Kila mwandishi wa kitabu anatakiwa kuwa mwandiko wake
rasmi. Mwandiko huo humtambulisha mwandishi kila kazi yake inapochapishwa na
kuingizwa sokoni. Hiyo inatusaidia sisi wasomaji kutambua mwandiko wa mwandishi
husika.
Na mwandiko huo upo kwenye “Font Style”. Uchaguzi mzuri wa
mwandiko unamfanya mwandishi kuuza kazi zake kwa mwandiko rasmi.
Aidha, mwandiko huo hubeba alama ya mwandishi husika, bila
kubadili badili ‘Font Style’. Mathalani, mwandiko wa mwandishi Fadhy Mtanga
unafahamika. Tazama vitabu vyake utagundua ana “Font Style” rasmi inayokaa vema
kitabuni.
Pia jina la mwandishi linatakiwa kuwa na ukubwa unaoonekana
siyo mdogo kama ‘byline’ ya gazetini. Jina lako ni biashara, lazima lionekane
kuwavutia zaidi wasomaji kama sisi tunaopenda kutemea mate kidoleni na kufunua
ukurasa unaofuata. Mwandiko kama huu kitabuni unafaa kuendelezwa na ndugu
mwandishi wa riwaya hii. Ni mwandiko mzuri.
©Markus Mpangala
No comments:
Post a Comment
Maoni yako