March 12, 2018

SASA MWATUGAWA KWA ITIKADI ZA KISIASA.

NA. HONORIUS MPANGALA
 
WAKATI aliyekuwa Rais wa awamu ya kwanza wa taifa hili la Tanzania alikuwa kiongozi aliyewaunganisha watanganyika, sasa mambo yamekuwa tofauti kiasi. Katika hili wako ambao wanashindwa kukemea kutokana na mitazamo ya namna gani wataweza kuonekana mbele ya wenzao kiitikadi.

Hatuko kama majirani zetu kwasababuya  misingi iliyowekwa na waasisi wa taifa hili ni mizuri na inayowafanya wananchi wake kuwa na hofu ya mungu.
Ni jambo la kawaida sana kumkuta mtanzania wa kabila la kisukuma akiwa na mifugo yake katika bondel la mto Lwika huko wilayani Nyasa akiipa malisho mifugo hiyo. Ni kutokana na kazi kubwa iliyofanywa na waasisi wa taifa letu kwa kuondoa suala la ukabila miongoni mwa watanzania.
 Tangu taifa hili liasisiwe hakuja wahi tokea ugomvi wowote uliohusisha makabila moja na jingine. Hii ni kutokana na kujaliana kwetu na kufuata ile misingi ya ugugu baina yetu kama taifa moja. Katika upande wa masuala ya kiimani iliwahi kutokea mara moja katika utawala wa awamu ya tano,mgomo wa wakristo na waisalamu ambao ulihusisha suala la kuchinja.

Wakristo walikuja na hoja ya kutaka kuchinja pia huku wakihoji kwanini suala la kuchinja liwe kwa waislamu pekee. Mgogoro ule haukuchukua muda mrefu kwani uliisha kwasababu ya ubora wa watatuzi wa masuala ya kijamii na hata kuenzi ile tunu yetu kama taifa.

Viongozi wetu walifanikiwa katika sana katika kutufanya watanzania kuwa watu tunao ishi kama ndugu.Lakini kwa miakamya hivi karibuni kumekuwa na matukio au vitendo visivyo vya kawaida kutokea katika taifa letu.

Siasa imekuwa sehemu ambayo watu wanaitafsiri tofauti kulingana na matukio au mienendo yake katika taifa letu. Imefika wakati wazazi wa kitanzania wakiona motto wao anajiingiza katika masuala ya kisisasa basi huweza kukutana hata kauli za kutolewa maneno makali na mzazi kwani mvuto wa kujiynga na masuala ya siasa umepotea. Kupotea kwa mvuto huo kwa wazazi kunatokana na hofu yao juu ya matukio yanayohusisha wanasiasa katika asrdhi ya Tanzania.

Katika mienendo isiyo ya kawaida Watanzania wamefikia hatua hata ya kusaidiiana katika matatizo kwa kutazama ukubwa wa tatizo kupitia chama cha kisisasa.Ni jambo la kawaida siku hizi kukuta katika misiba wafuasi wa vyama vya siasa wakitinga sare zao misibani na kuendesha msiba kwa kutazama marehemu alikuwa mfuasi wa chama gani.

Niliwahi shuhudia misiba iliyokuwa inahudumiwa na wafuasia wa Chadema kwa kiasi kikubwa huku wakiwa wamevalia sare za chama chao. Swali langu kwao lilionekana kama nawakejeri kwani nilikuwa nauliza “kuna uhusiano gani wa msiba na chama cha kisiasa?” Lakini sikuweza kupata majibu yaliyonifanya nitosheke.

Hali hii haikuwa kwa chadema pekee bali hata CCM nao waliweza kufanya hayo katika misiba iliyowahusu wafuasi wao. Hivyo swali kama nililowauliza wafuasi wachadema hata nwao niliwauliza lakini unakutana majibu ya kushangaza sana kutoka kwa watanzania hawa.

Mra kazaa katika misiba inayomkuta mtu ambae hayuko karibu sana na masuala ya kisiasa basi kinachotokea hapo ni michango anayochangiwa mfiwa kuja kwa sura ya vyama vya siasa. Utakuta katika usomwaji michango unasikia chama Fulani cha kisaisa kimetoa kimetoa mchango kiasi Fulani. Jmabo hili limeweza kupenya katika ubongo wa watanzania na kufikia hatua ya kubaguana katika masuala ya kijamii kama misiba.

Ukitokea msiba wa mfuasi wa Cuf basi unakuta mfuasi wa CCM au Chadema akawa hana mwitiko mkubwa na tukio hilo labda awe ndugu.
Kasumba hii ya kugawa watu kisiasa imekuja wakati siasa za nchi hii zikiwa zimeshika kasi sana na mwitikio wa masuala ya kisiasa ukiwa mkubwa pia.Kumekuwa na masuala yasiyo ya kiutu baina ya wafuasi wa vyama vya siasa nchini.

Licha ya kwamba wale viongozi wakubwa wa vyama vyao wamekuwa na mwonekano wa kuyakemea haya masuala yanayoendelea kwa wafuasi wao lakini pia kwa namna moja ama nyingine bado hili suala halijapatiwa tiba na linazidi mkuendelea baina ya wafuasi wa vyama vya siasa.

Kila inapotokea masuala ya kisiasa kama vile kufanyika kwa uchaguzi mkuu au hata chaguzi ndogo ndogo za kuziba nafasi za wagombea waliojiudhuru au kufariki, changamoto kubwa sana hutokea hasa katika masuala ya ulinzi na usalama wa wafuasi wa vyama unakuwa sio wa kuridhisha.

Matukio ya kutekana au hata kuvamiwa na kusababisha vifo vya baadhi ya wafuasi wa masuala ya siasa au viongozi hujitiokeza sana. Na imekuwa kama tatizo sugu ambapo unakuja kusikia watenda kosa au tukio kutopatikana ikiwa ni jambo ambalo linazidi kuwafanya watanzania wengine kushindwa kuvielewa haraka vyombo vinavyohusika na masuala ya ulinzi na usalama wa raia.

Leo hii ziko familia ambazo zimejenga chukiza wazi dhidi ya wafuasi wa vyama fulani kutokana na yale wanayokutna nayo ndugu zao. Hata kama itatokea umma ukataka kuaminishwa kuwa matukio haya hayana uhusiano na masuala ya kisiasa unaweza kujikuta una umiza akili ili kujua ni masuala gani mengine ambayo kiongzoi wa Chausta anaweza kukutana nayo na yakatoka katika masuala binafsi na sio siasa anazofanya.

Tayari familia kama ya aliyekuwa katibu wa Chadema Kata ya Hananasif mkoani Dar es salaam, Daniel John inashindwa kuelewa kwanini ndugu yao alitekwa na kuteswa hadi kufa. Ni kipi ambacho kinaweza kikawa ni cha nje ya masuala ya kisiasa na ikafanya aje kupata matatizo haya ya kutekwa?

Na mara nyingi masuala ya mihemko iliyo juu na wafuasi kujifanya ni wako mstari wa mbele ili kutekeleza taratibu walizojiwekea kama chama. Kila chama kikiwa na lengo la kushika dola inahitajika utu na kuenzi tunu za taifa jambo ambalo linahitajika kufanyika ili kuwafanya watanzania kuwa wamoja.

Nimewahi kushuhudia msiba wa mfuasi wa CCM vijsns wengi katika eneo hilo la msiba walikuwa ni wafuasi wa Chadema basi waligoma kwenda kuchimba kaburi kwasababu tu ya kumbukumbu zao juu ya familia ya marehemu na marehemu kuwa wafuasi wakubwa wa chama cha mapinduzi. Unaweza kuluiona kama jambo dogo lakini kwa jinsi linavyotafsiriwa na jamii ni tofauti na linapanda mbegu mbaya miongoni mwa jamii.

Wanasiasa waacheni wafuasi wavyma vya siasa wafanye siasa zao katika hali ya utulivu na amani. Vitendo vya vitisho na kufikia hatua ya kuviziana kisa tu siasa itafika wakati tutashindwa kujua tumlaumu nani,mamlaka au sisi kama jamii.

Siasa za kuviziana sio za kimaendeleo maana watu husubiri wapi utaharibu ili wachukue hoja ya kuweza kuiongeza mbele yaw engine. Maendeleo unakuja kwa ushirikiano uliopo baina ya jamii na viongozi wao wa kisiasa,kitaalua na msiache mbegu mbaya au roho ya visasi ikataka kuota katika mioyo hiyo. Yale yanayotokea leo yataweza kusishi kwa miaka mingi na kuwafanya watu kuwa na roho za visasi.

Viongozi wa kisiasa wana kila sababu ya kujitazama tena na kuona kama haya matukio yanayotokea wakati wa harakati zakiuchaguzi ni kweli hayana mahusiano na siasa.Vyombo vya ulinzi na usalama wa raia wana kila sababu ya kuwajuza watanzania namna gani wanafanikisha kukabiliana na matukio yasiyo na utu katika nyakati za matukio ya kisiasa.

No comments:

Post a Comment

Maoni yako