umasikini wa kipato. Hakuna aliye tayari kuona ghasia za uchumi duni, shida zilizojaa pomoni kwa mwananchi wa Tanzania, ambao unachochea kuchanganyikiwa kijamii. 

Na kuchanganyikiwa huku hata askari wetu wametuhumiwa kupora milioni 150 za majambazi waliokamatwa. Sote tunaona. Hii ni ishara kwamba kuchanganyikiwa huku ni kukubwa mno. Tumechanganyikiwa kijamii na madhara yake hata kwenye uongozi ndiko kumechanganyikiwa kabisa, kumepumbaa,wameduwaa hawajui tufanye nini katika Tanzania ya leo kuondokana na vijitukio vya kuhasimiana nchini.
Na hakika kuchanganyikiwa huku ni kukubwa kuliko kitu chochote. Wimbi la nyumba za ibada ni kubwa mno lakini cha ajabu matendo yenye dhambi yanazidi kushamiri. Hakuna hata lenye kificho kwamba, kama serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania haichukui wakati kujisaili yenyewe basi itakuwa kila hotuba za kila mwezi ni kujitetea kwingi zaidi na zaidi.
Istilahi za kuishi kisungura kumetufanya tuone tofauti zetu za kidini ni moja ya mambo yanayotakiwa kuchukiwa badala ya kuishi kwa amani na upendo huku tukikubali kuwa hilo ni suala la imani ya mtu. Serikali huwa inatamba ina mkono mrefu, lakini leo hii tunashindwa, tumelemaa, tumekwama hata kuchunguza masuala mepesi, lakini kinachofanyika ni walete FBI au CIA na kadhalika. 

Lakini hawa hawa FBI, CIA ndio waliofanikiwa kuivuruga Afhanistan iliyokuwa imetulia chini ya Maflme Najibullah. Kwa vigezo vya nchi zao wakadhani utawala wa kifalme Afghanistan haina demokrasia. Ulaghai huu ukajikita, Mfalme Najibullah hayupo leo, Hamid Karzai amebaki kuwa kibaraka wa Marekani na sasa tuhuma kubwa ya kupokea fedha kutoka CIA ni kubwa mno. 

Gazeti la The New York Times limeripoti tuhuma hizi kwa kirefu sana wiki iliyopita, na kumtia kigugumizi Rais Hamid Karzai. Yote haya yanafanyika kwa udhamini huu huu wa kudhani FBI au CIA ni wapendwa sana. Tumechanganyikiwa hata makachero wetu hatuwaamini wakati tunatumia fedha nyingi kuwasomesha ughaibuni na hapa nchini.
Makachero ambao tumewapa mafunzo ya kila namna lakini tunawakejeli kwa kuwaletea FBI. Ugonjwa uleule wa ukoloni tunajaribu kuurudisha kwa mlango wa nyuma. Na sifa ya ukoloni kwa sasa ni kurejea katika njia za utamu utamu na vitu vyote vyenye utamu. Kuchanganyikiwa kwetu huku ni kukubwa sana. Mimi nadhani lazima tuchukue hatua za msingi na kuwa wakali. 

Serikali ya nchi yoyote sio lazima ipendwe kwakuwa inawajali wananchi kwa kuwaachia wajichane na kustarehe kwa uhuru, bali hata ukali na kuwaadabisha raia wake ni njia moja wapo ya kupendwa kwa serikali. Wimbi la uchochezi linaibuka katikati ya kulemaa kwa kusimamia masuala ya msingi. Tunazo sheria za kila namna lakini tilichoweza kukifanya ni kuachia mambo yajiongoze yenyewe halafu baadaye tuseme kila mwezi kwa hotuba dhaifu na kujitetea. 

Benjamin Mkapa alinukuliwa siku za karibuni kuwa viongozi wa kizazi kipya wameshindwa kazi hivyo wanachotakiwa ni kuwapisha wale kizazi cha kale. Lakini kwa upande wake Mheshimiwa Zitto Kabwe aliwahi kudokeza kuwa nchi yetu haiwezi kujikwamua hapa ilipo kwa kutegemea uongozi au kiongozi aliyetokana na zama za ukoloni yaani waliozaliwa kipindi hicho. 

Shida hapa sio kuzaliwa lini, bali namna gani hatua stahiki zitatuondoa kwenye kuchanganyikiwa huku ndani ya jamii yetu. Tumechanganyikiwa kiasi kwamba suluhu yake ni kuziba pacha za mitihani kwa kuwadekeza wanafunzi waliochora zombi, Messi na kadhalika. Uonevu huu baadhi ya wananchi wananiuliza, tumeikosea nini nchi hii? Kuchanganyikiwa kwetu huku ni kukubwa mno hata nashangazwa na Baraza la Mawaziri kuidhinisha kufutwa mitihani. Kisa? Hakuna jingine zaidi ya kuchanganyikiwa kiuongozi. Tuko pabaya sana, lakini tunaelekea mahali pazuri sana kadiri tunavyozidi kuchanganyikiwa. Amani iwe nasi daima.

Baruapepe; mwanazuoni27@gmail.com